Pendo Julliet
JF-Expert Member
- Sep 15, 2017
- 243
- 324
Hili ni kwenu vijana wa kitanzania wasomi wa vyuo vikuu.
Vijana hamfahamu hata HAKI zenu za msingi yani hamjielewi, hamjitambui na mpo mpo tu kama juzi na jana vile.
Mambo mengi ya hovyo yanayoendelea kufanywa na wabinafsi wachache walohodhi madaraka ya nchi huko Tanzania yanathibitisha hili la vijana kutojitambua.
Mfano wa hivi karibuni ni Mikopo ya elimu ya juu, hapa HAKI zenu zimepokwa wachache wamepata na wengi wamebaguliwa kwa kukosa mikopo hivyo kupoteza HAKI ya kimsingi sana ya kueza kupata elimu ya juu kwa kushindwa kumudu gharama za masomo.
Wengine ni continuing student mwaka ulopita walipata mkopo mwaka unaofata wananyimwa kwa sababu zisizo na mantiki tena huu ni ubaguzi tu kama ule wa makaburu wa South Afrika.
Sasa ajabu sana kwa vijana wa kitanzania ambao ni wasomi wanashindwa kudai HAKI zao na utagundua hata viongozi na mashirikisho ya vyuo vikuu sijui wanaita TAHLISO nao wanashiriki katika kupoka HAKI za wenzao wahitaji wa mikopo kwa kuendelea kubaki kimya bila hata kuonesha kupinga hata kwa kukemea tu au kulaani. Kwanza hawa viongozi hawastahili kuendelea kuongoza hayo mashirikisho.
Wasomi kwa nchi zilizoendelea wanakuwa ni mfano wa kuigwa kwenye jamii na kuhakikisha mambo yote yanaenda sawa kwa kufata taratibu zinazotakiwa, sheria na HAKI bila dhulma na uonevu unaojengwa kwenye misingi yoyote ile.
Wanaotarajia huruma za wadhalimu na wabaguzi ili kupata mikopo bila kuchukua hatua za kudai HAKI zenu hilo msahau mtalia sana wenzenu wanafurahia kuwaona mkilia hivyo.
Tena mkiendelea kulala mafanikio mtaendelea kuyaskia kwa wenzenu wa Asia, Amerika na Ulaya kazi yenu itakuwa kuwakaribisha kwenu wakija kwa jina la 'wawekezaji/wahisani/wadau wa maendeleo'
hali wanakuja kuwatawala kwa mara nyingine tena.
Amkeni na chukueni hatua kulialia hakusaidii HAKI hutafutwa.
'MWANANGU MSHIKE SANA ELIMU NA USIMUACHE AENDE ZAKE '.
[HASHTAG]#HAKI[/HASHTAG].
Vijana hamfahamu hata HAKI zenu za msingi yani hamjielewi, hamjitambui na mpo mpo tu kama juzi na jana vile.
Mambo mengi ya hovyo yanayoendelea kufanywa na wabinafsi wachache walohodhi madaraka ya nchi huko Tanzania yanathibitisha hili la vijana kutojitambua.
Mfano wa hivi karibuni ni Mikopo ya elimu ya juu, hapa HAKI zenu zimepokwa wachache wamepata na wengi wamebaguliwa kwa kukosa mikopo hivyo kupoteza HAKI ya kimsingi sana ya kueza kupata elimu ya juu kwa kushindwa kumudu gharama za masomo.
Wengine ni continuing student mwaka ulopita walipata mkopo mwaka unaofata wananyimwa kwa sababu zisizo na mantiki tena huu ni ubaguzi tu kama ule wa makaburu wa South Afrika.
Sasa ajabu sana kwa vijana wa kitanzania ambao ni wasomi wanashindwa kudai HAKI zao na utagundua hata viongozi na mashirikisho ya vyuo vikuu sijui wanaita TAHLISO nao wanashiriki katika kupoka HAKI za wenzao wahitaji wa mikopo kwa kuendelea kubaki kimya bila hata kuonesha kupinga hata kwa kukemea tu au kulaani. Kwanza hawa viongozi hawastahili kuendelea kuongoza hayo mashirikisho.
Wasomi kwa nchi zilizoendelea wanakuwa ni mfano wa kuigwa kwenye jamii na kuhakikisha mambo yote yanaenda sawa kwa kufata taratibu zinazotakiwa, sheria na HAKI bila dhulma na uonevu unaojengwa kwenye misingi yoyote ile.
Wanaotarajia huruma za wadhalimu na wabaguzi ili kupata mikopo bila kuchukua hatua za kudai HAKI zenu hilo msahau mtalia sana wenzenu wanafurahia kuwaona mkilia hivyo.
Tena mkiendelea kulala mafanikio mtaendelea kuyaskia kwa wenzenu wa Asia, Amerika na Ulaya kazi yenu itakuwa kuwakaribisha kwenu wakija kwa jina la 'wawekezaji/wahisani/wadau wa maendeleo'
Amkeni na chukueni hatua kulialia hakusaidii HAKI hutafutwa.
'MWANANGU MSHIKE SANA ELIMU NA USIMUACHE AENDE ZAKE '.
[HASHTAG]#HAKI[/HASHTAG].