Mikoa + wilaya mpya faida yake nini kwa mtanzania wa kawaida?

The Analyst

JF-Expert Member
Feb 26, 2011
464
246
Naomba kusamehewa kwa kushindwa kwangu kulielewa jambo hili mwenyewe na hivyo kuamua kuwashirikisha Greater Thinkers ili kupata logic. Nimesikia na kushuhudia baadhi ya wakaazi wa maeneo husika wakifurahia na kuwashukuru watawala kwa uamuzi wa kuwaundia mikoa au wilaya na kuweka makao makuu katika maeneo yao. Nisichokijua kwa uhakika ni je kuna chochote anachokipata mtanzania wa kawaida katika kuundwa wilaya au mkoa mpya ambacho asingekipata katika wilaya na mikoa ya awali?
Je si wazi kwamba fedha nyingi zitakazotumika kuendeleza makao makuu ya mikoa na wilaya mpya, kuwalipa wakuu wake na wasaidizi wao zingeweza kuleta maendeleo muhimu na makubwa katika mikoa iliyokuwapo awali? Tafadhali tutafakari pamoja swala hili. Was this decision that important to our poor country?
 
Naomba kusamehewa kwa kushindwa kwangu kulielewa jambo hili mwenyewe na hivyo kuamua kuwashirikisha Greater Thinkers ili kupata logic. Nimesikia na kushuhudia baadhi ya wakaazi wa maeneo husika wakifurahia na kuwashukuru watawala kwa uamuzi wa kuwaundia mikoa au wilaya na kuweka makao makuu katika maeneo yao. Nisichokijua kwa uhakika ni je kuna chochote anachokipata mtanzania wa kawaida katika kuundwa wilaya au mkoa mpya ambacho asingekipata katika wilaya na mikoa ya awali?
Je si wazi kwamba fedha nyingi zitakazotumika kuendeleza makao makuu ya mikoa na wilaya mpya, kuwalipa wakuu wake na wasaidizi wao zingeweza kuleta maendeleo muhimu na makubwa katika mikoa iliyokuwapo awali? Tafadhali tutafakari pamoja swala hili. Was this decision that important to our poor country?

Watanzania ni kama tulilogwa kaka. Hakuna faida hata chembe, maana hata ile iliyoanzishwa kabla iko mahututi!
Lakini sie ni mabingwa wa kushangilia kila ujinga wa serikali ya chama cha magamba
 
leo nimeona vx v8 zimeongozana zinatoka toyota workshop na vibao vya rc's tayari kwenda kuumiza wananchi
 
Miaka yote 2najua tuna mikoa 27, kugawa gawa nchi ovyo haipendezi. Jk anahangaika kutafuta ki2 cha yeye kukumbukwa anakosa anaamua? Kugawa nchi, kwa hili ha2tamkumbuka. Tuache historia ibaki kwamba 2na mikoa 21basi. Kila rais akiingia anaanza kutenganisha nchi 2likuwa na maraisi lakini huyu ni JANGA.
 
What do you mean by: 'Mtanzania wa kawaida'? Kuna Watanzania wengine ambao si wa kawaida!
Mtanzania wa kawaida ni simply mtu ambaye amefanana na wengine wengi katika jamii yake. Mimi kwa mfano ni mtanzania wa kawaida kwa maana ya kwamba sina sifa nyingi ambazo hazifanani na za walio wengi katika nchi hii. Rostam Aziz (kwa mfano) hawezi kuwa wa kawaida kwa kuwa sifa na ndoto zake ni tofauti sana na majority ya watanzania. Yeye anaweza kutaka nchi ibadilike na kufuata mwelekeo fulani tofauti na matakwa ya wengi akafanikiwa. Mfano a guy is a President Maker while I can not have a person run for presidency for my gain. We don't have that many king makers around. Ukitaka ufafanuzi zaidi tuwasiliane zaidi.
 
Lengo hasa la kuanzisha mikoa mipya ni pamoja na
1. Ukubwa wa kijiografia wa eneo husika na hivyo kufanya gharama za miundombinu kuwa juu ya uwezo wa bajeti
yetu (kwa kiasi kikubwa ni tegemezi)


2. Utoaji huduma duni kwa wananchi unaotokana na ama sabau ya ukubwa kijiografia au wingi wa watu na hivyo
kufanya utioaji wa huduma kwa wananchi.

Cha maajabu kabisa utekelezaji wake umekuwa ni kinyume kabisa. Wakati kuna kila dalili kuwa mikoa inaanzishwa kwa minajiri ya kutafutiana nafasi, Huduma zinazotolewa katika mikoa mipya hazitofautiani na zile za mikoa iliyoanzishwa zamani. Eeeh Mola tunusuru na haya masahibu.
 
Naomba kusamehewa kwa kushindwa kwangu kulielewa jambo hili mwenyewe na hivyo kuamua kuwashirikisha Greater Thinkers ili kupata logic. Nimesikia na kushuhudia baadhi ya wakaazi wa maeneo husika wakifurahia na kuwashukuru watawala kwa uamuzi wa kuwaundia mikoa au wilaya na kuweka makao makuu katika maeneo yao. Nisichokijua kwa uhakika ni je kuna chochote anachokipata mtanzania wa kawaida katika kuundwa wilaya au mkoa mpya ambacho asingekipata katika wilaya na mikoa ya awali?
Je si wazi kwamba fedha nyingi zitakazotumika kuendeleza makao makuu ya mikoa na wilaya mpya, kuwalipa wakuu wake na wasaidizi wao zingeweza kuleta maendeleo muhimu na makubwa katika mikoa iliyokuwapo awali? Tafadhali tutafakari pamoja swala hili. Was this decision that important to our poor country?

Kwa hilo tutasamehewa wengi. Kama walivyochangia wengine hapo juu ni kweli kugawa mikoa ni ili kutafutia watu posts aidha kwa habari ya wananchi kushangilia kuna makundi mawili kundi la kwanza ni wale beneficiaries wa post hizo directly and indirectly na kundi la pili ni la wajinga waliodanganywa kuwa hiyo ni njia ya kuwapelekea maendeleo wakati ni kuwagawa na kuwatala.
 
Hakuna faida yoyote ni kuogezea wananchi gharama ya uendeshaji,kinachotakiwa ni kujenga na kuiimarisha miundo mbinu,Wakati nchi za magharibi zinapunguza ukubwa wa serikali zao,sisi tunaongeza ukubwa na kuomba omba kwa hao wahisani.Tanzania kiukweli ni nchi ya kuwa na mikoa au majimbo manane tu.Kama imetushinda tuache visingizio.Je ukioa mke na akakuzalia watoto kumi unaigawa kuwa familia mbili?
 
Kupeana ulaji na kuendelea kutumia vibaya resources za nchi. Ukubwa wa kijiografia na utoaji huduma kama mchangiaji 1 hapo juu, nadhani si sahii, kwani tungepata model regions, cities and towns hapa Tanzania ambazo ni small geographically na huduma zake ni superb ningekubali. Lakini hata Dar tu au Bagamoyo licha ya kuwa ndogo bado mipango miji ni kama hakuna, huduma ndo kabisaaa.... wanasingizia msongamano na wing wa watu!!! Dodoma yenyewe na CDA yaleyale, sembuse mikoa mipya?
 
Back
Top Bottom