Mikhail Gorbachev alisaidia USA sasa Donald Trump anaisaidia China

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
713
1,136
Kwa yanayotokea Marekani hasa baada ya Trump kushika uongozi unaweza kabisa kuyalinganisha na yalitokea Russia mwishoni mwa miaka 80 na mwanzoni mwa miaka 90. Inasemekana Marekani ilimwandaa Gorbachev kuwa kibaraka wao kwa Urusi ili Marekani iweze kuishinda Urusi katika mambo yake.

Na kweli baadae Russia ilipitia mabadiliko makubwa ya kijamii, kiuchumi, kisiasa. Hatimaye USSR ikaanguka na kumeguka ikawa vipande vipande na huo ukawa ushindi mkubwa sana kwa USA kwani USSR kabla ya kumeguka ilikuwa tishio kubwa sana kwa Marekani na washirika wake wa Magharibi na NATO.

Sasa kwa kinachoendelea Marekani hasa tukio la jana la wafuasi wa Trump kuvamia bunge wakati likimuidhinisha Joe Biden kuwa rais wa Marekani ni kiashiria kibaya sana katika mstakabali wa Marekani.

Inawezekana sana pengine China walimuandaa Trump kwa muda mrefu ili aje kuivuga Marekani nao waweze ku take over. Kuna uwezekano mkubwa sana mvulugano huo wa Marekani ukawa ndio chanzo cha Dola ya Marekani kuanguka maana inaonekana mpaka katiba yao imeshindwa kutoa majibu ya nini kifanyike kwa wakati huu nchi ikiwa kwenye mtanzio na viongozi wa usalama wakiwa wana resign. Huu unaweza kuwa mwanzo mpya wa China kuwa SUPERPOWER wa ulimwengu.
 
Huyo Trump anatapatapa tu. Akimaliza kuandamanisha watu ajiandae kupelekwa mahakamani.
 
Kwa wamarekani na ujuzi wao wote wa kijasusi kushindwa kuona dalili na kunusa harufu ya ghasia zilizoandaliwa na Donald Trump na washirika wake.

Na kwa kuwa wahuni wengi wa kisiasa ambao ndo wapo nyuma ya Donald Trump walitaka kupindua matokeo ya uchaguzi.

Na kwa kuwa vyombo vyote vya kijasusi na usalama wa Marekani vilikaa pembeni kusoma hali halisi, bas waweza kuwa uko sahihi.

Hii ni "conspiracy at the highest level".
 
Kwa wamarekani na ujuzi wao wote wa kijasusi kushindwa kuona dalili na kunusa harufu ya ghasia zilizoandaliwa na Donald Trump na washirika wake.

Na kwa kuwa wahuni wengi wa kisiasa ambao ndo wapo nyuma ya Donald Trump walitaka kupindua matokeo ya uchaguzi.

Na kwa kuwa vyombo vyote vya kijasusi na usalama wa Marekani vilikaa pembeni kusoma hali halisi, bas waweza kuwa uko sahihi.

Hii ni "conspiracy at the highest level".
It happened on purpose,ukiangalia waandamanani wapo nje ya capital hill for hours,ina maana hakuna spy yeyote aliyegundua mpango wa kuvamia jengo??.They let it happen on purpose kama 9/11.
 
It happened on purpose,ukiangalia waandamanani wapo nje ya capital hill for hours,ina maana hakuna spy yeyote aliyegundua mpango wa kuvamia jengo??.They let it happen on purpose kama 9/11.
Naona hufahamu maana halisi ya conspiracy.

Hii ya hawa wahuni kuvunja utepe wa kwanza wa ulinzi wa jengo la bunge Capitol kuingia ndani na kuwatisha wawakilishi wa wananchi kutaka kubadilisha matokeo kinguvu.

Pia kuingia ofisi ya spika na kupiga picha miguu juu ya meza.

In America?

Really!!
 
Kwa wamarekani na ujuzi wao wote wa kijasusi kushindwa kuona dalili na kunusa harufu ya ghasia zilizoandaliwa na Donald Trump na washirika wake.

Na kwa kuwa wahuni wengi wa kisiasa ambao ndo wapo nyuma ya Donald Trump walitaka kupindua matokeo ya uchaguzi.

Na kwa kuwa vyombo vyote vya kijasusi na usalama wa Marekani vilikaa pembeni kusoma hali halisi, bas waweza kuwa uko sahihi.

Hii ni "conspiracy at the highest level".
Hao ni wahuni tu, ni kazi ya polisi wa kawaida kuwadhibiti.

hayo ya kusema kuna 'conspiracy' ni maneno ya kulikuza hili jambo tu.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom