Mikataba minne ya ujenzi wa barabara ya kuanzia Kabingo kwenda mpakani mwa Kigoma na Burundi (Km260) imesainiwa

winnerian

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
335
530
Imesainiwa mikataba minne na kwa ufupi tu fedha zote zinatokana na waafrica ikiwemo Watanzania maana ni za Bank ya Maendelo ya Africa lakini cha kusikitisha na kushangaza wote waliopewa zabuni hizi ni wakandarasi kutoka china, katika wakandarasi wote wanne wote ni wachina.

Naomba kama mzalendo wa Africa (Tanzania) jiulize maswali haya kisha utafakari na wazalendo wengine kwa ujumla ni wapi hasa tunataka kufika kimaendeleo kama iwapo pesa zetu wenyewe tumeziachia wachina na tumebaki kuwatumikia wao na kisha wanaenda kufanya maendeleo katika taifa lao huko uchina.

1. Je, Serikali yetu (Tanzania) inayo nia ya dhati kabisa ya kuendeleza sekta nyeti kama hizi (ukandarasi na usimamizi ikiwa ni consultants pamoja na wahandis) ambazo ndizo zinazochukua asilimia kubwa na bajeti yetu kila mwaka (kodi zetu)?

2. Kwanini wanasiasa wanashindwa kuonoa umuhimu wa kuwawezesha wakandarasi katika dhamira ya kweli kabisa (practically) ya kuwajengea uwezo kwa kutunga sera (policies) rafiki na wezeshi kwa wazawa kuweza kupata zabuni kubwa zenye bajeti kubwa na kepelekea kubakiza pesa zetu hapa hapa ndani?

3. Kwanini serikali na viongozi wa kisiasa wamekua ndio chanzo cha kuwasifia makandarasi kutoka nje ya nchi kama china huku wakiwasimanga wale wa ndani ambao wana nia ya kukua (sio wote wenye nia ya kukua, wengine ni matapali)?

Jiulize maswali mengi ukiwa unatafakari kwa kukumbuka yafuatayo:
1. Kumbuka kuwa miradi hii minne ina jumla ya Billion takrabani mia sita - Kama zingebaki hapa nchini zingeweza kulipa kodi, vijana wangepata ajira, mzunguko wa pesa ungekuwa mzuri na kikubwa sana tungekuwa wanufaika wa pesa za mkopo wa Bank ya Maendeleo ya Afrika kwasababu zingebaki mikononi mwetu lakini sasa hatutabaki hata na senti moja, zote zitanda china.

2. Kama wangepewa wazawa kwa kuwanunulia mitambo kisha kuwakata katika malipo yao ya kila mwezi (interim certificates) basi wa kufanya hivyo tungeweza kuwa na wakandarasi hodari na wenye uwezo wa kufanya kazi hata kimataifa kama wanavyofanya wachina wenyewe, sababu wangepata ujuzi, uzoefu, mitambo mipya na bora pamoja na fursa ya kukuza uchumi wao na wa nchi kwa ujumla.

3. Kwa kutumia mfano wa hii miradi minne ni dhahiri kwamba serika ina vingozi na wanasiasa wasiokua na maono ya kizazi kijacho kwa sababu moja kubwa, kama serikali ingetunga sera, sheria, kanuni, mikataba n.k zote hizi ziweze kumnufaisha mzawa wa Taifa lako inamaanisha hata wajukuu hawana cha kufaidika katika nchi ya wenyewe hapo baadae na watakuwa watumwa wa china.

4. Serikali yetu (Tanzania) inasomesha watalaamu wengi lakini wakimaliza masomo yao hawana cha kufanya maana zabuni zote kubwa kubwa wanafanya wachina na watu wengine kutoka mataifa ya mbali. Serikali haioni kama inapoteza nafasi ya kuajiri wananchi wake kupitia setka banafsi bali viongoze wetu wamebaki kuwaonea wivu matajiri na kuwanyanyasa wawezavyo huku wakiwamwagia sifa kemkem watu wa nje kuwa wanaweza kuliko wa ndani.

5. Siasa cha uchama na ukanda zimezidi kushamiri, wabunge wamezidi kuwa mbumbumbux1000000, hawana muda wa kutizama sera, sheria pamojoa na kanuni za kuwawezesha wazao badala yake wanaenda bungeni kusemana na kupigana vijembe, uccm, uchadema, ucuf na uact wazalendo ndio ajenda kuu ya Taifa letu.

Natoa rai kubwa kwamba sera na sheria zitungwe kuwawezesha wakandarasi wa ndani na sio kuwanyanyapaa kwamba hawawezi. Zitungwe sheria kalli ikibidi wekeni kipengele cha kunyonga kabisa kwa wale watakaoleta mzahaa katika kukuza uchumi na utaalaamu wa Taifa kwa maslahi wazao wetu wa hapo mbeleni.

Tenda kubwa zipewe wazao kisha serikali iwanunulie mitambo na iwakate kidogo kidogo katika malipo ya miradi itakayotoa.

Wasanifu na wasimamizi watoke hapa hapa ndani. Kwa sasa tunao wahandisi wa kutosha kufanya kazi kubwa na nzuri, hatupo tena miaka ya uhuru 1961 huko n.k n.k.

Ni mimi mzalendo mwenzenu. Tusibaki tu kwenye CCM na CHADEMA kunayo mambo mengine ya kuyaangazia macho yetu.
 
Mkuu umeongea vyema. Hayo makampuni ya china ni state owned companies na zinakuwa subsided na serikali yao.

Nasi tunaweza fanya kitu kama hicho ili in a long run tuwe tunabakiza pesa za mikopo kama hizo.
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,faw,sany,shackman,xcmg, shantui,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
 
Mkuu umeongea vyema. Hayo makampuni ya china ni state owned companies na zinakuwa subsided na serikali yao.
Nasi tunaweza fanya kitu kama hicho ili in a long run tuwe tunabakiza pesa za mikopo kama hizo.
Tukiamua tunaweza kuwa kama Marekani. Lakini ni pale tu ambapo wabunge watatambua majukumu yao na viongozi pamoja wanasiasa kwa ujumla wawe na nia dhahiri shahiri ya kulileta taifa pamoja na kuhimiza uzalendo kwanza vitendo pamoja na upendo.

Tuombe Mungu kizazi kijacho kiwe chenye kujielewa na upendo wa dhati kwa taifa lao (Tanzania) kitu ambacho nakiona maana kwakweli bila hivyo tutakua watumwa wa mataifa yalioendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao.
Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank).
Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa.
Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.
Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10. Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.



Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama? Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
Mzalendo na mwana maendeleo umenena mazuri yote lakini kama serikali yetu ikiweza kufungulia uwezo wa wananchi wake basi uelewe kwamba haitashindwa. Kama imeweza kuzuia mikutano ya wapinzani nchi nzima pia inaweza kuweka adabu pamoja na sera nzuri za kuifanya nchi isonge mbele kimaendeleo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumewapa nyanza road kipande cha kutoka nyakanazi mpaka kibondo km 90 tu mwaka wa 5 sasa hakijaisha na hakijulikani lini kitaisha

unategemea hawa wa nyumbani waendelee kupewa mikataba

Wenzetu wako kikazi zaidi kazi iishe apate ingine
 
Achanan nao uthieaamini sana, barabara ya Njombe wamesimamaaa hawanaga pesa, kule bariadi majangaaa hakuna ujenzi unaendleaaa na kwomingene kwingi

Don't make a promise you can't fulfill...
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao.
Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank).
Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa.
Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.
Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10. Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.



Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama? Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
Mungu akubariki sana kwa majibu mazuri ya kitaalamu.

Humu JF vijana wa Membe na ufipa + zitto wanavurugana usiku na mchana.
Imepelekea hata hadhi ya JF kuporomoka kwa kasi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu akubariki sana kwa majibu mazuri ya kitaalamu.

Humu JF vijana wa Membe na ufipa + zitto wanavurugana usiku na mchana.
Imepelekea hata hadhi ya JF kuporomoka kwa kasi.



Sent using Jamii Forums mobile app
Kama hatutafika mahali tuangalie tatizo lilipo kisha tulichimbe na kulitupa kwenye tanuru la moto basi tutabakia kuwa vibarua wa china na nchi nyingine zilizoendelea. Nakuambia wazi kuitana wezi wabinafsi pamoja na malofa haitusaidi sanaa inakunza chuki na ubinafsi sisi kwa sisi. Tunaweza kabisa kutunga sheria kali na taratibu nzuri za kujisimamia na tukafaidika na uchumi wa nchi yetu. Sawa makandarasi wa ndani wameonyesha kuwa na uwezo mdogo lakini je serikali na wahusika kwa ujumla ndio sababu kubwa ya kuwapuuza na kuwatelekeza? Fikiria upya tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
Mswahili ni mwizi sana :rolleyes::rolleyes::rolleyes:.

Kwa kweli tunafeli sana katika mambo mengi kwa sababu level ya integrity tuliyo nayo wengi ni 0%.
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.

Kuna watu wanafikiria hawapewi kwa sababu ya rangi Mkuu
Kumbe uhalisia ndio huu ila hatuukubali
Wizi na Rushwa sijui kama itakuja kwisha
Na tutabaki maskini mpaka tujitathmini


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.

Inawezekana hizo mashine zikawa owned na local banks, uliyoyasema yote yana majibu, shida hapa kuna ubinafsi ambao ni kama kawaida yetu waswahili. Ila mleta mada amesema kitu ambacho kitafanyiwa kazi in near future sababu kina mantiki.
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
Mwanzisha mada kaongea vizuri sana. Lakini wewe umekomelea ukweli ulivyo. Kwa maana mwanzisha mada kaongea siasa. Wewe umeongea practical.
Nitakupa mfano rahisi. Kisena ni mmiliki wa UDART lakini anajiibia mafuta aliyoagiza mwenyewe yaje kwenye depo yake. Ndio maana yuko ndani.
Contractor Mtz akipewa down payment ya mobilization anaenda kunununa landcruizer. Njaa tupu na uaminifu 0%.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.

Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.

Pia hizi sinotruck,sany,shackman,sany,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.

Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?

Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.

Samahani kwa comment ndefu.
Heko!.... Maelezo yako kuntu yamefunika kabisa hoja hii ya kutetea kandarasi wazawa kwenye miradi mikubwa ya miundombinu ya kimkakati kama huu wa barabara ya Nyakanazi-Kibondo-Kasulu-Manyovu.

Kipande cha Nyakanazi-Kabingo kina kilometa 50, kapewa mzawa- Nyanza Construction Works huu ni mwaka wa nne sasa, kipande kilichojengwa lami ni kifupi sana hata daraja kubwa kwenye mto Moyowosi bado halijajengwa!. Vifaa vilivyoko kwenye eneo la kazi ni vichache na duni sana.... Hawana uwezo wale.
 
serikali inanunua vifaa inakodisha kwa kandarasi zijenge barabara zetu tunakatana kwenye charges na kodi .
nchi yetu barabara nyingi hazijajengwa hasa huku mikoani
 
Imesainiwa mikataba minne na kwa ufupi tu fedha zote zinatokana na waafrica ikiwemo Watanzania maana ni za Bank ya Maendelo ya Africa lakini cha kusikitisha na kushangaza wote waliopewa zabuni hizi ni wakandarasi kutoka china, katika wakandarasi wote wanne wote ni wachina.

Naomba kama mzalendo wa Africa (Tanzania) jiulize maswali haya kisha utafakari na wazalendo wengine kwa ujumla ni wapi hasa tunataka kufika kimaendeleo kama iwapo pesa zetu wenyewe tumeziachia wachina na tumebaki kuwatumikia wao na kisha wanaenda kufanya maendeleo katika taifa lao huko uchina.

1. Je, Serikali yetu (Tanzania) inayo nia ya dhati kabisa ya kuendeleza sekta nyeti kama hizi (ukandarasi na usimamizi ikiwa ni consultants pamoja na wahandis) ambazo ndizo zinazochukua asilimia kubwa na bajeti yetu kila mwaka (kodi zetu)?

2. Kwanini wanasiasa wanashindwa kuonoa umuhimu wa kuwawezesha wakandarasi katika dhamira ya kweli kabisa (practically) ya kuwajengea uwezo kwa kutunga sera (policies) rafiki na wezeshi kwa wazawa kuweza kupata zabuni kubwa zenye bajeti kubwa na kepelekea kubakiza pesa zetu hapa hapa ndani?

3. Kwanini serikali na viongozi wa kisiasa wamekua ndio chanzo cha kuwasifia makandarasi kutoka nje ya nchi kama china huku wakiwasimanga wale wa ndani ambao wana nia ya kukua (sio wote wenye nia ya kukua, wengine ni matapali)?

Jiulize maswali mengi ukiwa unatafakari kwa kukumbuka yafuatayo:
1. Kumbuka kuwa miradi hii minne ina jumla ya Billion takrabani mia sita - Kama zingebaki hapa nchini zingeweza kulipa kodi, vijana wangepata ajira, mzunguko wa pesa ungekuwa mzuri na kikubwa sana tungekuwa wanufaika wa pesa za mkopo wa Bank ya Maendeleo ya Afrika kwasababu zingebaki mikononi mwetu lakini sasa hatutabaki hata na senti moja, zote zitanda china.

2. Kama wangepewa wazawa kwa kuwanunulia mitambo kisha kuwakata katika malipo yao ya kila mwezi (interim certificates) basi wa kufanya hivyo tungeweza kuwa na wakandarasi hodari na wenye uwezo wa kufanya kazi hata kimataifa kama wanavyofanya wachina wenyewe, sababu wangepata ujuzi, uzoefu, mitambo mipya na bora pamoja na fursa ya kukuza uchumi wao na wa nchi kwa ujumla.

3. Kwa kutumia mfano wa hii miradi minne ni dhahiri kwamba serika ina vingozi na wanasiasa wasiokua na maono ya kizazi kijacho kwa sababu moja kubwa, kama serikali ingetunga sera, sheria, kanuni, mikataba n.k zote hizi ziweze kumnufaisha mzawa wa Taifa lako inamaanisha hata wajukuu hawana cha kufaidika katika nchi ya wenyewe hapo baadae na watakuwa watumwa wa china.

4. Serikali yetu (Tanzania) inasomesha watalaamu wengi lakini wakimaliza masomo yao hawana cha kufanya maana zabuni zote kubwa kubwa wanafanya wachina na watu wengine kutoka mataifa ya mbali. Serikali haioni kama inapoteza nafasi ya kuajiri wananchi wake kupitia setka banafsi bali viongoze wetu wamebaki kuwaonea wivu matajiri na kuwanyanyasa wawezavyo huku wakiwamwagia sifa kemkem watu wa nje kuwa wanaweza kuliko wa ndani.

5. Siasa cha uchama na ukanda zimezidi kushamiri, wabunge wamezidi kuwa mbumbumbux1000000, hawana muda wa kutizama sera, sheria pamojoa na kanuni za kuwawezesha wazao badala yake wanaenda bungeni kusemana na kupigana vijembe, uccm, uchadema, ucuf na uact wazalendo ndio ajenda kuu ya Taifa letu.

Natoa rai kubwa kwamba sera na sheria zitungwe kuwawezesha wakandarasi wa ndani na sio kuwanyanyapaa kwamba hawawezi. Zitungwe sheria kalli ikibidi wekeni kipengele cha kunyonga kabisa kwa wale watakaoleta mzahaa katika kukuza uchumi na utaalaamu wa Taifa kwa maslahi wazao wetu wa hapo mbeleni.

Tenda kubwa zipewe wazao kisha serikali iwanunulie mitambo na iwakate kidogo kidogo katika malipo ya miradi itakayotoa.

Wasanifu na wasimamizi watoke hapa hapa ndani. Kwa sasa tunao wahandisi wa kutosha kufanya kazi kubwa na nzuri, hatupo tena miaka ya uhuru 1961 huko n.k n.k.

Ni mimi mzalendo mwenzenu. Tusibaki tu kwenye CCM na CHADEMA kunayo mambo mengine ya kuyaangazia macho yetu.

Kichekesho ni pale wanasiasa hao hao wanaposema tujitawale wenyewe kwa mantiki ya kulinda maslahi yao, lakini mikataba yote yenye hela wanawapa hao hao mabepari!
 
serikali inanunua vifaa inakodisha kwa kandarasi zijenge barabara zetu tunakatana kwenye charges na kodi .
nchi yetu barabara nyingi hazijajengwa hasa huku mikoani
Wazo zuri sana.
Serikali itenge kama 20B ya mitambo na spare, ila vifaa wapewe jeshi kama Sumajkt au katika kambi zao kulingana na kanda. Kisha jeshi liwachukue watu waliofanya kazi kwenye kampuni za kichina wenye uzoefu waingie ili kuendesha mitambo hiyo wakiwa chini ya usimamizi wa jeshi pia wanajeshi wapate ujuzi.Wakiwapa raia wa kawaida wanaweza kuiba mitambo kabisa au kung'oa vifaa ndani ya mitambo na kuuza. Usisahau mswahili ni mwizi sana.
Kisha Sumajkt wahakikishe wanafikisha ubora na wanakuwa wanaweza kuomba tenda za kimataifa za benki ya dunia, AFDB na mashirika mengine ya kimataifa. Kisha wapige miradi ya Tanzania halafu wakishapata uzoefu na kuongeza vifaa, wafanye miradi nchi zote za afrika mashariki na SADC.
(Ila wafanye manunuzi ya mitambo kimya kimya au watumie mbinu za kimafia, maana mchina hawezi akaruhusu kuandaa mazingira ya kukosa kazi mbeleni 😁)
 
Acheni utani Hawa nyanza road barabara ya km nne wanagalagala nayo miaka mitatu ije 260km?
 
serikali inanunua vifaa inakodisha kwa kandarasi zijenge barabara zetu tunakatana kwenye charges na kodi .
nchi yetu barabara nyingi hazijajengwa hasa huku mikoani
Nakwambia watatumia miaka miwili watauza Kama chuma chakavu, sido walijaribu kukopesha mashine za kazi walifikia wapi, wacha tu wachina waje, sie tutafanya kazi za ulinzi na kuchimba mtaro
 
Back
Top Bottom