Miji mikubwa duniani kote ndiyo huwa kitovu cha elimu lakini kwa Dar mbona tofauti sana?

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Nilikuws nasoma stori moja kuhusu Shanghai, Shanghai ni moja ya miji yenye watu wenye elimu ya kieango cha juu sana. Watoto wa shule za msingi walivyopimwa uwezo wa hesabu na sayansi walikuww ni moja ya wanafunzi bora duniani.

Watu kotoka miji ya ndani ya China walikuwa wwnatamani watoto wao wakasome Shanghai. Ilifika kipindi mamlaka za mji zikaweka sheria za watu wasio wa Shanghai kutosoma hapo maana shule zilikuwa zinazidiwa.
Kwa Dar ni tofauti sana, kihistoria watu walikuwa wanatoka Dar na kwenda kusoma mikoani. Dar ina shule shule chache sana. Fikiria Dar yenye wakazi zaidi ya 6m ina shule za sekondari zenye class size ya 40+ kama 240. Kilimanjaro yenye watu 2m na kidogo ina Shule kama hizo 275!. Ili Dar walau iwe na standard za kilimanjaro ilitakiwa kuwa na kama shule 800 hivi.
Kihistoria Dar huwa haifanyi vizuri kwenye matokeo ya shule za msingi, wala sekondari. Ukiachana na elimu ya chuo kikuu, huwezi kumsikia mtu wa mkoani eti anaenda Dar kufuata elimu bora. Kwanini huu mji upo tofauti na miji mingine mikubwa duniani? Wafanye nini ili walau wafikie Standard za Kilimanjaro?.
 
Kwahiyo dar haifanyi vizuri?

Hivi Feza kitovu kikuu Tanzania si kiko Dar?


Au hujaisikia hii shule?
 
Mtupumzishe watu wa dar!! Jua Lituandame....Jotooo!!!!!

Bado Na Nyie Mtuache kidogo asee
 
Dar, watu wanawaza vumbi la Congo, ukija huku Mundende mara kuridhushana nk. Elimu haina nafasi Bongo....
 
Mji wa waswahili; kila mtu ni mswahili.

Mwalimu mswahili
Mwanafumzi mswahili
Mama mswahili
Baba mswahili
Mtoto mswahili
Kaka mswahili
Dada mswahili
Mjomba mswahili
Shangazi mswahili
Bibi mswahili
Babu mswahili
Mchungaji mswahili
Mbunge mswahili
Jirani mswahili
Viongozi waswahili
Mpangaji mswahili
Konda mswahili
Dereva mswahili
Muuza chips mswahili
Muuza genge mswahili

Hiyo ndio sababu; kila mmoja kwenye hiyo list ana nafasi muhimu ya kuathiri matokeo Dar.
 
Mipango miji na sera ni tatizo...shule nyungi zipo.uswahilini maana shule ina ukubwa wa ekari 1 au 2. Pembeni ya shule kuna
Garage
Soko
Kituo cha bodaboda
Stand ya daladala
Barabara yenye kelele
Makazi ya watu kiasi kelele za mtaani kusikika hadi darasani
Hakuna mazingira tulivu kujisomea
 
Mipango miji na sera ni tatizo...shule nyungi zipo.uswahilini maana shule ina ukubwa wa ekari 1 au 2. Pembeni ya shule kuna
Garage
Soko
Kituo cha bodaboda
Stand ya daladala
Barabara yenye kelele
Makazi ya watu kiasi kelele za mtaani kusikika hadi darasani
Hakuna mazingira tulivu kujisomea
 
Back
Top Bottom