Mijadala ya Bajeti Bungeni iko Live, Kumekucha kimya kimya?

Mabibi na mabwana ITV wanaonekana live bungeni na mijadala ya bajeti inaendelea. Mambo sasa mwendo mdundo!

Kulikoni?

Itakuwa yale mambo yetu ya bunge live yamerejeshwa kimya kimya au ni kwa bajeti hii ya Mwigulu peke yake?

Je, au ndiyo rasmi kuwa yale ya watu kufanya kazi badala ya kuangalia mambo ya bunge sasa ndiyo basi?

Au je, pengine mabadiliko haya ni kwa sababu waliokuwa wanatuchelewesha kimaendeleo hawapo tena bungeni?

Au labda ni katika yale ya moto moto yajayo ya awamu ya sita ya mama Samia Suluhu rais wetu wa JMT kazi inapoendelea?

Si kuwa ilikuwa vyema ikajulikana kama huu ndiyo ulio msimamo mpya na kwa uwazi?

Ninawasilisha.
Aulizwe Nape mhuni alituharibia nchi sana nae akawekwa kando.
 
Mwendakuzimu akisikia huko kuzimu anaweza akafa tena Mara ya pili.

Pamoja na mapungufu yote, mdogo mdogo mama anaturejesha mstarini.

Mama atakapogonga kwenye katiba mpya kwa dhati, atakuwa kamaliza kila kitu. Mitano tena ya haki itamhusu!

Yule bwana alikuwa ametuchelewesha sana!
 
Aliyezuia bunge live kuwa watu wafanye kazi

Ndio huyo huyo aliyekua akiwapangisha watu foleni kwa hata masaa 3 wakimsubiri apite huku shughuli zao za kiuzalishaji zikikwama...
 
Kama wameamua kuwa live iwe kwa mujibu wa sheria, isiwe kwa matakwa ya watu wachache... maana huko mbele tukifanikiwa kumpata shujas mwingine ataliondoa tu na kutuchanganya.

Mwanzo mwema. Ni kweli isiwe kwa kudra za mtu bali kwa mujibu wa sheria.

Aibu kwao Mwape, Jobo nawe uliyetundika daruga ukutani pale Geita.
 
Aliyezuia bunge live kuwa watu wafanye kazi

Ndio huyo huyo aliyekua akiwapangisha watu foleni kwa hata masaa 3 wakimsubiri apite huku shughuli zao za kiuzalishaji zikikwama...

Yule bwana alipaswa kuiona Tanzania mpya.

Mama akaze uzi hapo hapo. Anakwenda vyema. Akapate ujasiri wa katiba mpya mapema iwezekanavyo.
 
Mwanzo mwema. Ni kweli isiwe kwa kudra za mtu bali kwa mujibu wa sheria.

Aibu kwao Mwape, Jobo nawe uliyetundika daruga ukutani pale Geita.
Mwanzo ni mzuri ila mtihani wa mwisho itakuwa ni jinsi atakavyohakikisha yale anayopatia hayavurugwi kirahisi na atayemfuatia
20210616_190556.jpg
 
Mwanzo ni mzuri ila mtihani wa mwisho itakuwa ni jinsi atakavyohakikisha yale anayopatia hayavurugwi kirahisi na atayemfuatiaView attachment 1820788

Uzuri ni kuwa anayo nia njema. Katamka mwenyewe - haki huinua taifa.

Hakumung'unya maneno dhidi ya watuhumiwa wazaliwa wa miaka ya '80.

Penye nia pana njia!
 
Yule bwana alipaswa kuiona Tanzania mpya.

Mama akaze uzi hapo hapo. Anakwenda vyema. Akapate ujasiri wa katiba mpya mapema iwezekanavyo.
Dikteta uchwara alitia mihimili yote 3 mfukoni na kumjibu Paschal Mayalla kuwa kuna mhimili umejichimbia chini chini kabisa..Jiwe alimfamya hadi Paschal akaunga juhudi za maendeleo uchwara na kina Masanja
 
Dikteta uchwara alitia mihimili yote 3 mfukoni na kumjibu Paschal Mayalla kuwa kuna mhimili umejichimbia chini chini kabisa..Jiwe alimfamya hadi Paschal akaunga juhudi za maendeleo uchwara na kina Masanja

Uzuri ni kuwa hata kina paschal wanajua vuguvugu la kuhifadhi mabadiliko halimtegemei mtu na Aluta Continua!
 
njaa mbaya sana mnalalamika nini sasa kwani hata mlipokuwepo bungeni mlifanya nini zaidi yakuwa mnajitahidi kupinga kila kitu sasa ndiyo wanaume wapo kazini sasa kuipangia nchi mambo mema

Mvuto hamna, hivyo hata mkilazimisha kuonekana watu hawawafagilii kihivyo. Kama mlikuwa hamtekelezi wasemayo wapinzani hatuna tatizo, ila walitimiza wajibu wao kwa usahihi.
 
Back
Top Bottom