Aulizwe Nape mhuni alituharibia nchi sana nae akawekwa kando.Mabibi na mabwana ITV wanaonekana live bungeni na mijadala ya bajeti inaendelea. Mambo sasa mwendo mdundo!
Kulikoni?
Itakuwa yale mambo yetu ya bunge live yamerejeshwa kimya kimya au ni kwa bajeti hii ya Mwigulu peke yake?
Je, au ndiyo rasmi kuwa yale ya watu kufanya kazi badala ya kuangalia mambo ya bunge sasa ndiyo basi?
Au je, pengine mabadiliko haya ni kwa sababu waliokuwa wanatuchelewesha kimaendeleo hawapo tena bungeni?
Au labda ni katika yale ya moto moto yajayo ya awamu ya sita ya mama Samia Suluhu rais wetu wa JMT kazi inapoendelea?
Si kuwa ilikuwa vyema ikajulikana kama huu ndiyo ulio msimamo mpya na kwa uwazi?
Ninawasilisha.
Mwendakuzimu akisikia huko kuzimu anaweza akafa tena Mara ya pili.
Kama wameamua kuwa live iwe kwa mujibu wa sheria, isiwe kwa matakwa ya watu wachache... maana huko mbele tukifanikiwa kumpata shujas mwingine ataliondoa tu na kutuchanganya.
Aliyezuia bunge live kuwa watu wafanye kazi
Ndio huyo huyo aliyekua akiwapangisha watu foleni kwa hata masaa 3 wakimsubiri apite huku shughuli zao za kiuzalishaji zikikwama...
Mwanzo ni mzuri ila mtihani wa mwisho itakuwa ni jinsi atakavyohakikisha yale anayopatia hayavurugwi kirahisi na atayemfuatiaMwanzo mwema. Ni kweli isiwe kwa kudra za mtu bali kwa mujibu wa sheria.
Aibu kwao Mwape, Jobo nawe uliyetundika daruga ukutani pale Geita.
Mwanzo ni mzuri ila mtihani wa mwisho itakuwa ni jinsi atakavyohakikisha yale anayopatia hayavurugwi kirahisi na atayemfuatiaView attachment 1820788
Dikteta uchwara alitia mihimili yote 3 mfukoni na kumjibu Paschal Mayalla kuwa kuna mhimili umejichimbia chini chini kabisa..Jiwe alimfamya hadi Paschal akaunga juhudi za maendeleo uchwara na kina MasanjaYule bwana alipaswa kuiona Tanzania mpya.
Mama akaze uzi hapo hapo. Anakwenda vyema. Akapate ujasiri wa katiba mpya mapema iwezekanavyo.
Dikteta uchwara alitia mihimili yote 3 mfukoni na kumjibu Paschal Mayalla kuwa kuna mhimili umejichimbia chini chini kabisa..Jiwe alimfamya hadi Paschal akaunga juhudi za maendeleo uchwara na kina Masanja
njaa mbaya sana mnalalamika nini sasa kwani hata mlipokuwepo bungeni mlifanya nini zaidi yakuwa mnajitahidi kupinga kila kitu sasa ndiyo wanaume wapo kazini sasa kuipangia nchi mambo mema