MIGONGANO YA KIFIKRA: Kujinyonga - "Ajinyonga Kwa Udanganyifu Katika Mitihani "

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
WanaJF, sijui mnazichukuliaje hizi habari za mwanafunzi kujinyonga? Hisia zangu kwa kweli baada ya kusoma tu hii habari zilikuwa za masikitiko, na ni maombi yangu Mwenyezi Mungu Amlaze Pahala Pema Peponi. Lakini pia hisia nyingine zilizo nijia moja kwa moja ni zile za viongozi wabadhirifu na mafisadi na uwajibikaji wao.

Naomba usome kwanza hii habari hapa chini:

Mwanafunzi ajinyonga kwa udanganyifu katika mitihani

Makubo Haruni, Musoma

HabariLeo; Friday,October 12, 2007 @00:02

MWANAFUNZI wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Magoto iliyopo wilayani Tarime Mkoa wa Mara, Joseph James (21) amejinyonga baada ya kukutwa na majibu ya mtihani wa kumaliza kidato cha nne.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, David Saibullu alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa tisa mchana ndani ya chumba alichokuwa amepanga mwanafunzi huyo. Alisema mwanafunzi huyo alijinyonga kwa tai yake baada ya kutolewa nje ya chumba cha mtihani na msimamizi, Joseph Menyei baada ya kukutwa na majibu ya mtihani.

Kamanda Saibullu alieleza kuwa mwanafunzi huyo alijiua baada ya kukamatwa na majibu ya somo la Baolojia na kutolewa ndani ya chumba cha mtihani, kitendo ambacho kilionekana kumkera na kuamua kwenda nyumbani alikokuwa amepanga katika Kijiji cha Magoto. Alisema James ambaye nyumbani kwao ni katika Kijiji cha Nyamwaga, kabla ya kujiua, aliacha ujumbe kuwa amefanya uamuzi huo kuondoa aibu katika jamii sambamba na kujivunjia heshima kwa kukamatwa na majibu hayo ya mtihani.

Wiki iliyopita, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta aliwaonya wanafunzi wa kidato cha nne walioanza kufanya mtihani Oktoba 8 mwaka huu, kuacha udanganyifu na kuwa waaminifu wakati wakifanya mtihani.

Pia aliwaonya wasimamizi kuacha udanganyifu kwa kujiepusha na vitendo vya rushwa na kwamba atakayekiuka atachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria. Kwa mujibu wa Waziri Sitta, watahiniwa wanaoendelea kufanya mitihani yao nchi nzima ni 127,988 na kati ya hao, wavulana ni 71,012 na wasichana ni 56,979, miongoni mwa wanafunzi 199,274 waliosajiliwa kidato cha kwanza miaka minne iliyopita.
Source: HabariLEO.

Sasa ndugu zangu lile ambalo ningependa kuuliza ni kuwa;
--Je, huyu kijana amekufa kishujaa au kinyonge?!

--Je, kujinyonga baada ya kughafirika ki aibu ni kitu cha kutetea?!

--Je, kijana huyu alivyofanya ni sawa na kujitoa mhanga?!

Pia kuna habari kama ifuatayo:
Japanese minister kills himself Japan's Agriculture

Minister Toshikatsu Matsuoka has died in hospital after apparently committing suicide.
_42977987_ap_japan203.jpg


The 62-year-old was found hanged in his Tokyo apartment hours before he was to face questions in parliament over his links to a political funding scandal. Opposition MPs had been calling for his resignation over unexplained expenses.

PM Shinzo Abe expressed regret over the news saying he was conscious of his "responsibility as prime minister, and as the one who appointed him".

"The effects on the cabinet will be great," Mr Abe added as he went to attend a wake for the deceased minister late on Monday.
Mr Matsuoka was found unconscious in his flat around lunchtime on Monday. Efforts to resuscitate him at hospital failed.
Police said he had hanged himself, but refused to comment on reports in the Japanese press that he had left a number of suicide notes in his apartment.

It is the first time a Japanese cabinet minister has killed himself since World War II, when the army minister committed suicide on news of Japan's surrender.


Habari zaidi HAPA, BBC.
Pia kuna hii ya CEO Uchina:
Chinese toy boss 'kills himself'

The boss of a Chinese toy firm involved in a huge safety recall has committed suicide, Chinese media has said. Zhang Shuhong, who co-owned the Lee Der Toy Company, was reportedly found dead at his factory in southern China.

About 1.5 million toys made for Fisher Price, a subsidiary of US giant Mattel, were withdrawn from sale earlier this month. Many were made by Lee Der. The recalled toys include characters from Sesame Street's Big Bird and Elmo, and Nickelodeon's Dora the Explorer.

Zhang killed himself on Saturday, according to the Southern Metropolitan Daily and other news sources. He reportedly hanged himself in his factory. "When I rushed there around 5pm, police had already sealed off the area," the newspaper quoted a manager at the firm as saying. "I saw that our boss had two deep marks in his neck."

The news report did not give a reason for Zhang's apparent suicide, but Lee Der was known to be under pressure after the huge product recall. Fisher Price announced on 2 August that it was recalling some of Lee Der's Chinese-made toys, in a move affecting 83 product-types sold around the world, including the US and the UK.

An internal investigation found the toys had been made using a non-approved paint pigment which contained excessive amounts of lead, violating safety standards. A manager at Lee Der blamed its paint supplier for the incident, according to the Southern Metropolitan Daily.

Chinese-made products have come under increasing international scrutiny in recent months, after a series of safety scandals.
A substance found in pet food made in China caused the death of a number of animals in the United States, and toxic ingredients were also found in Chinese-made toothpaste.


Source: BBC.

Pamoja na kuwa hata huko kwenye nchi zenye corporate responsibility ya hali ya juu kabisa matukio haya kuwa nadra, siishi kujiuliza: Is there a way out?!

I don't understand how commiting suicide can rectify a situation, but again, you cannot really fit yourself in the shoes of a desperate and guilty person. Anyhow, to me, commiting suicide may seem to be the honourable way out by many, but it does not fix the situation that is left behind.

Kwa sisi walalahoi, is this a means of escaping one's individual misery and wretched life or a way of rejecting completely the miserable and wretched social conditions and society one lives in?!

Lakini kuna lile la kujitoa mhanga kama linavyotokea Mashariki ya Kati kila mara; is suicide a way of saving face, gaining honour and redemption for oneself and one's family and associates?!

But even troubling, je baadhi ya wanasiasa wetu wengi wanaotajwa na wengi wanaojijua kuwa wameshiriki katika matendo ya kiuhujumu uchumi wafuate mfano wa huyo kijana huko Msoma kwa aibu wanazo zipatia familia zao na jamii zao kiujumla?!

SteveD.
 
SteveD

Naona viongozi wetu wengi bongo wanashangaa haya kwa sasa lakini yanakuja Tanzania kwa kasi kama umeme.
 
Kwa sisi walalahoi, is this a means of escaping one's individual misery and wretched life or a way of rejecting completely the miserable and wretched social conditions and society one lives in?!

Huu mgongano ni mgumu kuutolea maamuzi! Lakini hebu tuchambue hoja ya kujinyonga hatua kwa hatua. Mimi naanza hivi:-
Ni kweli kuwa huwezi kuwa katika mawazo ya yule anayejinyonga, kwamba anajisikiaje, hasa kujua kama anawajibika kwa kitendo chake ama kama anakwepa wajibu. Lakini mimi nadhani kuwa kujinyonga ni sehemu ya kukwepa kuwajibika kwa yale uliyotenda, ingawa ni ukatili na wala nisingependa mtu ajinyonge. Kwa mantiki hii, mimi nadhani kuwa kama mtu anajitoa uhai wake mwenyewe, atashindwaje kutoa uhai wa mwingine? (kumwajibisha). Mitazamo ya jamii na vyombo vya haki kama mahakama kuhusu wakosefu huweza kumsababishia mtu ajinyonge (humwajibisha kisaikolojia). Kwa mfano, mtu kama alibaka na akakamatwa na anajua kuwa kuna ushahidi wa kumtia hatiani, anaweza kujinyonga kwa kuogopa kwenda kukaa jela kwa maisha yake yote yatakayosalia hapa duniani baada ya hukumu, kwa hiyo kama anafahamu ama kasikia kuhusu mateso ya jela hatakuwa tayari kwena kuteseka. Mtuhumiwa huyu huyu wa ubakaji naweza pia kujinyonga kwa kuogopa aibu ya kuzomewa katika jamii kwa kitendo chake cha kinyama. Je anakwepa wajibu ama anawajibika?
Mtu X anatokea na kumpiga mwenzake Y, huyu mwenzake anazirai! Kwa kutojua, jamaa X aliyempiga mwenzie Y anajinyonga, kwa kuhisi kaua, kwa hiyo nae huenda akahukumiwa kunyongwa! Huyu anawajibika ama anakwepa wajibu?
Hali kadhalika, tumeshasikia mara kadhaa waathirika wa ukimwi wakijinyonga, ama kwa kuogopa unyanyapaa ama kwa kuogopa mateso yatokanayo na ukimwi. Wanakwepa wajibu ama wanawajika?
Tunafahamu kuwa kwa nchi kama China, kosa la rushwa hupelekea mtu kunyongwa kama atakutwa na hatia. Sasa hapa mtu anakwepa wajibu ama anawajibika?
Hata hivyo, wataalamu wa saikolojia wanasema kwamba, mtu anapokabiliwa na matatizo makubwa, uwezo wa kufikiri hupungua sana, na mara nyingi anakimbilia njia za mkato, ambazo hata hivyo hazitoi utatuzi wa kudumu wa shida za mhusika. Mnasemaje?
Naomba tuendelee kulumbana kuhusu kujinyonga.
 
SteveD

Naona viongozi wetu wengi bongo wanashangaa haya kwa sasa lakini yanakuja Tanzania kwa kasi kama umeme.

Dua ahsante, lakini je, yanakuja kwa kasi kutokana na ugumu wa maisha au uwajibikaji (kukua umetenda kosa hivyo kujinyonga)?!

SteveD.
 
Huu mgongano ni mgumu kuutolea maamuzi! Lakini hebu tuchambue hoja ya kujinyonga hatua kwa hatua. Mimi naanza hivi:-
Ni kweli kuwa huwezi kuwa katika mawazo ya yule anayejinyonga, kwamba anajisikiaje, hasa kujua kama anawajibika kwa kitendo chake ama kama anakwepa wajibu. Lakini mimi nadhani kuwa kujinyonga ni sehemu ya kukwepa kuwajibika kwa yale uliyotenda, ingawa ni ukatili na wala nisingependa mtu ajinyonge. Kwa mantiki hii, mimi nadhani kuwa kama mtu anajitoa uhai wake mwenyewe, atashindwaje kutoa uhai wa mwingine? (kumwajibisha). Mitazamo ya jamii na vyombo vya haki kama mahakama kuhusu wakosefu huweza kumsababishia mtu ajinyonge (humwajibisha kisaikolojia). Kwa mfano, mtu kama alibaka na akakamatwa na anajua kuwa kuna ushahidi wa kumtia hatiani, anaweza kujinyonga kwa kuogopa kwenda kukaa jela kwa maisha yake yote yatakayosalia hapa duniani baada ya hukumu, kwa hiyo kama anafahamu ama kasikia kuhusu mateso ya jela hatakuwa tayari kwena kuteseka. Mtuhumiwa huyu huyu wa ubakaji naweza pia kujinyonga kwa kuogopa aibu ya kuzomewa katika jamii kwa kitendo chake cha kinyama. Je anakwepa wajibu ama anawajibika?
Mtu X anatokea na kumpiga mwenzake Y, huyu mwenzake anazirai! Kwa kutojua, jamaa X aliyempiga mwenzie Y anajinyonga, kwa kuhisi kaua, kwa hiyo nae huenda akahukumiwa kunyongwa! Huyu anawajibika ama anakwepa wajibu?
Hali kadhalika, tumeshasikia mara kadhaa waathirika wa ukimwi wakijinyonga, ama kwa kuogopa unyanyapaa ama kwa kuogopa mateso yatokanayo na ukimwi. Wanakwepa wajibu ama wanawajika?

Tunafahamu kuwa kwa nchi kama China, kosa la rushwa hupelekea mtu kunyongwa kama atakutwa na hatia. Sasa hapa mtu anakwepa wajibu ama anawajibika?

Hata hivyo, wataalamu wa saikolojia wanasema kwamba, mtu anapokabiliwa na matatizo makubwa, uwezo wa kufikiri hupungua sana, na mara nyingi anakimbilia njia za mkato, ambazo hata hivyo hazitoi utatuzi wa kudumu wa shida za mhusika. Mnasemaje?
Naomba tuendelee kulumbana kuhusu kujinyonga.

Mtupori, ahsante kwa maelezo yako, lakini hilo swali lako juu naona ni gumu tu zaidi, maana ukishalijibu itabidi uingilie mambo ya euthanasia pia. Labda nisubiri tu maelezo ya wengine...

SteveD.
 
sawa Steve, labda tusubiri mawazo ya wengine. Ila tuna mengi ya kujifunza katika suala zima la kujitoa uhai, iwe kwa kujinyonga kwa kamba, kujisababishia ajali, kunywa vidonge nk.
 
Good topic Steve.

In my opinion, commiting suicide is what seem to be aftermath of crying for help for quite sometime. Usually, one, who ends up commiting such act, has helplessly try to seek rescue from the society. Each human being has demon(s) within. So when our demons try to take contol of our soul/energy, that is when we cry for help. However, the problem arises when the society is either not listening or ignoring our cry for help. When it gets to that point, that is when one's demon is succeeding in taking control of the soul/energy. As a result, whatever that demon decides to do, is going to happen...

Sasa tukiangalia hili tukio la kijana mwanafunzi wetu:

MWANAFUNZI wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Magoto iliyopo wilayani Tarime Mkoa wa Mara, Joseph James (21) amejinyonga baada ya kukutwa na majibu ya mtihani wa kumaliza kidato cha nne.

Sababu iliyomfanya ajinyonge: mwanafunzi huyo alijinyonga kwa tai yake baada ya kutolewa nje ya chumba cha mtihani na msimamizi, Joseph Menyei baada ya kukutwa na majibu ya mtihani.

Hofu yake: Amefanya uamuzi huo kuondoa aibu katika jamii sambamba na kujivunjia heshima kwa kukamatwa na majibu hayo ya mtihani.

My take
Ukisoma kwa makini hofu yake utagundua kuwa pengine demons wake walikuwa wanamvuruga/wanamtia uoga sana katika maandalizi yake ya mtiani huo. Huwezi jua, pengine alishawasilisha matatizo ya upeo wake wa kuelewa masomo kwa walimu au wanafunzi wake kwa nia ya kuomba msaada, lakini either hawakumtilia maanani au hawakuelewa tatizo lake lilikuwa ni nini. Matokeo yake, demons wake wakaiteka nafsi yake...
 
Good topic Steve.

In my opinion, commiting suicide is what seem to be aftermath of crying for help for quite sometime. Usually, one, who ends up commiting such act, has helplessly try to seek rescue from the society. Each human being has demon(s) within. So when our demons try to take contol of our soul/energy, that is when we cry for help. However, the problem arises when the society is either not listening or ignoring our cry for help. When it gets to that point, that is when one's demon is succeeding in taking control of the soul/energy. As a result, whatever that demon decides to do, is going to happen...

Sasa tukiangalia hili tukio la kijana mwanafunzi wetu:



My take
Ukisoma kwa makini hofu yake utagundua kuwa pengine demons wake walikuwa wanamvuruga/wanamtia uoga sana katika maandalizi yake ya mtiani huo. Huwezi jua, pengine alishawasilisha matatizo ya upeo wake wa kuelewa masomo kwa walimu au wanafunzi wake kwa nia ya kuomba msaada, lakini either hawakumtilia maanani au hawakuelewa tatizo lake lilikuwa ni nini. Matokeo yake, demons wake wakaiteka nafsi yake...

QM, thanks a lot for your good shot,

However, I have another concern brought about by your very expression above. The issue of demons, don't you see that this is rather another broad subject that some of us believe in and some don't?! Or in your opinion, is this thing for really (phyiscal) or is it a mere kind of 'thought forms'?!

Personally, I somewhat believe in 'thought forms' type of demons, just like your example above in red, they are mere personifications of concepts like fear, rage, desire/lust, envy and other emotions that someone would like to cast out of themselves.

Na nikikubaliana na hiyo form ya demons, basi kama unavyosema labda huyo kijana wa Musoma alikumbwa na hii type... tatizo swali lipo pale pale, ni kufa kishujaa au kinyonge?

(naomba kuto limit aina za hiki kifo, kama kuna khali nyinginezo zaidi ya ushujaa au unyonge naomba mtu aongezee).


SteveD.
 
--Je, kujinyonga baada ya kughafirika ki aibu ni kitu cha kutetea?!
--Je, huyu kijana amekufa kishujaa au kinyonge?!
--Je, kijana huyu alivyofanya ni sawa na kujitoa mhanga?!


2007-10-12 09:26:49
Na George Marato, Musoma

Alisema baada ya kumnyang`anya karatasi, mwanafunzi huyo alikimbia na kuingia katika moja ya vyumba vya madarasa katika shule hiyo.

Kamanda Saibull alisema kuwa baada muda walimfuatilia mwanafunzi huyo na kumkuta akiwa amejinyonga kwa tai aliyokuwa ameivaa na kuacha ujumbe uliokuwa ukisomeka, `ni vema nife kwani kukutwa na majibu hayo ya mtihani? kumemvunjia heshima katika jamii.
`

Habari za Kitaifa Habari nyingine zaidi!
Mwanafunzi ajinyonga kwa udanganyifu katika mitihani
Makubo Haruni, Musoma
HabariLeo; Friday,October 12, 2007 @00:02

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, David Saibullu alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa tisa mchana ndani ya chumba alichokuwa amepanga mwanafunzi huyo.
Alisema James ambaye nyumbani kwao ni katika Kijiji cha Nyamwaga, kabla ya kujiua, aliacha ujumbe kuwa amefanya uamuzi huo kuondoa aibu katika jamii sambamba na kujivunjia heshima kwa kukamatwa na majibu hayo ya mtihani.

Labda tuangalie makundi matatu kwanza ya watu wanaoamua kujiua;

1. Kundi la mwanzo linahusisha wanaojiua kwa sababu ya kumuumiza/kumkomoa mtu mwingine mfano mzazi wake, mpenzi'we, rafiki'ye nk kwa matarajio kitendo chake hicho 'huenda' kitamsononesha maisha yote huyo alomkusudia kwa kujilaumu na kulaumiwa na jumuia, nk.

--Je, kujinyonga baada ya kughafirika ki aibu ni kitu cha kutetea?!
Hapana, si la kutetea; ila la msingi tukumbuke kwamba mara nyingi wanaokuwa na tendency za kujidhuru, iwe kutishia kujiua, kujiunguza na sigara ama kujikata kata na visu, ama kujiua kweli, iwe kwa kusaga chupa, kujinyonga ama kunywa sumu nk, hawa wote wana hitilafu fulani katika ubongo. kwa maana nyingine ni, wenye tabia hii hurudia rudia kauli zao mpaka pale wanapotimiza azma yao hiyo. Kubwa panahitajika mental health consultancy ili kuweza kuwafariji na kuwapa nasaha za kuboresha fikra za watu wenye tendecy hizo.

2.Kundi la pili ni wale wanaoamua kujiua ama kutokana na maradhi ya muda mrefu pengine yasokuwa na tiba, (yakiwemo UKIMWI, Akili na ulemavu) , ulevi kupita kupindukia, utumiaji wa madawa ya kulevya nakadhalika, na walokumbwa na depression, kiasi kwamba hawaoni njia nyingine yeyote ya kujitoa katika matatizo hayo ila kwa njia hiyo ya mkato, na kwa kudhani hivyo wanauhakika kifo hakitaacha pengo lolote kwa jamii husika.

--Je, huyu kijana amekufa kishujaa au kinyonge?!
Kinyonge; kwa mtazamo wa 'hadithi' yenyewe,Hatuwezi jua msukumo ulompelekea kufikia uamuzi wa kutumia mlungula ili tu aweze kufaulu mtihani wake huo, kiasi kwamba hata alipokamatwa alionelea bora tu kujiua kuliko hatma ya kufutiwa mitihani yote baada ya kubainika na majibu ya mtihani.

3. Kundi jingine ni wale ambao wanaona hawana budi kujitoa mhanga kwa ajili ya watu wengine, hawa ni wale wenye mitizamo ya kidini zaidi mfano wanaopigania haki zao kwa mujibu wa itikadi zao za dini mfano; Budha's Monks, Religious Extremists, nk... na kisiasa; mfano wale wanaotetea maslahi ya kundi, nchi au sehemu fulani dhidi ya utawala wa kikandamizaji toka tabaka fulani la watawala mfano Extremists Sikhs walomuua Rajiv Gandhi, au 'Kamikaze Pilots' wakati wa vita vikuu vya dunia).

--Je, kijana huyu alivyofanya ni sawa na kujitoa mhanga?!
Hapana, sidhani kama kwa sababu tu amekamatwa na mlungula na kufukuzwa kwenye chumba cha mtihani ni sababu tosha ya kuamua kujitolea mhanga, kwani kosa linamuelekea yeye mwanafunzi.
 
Babu ajinyonga kwa kuchoshwa na maisha

2007-08-30 17:29:56
Na Mbonea Herman, Tanga

Mkazi wa Kwabaya Mashambani Ali Abdallah, 70 amejinyonga kwa kamba ya katani kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuchoshwa na maisha yaliyozidi kumuwia magumu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Simon Sirro amedhibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kueleza kuwa lilitokea jana, majira ya saa 1:30 asubuhi.

Aidha, Kamanda Sirro amesema mwili wa marehemu uligunduliwa na mtoto wa kiume wa marehemu aitwaye Abdallah ambaye alishangaa kuuona ukining�inia kwenye mti.

Akasema mtoto huyo aliweza kuubaini mwili wa marehemu mtini baada ya baba yao huyo kutoonekana kwa masaa kadhaa na wao kuamua kumsaka katika kila kona ya maeneo yao.

Hata hivyo, Kamanda akasema Polisi wanaendelea kufanya uchunguzi wa kifo hicho .

* SOURCE: Alasiri

Ajinyonga kwa waya wa simu

2007-08-02 17:49:22
Na Emmanuel Lengwa, Mlalakuwa

Mkazi mmpoja wa Mwenge Mlalakuwa Jijini Dar es Salaam, Bw. Kennedy Edward Urasa, 38, amekatisha maisha yake kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuchoshwa na maradhi ya muda mrefu yaliyokuwa yakimsumbua.

Tukio hilo limetokea leo mishale ya saa 11:00 alfajiri pale Mwenge Mlalakuwa nyumbani kwa mdogo wa marehemu aitwaye Joyce Urasa.

Alasiri imetinga mahali hapo leo asubuhi na kushuhudia Polisi wakiuondoa mwili wa marehemu na kwenda kuuhifadhi katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Mwananyamala.

Akizungumza na Alasiri, mdogo wa marehemu Bi. Joyce amesema kabla ya kaka yake huyo kujinyonga, alikuwa akisumbuliwa na homa za mara kwa mara.

Amesema kutokana na maradhi hayo yeye na mumewe walimzuia kupanga chumba na wakawa wanaishi naye nyumbani kwao ili iwe rahisi kumhudumia.

Bi. Joyce amesema kwa kawaida chumba alichokuwa akikitumia marehemu huwa hakifungwi usiku, ili kuwawezesha kwenda kumwangalia na kumjulia hali wakati wowote, lakini walishangaa siku ya jana, kila walipokwenda kumwona walikuta amefunga mlango.

`Kumbe usiku huo alitoka nje na kufungua waya wa simu ulifungwa kwa ajili ya kuanikia nguo, ambao aliutumia kwa kujinyonga,` amesema Bi.Joyce.

Bi. Joyce amesema marehemu hakuacha ujumbe wowote na kuwa enzi ya uahi wake alikuwa mpole asiye na makuu, hali inayosababisha waamini kuwa uamuzi wa kujinyonga ameuchukua kutokana na kusumbuliwa na maradhi.

Akaongeza kuwa kaka yake hakuwa na mke wala hakuacha watoto.

* SOURCE: Alasiri

MMwanamke ajinyonga kwa kukata tamaa

2003-12-19 22:49:19
Na Thobias Mwanakatwe, PST, Tanga

Mwanamke mmoja, Elizabeth Silvanus (39), mkazi wa Wilayani Muheza, amejiua kwa kujinyonga kwa waya wa simu kwa kile kilichodaiwa ni kutokana na kukata tamaa ya maisha.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga Bw. Brown Lekey, alisema mwili wa Elizabeth ulikutwa ukining’inia chumbani kwake.

Wakati huo huo, watu wanne wamejeruhiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka katika Barabara ya Mombasa-Tanga.

Kamanda Lekey alilitaja gari lililohusika katika ajali hiyo kuwa ni basi dogo la abiria lenye namba za usajili TAY 955 aina ya Nissan lililokuwa likisafiri kutoka Mombasa kuja Tanga.

Alisema ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mikweli na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya Bombo ambayo ni ya Mkoa wa Tanga.

Kamanda Lekey alisema basi hilo lilikuwa na abiria 12 na kwamba majeruhi wanane kati yao walitibiwa na kuruhusiwa kurejea makwao.

Alisema majeruhi wengine wanne ambao ni Neema Peyason, Rehema Peyason, Salome Yohana, wakazi wa Mkoa wa Morogoro na Maimuna Hamis, mkazi wa Muheza, bado wamelazwa hospitalini hapo.

Alisema katika tukio jingine lililotokea Msambiazi wilayani Korogwe, mwendesha baiskeli Abushir Amir (25), alikufa baada ya baiskeli yake kuvunjika akiwa kwenye mwendo mkali.

Kamanda Lekey alisema katika tukio lingine lililotokea Desemba 16, mwaka huu, mtoto John Emmanuel (6), alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari aina ya Fuso MSK 606.
Alisema dereva wa gari hilo anashikiliwa na polisi kutokana na tukio hilo.

Katika tukio lingine la Desemba 16, mwaka huu, gari aina ya Toyota Hilux 5924, lilipinduka eneo la Sindeni wilayani Handeni na kusababisha kifo cha Hemed Haidai (38) mkazi wa Handeni.

* SOURCE: Nipashe

Mfanyabiashara ajinyonga kwa khanga za mkewe!

2003-12-27 00:18:30
Na Mohab Dominick, Kahama

Mfanyabiashara mmoja maarufu mjini hapa, Peter Masele, amekutwa amejinyonga nyumbani mwake eneo la Majengo Sokola kwa kutumia khanga mbili za mkewe.

Regina Lemmy ambaye ni mke wa marehemu, ameiambia Komesha kuwa mumewe amekutwa amejinyonga kwenye chumba wanacholala watoto wao siku Jumapili, mishale ya saa 12:00 asubuhi.

Regina akaendelea kusimulia kuwa kabla ya kujinyonga, mumewe ambaye siku hiyo alikuwa ameamka mapema isivyo kawaida, aliwasiliana kwa simu ya mkononi na mdogo wake ambaye pia hujishughulisha na biashara jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, mwanamke huyo akasema kuwa yeye hakuelewa ni kitu gani walikuwa wakiongea ndugu hao wawili ambao mara tu baada ya kwisha kwa mazungumzo hayo, mumewe akatoka kwenye nyumba kubwa alimokuwamo na kwenda kwenye vyumba vya uani wanapolala watoto wao.

Baada ya hapo, akasema Regina kuwa mumewe hakurudi tena ndani alikomuacha yeye na pale alipoanza kumtafuta, akashangaa kumkuta kwenye chumba kimojawapo cha watoto akiwa ananing’inia kwenye kenchi baada ya kuwa tayari ameshajinyonga.

“Baada ya hapo, nikaanza kuitilia majirani. Kisha baadaye Polisi wakafika na kuanza kufanya uchunguzi zaidi juu ya kifo hicho. Nilipatwa na mshituko sana,” akasema Regina.

Hata hivyo baadhi ya jamaa wa karibu wa Marehemu huyo wamedai kuwa marehemu alikuwa na mawazo mengi juu ya gari lake jipya alilonunua hivi karibuni na kupata ajali mbaya katika eneo la Igunga.

Aidha, wakadai majirani hao wanaomjua vizuri marehemu kuwa tukio la ajali hiyo na madeni aliyokuwa nayo marehemu huenda ikawa ni miongoni mwa sababu zilizomfanya aamue kusitisha uhai wake.

Hili ni tukio la pili kutokea eneo la Majengo mjini Kahama kwa kipindi cha mwezi mmoja ambapo wafanyabiashara maarufu wamekuwa wakijinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mzigo wa madeni unaowakabili kutokana na shughuli zao mbalimbali za kibiashara ambapo mapema mwezi uliopita, mfanyabiashara Kulwa Wanga, naye alikutwa amejinyonga ndani ya chumba chake.

* SOURCE: Komesha

Mtuhumiwa ajinyonga mahabusu

na Zainab Kibao, Iringa


JESHI la Polisi mkoani hapa kwa kushirikiana na raia wema, limefanikiwa kuwakamata watu watatu wanaotuhumiwa kukutwa wakijiandaa kwenda kufanya uhalifu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Advocate Nyombi, alisema ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita majira ya saa 3:45 asubuhi kwenye Mtaa wa Changalawe, Wilaya ya Mufindi.

Aliwataja waliokamatwa kuwa ni Christopher Kabwa (32), mkazi wa Ifunda, Iddi Kiyegeu (29) mkazi wa Ukumbi - Dabaga Wilaya ya Kilolo na Maiko Mfugale (26) mkazi wa Mbarali mkoani Mbeya.

Alisema polisi walipata taarifa toka kwa raia wema kuhusiana na watu hao na walipofuatilia ndipo wakafanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa ma bastola ya Kichina yenye namba 541922 - 6619958 ikiwa na rasasi tisa.

Aidha, Kamanda Nyombi alisema walipokamatwa na kohojiwa, watu hao walikiri kuhusika kwenye matukio mengi ya uhalifu likiwamo tukio la uporaji katika duka la jumla mkoani Mbeya ambapo askari mmoja aliuawa.

Hata hivyo, Kamanda Nyombi alisema Mfugale alifariki dunia akiwa hospitali ya wilaya ya serikali wakati akipatiwa matibabu baada ya kujinyonga akiwa rumande.

Kamanda Nyombi alisema kuwa askari aliyekuwa anafanya ukaguzi katika mahabusu walimokuwa wamewekwa watuhumiwa hao, alimkuta Mfugale akiwa ananing’nia baada ya kujinyonga kwa kutumia shati huku akiwa anakaribia kukata roho.

Samahani kwa makala ndefu, lakini tuendelee na uchambuzi wa hoja hii ambayo inaleta sana utata katika jamii zetu. Angalia sababu za watu hao kujinyonga, nimeziwekea wino mweusi sana makusudi kuonyesha msisitizo.
 
Samahani kwa makala ndefu, lakini tuendelee na uchambuzi wa hoja hii ambayo inaleta sana utata katika jamii zetu. Angalia sababu za watu hao kujinyonga, nimeziwekea wino mweusi sana makusudi kuonyesha msisitizo.

-Kuchoshwa na maradhi yanayomsumbua'
-Kuchoshwa na maisha, kukata tamaa ya maisha, mzigo wa madeni...nk...

2.Kundi la pili ni wale wanaoamua kujiua ama kutokana na maradhi ya muda mrefu pengine yasokuwa na tiba, (yakiwemo UKIMWI, Akili na ulemavu) , ulevi kupita kupindukia, utumiaji wa madawa ya kulevya nakadhalika, na walokumbwa na depression, kiasi kwamba hawaoni njia nyingine yeyote ya kujitoa katika matatizo hayo ila kwa njia hiyo ya mkato, na kwa kudhani hivyo wanauhakika kifo hakitaacha pengo lolote kwa jamii husika.

...Hivi, depression kwa kiswahili sanifu/tafsiri yake ni nini?
 
Hivi, depression kwa kiswahili sanifu/tafsiri yake ni nini?

Niweke wazi kuwa sina uhakika na tafsiri ya neno depression kwa kiswahili, ila kuna neno linaitwa msongo wa mawazo ambalo mara nyingi watu hupenda kulitumia kumaanisha kitu kama depression. Labda Steve atusaidie tafsiri hii.
 
Niweke wazi kuwa sina uhakika na tafsiri ya neno depression kwa kiswahili, ila kuna neno linaitwa msongo wa mawazo ambalo mara nyingi watu hupenda kulitumia kumaanisha kitu kama depression. Labda Steve atusaidie tafsiri hii.

Depression

-Persistent sad, anxious, or "empty" mood
-Feelings of hopelessness, pessimism
-Feelings of guilt, worthlessness, helplessness
-Loss of interest or pleasure in hobbies and activities that were once enjoyed, including sex
-Decreased energy, fatigue, being "slowed down"
-Difficulty concentrating, remembering, making decisions
-Insomnia, early-morning awakening, or oversleeping
-Appetite and/or weight loss or overeating and weight gain
-Thoughts of death or suicide; suicide attempts
-Restlessness, irritability
-Persistent physical symptoms that do not respond to treatment, such as headaches, digestive disorders, and chronic pain

Types of Depression

Major depression is manifested by a combination of symptoms (see symptom list) that interfere with the ability to work, study, sleep, eat, and enjoy once pleasurable activities. Some people have a single episode of depression, but many have episodes that recur.

Dysthymia is a less severe type of depression that lasts a long time but involves less severe symptoms. If you suffer from dysthymia you probalby lead a normal life, but you may not be functioning well or feeling good. People with dysthymia may also experience major depressive episodes at some time in their lives.

Bipolar Disorder (also called manic-depression) is another type of depressive disorder. Bipolar disorder is thought to be less common than other depressive disorders. If you have bipolar disorder you are troubled by cycling mood swings - usually severe highs (mania) and lows (depression). . Mania, left untreated, may worsen to a psychotic state, where the person is out of touch with reality.

...na kwa kipengele hiki;...
Kwa sisi walalahoi, is this a means of escaping one's individual misery and wretched life or a way of rejecting completely the miserable and wretched social conditions and society one lives in?!
...naweza jibu ifuatavyo;...


...Kwa mtazamo wangu, kuna uwezekano mkubwa wa mlipuko wa 'msongo huo wa mawazo' unawakumba wengi tu, ila Diagnosis ya kinyumbani (Tz) bado sana. Treatment na counselling yake haijaboreshwa, ndio maana matukio haya 'machache' yanayoripotiwa sasa yanaashiria kwa kiasi fulani huko tunakoelekea 'yatazidi'! (pia, iwapo hakutakuwa na 'ahueni' kwenye maisha ya mwananchi).
 
Depression pia inaitwa sonono.

Diagnosis ipo wazi, nafikiri tatizo ni jinsi ya kutibu, kwani matibabu yake mengi yanategemea 'social welfare' pamoja na support ya community.
 
HAO WAMEFANYA HIVYO BAADA YA KUONA WANA HATIA NA HAWANA SABABU YA KUISHI, KWA VIONGOZI WETU WA SERIKALI YA TANZANIA NANI KATI YENU ANAWEZA KULIONA HILO, NANI KATI YENU WALA RUSHWA MAFISADI MNAWEZA KUONA THAMANI YA MAISHA YAMEKWENDA KWA SABABU TU YA WOGA KUITWA MLA RUSHWA HUYU MWANAFUNZI ALIONA AIBU KWANI AKIPITA MITAANI ATAITWA MGANDAMIZIAJI. WEWE KAMA KIONGOZI WA SERIKALI HUNA AIBU KUIKUMBATIA RUSHWA
 
pia watu huchukua uamuzi wa kujinyonga pale wanapojiridhisha wenyewe kuwa ulimwengu umewatenga na hivyo hauwataki tena.

wakati mwingine hudhani kila wanayekutana naye anajua jambo walilolifanya, au kuwa anawakinai.

hujiridhisha kuwa milele na milele hatatokea mtu wa kuwafariji na hivyo kuchukua uamuzi wa kukatisha maisha yao.
 
Depression pia inaitwa sonono.

Diagnosis ipo wazi, nafikiri tatizo ni jinsi ya kutibu, kwani matibabu yake mengi yanategemea 'social welfare' pamoja na support ya community.

Heshima mbele wana JF kwa mada hii nzuri.
Kasana, kama ulivyodai hapo, 'social welfare' ina nafasi yake kubwa sana katika maisha ya kawaida ya wanajamii. Tulishaliongelea hili katika mifano mada mama hapo juu, hasa tulipoangalia mifano ya matukio ya sababu za watu kujinyonga. Kwamba mtu anajihisi kama jamii imemtenga ama haimtendei vile anavyotaka. Maisha ya kibepari yanayosisitiza sana 'ubinafsi' ama 'kutotegemeana' yanasababisha vifo vingi vingi sana ktk nchi tajiri. Idadi ya watu wanaojiua kwa nchi zilizo na maendeleo ya juu ni kubwa mno kwa sasa kutokana na mfumo wa huu wa maisha.
Kuna wazungu wanatamani maisha ya Afrika hata kama ni ya kimasikini. Kisa? Watu wanajuliana hali, wanasaidiana katika sida na raha wanajaliana. Katika nchi zilizoendelea, hasa Ulaya Magharibi, ukiwa na tatizo kama kufiwa ama kuishiwa, hilo ujue unajitwisha, kwani hakuna kushirikiana kama ilivyo kwa jamii nyingi za Afrika.
Ndio hapa ambapo ummuhimu wa 'social integration' unapoonekana.
Kwa hitimimisho langu, maisha ya kibepari ni mojawapo ya sababu za watu kujiua.
Tuendelee kujadili, ningependa kupata mawazo kutoka kwa wenzangu kuhusu namna ya kukabili tatizo hili la watu kujiua.
 
kujinyonga kunaweza kutafsiriwa kutokana na historia ya pahala.

kwa nchi kama Japani, kujinyong'a kwa kiongozi kunachukuliwa kama kitendo cha kishujaa. hii haikuanza leo wala jana, katika enzi za samurai, walipokuwa wakienda vitani na wakishindwa kulinda kile walichokiamini, badala ya kurudi kijijini na aibu ya kushindwa, walikuwa wakifanya 'harikiri' ambayo ni kujikata kwa upanga wako sehemu ya tumboni ili kujiuwa.

samurai alikufa vitani na yule alikufa kwa kujiuwa mwenyewe wote walichukuliwa kama mashujaa katika jamii.

historia hii imekuwa ikirithishwa vizazi hadi vizazi, na hadi sasa kwa japani, kujiuwa si jambo la ajabu sana.

mtendaji wa serikali anaposhindwa moja kwa moja kutetea makosa yake, anaweza kuchukua hatua ya kujiuwa, ambayo haionekani kama mbaya kwa jamii

mtoto wa kijapani anapojiuwa, jamii inasikitika kwa kukosa uhai wa mtoto yule, ila haishangai kwa kujiuwa huko, kwa vile anafata vitendo vya ma bibi na mababu zake

tunapokuja kwa upande wa tanzania sasa
sisi hatuna mila za namna hiyo. kujiuwa ni kosa na wala hakuna sehemu yoyote kitendo hicho kilipowahi kusifiwa.

anaejiuwa, anatenda makosa kijamii, na kwa mawazo yangu, watanzania hujiuwa kwa kukosa mtu wa kumuhadithia matatizo yao.

chukua mfano mtoto huyo, labda kwake yeye ameingiziwa akilini kuwa ni lazima apasi mtihani, apate kuendelea ili waweze kujikomboa kimaisha yeye na wazee wake. familia yake yote pengine inamtegemea kwa yeye kufaulu mtihani huo.

kila mtoto na uwezo wake kisaikolojia, kwa mwengine ni jambo zito kisaikolojia kulikomnyima raha ya kufikiri na kutafakari, na hasa ukitazama hana wa kusema nae kuwa anahisi hawezi kufaulu kwa vile wazee wanamtegemea. baada ya kukamatwa na "kibomu" kwenye mtihani, anaona matumaini yake yameisha na ni aibu kwa wazee wake, anaamua kujiuwa.

nafikiri kujiuwa kunatokana na ukosefu wa mtu wa kusema nae matatizo yako wakati matatizo hayo yanapokuwa mazito zaidi kwenye akili yako
 
.....
tunapokuja kwa upande wa tanzania sasa
sisi hatuna mila za namna hiyo. kujiuwa ni kosa na wala hakuna sehemu yoyote kitendo hicho kilipowahi kusifiwa.

anaejiuwa, anatenda makosa kijamii, na kwa mawazo yangu, watanzania hujiuwa kwa kukosa mtu wa kumuhadithia matatizo yao.

chukua mfano mtoto huyo, labda kwake yeye ameingiziwa akilini kuwa ni lazima apasi mtihani, apate kuendelea ili waweze kujikomboa kimaisha yeye na wazee wake. familia yake yote pengine inamtegemea kwa yeye kufaulu mtihani huo.

kila mtoto na uwezo wake kisaikolojia, kwa mwengine ni jambo zito kisaikolojia kulikomnyima raha ya kufikiri na kutafakari, na hasa ukitazama hana wa kusema nae kuwa anahisi hawezi kufaulu kwa vile wazee wanamtegemea. baada ya kukamatwa na "kibomu" kwenye mtihani, anaona matumaini yake yameisha na ni aibu kwa wazee wake, anaamua kujiuwa.

nafikiri kujiuwa kunatokana na ukosefu wa mtu wa kusema nae matatizo yako wakati matatizo hayo yanapokuwa mazito zaidi kwenye akili yako

Gaijin,
Kwanza kabisa, ahsante kwa mchango wako. Kwenye hilo nililoweka wekundu, kama sijakosea, mbona nakumbuka kwenye historia yetu kuna mtemi (Mkwawa) alijiua ili asikamatwe akiwa hai na Wajerumani, na tendo hili kama jinsi vitabu vyetu vingi vya historia vilivyo andika ni tendo la kishujaa... au una maanisha jamii ya maisha ya hivi karibuni tu?! Ahsante.

SteveD.
 
Heshima mbele wana JF kwa mada hii nzuri.
Kasana, kama ulivyodai hapo, 'social welfare' ina nafasi yake kubwa sana katika maisha ya kawaida ya wanajamii. Tulishaliongelea hili katika mifano mada mama hapo juu, hasa tulipoangalia mifano ya matukio ya sababu za watu kujinyonga. Kwamba mtu anajihisi kama jamii imemtenga ama haimtendei vile anavyotaka. Maisha ya kibepari yanayosisitiza sana 'ubinafsi' ama 'kutotegemeana' yanasababisha vifo vingi vingi sana ktk nchi tajiri. Idadi ya watu wanaojiua kwa nchi zilizo na maendeleo ya juu ni kubwa mno kwa sasa kutokana na mfumo wa huu wa maisha.
Kuna wazungu wanatamani maisha ya Afrika hata kama ni ya kimasikini. Kisa? Watu wanajuliana hali, wanasaidiana katika sida na raha wanajaliana. Katika nchi zilizoendelea, hasa Ulaya Magharibi, ukiwa na tatizo kama kufiwa ama kuishiwa, hilo ujue unajitwisha, kwani hakuna kushirikiana kama ilivyo kwa jamii nyingi za Afrika.
Ndio hapa ambapo ummuhimu wa 'social integration' unapoonekana.
Kwa hitimimisho langu, maisha ya kibepari ni mojawapo ya sababu za watu kujiua.Tuendelee kujadili, ningependa kupata mawazo kutoka kwa wenzangu kuhusu namna ya kukabili tatizo hili la watu kujiua.

Mtupori, Ahsante sana kwa mchango wako.
Kwenye wekundu hapo nami nakuunga mkono. Sababu alizoelezea mchongoma zifuatazo mojawapo naona inahusika na hilo:
-Persistent sad, anxious, or "empty" mood
-Feelings of hopelessness, pessimism
-Feelings of guilt, worthlessness, helplessness
-Loss of interest or pleasure in hobbies and activities that were once enjoyed, including sex
-Decreased energy, fatigue, being "slowed down"
-Difficulty concentrating, remembering, making decisions
-Insomnia, early-morning awakening, or oversleeping
-Appetite and/or weight loss or overeating and weight gain
-Thoughts of death or suicide; suicide attempts
-Restlessness, irritability
-Persistent physical symptoms that do not respond to treatment, such as headaches, digestive disorders, and chronic pain
Wengi wanaojiua katika nchi zilizoendelea ambao hawaonyezi dalili nyinginezo za SONONO na wana maisha ya kuweza kuitwa 'matajiri', wanajiua kutokana na kujiona wamekamilisha yote maishani na hawana cha nyongeza 'bali kujaribu kifo'.

Hebu fikiria uwemwanadamu uliyebarikiwa na kuwa na yote, (apart from hilo la kuondoa hisia za kujiua), unapesa, umefanya mapenzi utakavyo, umesafiri na kuona yote ulikopenda, kwenye Mwezi pia umeenda, kwenye space station pia umefika, kwenye chemichemi za maji baharini umefika, myth za aliens nazo unajua jibu lake, imani ya kidini nayo huna... kilichobakia nini hapa duniani?!

SteveD.
 
Back
Top Bottom