MIGONGANO YA KIFIKRA: Je, Kuua Kazini Ni Kosa Au Dhambi?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Ndugu wasomaji,
Naomba mawaidha yenu katika maswala yafuatayo bila kujali kama yamekukuta, yamekuhusisha au laa:

  • --Kama wewe ni Mwanausalama, unajisikiaje pale ulipo amua kumpiga mtu risasi na kufa ukiwa vitani au ukiwa katika doria?
  • --Kama wewe ni Raia, unajisikiaje pale ulipo amua kumuua mtu ukijihami baada ya kuvamiwa nyumbani kwako au katika ugomvi?
  • --Kama wewe ni Daktari, unajisikiaje pale ulipo amua kukatisha matibabu ya mgonjwa mahututi ili bora afe?
  • --Je, unajisikiaje pale ulipo ua mtu bila kukusudia - mfano katika ajali?
  • --Kama wewe ni Mwenye mamraka kisheria, unajisikiaje pale ulipotoa hukumu ya kifo?

Naomba kuzingatia moja wakati unatafakari jinsi ya kutoa maoni yako; nalo ni kwamba, maswali haya yanahusu 'aftermath' ya tukio, kile unachohisi ulihusika nacho kina kuletea kero gani moyoni mwako kama lipo. Unajua pale unapotenda kitu ukitegemea kuwa umefanya la maana, lakini baadae unaanza kuwa na majuto, basi ni katika hiyo hali ya 'ki professional' au mazingira yanayopelekea hilo tukio na aftemath yake. Cha nyongeza ni kuwa jamii haijengwi kwa majuto, lakini majuto tunaishi nayo, basi na hapa ni namna tu ya kuyajadili.

Ahsanteni.


SteveD.
 
Na wewe kwa kuanzisha mada zenye utata, hujambo!
Hebu nenda kwa brazameni! (just kidding)!

Kwa mtazamo wangu.
1. Kwa upande wa wanausalama, kuna sheria inasema kwamba iwapo mtu anayetarajia kukamatwa na wanausalama kwa makosa fulani ana silaha (hasa ya moto) na ana nia ya kuitumia, ama anaitumia ili kuzuia wana usalama wasimkamate, basi itamlazimu mwanausalama huyo kutumia silaha yake, lengo la awali la matumizi haya ya silaha siyo kuua, ila kummaliza nguvu huyu mhusika. Hii ni pamoja na kumpiga risasi maeneo ambayo yatamfanya mhusika asife! Lakini iwapo mhusika anaonyesha dalili za hatari, basi hawa wanausalama huruhusiwa kuua, kwa minajili ya kujitetea!

2. Katika ajali kuna namna kadhaa za mtu "kuua".
Kwanza, iwapo umemgonga mtu kwa makusudi, hapo umeua kwa makusudi, inabidi upatilizwe kwa adhabu stahili!
Pili, kama ulikuwa unaendesha chombo cha moto kwa spidi kubwa (kama 100 ama 120) katika maeneo ambayo huruhusiwi kwenda kwa spidi hiyo (kama vile vivuko vya waenda kwa miguu), hapo unakuwa na kosa la kuua pia!

Nadhani wataalamu wa sheria watafafanua zaidi!
 
If you can't stand the heat, forget about getting out of the kitchen, don't even get in there in the first place.

The best way to stop smoking is by not starting.

To quote a Jay-Z classic (22 Two's)

"I don't follow any guidelines, cause too many ni**az try to rob mine so I switch styles every two lines"

I am a relativist, it is all relative to the specifics of the situation, there is nothing absolute in this world, even under ceteris paribus if at all it exist.
 
I am a relativist, it is all relative to the specifics of the situation, there is nothing absolute in this world, even under ceteris paribus if at all it exist.

Pundit, intriguing concept you raise, nakuomba basi utufafanulie kiundani zaidi. Ahsante.


SteveD.
 
Babu una-sound kama unaandika paper vile...kwikwikwiii

Ha ha ha, ningekuwa nafanya hivyo ningekuambieni ndugu zangu, kama Kithuku tu alivyofanya... haya ninayouliza ni maswali yalikuwa yamenikaa moyoni kwa miaka zaidi ya minane iliyopita... ndiyo uzuri wa ICT sikuhizi, wabongo kwa wabongo tunaweza kuulizana... sasa kwanini tusifanye hivyo? wenzetu njia za mawasiliano wamezihimu muda mrefu... na maendeleo bila kuulizana na ku-document yaliyomoyoni na yale tunayokutana nayo katika mazingira yetu mimi nadhani haiwezi kutufikisha mbali.

Saa nyingine huwa nawaza na kufikiri, tungelikuwa wapi iwapo histori ya jamii ya Kiafrika ukiondolea mambo ya Wamisri ingelikuwa iko documented kwa angalau miaka 1500 hivi... si ma reference tungelikuwa nayo kemkem...... hapo angekuja kijana fulani hivi in my reincarnation anayeitwa DUNDUBI na swali lake kuhusu jambo kama hili na kuambiwa, aaah, hilo liliandikwa na SteveD tayari miaka kama 456 iliyopita... na mambo mengine kama hayo.. naona unanipata Nyani.. lol

SteveD.
 
SteveD you damn hot men your topics roc dude.
Mimi nadhani kuua kazini kama ilikuwa in self defence its real fine si kosa.Ila kuhusu Dhambi kwa kweli naomba niwaachie religionists.
Kwenye issue ya hukumu mimi ni mwanafunzi wa sheria,some times hukumu haiepukiki kama kifingi cha sheria kinadai hivyo basi ni wajibu kitekelezwe.
Sometimes you have to make bitter decisions for the better.
 
SteveD you damn hot men your topics roc dude.
Mimi nadhani kuua kazini kama ilikuwa in self defence its real fine si kosa.Ila kuhusu Dhambi kwa kweli naomba niwaachie religionists.
Kwenye issue ya hukumu mimi ni mwanafunzi wa sheria,some times hukumu haiepukiki kama kifingi cha sheria kinadai hivyo basi ni wajibu kitekelezwe.
Sometimes you have to make bitter decisions for the better.
...The analogy: America justifies in the same manner the letting off of the two bombs on Hiroshima and Nagasaki!!
 
it takes my breath.....! u know stmes it happens to what stand u take (religion/real situation)
chukua mfano wewe ni mwalimu........ umetambua kuwa wanafunzi 3 majibu yanafanana.... you take away 15% marks as adhabu......!
baada ya uchunguzi wa kina unagundua you had a wrong mtazamo......! actually you feel pitty and regret for what you have done.....! lakini ukatazama on your side you find that you either were not wrong kutokana na mazingira yako then you dont regret....!
but.......! UNAPOTEKELEZA 'JAMBO' KUTOKANA NA KAZI YAKO..........YOU BECOME RIGHT...!
 
Ndugu wasomaji,
Naomba mawaidha yenu katika maswala yafuatayo bila kujali kama yamekukuta, yamekuhusisha au laa:

  • --Kama wewe ni Mwanausalama, unajisikiaje pale ulipo amua kumpiga mtu risasi na kufa ukiwa vitani au ukiwa katika doria?


    ...bahati nzuri au mbaya, mwanausalama unafundishwa kuua, kwani katika fani hii kuna mawili maji yakikufika shingoni, ama uue au uuliwe! Self defence haihitaji regrets.


  • --Kama wewe ni Raia, unajisikiaje pale ulipo amua kumuua mtu ukijihami baada ya kuvamiwa nyumbani kwako au katika ugomvi?

    ...kama ulivamiwa nyumbani kwako, chochote kilicho karibu nawe kitachokusaidia kujihami hata kama kitasababisha kifo ni sawa tu, self defence-without regrets, hata kama uliua bila kukusudia

    ...lakini kwenye ugomvi, majuto ni mengi, ...the best defence kwenye ugomvi ni ku control temper yako kwani hakuna mshindi katika hilo ila hasara, hata ikibidi kimbia!


  • --Kama wewe ni Daktari, unajisikiaje pale ulipo amua kukatisha matibabu ya mgonjwa mahututi ili bora afe?


    ...It's all about consent ya mgonjwa au ndugu wakati wote wa matibabu, kama kila tiba imefanyika na hakuna tena alternative ya kumsaidia mgonjwa kwa kujua jinsi mgonjwa anavyoendelea kuishi anazidi kuteseka, then hamna regrets, jitihada zote zilishafanyika!


  • --Je, unajisikiaje pale ulipo ua mtu bila kukusudia - mfano katika ajali?


    ...Hapo regrets mpaka siku kwenda kaburini!...ni mbaya sana ikikutokea, lakini hatma yake ni kupiga moyo konde kwamba halikuwa kusudio lako and face the reality.


  • --Kama wewe ni Mwenye mamraka kisheria, unajisikiaje pale ulipotoa hukumu ya kifo?

    ...urahisi wa hili (kama wewe ni judge) ni kwamba si wewe peke yako unayebeba jukumu hili, ...its all about jury's verdict! wewe ukiwa judge unapitisha tu adhabu kwa mujibu wa vifungu vya sheria, halafu mpira unamuachia 'Mtukufu' rais amwage saini yake!

    Sijui Rais anajiskiaje juu ya hili! sitataka hapa kuelezea 'ningekuwa rais' ningejiskiaje... kwani inaonekana ukishakuwa rais una 'loose the touch of reality!'
 
Ndugu wasomaji,
Naomba mawaidha yenu katika maswala yafuatayo bila kujali kama yamekukuta, yamekuhusisha au laa:


Ahsanteni.


SteveD.


SteveD,

Nitajaribu kuchangia mada hii japo sina uhakika kama nitachangia kama ilivyotakiwa, so bare with me and correct if i might be wrong please.


[*]--Kama wewe ni Mwanausalama, unajisikiaje pale ulipo amua kumpiga mtu risasi na kufa ukiwa vitani au ukiwa katika doria?

Kwa wanausalama, Wanajeshi wakiwa vitani nafikiri kwa wao kuua it's okay na nafikiri is very rare to find a person regrecting after the action endapo tu yule aliyemuua atakuwa ni adui, na kwamba huyo adui alikuwa na nafasi na nyenzo vya kuua endapo asingewahiwa kuuwawa. Mtu anaweza jutia pale tu inapotokea "Mistakes of fact". kwamba alifikiri jamaa ni adui na kumbe ni mwenzake na akajikuta amemshoot na kumuua.

Upande wa Police Officers; Of course they are trained to use deadly force, but what I know ni kwamba wanatakiwa kutumia hizo deadly force (eg shoot to kill) as a last resort na sio katika kila kosa/issue. Mfano, they can shoot and kill endapo mshitakiwa "Note, mshtakiwa and not mtuhumiwa" wa makosa kama kubaka na mauaji alikuwa anakimbia kukamatwa ama alikuwa na silaha ambayo bila kuuwawa basi angesababisha mauaji kwa Askari huyo (self defence) ama kwa mtu mwingine ambaye this askari has the duty to care (eg mwananchi, VIP etc), na kwamba mpaka askari akaamua kushoot and kill this person, njia zote za kuminimize hiyo threat zimeshindikana hence the use of firearm as a last resort. All in all, justification needed.


Kama wewe ni Raia, unajisikiaje pale ulipo amua kumuua mtu ukijihami baada ya kuvamiwa nyumbani kwako au katika ugomvi?

Self defence, Ninafikiri its okay and no crime on this endapo umevamiwa nyumbani na waliokuvamia wana silaha or they made you to belive that wana silaha (eg pointing a toy pistol on you).

Kwa suala la ugomvi kwa kweli jiandae tu kuface Manslaughter.


[*]--Kama wewe ni Daktari, unajisikiaje pale ulipo amua kukatisha matibabu ya mgonjwa mahututi ili bora afe?

Kwa madaktari if there is a concent ya mgonjwa, nafikiri kuna sheria inaruhusu na huyu Daktari hatakuwa na kosa. Na sidhani kama itamuhunt kwani mpaka mgonjwa kuamua kuchagua kufa kuliko kuishi, na Daktari ama jopo la madaktari kuamua kusitisha maisha ya mgonjwa huyo, then inawezekana hali ilikuwa ni mbaya sana and that there was no way out kwamba mgonjwa huyu angekuja kupona, na kwamba its better for him/her to rest is better kuliko mateso aliyokuwa akiyapata.

[*]--Je, unajisikiaje pale ulipo ua mtu bila kukusudia - mfano katika ajali?

Well, inaumiza sana na inaweza kukuhunt kwa muda mrefu sana and if you are not strong unaweza fanya maamuzi ya ajabu pia. Face it, be strong, though.................. Sheria itaangaliwa how it happen then unaweza hukumiwa kuua kizembe (causibg death by dangerous driving) ama kwa ajali ya kawaida (i think they call it fatal accident), most of the time wanalipa fine. Inategemea na kesi na ushahidi wa kesi husika. Pia waweza kuwa charged na mudred kama utakuwa umeua kwa kukusudia kwa kutumia chombo cha usafiri, in this case, itahama from traffic case na itakuwa criminal case.

[*]--Kama wewe ni Mwenye mamraka kisheria, unajisikiaje pale ulipotoa hukumu ya kifo?

Mh, difficult one. Ila sidhani kama mtu atajisikia vibaya sana coz mpaka mtu kuhukumiwa adhabu ya kifo, that means hata yeye aliyoyatenda sio madogo. It's even more than what he will be facing. Haiwezi ku hunt sana, ni sheria inasema afanyiwe hivyo. Itakuwa kosa la mauaji (murder) if it will be proved kwamba huyu mwenye kutekeleza sheria (mnyongaji) atafanya hivyo kwa personal reasons/nia ovu/motives, let say he/she was supposed to go on retirement, he/she decided to postipone his/her retirement ili kutimiza lengo lake (kumnyonga 'y')



Thats all form my side.

Lizy
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom