Migomo hii ina maana pana zaidi Kisiasa

MushyNoel

Senior Member
Jan 13, 2011
104
9
Tumeshuhudia migomo Mbalimbali katika vyuo vyetu vikuu.Maana halisi ya kugoma ni kuonesha kwamba mfumo flani una ufa unaoweza kufanya haki flani isipatikane.Hivyo kama kwa macho ya kawaida uzibaji huo wa ufa kwa njia ya busara kama unaonekana kuwa mgumu wagomaji huamua kushinikiza/kugoma ili kumwamsha mtawala kwamba ziba ufa mzee.Tumeona wahadhiri wakigoma kwa kile ambacho ni haki yao.Wanafunzi vyuoni nao wanagoma.mambo haya yana tafsiri pana kwenye siasa zetu.Ukiangalia katika migogoro hii ipo ambayo ( UDOM -wahadhiri ) imesababishwa na uingiliaji wa wanasiasa katika sehemu za kitaaluma.Ipo kazi pale ambapo tunaona kwamba kwa hali yeyote ngumu ijayo kama Gharama za umeme,mishahara kwa waajiriwa n.k kila mtu atatamani kugoma ili kuwaonesha wanasiasa kwamba maamuzi yanayofanywa kisiasa pengine ni hatari zaidi kuliko vifaru vya adui.
 
Back
Top Bottom