Migodi hatarini kufungwa kufuatia agizo la Rais Magufuli

Ni nini kisicho sawa? Watanzania wanaendeshwa kwa hisia. Niliwahi kufanya utafiti wa kodi zinazotozwa kwenye migodi ya Tanzania, nikalinganisha na mataifa mengine, sisi tupo kwenye kundi linalotoza kodi kubwa, japo siyo juu kushinda mataifa yote. Tunatoza corporate tax 30%, hakuna anayetoza zaidi ya hiyo lakini wapo wanaotoza pungufu. Tunatoza mrabaha 4%, ya juu kabisa inatozwa na Zimbabwe 7% lakini wao wanatoza corporate 28%, nchi kama Canada na Australia mrabaha ni asilimia sifuri. Tunasema tunaibiwa, tunajua tunachoibiwa?

Sidhani ban ya kupeleka nje concentrate imetokana na kuibiwa. Nadhani ni kutaka kuwalazimisha Acacia kujenga mitambo ya kuchenjulia shaba ndani ya nchi kwa nia ya kuongeza ajira na wala siyo kwa nia ya kuzuia 'kuibiwa', kama wengi wanavyoropoka.
Ndugu yangu inaelekea Siasa zinakupeleka mahali pabaya. Kama ungekuwa umefanya utafiti usiokuwa na mawaa si ungegundua ukweli kuwa Acacia tangu wawekeze kwenye dhahabu hapa nchini hawajawahi kulipa CIT? Sasa kuna mantiki gani kuwa na ulichokiita tozo kubwa ya CIT (30%) wakati wala tozo hiyo hailipwi? Lakini iwapo ulifanya utafiti kweli si ungegundua kuwa Zambia inatoza CIT asilimia 35 kwa Shaba yake? Lakini si ungegundua kuwa GGM walianza kulipa CIT waka 2012? na Resolute Mining vilevile? Sasa hizo discouraging CIT payables yamelipa makampuni gani? Ndugu yangu unafunikwa/utafiti wako umefunikwa na mahaba ya Siasa za upande fulani.
 
Raisi wangu wa sasa hana hadaaa tishieni kufunga kama kawaida yenu ila hapa kazi tu wizi wizi hatutaki muwe smart. Magufuli akiwapa extension ya mda mtafungaaaa mgodi
 
Mkuu umejaribu kujenga Hoja na zinashawishi ila tatizo naloona kwenye hoja zako hakuna Namba, wewe unasema hatuibiwi, kwa nini kwa mfano usiweke namba kwa mfano walipata copper, fedha etc kwenye hayo mabaki kwa kiasi hiki?
Je unajua ni kiasi gani wanapata kwenye huo mchanga?
Wanaosema ni wataalamu tunaomba wasitumie njia za waganga wa jadi ( ubashiri) tunaomba namba,na mseme mtambo unaghalimu kiasi gani?
Kuna taarifa kwamba mtambo uliofungwa kwenye kiwanda cha vigae Mkuranga unaweza kuwa na uwezo wa kufanya hizo smelting mnazotuambia je ni kweli au sio kweli? maana wachina hawajatulia yawezekana tayari wana Technology nafuu ya kufanya huu uyeyushaji, tunaomba mtuambie ghalama zikoje za kuweka mtambo na sasa ni kiasi gani hao jamaa wanapata kwenye huo mchanga

Hii nchi ni kama ina watu waliolaaniwa. Mtu hajui hata 'a' kwenye madini, lakini anajua kuwa tunaibiwa. Tunaibiwa nini, hawezi kukuambia. Wengine ni watu mpaka wana degree za vyuo vikuu lakini hakuna walichokipata huko, nao wanarudi kuungana na wasio na elimu kabisa, kuwa gosipers.

Watanzania, vueni mioyo ya chuki, mioyo ya umaskini, mioyo ya wivu, mioyo ya ubinafsi. Jivikeni mioyo ya kutafuta elimu, kutafuta ufahamu na ukweli, kutokupenda kuropoka hata katika mambo ambayo hamna uelewa nayo, jivikeni mioyo ya kuutafuta utajiri. Kumchukia tajiri hakuwezi kukufanya wewe kuwa tajiri.

Nimefanya kazi mgodi wa Bulyanhulu tokea nafasi ya utafiti mpaka uzalishaji, nimeshiriki vikao vya management katika ngazi ya juu, nimefanya kwenye mgodi wa Golden Pride Nzega, nimefanya West Afrika na kushiriki vikao vingi vya management na vya kitaalam Afrika Kusini, Canada, Mali, Ghana, Liberia na hapa nchini, sijawahi kusikia hata kampuni moja ya kigeni tukiambiwa tutafute mbinu za kukwepa kulipa kodi. Ninachokumbuka kuna wakati President wa Barrick alieleza kuwa 'it is more profitable to work within the boundaries of the Law than outside'.

Mimi nasema Tanzania hakuna tunachoibiwa kwenye madini, kuibiwa zimekuwa ni fikra za kimaskini za kudhani kila mwenye maendeleo amekuibia.

Tanzania itapata hasara zaidi kwa wawekezaji kuondoka nchini kuliko hasara watakazopata wawekezaji. Na watu wasidhani kwamba jambo hili litakuwa kwa sekta ya madini tu bali itaenda kwenye sekta zote. Hakuna mwekezaji wa nje atakayeiamini Tanzania.

Leo hii uwekezaji katika utafiti wa madini nchini Tanzania umepungua sana. Kwenye utafiti, kwa wastani ni leseni moja tu huwa mgodi katika kila leseni 1000 zilizofanyiwa utafiti. Utafiti pekee yake, hata madini yasipopatikana, ni chanzo cha mapato. Leo makampuni yanafanya sana utafiti Kenya na Afrika Magharibi, yanaondoka Tanzania.

Kama tunadhani ni rahisi kujenga uchumi kwa kutegemea uwekezaji wa ndani tu, tukamwulize Mugabe.
 
Kwa hili bila soni namuunga mkono Maghufuli. Hii mikataba mibovu ilikuwa na 10percent za watu tena ndani ya system. Wafunge mazungumzo yafanyike upya

..too late.

..Magufuli alikuwepo serikalini wakati mikataba hiyo mibovu ikisainiwa.

..hakupinga wakati huo, anakuja kupinga miaka 10, 15, baadaye.

..dhahabu ya kanda ya ziwa ilitakiwa iwafaidishe wananchi wa kanda hiyo pamoja na Tz nzima kwa jumla.

..Magufuli, Chenge, Sitta, Kapuya, pamoja na viongozi wengine wa kanda hiyo wanapaswa kubeba mzigo wa lawama kwa hujuma na hasara iliyotokana na mikataba mibovu ya madini.

NB.

..wanaharakati kama Tundu Lissu waliipinga sana mikataba ya hovyo-hovyo iliyokuwa ikisainiwa lakini wabunge wa kanda ya ziwa hawakutoa ushirikiano wowote.
 
..too late.

..Magufuli alikuwepo serikalini wakati mikataba hiyo mibovu ikisainiwa.

..hakupinga wakati huo, anakuja kupinga miaka 10, 15, baadaye.

..dhahabu ya kanda ya ziwa ilitakiwa iwafaidishe wananchi wa kanda hiyo pamoja na Tz nzima kwa jumla.

..Magufuli, Chenge, Sitta, Kapuya, pamoja na viongozi wengine wa kanda hiyo wanapaswa kubeba mzigo wa lawama kwa hujuma na hasara iliyotokana na mikataba mibovu ya madini.

NB.

..wanaharakati kama Tundu Lissu waliipinga sana mikataba ya hovyo-hovyo iliyokuwa ikisainiwa lakini wabunge wa kanda ya ziwa hawakutoa ushirikiano wowote.
Ndo tunarekebisha sasa maumivu lazima tuyapate kwenye kila mabadiliko
 
Kazi ipo..ila wakuu wapo sawa
Hao jamaa hawauzi dhahabu kuendesha migod hyo bali wanategema hyo copper concentrate ku run daily production costs ikiwemo kulipa mishahara ya wafanyakazi.na hyo product sio main product kama mkataba wao unavyoelekeza,dhahabu inakwenda kuhifadhiwa nchi za watu.sasa unaweza kupata picha huo mchanga una thamani kias gani.hongera president
 
Safi mkuu kwel mikataba yao imejaa uporaji tu
Hii kusema hawapati kitu ni kuitia woga serikali tu mfano mzuri ni buzwagi gold mine huwa mara kwa mara wakiona husema wanafunga ila hawafungi nani anakubali ku run kwa hasara kama sio siasa tu
 
Kwa hili bila soni namuunga mkono Maghufuli. Hii mikataba mibovu ilikuwa na 10percent za watu tena ndani ya system. Wafunge mazungumzo yafanyike upya
Mikataba tulishaingia nao . Anae kataza leo alikuwa sehemu ya maamuzi. Ss ukiwakataza lzm watashitaki n tutashindwa n fidia kubwa tutalipa. Na hapo nchi itafilisika kabisa.
 
Mikataba tulishaingia nao . Anae kataza leo alikuwa sehemu ya maamuzi. Ss ukiwakataza lzm watashitaki n tutashindwa n fidia kubwa tutalipa. Na hapo nchi itafilisika kabisa.

Mikataba ya siri utajuaje kama ina kipengele kinachosema lazima waruhusiwe kuuza mchanga? Labda Rais ameiona hiyo mikataba na akaona haimzuii kukataza kuuza mchanga nje.

Ni vema kufahamu vile vile Rais atakuwa amepata ushauri toka kwa Waziri Muhongo ambaye amebobea kwenye haya mambo.

Msambichaka anasema Canada na Australia huwa hawadai mrahaba. Kampuni ni zao kwa nini wadai mrahaba?
 
Hivi wewe mining Industry unaifahamu au unaongea kishabiki.Mimi ndiyo professional yangu na huko West Africa siyo kwamba nimeongea kiushabiki.Nimefanya kazi kwenye mining Industries za Ghana,Senegal,Mali,Burkina Faso napafahamu vizuri.Ninaifahamu vizuri mining industry vizuri kuanzia kwenye booming ya 1990s.Rais wa Senegal Mack Sall ni Geologist by Professional nenda kaangalie anachokifanya nchini mwake kwenye mining.Ghana,Mali(achana na south afrika) wanatuzidi sana kwenye uzalishaji wa dhahabu Afrika.Tatizo wabongo ujuaji mwingi.Mimi nasema hatuibiwi tunakosa sera nzuri tu.Tusijidanganye Acacia na Anglo wakifunga migodi yao Uchumi utayumba hatari
Kwani wawekezaji wako peke yao dunia nzima?
 
Labda kama sielewi vizuri ila mimi ninavyojua waliomtangulia walisaini mikataba na haya makampuni tena ya kimataifa tutasikia serikali imeitwa kule uingereza kwenye mahakama ya biashara sidhani kama tuna mawakili wa kwenda huko kwani historia inaonyesha hatujawahi kushinda huko.
Mkataba hauhusishi mchanga hapelekwi mahakama yoyote
 
Mkuu, Tanzania tuna mazombie mengi mno! Ndo maana mengine yameng'ang'ania kutuongoza huku yana vyeti vya wizi! Eti kuna taahira jingine humu linasema tuna furnace za kuyeyusha huo mchanga, nabaki mdomo wazi ni lini hiyo mitambo ilijengwa hapa nchini? Kwa ufupi Rais wangu anakurupuka sana bila kupata ushauri kutoka kwa wadau wengine, anajifanya yeye ndo final say kumbe uelewa wake ni average sana na hana tofauti na mwananchi wa kawaida tu!! Wachumi wamshauri, wataalam wa madini wamshauri. Nashangaa Muhongo naye mtaalam wa madini madini lakini anabaki kuwa yes man tu!!
Kiwanda tunacho na rais hakurupuki period
 
Ni nini kisicho sawa? Watanzania wanaendeshwa kwa hisia. Niliwahi kufanya utafiti wa kodi zinazotozwa kwenye migodi ya Tanzania, nikalinganisha na mataifa mengine, sisi tupo kwenye kundi linalotoza kodi kubwa, japo siyo juu kushinda mataifa yote. Tunatoza corporate tax 30%, hakuna anayetoza zaidi ya hiyo lakini wapo wanaotoza pungufu. Tunatoza mrabaha 4%, ya juu kabisa inatozwa na Zimbabwe 7% lakini wao wanatoza corporate 28%, nchi kama Canada na Australia mrabaha ni asilimia sifuri. Tunasema tunaibiwa, tunajua tunachoibiwa?

Sidhani ban ya kupeleka nje concentrate imetokana na kuibiwa. Nadhani ni kutaka kuwalazimisha Acacia kujenga mitambo ya kuchenjulia shaba ndani ya nchi kwa nia ya kuongeza ajira na wala siyo kwa nia ya kuzuia 'kuibiwa', kama wengi wanavyoropoka.
Kwahiyo rais ni muongo kusema tunaibiwa? Je kikijengwa kiwanda cha kuchenjua mchanga watanzania wakapata ajira kuna ubaya? Japo tunacho kimoja tayari mkuranga
 
Tuliache liongoze linavyotaka, lakini mwisho wa siku atakuwa mdogo kuliko hata piriton! Anafikri wawekezaji wanajipelekea tu huo mchanga bila makubaliano? Wacha tuone. Tatizo naye anafanyiakazi hata habari za mitaani kwenye vijiwe vya wanywa kahawa na wabrash viatu! Akisikia wananchi wanaongelea habari za mchanga kusafirishwa naye anakuja kuropoka huku kwamba tunaibiwa sana! Unaibiwa nini? Mbona hujapiga marufuku ndege zinazotua ngorongoro na kuondokea huko huko bila ukaguzi?
Kwahiyo akipiga marufuku ndege ngorongoro ndio inaleta uhalali wa kuzuia mchanga? Amefuata malalamiko ya wananchi vijiwe vya kahawa. Je wananchi ni waongo asilimia 100? Hao ni wananchi wa nchi gani? Mbona swala la mchanga limeongelewa sana na wanasiasa hasa wa upinzani nao ni waongo?
 
Back
Top Bottom