Migiro (for Presidency 2015) na Tibaijuka (Uwaziri Mkuu 2010) Wanatosha Kuitakasa CC

Tatizo la siasa zetu ni za "personality cult", tunaweka rehani future ya watu million 40 na kitu kwa mtu fulani! Yaliyotupata na serikali hii JK bado haijatufundsha! Jirani zetu Kenya, ambo matatizo yao yalikua makubwa zaidi wameanza kufunguka macho. Sasa wako kwenye mchakato ulionza na katiba mpya na unaendelea na kujenga "institutions" au taasisi ambazo zitawahakikishia utawala bora! Mfano ni process ya kumpata jaji mkuu imefanywa kwa umakini mkubwa na sasa wanendelea na taasisi nyingine! Sisi bado tunajadili watu, oh Migiro! Watanzania! Kikubwa sasa ni Katiba Mpya, amabayo Itatuhakikishia Uchaguzi huru na wa haki, Bunge Huru na lenye standard, Serikali inayoweza kuwajibishwa, Mahakama Huru... Tubdilike tupigania katiba mpya na uundwaji wa taasisi madhubuti! Obama alitupa waafrika ushauri wa maana sana. Ninamnukuu katika tafsiri: Afrika haiitaji strong men, Afrika inahitaji taasisi madhubuti! Miaka 50 ya Uhuru tusirudie makosa tujifunze kutokana na makosa!
 
Nashukuru hii hoja imeletwa hapa Jamvini. Mazungumzo yanyoendelea sasa hivi kwenye corridor za wakubwa ni kwamba kuna watu wangetaka huyu mwanamama agombee 2015. Nadhani wengi wenu mtakuwa mmeshughudia kuja kuja kwake hapa nyumbani (pengine kwa mapumziko) ila kila akija anakutana na wanasiasa. Week iliyopita alikuwa Zanzibar anajenga mtandao kwa upande huo. Na mbinu kubwa inayotumiwa (naomba kusisitiza hapa) ni kwamba watamnadi kama MWANAMKE!. Kwa sasa hivi wanaandaa maneno mazuri ya kulainisha watanzania kuwa ni zamu ya mwanamke, na UWT ikiongozwa na Mama Sophia Simba ndio watakuwa wapuliza vuvuzela.

Binafsi sina shida kuwa na Rais mwanamke na ningefurahi sana kama hili lingetokea. Wasiwasi wangu uko kwenye hoja kwamba tuchague mtu kwa sababu ya JINSIA yake! Tukumbuke tayari tumeshapewa 'mwanamke' badala ya Spika. Mama Makinda alinadiwa kwa sifa hiyo moja tu na hakushindanishwa na wanawake wengine ndani ya ccm badala yake waliongea na waombaji wengine kiaina kama Jenista Mhagama, Anne Kilango ili wajitoe kwenye kinyang'anyiro. Hivi Watanzania tumepata nafuu gani kwa kuwa na Spika mwanamke? Kuna tofauti gani ndani ya bunge letu tofauti na kipindi cha uongozi wa mwanaume e.g Sitta?

Maslahi ya wanawake
Given what Tanzania is going through, (natafsiri) kwa jinsi mambo yanavyoenda hapa Tanzania, pamoja na changamoto tulizonazo kama Taifa tutakosea sana tena sana kuchagua kiongozi kwa sababu tu ni wa jinsia fulani! Dr Migiro alishashika wadhifa serikalini na atakuwa na maswali ya kujibu. Kwa mfano alipokuwa anaongoza wizara inayoshughulika na watoto alifanya nini kuondoa tatizo la watoto wa barabarani? Na hii jinsia ya kike wanayoandaa kumnadia, je alinusuru wanawake wangapi toka kwenye 'domestic violence"'? Alifunga wanaume wangapi waliobaka wasichana wadogo wa shule na/ama kulawiti wavulana wadogo? Aliwasaidiaje watoto wa kike wanaopata mimba wakiwa shuleni ili waendelee na masomo? (au ni viherehere?). Kwa ujumla wanawake wa Tanzania walipata nafuu gani wakati Dr Migiro akiwa waziri wao tofauti na sasa?

Kwenye utawala bora
Dr Migiro anatakiwa ajibu, anaamini kuwa Tanzania kuna ufisadi? Hilo tu.
 
ni rekodi gani ya kiuongozi ambayo mleta mada unadhani yeye anawazidi wenzake ktk magamba kuweza kuchaguliwa kuwa mgombea urais kwa chama chako?
 
unajua watu ambao ni jamii ya ff na fikra zao za kimagamba wanafikiria juu juu sana.hawapendi kujishughulisha na kuchimbua ukweli halisi.wamesahau kuwa hata waliomnadi jk walikuja hivo,mara oh anatabasamu,handsom,anackiliza watu! Baada ya kugeukana wao wenyewe ndo wanakuja na kutuambi el anaweza kuchukua maamuzi magumu,.ukiuliza yapi? Utackia,ya kuleta rich..mond.-sasa hiv wanaleta sera ya mwanamke ili wamtumie kutuibia. Kumbuken watanzania akili zao zinabadilika,wale wa enzi za nyerere 4 yrz to com watakuwa wamepungua sana!
 
unajaribu kusemakuwa tibaijuka hana sifa hata moja ya uongozi sio?
Nitajie sifa moja aliyo nayo hadi aonekane anafaa kuwa Raisi.
Kama Waziri amepigania kitu gani na kupata mafanikio gani ?
Kama hakufanikiwa kwa sababu zozote zile amewajibika vipi ?

Tanzania tuache huu utamaduni wa kummwagia sifa kiongozi hata pale ambapo ameonesha udhaifu katika kutoa maamuzi mazito.
Kama amekwamishwa kwa kuwekewa mizengwe kiutekelezaji lakini akaendelea na nyadhifa zake, huo ni unafiki na hatufai.
Kiongozi bora huwezi kusimamia kile usichokiamini au ambacho unachoona si haki, hapo utakuwa bora kiongozi na hutufai.
Nyota anayoanza nayo kiongozi toka mwanzo haitakiwi kufifia siku zinavyokwenda, hizo ni nguvu za soda na hivyo hatufai.
 
unajua watu ambao ni jamii ya ff na fikra zao za kimagamba wanafikiria juu juu sana.hawapendi kujishughulisha na kuchimbua ukweli halisi.wamesahau kuwa hata waliomnadi jk walikuja hivo,mara oh anatabasamu,handsom,anackiliza watu! Baada ya kugeukana wao wenyewe ndo wanakuja na kutuambi el anaweza kuchukua maamuzi magumu,.ukiuliza yapi? Utackia,ya kuleta rich..mond.-sasa hiv wanaleta sera ya mwanamke ili wamtumie kutuibia. Kumbuken watanzania akili zao zinabadilika,wale wa enzi za nyerere 4 yrz to com watakuwa wamepungua sana!
Nakubaliana na kauli yako ila tu ile sentenso ya mwisho. Usitutakie tupungue sana 4yrz to com sisi tuliokuwepo enzi za Nyerere. Tutabanana hapo hapo.
 
....
Tanzania tuache huu utamaduni wa kummwagia sifa kiongozi hata pale ambapo ameonesha udhaifu katika kutoa maamuzi mazito.
Kama amekwamishwa kwa kuwekewa mizengwe kiutekelezaji lakini akaendelea na nyadhifa zake, huo ni unafiki na hatufai.
Kiongozi bora huwezi kusimamia kile usichokiamini au ambacho unachoona si haki, hapo utakuwa bora kiongozi na hutufai.
Nyota anayoanza nayo kiongozi toka mwanzo haitakiwi kufifia siku zinavyokwenda, hizo ni nguvu za soda na hivyo hatufai.
Kwa vigezo vya vipimo hivyo, ni yupi labda katika duru la viongozi tulionao (au raia yeyote) unaedhani anafaa?
 
Kwa vigezo vya vipimo hivyo, ni yupi labda katika duru la viongozi tulionao (au raia yeyote) unaedhani anafaa?
Kwanza tukubaliane ni Tanzania ya aina gani tunayoitaka halafu ndio tuanze kupima ni nani ambaye anaonekana ana ari (determination) ya kutufikisha huko. Tunataka kiongozi anayechukia rushwa. Na kama alivyosema Mwalimu, aonekane kabisa kuwa anachukia rushwa na atachukua hatua kadri ya uwezo wake kupambana na rushwa. Tunataka kiongozi atakayeonyesha dhahiri kuwa anajali adha zinazowakumba Watanzania na amejitolea kwa kadri ya uwezo wake kupambana na adha hizo. Tunataka kiongozi atakayeonyesha kuwa amepania kuwashirikisha kikamilifu raia wa Tanzania katika uwekezaji na utumiaji (exploitatiion) wa maliasili zao kwa manufaa yao, na wawekezaji watakaokuja waje kwa manufaa ya Tanzania.
 
ufisadi na CCM damudamu, hawezi kua rais sababu hataweza ponda uongozi wa Kikwete ambao naamini watu wengi wameutilia shaka.
 
Nimejaribu kukitafakari chama cha magamba nikaona kwa sasa hali yao ni ngumu sana kwenye kupata mtu wa kumsimamisha 2015. Je mnadhani kuwa Dr. Migiro (wa UN) anaweza kuja kusimamishwa kugombea urais kwa CCM? Je ataweza kusimama na Dr. Slaa?

N'tahamia Somalia
 
Kwa sasa sina imani na mtu yeyote anayetoka ccm. Hata Dr. Slaa akihamia ccm sitampigia kura kamwe. Ccm ni sumu kali inayoua uzalendo na fikra sahihi za kuikomboa nchi hii kiuchumi. Inawezekana sumu yenyewe ipo ndani ya kadi kwamba ukikabidhiwa kadi na kuiweka mfukoni au hand bag basi sumu inafanya kazi yake. Watanzania tuachane na huyu mdudu anayeitwa ccm.
 
Sidhani kama Katiba ya sasa itamruhusu Dr. Migiro kusimama kuwa Rais. Katiba inasema kuwa mtu kugombea Urais ni lazima awe ameishi Tanzania kwa miaka mitano mfulilizo iliyopita. Dr. Migiro amekuwa akifanya kazi huko New York toka 2007 na nafikiri ataendelea hadi 2015. Hata kama akijiuzulu kazi yake sasa [2011] mpaka ifikapo 2015 hatakuwa na hiyo miaka mitano mfulilizo unless Katiba inabadilishwa na kifungu hiki kufutwa.
 
Sidhani kama Katiba ya sasa itamruhusu Dr. Migiro kusimama kuwa Rais. Katiba inasema kuwa mtu kugombea Urais ni lazima awe ameishi Tanzania kwa miaka mitano mfulilizo iliyopita. Dr. Migiro amekuwa akifanya kazi huko New York toka 2007 na nafikiri ataendelea hadi 2015. Hata kama akijiuzulu kazi yake sasa [2011] mpaka ifikapo 2015 hatakuwa na hiyo miaka mitano mfulilizo unless Katiba inabadilishwa na kifungu hiki kufutwa.
Aliyeko nje ya nchi kwaajili ya kuiwakilisha nchi ubalozini, AU ama UN anakuwa exempted. Kwa hiyo bado anaruhusiwa kugombea kisheria
 
Yanni hadi leo na matatizo yaliyojaa nchini bado unataka ccm yako iongoze tena?

Weye fisa nini au unakula nao hawa wanaokula haki za wananchi?
 
Yanni hadi leo na matatizo yaliyojaa nchini bado unataka ccm yako iongoze tena?

Weye fisa nini au unakula nao hawa wanaokula haki za wananchi?
Results za uchaguzi mdogo wa huko igunga ndio zitatoa ishara ya picha halisi ya matokeo ya uchaguzi wa 2015
 
Hapati kitu, target yao magamba ni misaada toka nje, wanataka ku'use advantage ya umaarufu wa migiro kupata misaada!
 
Back
Top Bottom