Mifuko ya jamii yaonywa kuhusu ujenzi wa viwanda

Cannabis

JF-Expert Member
Jan 20, 2014
8,937
25,279
kiwanda.jpg


Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru amesema kabla mifuko ya hifadhi ya jamii haijaanza kujenga viwanda, wataalamu wanapaswa kutengeneza mpango mkakati ili kutoathiri malipo kwa wanachama.

Mafuru alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kutoa tuzo za Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE), akifafanua mapendekezo ya Rais John Magufuli kwa mifuko hiyo kuacha kujielekeza kwenye ujenzi wa majengo, badala yake ifanye hivyo kwa viwanda.

Akizindua jengo la PPF Mjini Arusha Mei, Rais Magufuli aliwataka viongozi na wataalamu wa mifuko hiyo kuanza kujenga viwanda ambavyo vitakuwa na manufaa kwa Watanzania hasa ajira kwa vijana.

Muda mfupi baada ya pendekezo hilo, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulitoa mkopo wa Dola 2.1 milioni za Marekani kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa kiwanda cha viuatilifu Kibaha mkoani Pwani. Kiwanda hicho kinamilikiwa na Shirika la Maendeleo Taifa (NDC).


Chanzo: Mwananchi
 
Enzi za Vasco,huu ushauri ungetolewa bila kupepesa macho.....and straight to point.Ila sasa,lazima kwanza ununue kamusi/dictionary,kisha usome vizuri ''katiba'' na ''mood'' ya ''mtukufu.Baadae unawasilisha kwanza kwa maandishi,ndio unayatoa hadharani.................:D:D..hiki ni kibwagizo tu..
 
Ni kweli wawe makini na hizo hela maana mwisho wa siku ni maumivu kwa wanachama.
 
kama nilivyosema mtakubali tu,maneno yangu pale niliposema miaka hii mitano itaisha kwa kusikia na kuona mambo mengi ya ajabu hasa kutoka kwa watu tuliokuwa tunawategemea kutuletea maendeleo
 
Ushauri wa ovyo kabisa kwani viwanda vitajengwaje?Mafuru anatumika na mafisadi anamuhujumu raisi wetu kipenzi
 
Back
Top Bottom