amatolo
JF-Expert Member
- Jul 24, 2017
- 690
- 711
Kuna tetesi nmezipata mahali ingawa sijathibitisha kama ni kweli. Jumomosi nilikuwa nmekaa na mchumi mmoja mahali fulani(jina la sehemu na mhusika nahifadhi).
Inasemekana bwana mkubwa amepanga kuunganisha kama sio kuvunja mashirika yote ya hifadhi ya jamii na kubakiza moja la serikali na moja la binafsi, pia inasemekana wakurugenzi wa haya mashirika yote ya hifadhi walishaitwa na kupewa huo utaratibu na kuambiwa kuwa hiyo ni amri na ole wao waje kulopoka huku mtaani.
Watumishi wote wa serikali watalazimika kuhifadhi fedha zao kwenye mfuko wa hifadhi wa serikali(ni lazima) na watumishi wa sekta binafsi wanaweza kuchagua ni mfuko gani wahifadhi hela zao.
Kuna miradi iliyokuwa inatekelezwa na mashirika hayo miingine inaonekana kusimama, mkulu kasema hata serikali inaweza kuiendesha. Kama ni kweli hili swala linaweza kuathiri uchumi?
Inasemekana bwana mkubwa amepanga kuunganisha kama sio kuvunja mashirika yote ya hifadhi ya jamii na kubakiza moja la serikali na moja la binafsi, pia inasemekana wakurugenzi wa haya mashirika yote ya hifadhi walishaitwa na kupewa huo utaratibu na kuambiwa kuwa hiyo ni amri na ole wao waje kulopoka huku mtaani.
Watumishi wote wa serikali watalazimika kuhifadhi fedha zao kwenye mfuko wa hifadhi wa serikali(ni lazima) na watumishi wa sekta binafsi wanaweza kuchagua ni mfuko gani wahifadhi hela zao.
Kuna miradi iliyokuwa inatekelezwa na mashirika hayo miingine inaonekana kusimama, mkulu kasema hata serikali inaweza kuiendesha. Kama ni kweli hili swala linaweza kuathiri uchumi?