Microsoft starts biting in DAR!

LazyDog

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
2,473
189
Got this from eThinkTankTz

Copyright infringement lands technician in the dock

A TECHNICIAN with Sunrise Computers, Msabaha Salu (26), was on Thursday brought to the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar es Salaam where he was chred with infringement of copyright law. Assistant Inspector of Police Edwin Boniface alleged before Principal Resident Magistrate Sivangilwa Mwangesi that on April 11, this year, at Sunrise Computers along Uhuru Street in the city, the accused did infringe on a commercial basis copyright of Microsoft Corporation by selling a computer with serial number 02745835 to Wakianda Michael that contained pirated Windows Professional 2002 edition.

In the second count it was alleged that on the same date and place the accused was found with a clone computer with serial number NE8527A5M which contained a pirated Microsoft Office 2003 edition, copyright works of Microsoft Corporation. It was further alleged that on the same day and place, the accused was found with a Dell computer with’ serial number 065891 which contained a pirated Microsoft Office 2003 edition. The accused pleaded not guilty to the charge and the court adjourned the case to April 30, this year, for another mention. Meanwhile, another businessman, Jabir Bhimji (33), was arraigned in the same court for infringement of copyright.

Assistant Inspector of Police Edwin Boniface alleged in court that on March 19, this year, at Q-Print Ltd situated along Samora Avenue in the city, the accused did willfully and on a commercial basis infringe he copyright words of Microsoft Corporation by selling a counterfeit Microsoft Windows Professional installation disk. The disk, with serial number 00089-181-570-538 and product keys K46V7-8Q9YZ- WTFT4-RTWG89C9B, was allegedly sold to Michael Berenju by the accused.

The accused pleaded not guilty to the charge. The case comes p for mention on April 30, this year.
By Correspondent Rosemary Mirondo- The Guardian 21st April 2008
 
Tukiendelea na mwendo huu wa Microsoft, nadhani wasanii na watunzi wa vitabu Tanzania watakuwa na maisha mema, kwani wamekuwa wakilia sana kwamba kazi zao zinaibwa kupita kiasi.

Makosa na lawama zote tubebe sie raia kwa kutowasaidia COSOTA na polisi kufichua maovu haya ya wizi wa kazi hizi!
 
HAPO MWANZO NILIWAHI KUANDIKA SOFTWARE PIRACY -- SAFARI IMEANZA WABONGO HAWANA MACHO HAWAKUJUA MAKALA ILE NA WAKATI ULE
 
Askari wa kwetu wakilipata hili, basi ulaji kwao nje nje.

Makosa na lawama zote tubebe sie raia kwa kutowasaidia COSOTA na polisi kufichua maovu haya ya wizi wa kazi hizi!

Kwa kweli hapa kuna utata. Kazi ya kuwakamata wahalifu wa Haki Miliki si ya COSOTA wala polisi; hii ni kazi ya mmiliki wa Haki Miliki. COSOTA ni mashahidi tu km mmiliki aliweka rekodi ya kazi yake itakiwavyo. Hata hawa COSOTA wenyewe hawajui kuwa wao si "polisi" wa wahalifu hao.

Kingine ni kuwa, waandishi, wasanii, n.k. hawajui ni vipi wajiwekee rekodi za kazi zao, ambazo zinaweza kutumika km ushahidi.
 
Kazi kweli kweli... Sijui watazinasa kampuni ngapi kwa Bongo?

Almost kila kampuni, sema tofauti itakuwa ni aina ya software iliyomo katika pc zao. Softwares za wizi hapa bongo ni kila mahali.
 
Mimi nahisi kwamba hawa jamaa wana access na hizo packages zote za windows na office na wanachofanza ni kuzi-copy na kuzi-install katika computers za watu wengine.

Kwa hio biashara hio ambayo hata huku Cyber Village ni kubwa katika magulio mbalimbali, ina matatizo yake ikiwa mnunuzi ana ufahamu na mambo ya computers na inabidi aulize uhalali wa hizo software packages.

Hata kama unapata pirate package kwa mfano ya windows operating system, inapo-install kwa mara ya kwanza na unapomaliza installation yenyewe itataka kwenda katika internet ku-register au itakuuliza kama unapenda kutumia simu ya kawaida kufanza hio registration.

Sasa siku hizi microsoft wana kitu kinaitwa Windows Genuine Advantage, program ambayo kazi yake ni kuhakikisha kwamba mteja halali alie na product yao anafaidika na msaada wowote kama live security updates na mengine kwa kui-validate hio software.

Sasa kama mtu ana ufahamu wa mambo haya akiunganisha computer katika internet na unapotaka ku-validate iwe office au windows operating system microsoft watakwambia kwamba product yake ni halali au sio halali.

Kwa hio kuzidi kuelimika kwa wateja kwamba kuna pirate packages au so ndio kuzidi kupata watu wengi wenye computer zenye kuleta performance inayotakiwa.

Shukran.
 
Microsoft abused monopoly power in its handling of operating system sales

Microsoft was blocking its competitors out of the market through anti-competitive practice

Kazi kweli kweli... Sijui watazinasa kampuni ngapi kwa Bongo?

Almost kila kampuni, sema tofauti itakuwa ni aina ya software iliyomo katika pc zao. Softwares za wizi hapa bongo ni kila mahali.

Most commercially exploited proprietary software is developed in the United States, Japan and Europe, hence for those located in economically disadvantaged economies it can be prohibitively expensive to pay for all the end user licenses for those products rather than to purchase just one license and then copy the software without paying any additional licensing fees. Some critics in the developing countries of the world see this as an indirect technology transfer tax on their country preventing technological advancement and they use this type of argument when refusing to accept the copyright laws that are in force in most technologically advanced countries. This idea is often applied to patent laws as well.

Mere possession of unauthorized copy could be a ground for an offense depending on provisions of existing laws of a country.

SOURCE
 
Tukiendelea na mwendo huu wa Microsoft, nadhani wasanii na watunzi wa vitabu Tanzania watakuwa na maisha mema, kwani wamekuwa wakilia sana kwamba kazi zao zinaibwa kupita kiasi.

..point is lazima mtu amshitaki mtu kwamba anamwibia!

..halafu unayeshitaki lazima uwe na kajisenti ka kuhangaika kukusanya huo ushahidi.

..sio kazi rahisi,inabidi uwe umepania!

Makosa na lawama zote tubebe sie raia kwa kutowasaidia COSOTA na polisi kufichua maovu haya ya wizi wa kazi hizi!

..idimi,

..wewe hauna hata kitu kimoja ambacho kimegushiwa au kuibwa copy?

..kwa mfano,huyo aliyekamatwa itakuwa mambo ya kuchomana tu kwa sababu fulani fulani.

..ofisi ngapi bongo zinatumia pirated software? unataka kusema hivi viduka vya secretarial services vina registered softwares?na wanalipia licence?

..ni kwavile tuna uchumi mdogo ambao sehemu yake ndogo ndo iko mainstream,hivyo hatuwezi kuripoti chochote kuhusu haya!

..halafu ni utamaduni wetu kupenda na kutumia vya bure! bisha!
 
Mimi kwa mtazamo wangu ni kuwa kwa sisi nchi tunazoendelea Pirate ni kitu cha lazima mno kama kula,Unajua hizi nchi zilizoendelea huwa wanatutia ujinga sana nitaelezea kiufundi zaidi.

Kutokana na Maslow's motivation model,yeye anasema binadamu huwa na stages zinazoathili maamuzi yake na hutokana na level ya motivation aliyopo,kwa mfano kitu basic ni kula,kunywa na kulala(hapa chakula atakula ugali na dagaa,atavaa mitumba na atalala kwenye Banko) then binadamu uhakikisha hii stage imekidhi matakwa yake baada kuanza kula mapochopocho,kulala kwenye nyumba nzuri.. then mtu akilizika huanza kufukiria usafiri na mlinzi wa kimasai then huendeleaa kufikiria kuwa na mchumba mzuri....mpaka mwisho huanza kufikiria masuala ya Ubora wa mazingira.Sasa kwetu sisi kutokana na kuwa chini kitechnolojia sisi kwa sasa mtu anachotakiwa ni kupata Computer yenye OS no matter ni feki au la ili mradi inafanya kazi za kawaida(Hapa nawaondoa wale waliopita hii stage,wenye makampuni makubwa nk) then huko baadaye tukifika huo muda tutaanza kucare kuhusu pirate.

Serikali nayo iwe wajanja kwani nakumbuka China unanunua OS kwa Ghilingi 680/= ya kitanzania chini ya hata dola moja na software karibu zote zinapatikana Online Bureeeeeeeeeeeee ikiwemo na hizo Windows,linux,mac...wewe kwako kazi ni kuwa na enternet tu ambayo ni kama bure. Hawa microsoft huwa wanapiga biti sana na serikali huwa wanafanya msako wa zuga toto kwa siku kama mbili wanaonesha kwenye TV kuwa wamekamata DVD kibao feki then Myeupe inalizika na vijana wa njano baada ya muda kazi ileile.

Sasa hii inawasaidia kuwa hata watoto wa darasa la saba anakuwa na knowledge ya vitu vingi.Hapa unaweza kuonana na mzee ambaye hata kusoma hajui anakukuuliza unataka Windows? anatoa pochi kuna misoftware kibwena.

La muhimu ni kuwa wananchi waelimishwe ili isije watu wakawa wanauza hizo software kwa bei ya original kumbe ni fake,sasa hapo ni maumivu kwa watu wetu.

Ni matazamo tu jamani
 
..point is lazima mtu amshitaki mtu kwamba anamwibia!

..halafu unayeshitaki lazima uwe na kajisenti ka kuhangaika kukusanya huo ushahidi.

..sio kazi rahisi,inabidi uwe umepania!



..idimi,

..wewe hauna hata kitu kimoja ambacho kimegushiwa au kuibwa copy?

..kwa mfano,huyo aliyekamatwa itakuwa mambo ya kuchomana tu kwa sababu fulani fulani.

..ofisi ngapi bongo zinatumia pirated software? unataka kusema hivi viduka vya secretarial services vina registered softwares?na wanalipia licence?

..ni kwavile tuna uchumi mdogo ambao sehemu yake ndogo ndo iko mainstream,hivyo hatuwezi kuripoti chochote kuhusu haya!
..halafu ni utamaduni wetu kupenda na kutumia vya bure! bisha!



Mkuu Dar SI Lamu,
Kosa haliwezi kuhalalisha kosa jingine!
Najua tuna bidhaa nyingi sana ambazo si halisi lakini hatuwezi kukaa kimya, lazima tuseme. Ni ofisi nyingi sana bongo, nyingine ni za serikali, zinazotumia kazi hizi za wizi (pirated softwares).
Tatizo la kiuchumi, kama wengi walivyosema hapo juu ndio haswa chanzo cha watu kununua kazi zisizo halisi. Kwa mfano mie mwenyewe nilikuwa natafuta software fulani ya kuchorea michoro, nikakuta bei yake ni dola 4000 za Kimarekani!Sikuinunua kwa sababu sina pesa hizo na siwezi kununua kazi za wizi.
Sasa kwa mazingira ya Tanzania, ni mtu gani binafsi anayeweza kununua software kwa bei hiyo!
Lakini pamoja na hayo, siwezi kushabikia wizi!
 
“Don’t tell them that I love it” - Christopher Dawson

It is about Ubuntu 8.04

Christopher Dawson said:
From my perspective, however, it makes sense to give students an OS that is not only free, but largely malware-free and now so user-friendly as to be an easy Windows substitute. If you don’t have applications that demand one platform over another, the ongoing evolution of Linux (especially *buntu) makes Windows a tougher sell every day, especially during further recession-induced budget cuts.



Pjotr said:
My own kids do prefer Linux (don't *love* it either, but prefer it) over Windows. But then I presented them with a neatly finished and polished installation. Just like you did with Hardy.

Tip: wait with deployment of Hardy on a large scale in your school, until the release of 8.04.1 on July 3rd. Although Hardy is pretty good already, there are some minor issues still.

For example: Firefox 3 shows, at intervals, high CPU usage and hard disk activity. I myself have switched temporarily to Epiphany for that reason. By the way: Epiphany automatically uses the same plugins that you have already installed for Firefox, because it's also Mozilla-based.

Soma zaidi different views za wachangiaji wengine kwenye link hapo juu.
 
Hawa watanzania bwana! Hivi mnaonaje tukiongelea hali halisi ya hao wateja wa hizo software kwanza? najua wengi kati ya tutakaounga mkono hizo kamata kamata ni sisi maprograma tunaotegemea kuibiwa hivi karibuni! thas fine, but vipi pale tulipokuwa pale chuo? Wangapi tuliweza kununua hizo kompyuta achilia mbali hizo maikronini sijui! mbona ilikuwa bila mkopo hakuna kinachoenda?
Kama kuna mtu anayeota kuwa hii nchi teknolojia yake imekuwa kwa kiwango hicho cha watu kuona wenyewe umuhimu wa kununua hizo software,basi ile nchi siyo hii.Unaweza usielewe lakini mimi najua kuwa kwa watanzania wengi bado maisha ni ya kuunga sana in such a way kujigharimia mahitaji ya msingi (sustainance needs) bado ni tatizo! Sasa tell me guys jinsi ambavyo mtu aliyetoka nyumbani bila kunywa chai anavyoweza kukumbuka kununua software wakati huenda na mchana anapiga dash...Usiniambie hapigi,kwani ni kwa nini aspige wakati amefika ofisini na umeme wamekata? Huyu mwenzetu ndo ana steshenari sasa! Hajashinda njaa huyu?
Sasa haya mambo ni mengi na hawa watu ni wengi. Labda kama wote tunaoongea tumetoka hotpot family. Ila kwa waTZ wa kawaida wataelewa fasta. So kwa nchi kama hii yenye watu kama hawa hata hizo kompyuta wanatumia basi tu kwamba ndiyo kitendea kazi kinacholazimu kutumika.
At mean time mimi nadhani kuna haja ya kuelekeza nguvu kwenye maswala ya msingi zaidi(sisemi hili siyo la msingi) yanayofanya uchumi wa hawa watu uwe duni hivyo. Wakishapona njaa then tuje kuwaelimisha umuhimu wa kupata software halali. Ningefurahi sana kama (ingawa haiwezi kuwa) kwa sasa watumiaju wa aina hii wasingechukuliwa kama wezi wa software ila wahesabike kwenye makundi ya maskini wasiojikimu ambao software hizo zimesaidia angalau wasogeze mbele siku zao chche za dhiki zilizowasalia kwenye dunia hii ya mola!.........Kama vile ungeingia kwenye shamba lolote ukachimba muhogo ukatafuna kwa sababu umezidiwa kabisa na njaa.! Sidhani kama mwenye shamba akikukuta akauliza ukamweleza eti hatakuelewa....Haiwezekani awe amezaliwa....
No offece!
 
Hivyo ni visa vya kibiashara kati teana kati ya watu binafisi Microsoft has nothing to do

Kwanza Polisi wanajuaje kuwa MIcrsoft fulani ni pirated au wamejuaje windows tena 2002 amabyo ilikuwa haina mambo ya WGA kuwa ni pirated.


Sio mwanasheria lakini ningekuwa nina uwezo ningependa niwe mtetezi wa huyo jamaaa nione. teh teh teh
 

Mkuu Dar SI Lamu,
Kosa haliwezi kuhalalisha kosa jingine!
Najua tuna bidhaa nyingi sana ambazo si halisi lakini hatuwezi kukaa kimya, lazima tuseme. Ni ofisi nyingi sana bongo, nyingine ni za serikali, zinazotumia kazi hizi za wizi (pirated softwares).
Tatizo la kiuchumi, kama wengi walivyosema hapo juu ndio haswa chanzo cha watu kununua kazi zisizo halisi. Kwa mfano mie mwenyewe nilikuwa natafuta software fulani ya kuchorea michoro, nikakuta bei yake ni dola 4000 za Kimarekani!Sikuinunua kwa sababu sina pesa hizo na siwezi kununua kazi za wizi.
Sasa kwa mazingira ya Tanzania, ni mtu gani binafsi anayeweza kununua software kwa bei hiyo!
Lakini pamoja na hayo, siwezi kushabikia wizi!

Mkuu l Nitatofautiana na wewe kidogo . Unajua China inaendelea sababu ya kazi za wizi.? Tujiulize
  • Wizi huo unaumiza watazanzania wangapi?
  • Wizi huo unatengeneza ajira halali ngapi?
CHina kuna vyuo wanafunidhsa how to break the law technologicaly na kuongeza ubunifu na kurahisiha mambo. Nilisikiliza kipindi kimoja proffesor mmoja youtube anasema ukiwa nyuma sana kimanedelo huwezi kuendela kwa kufuata rules zilizoweka na mataifa yaliondolea . Utabakia kuwa end user tu.

Ni sababu ya mambo hayo ya piracy china ndio maana hata makampuni yanalazimika kufungua matawi china sababu ukifungua tawi china basi serikali inakuwa beneti kuzuia bidhaa pirated. Kama huna tawi mean huna faida kwa wachina wanapirate wanakuwa na faida zaidi. yaani kuna very goo % ya manedelo ya china yalinzishwa na piracy . Wangekalia usamaria ndio wangekuwa kama sisi hadi leo hii.

So sometime Kucheza ngoma tu bila kujua kama taifa inatunufaishaje ni tatizo. Sasabu wamarekani wana sheria kali za piracy na na ugaidi basi na sisi tunaiga . Tanzania bana

Sisi tanzania tatizo ni letu ni Ufisadi . Piracy na ugaidi ni vitu vya mwisho kabisa.

Akitoea mbunifu akatengenza fuel filter za toyota .amevunja sheria akamatwe apelekwe jela. Wakatai toyota hawafungui japo kiwanda cha seat cover wala kutoa mafuzo w amafundi japo 20 kila mwaka . yaani Serikali inatakiwa iwasaidie watu kama hao kujifanya kama haioni. Ndio China wanafanya hivyo Unazuia CD feki ya Tanzania alafu urahusu za china sbababu tu zina lable feki ya genuine . teh teh teh

HAPO MWANZO NILIWAHI KUANDIKA SOFTWARE PIRACY -- SAFARI IMEANZA WABONGO HAWANA MACHO HAWAKUJUA MAKALA ILE NA WAKATI ULE

Shy bana ebu tuambie wewe kompyuta yako gharama ya OS pamoja na software zote ulizonano ni shilingi ngapi?

Any home user shoud nver think buying a software. Mm mtu akitaa msaada nampa pirated nikimua kucmahage namcharge muda wangu wa kazi tu sio software na namwambia nimekuwekea hiyo bure kama anataka kununua namuonyesha website.

teh teh teh
 
Sasa hii itakuwa ni balaa mimi nishawahi kuongea kuhusu hichi kitu eti mtu uwe na original os,utaipata wapi,wakati copy moja ya windows 7 premium mlimani city inauzwa dola 450 na wewe una kompyuta 10 unataka ufunge si mtaji wote utaishia kwenye hizo sijui original copy za windows os?
 
Mimi nahisi kwamba hawa jamaa wana access na hizo packages zote za windows na office na wanachofanza ni kuzi-copy na kuzi-install katika computers za watu wengine.

Kwa hio biashara hio ambayo hata huku Cyber Village ni kubwa katika magulio mbalimbali, ina matatizo yake ikiwa mnunuzi ana ufahamu na mambo ya computers na inabidi aulize uhalali wa hizo software packages.

Hata kama unapata pirate package kwa mfano ya windows operating system, inapo-install kwa mara ya kwanza na unapomaliza installation yenyewe itataka kwenda katika internet ku-register au itakuuliza kama unapenda kutumia simu ya kawaida kufanza hio registration.

Sasa siku hizi microsoft wana kitu kinaitwa Windows Genuine Advantage, program ambayo kazi yake ni kuhakikisha kwamba mteja halali alie na product yao anafaidika na msaada wowote kama live security updates na mengine kwa kui-validate hio software.

Sasa kama mtu ana ufahamu wa mambo haya akiunganisha computer katika internet na unapotaka ku-validate iwe office au windows operating system microsoft watakwambia kwamba product yake ni halali au sio halali.

Kwa hio kuzidi kuelimika kwa wateja kwamba kuna pirate packages au so ndio kuzidi kupata watu wengi wenye computer zenye kuleta performance inayotakiwa.

Shukran.

hii kaka mbona zamani sana imeshapotea hiyo. windows au office kibao utazodownload kutoka torrent ni genuine na ukizi validate zinakubali fresh, na zinakubali update kama sahani na kawa.
tokea mwaka 2008 non-genuine windows zinaonekana kama genuine kwani mahhackers wameshazifanyia hivyo. nayo wamefanikiwa baada ya kuweza kuichakachua ile genuine advantage na validattion za microsoft.
kwani humu JF wangapi wanatumia genuine windows ambayo inauzwa zaidi ya laki moja ya TSh.
Kwa maisha haya ya Bongo.......kwa usawa huu.... Piracy is no more an option. it is a MUST
 
hii kaka mbona zamani sana imeshapotea hiyo. windows au office kibao utazodownload kutoka torrent ni genuine na ukizi validate zinakubali fresh, na zinakubali update kama sahani na kawa.
tokea mwaka 2008 non-genuine windows zinaonekana kama genuine kwani mahhackers wameshazifanyia hivyo. nayo wamefanikiwa baada ya kuweza kuichakachua ile genuine advantage na validattion za microsoft.
kwani humu JF wangapi wanatumia genuine windows ambayo inauzwa zaidi ya laki moja ya TSh.
Kwa maisha haya ya Bongo.......kwa usawa huu.... Piracy is no more an option. it is a MUST

Sio bongo tu mkuu Download music, movies, games, software! The Pirate Bay - The world's most resilient BitTorrent site ni site 95 kwa umaarufu kupokea trafic kubwa. USA . Tena USA wana sheria kai na ndio makampuni mengi ya software na music na Movies zao zinachakachuliwa huko lakini bado.

Kwa hiyo Hata USA wana kazi kubwa.
 
kwani jamani piracy ndio wizi ? na wengi wenu muliochangia mada huyu mtuhumiwa munaeleza kuwa ni mwizi. kosa lake ni kuvunja sheria ya hati miliki. sio mwizi.
I dont believe in copyright infringement or any violation in copyright. and I will defend my opinion to the death.
na kama kuna mtu anataka software yoyote mie nampatia buree cha muhimu niwe ninayo tu. Haya mambo ya wazungu na sheria zao, na hivyo jinsi munavyozikomalia utadhani sheria za mungu.
I hate it
 
Back
Top Bottom