Michezo ya utotoni, ni hatari katika ukuaji wa mtoto.

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,269
40,054
Nakumbuka nilipokuwa mdogo, shule ya msingi nilikwenda kumtembelea ndugu yangu mmoja, alikuwa anafanya kazi kijiji kimoja huko kanda ya ziwa, miaka hiyo.

Baada ya kufika kule kijijini, nikakutana na marafiki wa rika langu; wakawa wananitembeza mtaa kwa mtaa, ili niweze kufahamu mazingira ya huko kijijini.

Siku iliyofuata, tukapanga tuende tukawinde ndege; tukatafuta mapila yale ya kuvutika, pamoja na waya. Tukachukua vipande vidogo vitatu (3) vya miti; vile vipande, tukavigongelea chini vikatengeneza umbo la pembe tatu.

Vipande viwili tukavifunga mapila, na kile cha tatu kikawa ni kiegemeo cha mpira, ili tutakapofyatua mtego uweze kupiga ndege.

Baada ya kuweka mtego vizuri, tukamwagia pumba na tukaunganisha na kamba ndefu, ili ndege wakifika tuweze kufyatua mtego.

Baada ya lisaa kama limoja hivi, walikuja ndege wengi wakaanza kula pumba. Ndipo mmoja wetu, akasema sasa ni muda muafaka wa kufyatua mtego; baada ya kufyatua mtego, ndege kama saba hivi walipigwa, wakashindwa kupaa, na tukaenda kuwakamata.

Baada ya hapo, tukaanza kuseti tena mtego; wakati tunarudishia kijiti cha pili; kile cha kwanza kilifyatuka na kikaja kunipiga kwenye korodani moja; hapo niliona giza ghafla pamoja na maumivu makali, nikasema hapa roho ndio inaanza kuchomoka nini!

Nilijigeuza geuza huku nikisikilizia maumivu kwa muda mrefu kidogo; baada ya maumivu kupungua, nikawaambia marafiki zangu tuondoke, hapa sio mahali salama.

Katika ukuaji wangu, nikajua hapa uzazi ulishaharibika. Lakini, Mungu mkubwa, baada ya miaka kwenda hakukuwa na tatizo; na hatimaye nakimbilia kuja kulea wajukuu.

Ila michezo ya utotoni, ni hatari katika ukuaji wa mtoto.
 
Nakumbuka nilipokuwa mdogo, shule ya msingi nilikwenda kumtembelea ndugu yangu mmoja, alikuwa anafanya kazi kijiji kimoja huko kanda ya ziwa, miaka hiyo.

Baada ya kufika kule kijijini, nikakutana na marafiki wa rika langu; wakawa wananitembeza mtaa kwa mtaa, ili niweze kufahamu mazingira ya huko kijijini.

Siku iliyofuata, tukapanga tuende tukawinde ndege; tukatafuta mapila yale ya kuvutika, pamoja na waya. Tukachukua vipande vidogo vitatu (3) vya miti; vile vipande, tukavigongelea chini vikatengeneza umbo la pembe tatu.

Vipande viwili tukavifunga mapila, na kile cha tatu kikawa ni kiegemeo cha mpira, ili tutakapofyatua mtego uweze kupiga ndege.

Baada ya kuweka mtego vizuri, tukamwagia pumba na tukaunganisha na kamba ndefu, ili ndege wakifika tuweze kufyatua mtego.

Baada ya lisaa kama limoja hivi, walikuja ndege wengi wakaanza kula pumba. Ndipo mmoja wetu, akasema ni sasa ni muda muafaka wa kufyatua mtego; baada ya kufyatua mtego, ndege kama saba hivi walipigwa, wakashindwa kupaa, na tukaenda kuwakamata.

Baada ya hapo, tukaanza kuseti tena mtego; wakati tunarudishia kijiti cha pili; kile cha kwanza kilifyatuka na kikaja kunipiga kwenye korodani moja; hapo niliona giza ghafla pamoja na maumivu makali, nikasema hapa roho ndio inaanza kuchomoka nini!

Nilijigeuza geuza huku nikisikilizia maumivu kwa muda mrefu kidogo; baada ya maumivu kupungua, nikawaambia marafiki zangu tuondoke, hapa sio mahali salama.

Katika ukuaji wangu, nikajua hapa uzazi ulishaharibika. Lakini, Mungu mkubwa, baada ya miaka kwenda hakukuwa na tatizo; na hatimaye nakimbilia kuja kulea wajukuu.

Ila michezo ya utotoni, ni hatari katika ukuaji wa mtoto.
Duh pole sana, mimi nikiwa mdogo niliangukiwa na body la tipa kisa michezo. Home kwa nje kulikuwa na bodi la tipa liko juu ya mawe. Katika kucheza nikawa nafukuza kuku akapanda juu ya hilo bodi na mimi nikapanda likapoteza balance nilitangulia chini linyewe likaja juu.
Watu walioshuhudia wakaja kuinua kutoa maiti, nasikia mzee na ndugu zangu walifuatwa shuleni kuambiwa nimekufa.
Sikumbuki chochote zaidi ya kuzinduka nikajikuta hospital nina madrip ila it seems sikuumia sana. Sikumbuki nilikaa siku ngapi hospital nikatoka na huyo kuku akachinjwa siku nilipotoka nikamtafuna
 
Duh pole sana, mimi nikiwa mdogo niliangukiwa na body la tipa kisa michezo. Home kwa nje kulikuwa na bodi la tipa liko juu ya mawe. Katika kucheza nikawa nafukuza kuku akapanda juu ya hilo bodi na mimi nikapanda likapoteza balance nilitangulia chini linyewe likaja juu.
Watu walioshuhudia wakaja kuinua kutoa maiti, nasikia mzee na ndugu zangu walifuatwa shuleni kuambiwa nimekufa.
Sikumbuki chochote zaidi ya kuzinduka nikajikuta hospital nina madrip ila it seems sikuumia sana. Sikumbuki nilikaa siku ngapi hospital nikatoka na huyo kuku akachinjwa siku nilipotoka nikamtafuna
Hatari sana mkuu :D:D
 
Hatari sana mkuu :D:D
Tukio lingine ndugu yangu akajikuta jet lee alinichana na kisu kwenye eye lid. Yani nusura nitoe jicho. Mpaka leo hiyo alama ninayo. Ndugu yangu mwingine alinipaisha mtama nikatenguka mkono 🤣🤣🤣. Nilikuwa youngest halafu wamenizidi sana nataka kucheza nao na wenyewe watoto sometimes wananitreat kama wao.
 
Tukio lingine ndugu yangu akajikuta jet lee alinichana na kisu kwenye eye lid. Yani nusura nitoe jicho. Mpaka leo hiyo alama ninayo. Ndugu yangu mwingine alinipaisha mtama nikatenguka mkono 🤣🤣🤣. Nilikuwa youngest halafu wamenizidi sana nataka kucheza nao na wenyewe watoto sometimes wananitreat kama wao.
Unabahati sana, ungepoteza jicho, sasa hivi ungekuwa omba omba🤣🤣🤣
 
Unabahati sana, ungepoteza jicho, sasa hivi ungekuwa omba omba🤣🤣🤣
Hahaha ningekuwa napigilia sun glasses. Utoto raha sana. Nilikuwa na zile baiskeli za bmx haina brake, brake sole ya kiatu changu hata kwenye mteremko mimi nakwenda tu. Viatu vyote vimeishiria sole upande.
Nilivyokuwa rofa sasa nilikuwa nadhani trafiki wanakamata waendesha baiskeli nikikutana na trafiki nateremka nasukuma nikishawapita najiona mjanja napanda. 🤣🤣
 
Nakumbuka nilipokuwa mdogo, shule ya msingi nilikwenda kumtembelea ndugu yangu mmoja, alikuwa anafanya kazi kijiji kimoja huko kanda ya ziwa, miaka hiyo.

Baada ya kufika kule kijijini, nikakutana na marafiki wa rika langu; wakawa wananitembeza mtaa kwa mtaa, ili niweze kufahamu mazingira ya huko kijijini.

Siku iliyofuata, tukapanga tuende tukawinde ndege; tukatafuta mapila yale ya kuvutika, pamoja na waya. Tukachukua vipande vidogo vitatu (3) vya miti; vile vipande, tukavigongelea chini vikatengeneza umbo la pembe tatu.

Vipande viwili tukavifunga mapila, na kile cha tatu kikawa ni kiegemeo cha mpira, ili tutakapofyatua mtego uweze kupiga ndege.

Baada ya kuweka mtego vizuri, tukamwagia pumba na tukaunganisha na kamba ndefu, ili ndege wakifika tuweze kufyatua mtego.

Baada ya lisaa kama limoja hivi, walikuja ndege wengi wakaanza kula pumba. Ndipo mmoja wetu, akasema sasa ni muda muafaka wa kufyatua mtego; baada ya kufyatua mtego, ndege kama saba hivi walipigwa, wakashindwa kupaa, na tukaenda kuwakamata.

Baada ya hapo, tukaanza kuseti tena mtego; wakati tunarudishia kijiti cha pili; kile cha kwanza kilifyatuka na kikaja kunipiga kwenye korodani moja; hapo niliona giza ghafla pamoja na maumivu makali, nikasema hapa roho ndio inaanza kuchomoka nini!

Nilijigeuza geuza huku nikisikilizia maumivu kwa muda mrefu kidogo; baada ya maumivu kupungua, nikawaambia marafiki zangu tuondoke, hapa sio mahali salama.

Katika ukuaji wangu, nikajua hapa uzazi ulishaharibika. Lakini, Mungu mkubwa, baada ya miaka kwenda hakukuwa na tatizo; na hatimaye nakimbilia kuja kulea wajukuu.

Ila michezo ya utotoni, ni hatari katika ukuaji wa mtoto.
kwahio ukapigwa kwenye mbupu 😀
 
Hahaha ningekuwa napigilia sun glasses. Utoto raha sana. Nilikuwa na zile baiskeli za bmx haina brake, brake sole ya kiatu changu hata kwenye mteremko mimi nakwenda tu. Viatu vyote vimeishiria sole upande.
Nilivyokuwa rofa sasa nilikuwa nadhani trafiki wanakamata waendesha baiskeli nikikutana na trafiki nateremka nasukuma nikishawapita najiona mjanja napanda. 🤣🤣
Wangekurukisha kichura chura
 
Ilikuwa hatari sana, nikaona giza, nikajua hapa roho inataka kuachana na mwili 🤣 🤣 🤣
sitosahau ile siku nimeenda bushi kusalimia apo ndo kipindi hiko ukiwa unakaa dar ukirudi bush unaonekana mwamba sana umenunuliwa american boot au italy boot na tracksuit full ni full kuwaoshea wajuba wa bush.
sasa siku hio wana wakanambia twende tukacheze kwenye mawe mtoni pia tukaogelee, vijana wakafungua mbuzi watano, tukaenda nao malishoni 😀 sasa ile kufika mchezo ikawa ni kukamata mbuzi na kuwarusha kwenye majiili tuwaone wanavoogelea na kuvuka upande wa pili wa mto😀. shughuli inaanzia upande wa pili wa mto kulikua na kajimsitu kadogo mwanaume nikajitosa kwenda kukimbiza mbuzi ili nimkamate nimrudishe kwenye maji nikaingia adi msituni kuna majani fulani yalinigusa mwilini nikaanza kujisikia muwasho usio na kifani. shughuli ikawa ni kujikuna badala ya kukamata mbuzi, nilianza kulia wenzangu wakanambia upupu huo jirushe kwenye maji ndo muwasho utapungua😂.

basi bila kujiuliza nikavua nguo na kujitosa kwenye maji na chupi yangu ya sambusa, na ukumbuke huo mto ulikua na mawe mengi sana baada ja kujitosa jiwe likanikwarua matako mpaka leo nina kovu😂😂😂😂.
ile ilikua siku mbaya kuwahi kutokea duniani:(
 
Hahaha ningekuwa napigilia sun glasses. Utoto raha sana. Nilikuwa na zile baiskeli za bmx haina brake, brake sole ya kiatu changu hata kwenye mteremko mimi nakwenda tu. Viatu vyote vimeishiria sole upande.
Nilivyokuwa rofa sasa nilikuwa nadhani trafiki wanakamata waendesha baiskeli nikikutana na trafiki nateremka nasukuma nikishawapita najiona mjanja napanda. 🤣🤣
Hapana haukuwa mjinga kuna mkoa nilienda ndani ndani huko eeh si trafik anasimamisha baiskeli na anakagua break na taa..
Mwaka juzi hii ..
 
Nakumbuka enzi ya utoto tulikuwa na mchezo wa kuingiza punje ya maharage puani ilikuwa ukiweka puani unafanya kama unapenga kamasi and then inatoka, Basi bwana mchezo ukaendelea nikaweka punje puani ile kupenga wapi punje haitoki Imeng'ang'ania huku macho yamenitoka watoto wote wakakimbia nikabaki nalia ilikuwa noma sana Mama anakuja kila wakijaribu kuitoa haitoki masaa kama matatu wanaangaika, kwa bahati nzuri alikuwepo mzee wa kimakonde ikabidi atafute Ugolo akaniwekea puani ile kupiga chafya ile punje ikatoka asee siwezi kusahau ile siku ilikuwa atari sana
 
Mi kuna siku na wanangu tulikua tunalina asali mchana picha linaanza baada ya ugunduzi wa asali kuna jamaa angu alichovya kijiti kwenye asali sasa akataka aonje aisee kumbe kulikua na nyuki nyuki akamuuma mdomo na ulimi basi tukacheka kwel kwel sasa baadae kidogo tukawasha moto mkal hapo ndo balaa likaanza nyuki walitibuka aisee wanangu wakakimbilia ndan asa mimi kuwafuata wakafunga mlango wa chumba cha kwanza kwenda cha pil wakawa wamejaa nikaanza kukimbia hovyo hovyo dk za mwisho nikatokomea chooni ndo ikawa pona pona yani
 
Nakumbuka nilipokuwa mdogo, shule ya msingi nilikwenda kumtembelea ndugu yangu mmoja, alikuwa anafanya kazi kijiji kimoja huko kanda ya ziwa, miaka hiyo.

Baada ya kufika kule kijijini, nikakutana na marafiki wa rika langu; wakawa wananitembeza mtaa kwa mtaa, ili niweze kufahamu mazingira ya huko kijijini.

Siku iliyofuata, tukapanga tuende tukawinde ndege; tukatafuta mapila yale ya kuvutika, pamoja na waya. Tukachukua vipande vidogo vitatu (3) vya miti; vile vipande, tukavigongelea chini vikatengeneza umbo la pembe tatu.

Vipande viwili tukavifunga mapila, na kile cha tatu kikawa ni kiegemeo cha mpira, ili tutakapofyatua mtego uweze kupiga ndege.

Baada ya kuweka mtego vizuri, tukamwagia pumba na tukaunganisha na kamba ndefu, ili ndege wakifika tuweze kufyatua mtego.

Baada ya lisaa kama limoja hivi, walikuja ndege wengi wakaanza kula pumba. Ndipo mmoja wetu, akasema sasa ni muda muafaka wa kufyatua mtego; baada ya kufyatua mtego, ndege kama saba hivi walipigwa, wakashindwa kupaa, na tukaenda kuwakamata.

Baada ya hapo, tukaanza kuseti tena mtego; wakati tunarudishia kijiti cha pili; kile cha kwanza kilifyatuka na kikaja kunipiga kwenye korodani moja; hapo niliona giza ghafla pamoja na maumivu makali, nikasema hapa roho ndio inaanza kuchomoka nini!

Nilijigeuza geuza huku nikisikilizia maumivu kwa muda mrefu kidogo; baada ya maumivu kupungua, nikawaambia marafiki zangu tuondoke, hapa sio mahali salama.

Katika ukuaji wangu, nikajua hapa uzazi ulishaharibika. Lakini, Mungu mkubwa, baada ya miaka kwenda hakukuwa na tatizo; na hatimaye nakimbilia kuja kulea wajukuu.

Ila michezo ya utotoni, ni hatari katika ukuaji wa mtoto.
Nilidhani mlicheza mchezo mibaya kumbe hivyo , dah nilikua na hofu
 
Wahenga tumefaidi mno michezo ya utotoni tofauti na kizazi hiki cha kuku wa kizungu ambapo mtoto anacheza na kompyuta tu bila hata kutokwa jasho
 
Back
Top Bottom