(Michezo ya Olimpiki ya Tokyo) Wasichana wa China na Marekani waonesha kwa vitendo moyo wa uanamichezo

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,006
1,026
VCG111342144199.jpg

VCG111342140123.jpg

VCG111342146609.jpg

Kwenye fainali ya balance beam ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo iliyofanyika tarehe 3, Agosti, msichana wa China Guan Chenchen mwenye umri wa miaka 16 alipata medali ya dhahabu. Ushindi huu umetokana na juhudi za miaka kumi umetia moyo, lakini kilichovutia zaidi ni moyo wa uanamichezo ulionekana chini ya jukwaa wakati Guan alipokuwa anaendelea kucheza.

Kulikuwa na wachezaji wanane kwenye fainali hiyo, wakiwemo wasichana wawili wa China na wawili wa Marekani, na wote walikuwa na uwezo wa kupata medali. Mchezaji Tang Xijing wa China alikuwa wa pili kucheza, mchezaji maarufu wa Marekani Simone Biles ambaye ni bingwa mara tatu wa balance beam duniani alikuwa wa tatu, akifuatiwa na mwenzake Sunisa Lee, na Guan Chenchen alikuwa wa mwisho.

Baada ya mchezaji wa saba kumaliza kucheza, Tang Xijing alikuwa nafasi ya kwanza na Biles alikuwa nafasi ya pili. Hii ina maana kuwa kabla ya Guan Chenchen kucheza, China ilikuwa imepata medali ya dhahabu.

Guan Chenchen alianza kucheza, na walionaswa kwenye kamera ya moja kwa moja televisheni ni pamoja na Guan Chenchen aliyekuwa anaendelea kucheza kwenye beam pamoja na makocha na wachezaji wa timu ya Marekani waliokaa karibu sana na Guan Chenchen chini ya jukwaa. Wao walikuwa wakimwangalia Guan Chenchen akicheza, na ndani ya muda wa dakika moja na nusu, walipiga makofi mara zaidi ya 10. Haswa wakati Guan Chenchen alipojiandaa kufanya kitendo chake cha mwisho na kuruka kwenye beam, makocha wa Marekani walimpigia makofi na kumtia moyo, na wakati Guan Chenchen alipomaliza shindano lake kwa mafanikio na kutoa heshima kwa majaji, makocha na wachezaji wa Marekani walimshangilia kwa makofi makubwa kumpongeza. Baada ya kutoka jukwaani, Guan Chenchen alipowapita makosa wa Marekani na wachezaji wawili Biles na Sunisa, wao walimkumbatia mtawalia na Guan Chenchen naye pia alijibu kwa udhati.

Hili ni kumbatio la dhati zaidi nililowahi kuliona katika mashindano ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo. Kumbatio hilo limetoka kwa wachezaji hodari wa Marekani na timu ya makocha wake, na cha kuthaminiwa ni kuwa wakati ule walikuwa wanajua kuwa kwa sababu Guan Chenchen alimaliza mchezo wake vizuri, timu ya Marekani ilipoteza medali moja ya fedha. Matokeo ya fainali hiyo ni kuwa wasichana hao wawili wa China walipata medali za dhahabu na fedha, na mchezaji wa Marekani Biles alipata medali ya shaba.

Katika hafla ya kutoa medali, mtangazaji wa China aliyetoa maelezo kwenye mchezo huo alipomzungumzia mchezaji Biles alisema, “Biles ni kama bendara ya mchezo wa gymnastics kwa upande wa wanawake, hili ni jambo lisilo na ubishi. Idadi ya medali za dhahabu alizopata kwenye michezo ya olimpiki na mashindano ya dunia ya ubingwa inaonewa wivu na ni vigumu kufikiwa na wachezaji wengine……lakini katika michezo ya Olimpiki ya Tokyo Biles hakuonesha uwezo wake ipasavyo, na kubakiza majuto kwenye michezo ya olimpiki ambayo pengine ni mara yake ya mwisho kushiriki.” Tunaweza kusikia jinsi mtangazaji huyo alivyomheshimu na kumwonea huruma mchezaji huyu hodari wa Jimnastiki duniani.

Kwenye jukwaa la mashindano, wachezaji hao wa China na Marekani ni washindani wakubwa, lakini chini ya jukwaa wanaelewana na kutosita kutiana moyo na kupongezana. Picha na video za kukumbatiana kwao vimesambaa kwenye mtandao wa internet wa China na kuzusha mjadala, na watu wengi waliguswa nao. Mwanamtandao mmoja alisema, “kwa kuangalia picha tu, naweza kusikia mioyo yao ya kupeana pongezi za dhati. Huu ni wakati wa kuvutia, pia ni moyo halisi wa Olimpiki.”

Hadi kufikia tarehe 4, Agosti, China na Marekani zinashika nafasi ya kwanza na ya pili kwa medali ya dhahabu 32 na 24 kwenye orodha ya medali ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo. Sijui kama watu wa Marekani walitazama fainali hizo na walijisikia vipi baada ya kuona. Bila shaka, medali ya dhahabu ni muhimu, lakini cha muhimu zaidi ni moyo wa uanamichezo walionesha wachezaji hao wa China na Marekani. Dunia ya leo inahitaji sana mshikamano, haswa wakati janga la virusi vya Corona linaikumba dunia nzima. Zikiwa nguvu kubwa zaidi duniani, ni jambo la kwanza kwa China na Marekani kufanya juhudi kila upande kutafuta maendeleo yao, lakini pia zinapaswa kuheshimiana kwenye mashindano yao kama walivyoonesha wachezaji hao na kupeana pongezi kwa dhati, wakati upande mwingine unapopata mafanikio. Kama kauli mbinu mpya ya Olimpiki katika Michezo ya Olimpiki ya Tokyo inavyosema, sio tu tunahitaji “haraka zaidi, juu zaidi na nguvu zaidi”, pia tunataka “mshikamano zaidi”.
 
Back
Top Bottom