Michepuko hii, kuna muda unajikuta umemkosea mwanaume mwenzako bila kujua

DeepPond

JF-Expert Member
Nov 18, 2017
40,454
99,086
Ntajaribu kuifupisha Sana hii kadiri ya uwezo wangu

NI HIVI,
Bila shaka mnamkumbuka yule Mchepuko Wangu anaesoma chuo kikuu ambae ni mdg wake na mamaJ.

Uyu Binti mahusiano yangu na yeye yapo yapo TU kwa msimu. sometimes ON, sometimes OFF
Yaan kwa mwez tunaweza kuonana Mara 1 au Mara 2 tu kufanya na kuondoka zetu. Mawasiliano yetu sio kiviiile Sana labda akiwa na shida shida zake binafs ndo huwa ananitafuta.

Nakumbuka nilishawaambia nilishamhamisha hostel na kwenda kupanga chumba mtaan jiran na chuo.
Kumbe Sasa chumba kile akawa anashea na Binti mmoja wa uko kwao mkoani kabila moja wanachangia ndani kila kitu.

Baadae akanambia anahitaj MDA mwingi wa kua na mm, ila Sasa ile kua tunakutana lodge kila Mara na namuachia posho yake tukiwa lodge baada ya tendo anajihisi Kama anakua anajiuza tu kwangu, hapendi ile kitu kabisa.

Nikamwambia najua upendi ndio, ila Ndo hivo haina jins mimi chumban kwako pale siwez kuja ukzingatia unaishi na mwenzio pale. Akasema anaomba kuhama pale atafute chumba kingine mtaa mwingine ili niwe nakwenda kwake kwa Uhuru maana ananimiss Sana. Na yeye anahitaj MDA wakua anaenjoy na mimi. Nikasema sawa.

Mwezi wa 3 mzima wote tunatafuta nyumba, na hatimae ijumaa ya juz asbh kanifahamisha kwamba kapata chumba kimoja kizur kina choo ndani anataka akanionyeshe. Nikamwambia saa 10 nikishafunga ntakuja Uko.

Sasa kutokana na ubize mwing, kanipigia sim sn sijaipokea. Nikajisemea uyu msumbufu tu nikimaiza ratiba zangu ntaenda kwake. Kwanza Haina ulazima Sana iwe leo leo .

Nmemaliza ratiba zangu saa 12 nikasema hebu nimpigie nimfahamishe nakuja, hajapokea sim. Nikaona niende Moja kwa Moja kwake. Nmefika saa 1 usiku nmepaki mbali kidg napiga sim yake haipokelewi. ikabd niende mpk penyewe nikagonge mlango wa chumba maana naona Uko wazi.

Nmefika nmegonga kaja mlangoni kapiga pazia kastuka sana kuniona Ni mimi. Ananambia kwa hofu karibu ingia ndani, nmeingia ndan namkuta kijana mmoja kakaa kitandani kwake kashika Simu ya Binti. Mi Nikakaa zangu kwenye kistuli kisha Nikamwambia anipe maji ya kunywa nna kiu sana.

Kamaliza kunipa maji nikainuka na glass yake nikatoka nayo nje Nikamwambia,
"Nakuja mara Moja nmesahau kupandisha vioo vya gar" nikaondoka kuelekea kwny gar. Kufika kwny gar nikataka kuondoka zangu moja kwa Moja. Nikaona utakua ujinga sasa huu, hawa mabinti wajanja wajanja ni wa kwenda nao hivyo hivyo tu.
Ukizingatia mi mwnyw mpitaji TU.

Basi Baadae nikarud,
Nmesimama mlangoni naskia wanalaumiana uko ndani Binti anamshinikiza kijana aondoke pale, kijana anakataa Akitaka kujua Mimi Ni Nani kwanza. Binti anamwambia Mimi Ni mjomba wake aondoke HARAKA asije mletea kesi nyumban kwao. Maana yeye hatambuliki.

Baadae nikaona Hapa tunapotezeana tu MDA wangu, nikaingia nikiwa serious.
Nikamwambia binti jiandae haraka twende Sina MDA wa kupoteza hapa. Yule kijana nikaona nae kainuka anatoka nje.
Mle ndani tukabak wawili mm na Binti, uku anavaa haraka haraka. Kamaliza kuvaa tumetoka nje tunaondoka namuona yule kijana kakaa kubarazan kainamisha kichwa chini Yuko na mawazo mengi.

Tumeondoka pale tunaelekea lilipo gar nikamuona kijana kwa mbali anafata nyuma nyuma. Tumeingia kwny gar tunapiga reverse. nikamuona kijana kwa nyuma, nikamuonesha Binti
"Uyu kijana wako vipi mbona anakufata fata Sana Hadi uku?"

Binti Akasema,
"Atakua na mambo yake uyo, ujue Ni mwanachuo mwenzetu uyo anakaa chumba Cha jirani. Alikuja kwangu kuangalia Tv anamsubir Dem wake yule nnae kaa nae pale " nikasema "sawa". Japo najua uyu kanidanganya. Ukimchunguza Sana Bata huwez kumla.

Tumeenda tumeiona nyumba nmeridhika nayo, chumba kimoja kikubwa kiasi Ila kina choo ndani. Tumeonana na mwny nyumba kasema anapokea kuanzia miez 3. Nmemuachia ya mwezi mmoja pale pale, nyingne atalipwa kesho yake. Binti kafanya usafi wa haraka haraka pale na kusema kesho yake anahamia Moja kwa moja .
Na kaomba kabisa niende nikamsaidie kuhamisha baadhi ya vitu vyake. Nikasema sawa.

Kesho yake JMosi nmeenda kwake kuhamisha vitu nikaifikisha gar mpk mlangoni KABISA. Tumeanza kusomba vitu tunaingiza kwny gar Mara yule kijana akafika anatuangalia TU. Nami kimya kimya sijamsemesha chochote.

Nikaskia anamsemesha Binti, "rose Mambo vipi" Binti kavuta mdomo.

Kijana kamfata kamvuta mkono kwa Nguvu, Binti kakataa mkono wake na kusukumizia kule kijana kaanguka chini. Kijana kainuka kapukuta suruali yake akaja kwa hasira kama anataka kumpiga binti. Ikabd kuingilia Kati.
Nikasimama kati yao Binti na kijana bila kusema chochote kile. Nikimkazia macho kwa umakini sana kijana nione atamfanya nn yule binti pale tuliposimama.

Nikaona kijana kashuka jazba yake na kwenda kukaa zake kibarazani pembeni akipiga simu uku kainamisha kichwa chini uku kama analia kwa hasira.

Nikahs kuna mtu alkua anamfahamisha kwann Rose anamfanyia vile, kaleta mwanaume pale nyumban kwake na Kama alikua hampendi Si angemwambia kuliko alichomfanyia. Binti yuko kimya kavuta mdomo uku anasomba vitu vyake, nami sikutaka kuingilia ugomvi ule nikaendelea Kupanga vitu kwny Gari anavyoleta mchepuko.

Tumemaliza kusomba vitu, tumeingia kwny gar, ikabd nimuulize Mchepuko.
"Ebu kwanza weka sawa ayo mambo yako na uyu kijana wako, naona analia Sana pale. halijakaa sawa kabisa Hili"

Mchepuko akalalamika, Basi ubishi ukawa ubishi mle ndani anasema Hana mahusiano nae, nikasema isiwe kesi ngoja nikakague upepo kwny tairi za nyuma tuondoke. Nmetoka nje namuona kijana kasimama nyuma ya Gari kimya kaniangalia TU macho mekundu.

Kuna mda wazo likaniijia nkataka kijana nimsemeshe nipate mawili matatu, ila Kwasababu Binti nmemuacha Kwny gar na keshapanik tayar nilipomwabia habar zile za yule kijana.ikabd nipotezee kimya.

Nmekagua tairi zote ziko sawa Kisha nikaingia Kwny Gari na kuondoka eneo lile, kijana namuona kwny side mirrors kwa mbali kaiangakia Gari mpk inaishia kwenye Kona.

Nmefika kapanga vitu vyake, tumefanya ya kufanya Kisha nikamuomba anifatie vocha duka la jirani. Alipotoka nmechukua Simu yake nmekagua nmekuta sms lukuki za uyo kijana. Nikaforwad zote kwenye Simu yangu pale pale. Kisha nikafuta sent history

Nmetulia nmezisoma Moja baada ya nyingine nmegundua kweli yule kijana anamahusiano nae, ila hayana mda mrefu Sana . Na wiki moja nyuma wametoka hospitali kupima afya zao na siku tatu nyuma kijana keshatoka kumtambulisha uyu binti nyumbani kwao. Kijana alimpeleka binti TANGA kumtambulisha.

Yule mtu kijana alokua anampigia Simu kulalamika pale tulikohama siku Ile ya ugomvi wao kumbe ni yule Binti wanaeishi nae pamoja pale alikohama. Kuna sms bint anamuuliza uyu kilichompata, kijana yule kampa taarifa hazijakaa vizuri. Ila Mchepuko hakuijibu iyo sms.

Tumemaliza kufanya, nmemuachia ya miez 2 ilobaki na ela yake ya kula. Kisha nmeondoka zangu bila kumuuliza chochote Tena khs yule kijana. Nikaendelea na ratiba zangu.

Sasa baada ya hapo vitu kibao vikawa vinanijia kichwan mwangu

1. Uyu Binti anakwepa nn kuweka wazi mahusiano na kijana yule.Inavoonekana labda hajampenda au ananihofia mm au vipi.
Mbona akisema mi sina tatizo namruhusu TU maana kiukweli pale mm nmeegesha TU. Hana maajabu Sana yule.

2. Walikofikia na kijana mbona palikua hatua kubwa Sana, Binti anakwenda kurisk mahusiano yake serious na kuegemea kwangu wkt anajua Niko na dada ake tayar na yeye anajijua Ni wakupita.

3. Uyu kijana nimsaidieje maana najihisi Kuna namna nmemkosea sana, na anaonekana alikua na malengo Sana na binti.

4. Kuna MDA akili inanambia laiti Kama kijana uyu angekuja kunambia live anaomba nimuachie uyu binti, ningemuachia TU kiroho Safi aendelee nae. Maana binafs najijua pale nmeegesha TU kwa dharura. Sina mipango nae yoyote ya MDA mrefu.

Ila sasa Kuna akili inanambia hata nikimuachia, Kama binti mwnyw hamtaki na anamuonyeshea hadharani itakua nmefanya Ni kazi bure. Binti mpk sahv anakana kwangu katukatu Hana mahusiano nae.

5. Au Nimuache TU kijana mwnyw apambane na Hali yake

Karibuni Sana kwa USHAURI
 
pesa zako ndo zinakupa jeuri..

huo ni uonevu wa waziwazi
Kwa pesa zipi Sasa?
Binafsi Sion Kama pesa inahusika kabisa hapa na Sion popote nilipomuonea kijana,

Kijana yeye ndo kaingilia mahusiano yangu, mi kiuhalisia nmemtangulia.

Sema kutokujua TU,
Kijana anahisi nmemshawishi binti amfanyie jeuri au amjibu vibaya vile au nmemfata wakiwa kwny mahusiano wkt mi Sijui chochote kile nmekwenda kwa issues tofauti kabisa


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom