Michakato na vikao vya CCM vinapokaa hufuatiliwa kwa karibu na Mamilioni ya Watanzania

Hamna mtu anapenda chama cha zamani hivyo, ndio maana mbeleko ya dola imekuwa nguvu kuu ya kubaki madarakani kwa shuruti.
Hakuna mbeleko yoyote itumikayo, Hata hivyo Hivi kwa akili yako unazani Kuna mtu mwenye Akili Timamu anayeweza kuunga mkono upinzani wa nchi hii!
 
Mimi Ni CCM na nitaendelea kuwa CCM, kwa kuwa hiki Ni chama chenye dira na muelekeo wa kueleweka na hayo unayoyasema hayawezi kutokea kwangu, Mimi Ni mzalendo wa dhati kwa chama changu na kwa serikali ya chama changu,Nakitetea chama changu na serikali yangu popote nilipo kaa pale panapotokea upotoshaji wa watu wachache
Ni suala la muda tu, mbona malengo yako yasipotimia utakuja humu na Id nyingine ukiponda mbaya kabisa.

Sio wewe tu wapo wengi kabla yako na tunawajua tangu enzi za Kikwete humu. Kwa ushauri hebu mtafute bro Pasikali akupe moja na mbili kuhusu hao viwavi jeshi.
 
Mimi Ni CCM na nitaendelea kuwa CCM, kwa kuwa hiki Ni chama chenye dira na muelekeo wa kueleweka na hayo unayoyasema hayawezi kutokea kwangu, Mimi Ni mzalendo wa dhati kwa chama changu na kwa serikali ya chama changu,Nakitetea chama changu na serikali yangu popote nilipo kaa pale panapotokea upotoshaji wa watu wachache
Nani asie wajua nyie madungayembe!? Zaidi ya kujipendekeza angalau muende chooni hata mara mbili kwa siku mna kipi kipya?
 
Nani asie wajua nyie madungayembe!? Zaidi ya kujipendekeza angalau muende chooni hata mara mbili kwa siku mna kipi kipya?
Hapana sijipendekezi Ila Ni Upendo wangu kwa chama na serikali hii ya CCM inayofanya kazi usiku na mchana kututumikia watanzania wanyonge
 
CCM Ni Kama maji usipoyanywa utayaoga tu, kila kitu ifanyacho CCM lazima kiguse maisha yako, Hata ukiichukia CCM mwisho wa siku itakulazimu usipende tu maana Ni chama chenye Sera na ajenda nzuri za kugusa maisha yetu
Sio kwa hiyari yetu, bali ni CCM kuanzia 2016 imeanza kulazimisha itutawale kwa nguvu.
 
CCM Ni Kama maji usipoyanywa utayaoga tu, kila kitu ifanyacho CCM lazima kiguse maisha yako, Hata ukiichukia CCM mwisho wa siku itakulazimu usipende tu maana Ni chama chenye Sera na ajenda nzuri za kugusa maisha yetu
CCM mwisho wa uhai wake ni 2026. Ameeeen
 
Hakuna mbeleko yoyote itumikayo, Hata hivyo Hivi kwa akili yako unazani Kuna mtu mwenye Akili Timamu anayeweza kuunga mkono upinzani wa nchi hii!

Ni kweli hakuna atakayeunga mkono upinzani wa nchi, je ule wizi wa kura na kunajisi uchaguzi hua kunafanyika kwa ajili gani?

Ni hivi boss, CCM sio chama cha kizazi hiki, ndio maana kinatumia nguvu kubwa kuendelea kubaki madarakani. Kizazi kikishageuka hata mfanye nini itakuwa ngumu kuendelea kukaa madarakani. Machafuko tu au mapinduzi ndio yatawatoa madarakani. Na mkitoka madarakani kwa machafuko mjiandae kufia jela.
 
Ni kweli hakuna atakayeunga mkono upinzani wa nchi, je ule wizi wa kura na kunajisi uchaguzi hua kunafanyika kwa ajili gani?

Ni hivi boss, CCM sio chama cha kizazi hiki, ndio maana kinatumia nguvu kubwa kuendelea kubaki madarakani. Kizazi kikishageuka hata mfanye nini itakuwa ngumu kuendelea kukaa madarakani. Machafuko tu au mapinduzi ndio yatawatoa madarakani. Na mkitoka madarakani kwa machafuko mjiandae kufia jela.
Hakuna wakuleta machafuko nchi hii chini ya uongozi wa CCm, maana CCM kimekuwa Ni chama sikivu na masikio yake Ni sikivu kwa wananchi, Watu wanasikilizwa kero na matatizo yao yanafanyiwa kazi kwa kutafutiwa majibu sahihi Tena kwa wakati,

Hiyo ndio sababu unawaona viongozi wa CCm kuanzia Shina Hadi Taifa wakiwa muda wote kwa wananchi kuwasikiliza na kutatua kero, Tofauti na vyama vingine visivyo toa fursa ya kusikiliza kero za watu, Ndani ya CCM Leo utamuona Shaka yupo huku kukagua ilani, kesho unamuona ndugu chongolo yupo kule akitoa maelekezo, keshokutwa unamkuta kule ndugu Kinana akitoa matumaini na siku inayofuata unamuona mama shupavu mh Samia akitoa kauli ya kuwasaidia wananchi, mambo Kama haya hufanywa na vyama vichache Sana Duniana kwote , Ndio sababu ya CCM Kuendelea kuaminiwa na kuwepo madarakani Hadi leo
 
Sio kwa hiyari yetu, bali ni CCM kuanzia 2016 imeanza kulazimisha itutawale kwa nguvu.
Hapana siyo kweli, ukweli Ni kuwa Ni ajenda Sera na ilani nzuri na Bora ya CCM inayofanya wananchi waendelee kuwa na Imani nayo na kuipa kura katika kila uchaguzi unapowadia
 
Hakuna wakuleta machafuko nchi hii chini ya uongozi wa CCm, maana CCM kimekuwa Ni chama sikivu na masikio yake Ni sikivu kwa wananchi, Watu wanasikilizwa kero na matatizo yao yanafanyiwa kazi kwa kutafutiwa majibu sahihi Tena kwa wakati,

Hiyo ndio sababu unawaona viongozi wa CCm kuanzia Shina Hadi Taifa wakiwa muda wote kwa wananchi kuwasikiliza na kutatua kero, Tofauti na vyama vingine visivyo toa fursa ya kusikiliza kero za watu, Ndani ya CCM Leo utamuona Shaka yupo huku kukagua ilani, kesho unamuona ndugu chongolo yupo kule akitoa maelekezo, keshokutwa unamkuta kule ndugu Kinana akitoa matumaini na siku inayofuata unamuona mama shupavu mh Samia akitoa kauli ya kuwasaidia wananchi, mambo Kama haya hufanywa na vyama vichache Sana Duniana kwote , Ndio sababu ya CCM Kuendelea kuaminiwa na kuwepo madarakani Hadi leo

Narudia tena, machafuko ndio njia iliyobaki kuwaondoa madarakani, na hilo halipo mbali. Kama huamini jaribu kuangalia viongozi wa CCM wanavyopata mahudhurio madogo ya wananchi wanapitisha mikutano. Na kutokana mnavyochezea box la kura, wananchi wengi wamelipuuza maana hawana muda wa kuwachagua nyie chama cha kizee.
 
Ndugu zangu huo ndio utafiti unavyoonyesha kuwa kila CCM inapokuwa na vikao vyake vya ndani ngazi ya Taifa hufuatiliwa kwa karibu Sana na Mamilioni ya Watanzania, huku waandishi wa habari wakiongoza kupiga kambi katika viunga kunakofanyika vikao ili kufahamu yanayoendelea na maazimio ya vikao hivyo,

Watanzania wengi walipoulizwa sababu ya Jambo Hilo kutokea wamejibu kwa kusema kuwa CCM ndio iliyobeba dhamana na matumaini ya mamillioni ya watanzania, wanasema kuwa maamuzi ya CCM yanamchango mkubwa katika maisha yao, kwa kuwa CCM hutoa dira na muelekeo wa maisha yao na huamua kwa maslahi ya Taifa, Ndio sababu watu huwa karibu ya vyombo vya habari kufahamu maazimio ya vikao vya CCM,

Wanaendelea kusema kuwa Hata uteuzi wa viongozi kugombea nafasi mbalimbali ndani na nje ya chama hufuatiliwa kwa ukaribu kutokana na Imani kubwa walio nayo wananchi kwa CCM, wanaamini kuwa viongozi walioteuliwa na CCM ndio wenye kujuwa matatizo na kero za wananchi, pia ndio wenye majibu sahihi ya matatizo yao.

Wanasema wapinzani ukiwachagua ukaja kuwauliza mbona hiki na hiki hujatekeleza wanajibu kuwa hiyo Ni kazi ya serikali, wanauliza Sasa nyie kazi yenu wapinzani Ni Nini? Ni kula na kujikusanyia maposho? Ndio sababu kwa Sasa wamewapuuza wapinzani na kuwanyima kura kila uchaguzi ukijotokeza.

Hongera sana chama changu Cha CCM kwa Kuendelea kuaminiwa na watanzania wote, Rai yangu kwa viongozi wangu wakiongozwa na mh Mwenyekiti wetu Taifa mh mama Samia Ni kuhakikisha mnatuteulia viongozi wenye uchungu na wazalendo wa dhati, viongozi watakaokuwa na moyo wa kujitoa kwa ajili ya kuwatumikia watanzania, viongozi watakao kuwa na masikio ya kusikiliza matatizo na kero za wananchi, viongozi watakao kuwa wanyenyekevu na wasikivu, viongozi watakao kuwa na upendo kwa wananchi,

viongozi watakao juwa uongozi ni dhamana na utumishi kwa watu,viongozi watakao juwa kuwa uongozi ni wakupita tu, viongozi watako juwa kuwa Bora jina zuri kuliko Mali nyingi, viongozi watakao kuwa na kiu ya kuonana na wananchi wenye mizigo ya matatizo ili wawatue kwa kuwasaidia kutatua, viongozi watakao Leta matumaini kwa wananchi wote, viongozi watakao kuwa na kauli moja tu kuwa cheo Ni dhamana na sitakitumia cheo changu kwa maslahi yangu binafsi

Kazi iendeleee, Tanzania Ni imara Sana chini ya serikali ya CCM na uongozi shupavu wa mh mama Samia suluhu Hassani

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu


Sababu ni kwamba hakuna demokrasia Tanzania. Hata Chama cha Putin ni hivyo hivyo.
 
Narudia tena, machafuko ndio njia iliyobaki kuwaondoa madarakani, na hilo halipo mbali. Kama huamini jaribu kuangalia viongozi wa CCM wanavyopata mahudhurio madogo ya wananchi wanapitisha mikutano. Na kutokana mnavyochezea box la kura, wananchi wengi wamelipuuza maana hawana muda wa kuwachagua nyie chama cha kizee.
Jaribu kuleta hayo machafuko ili upate majibu yake
 
Wizi wa kura wakubwa nyie.
Hapana nyinyi imarisheni vyama vyenu na muwe na Sera na ajenda za kueleweka kwa wananchi ndio mtaanza kusikilizwa na wananchi, lakini nje ya hapo mtaendelea kupuuzwa na watanzania Kama ilivyo kwa Sasa na kukalia habari za kuibiwa kura kila siku, kwa Sasa Hakuna mwenye uchungu na nchi hii anayeweza kuwapa kura au kuwaunga mkono
 
Jaribu kuleta hayo machafuko ili upate majibu yake

Majibu yake wako watakaopoteza maisha, na wengine kubaki na vilema vya maisha, ila ndio mabadiliko ya kweli yatatokea. Mtu hata kama humuwezi, pigana naye, hata akikupiga atakuheshimu. Na baada ya hayo machafuko ndio itakuwa mwisho wa CCM kutawala nchi hii.
 
Back
Top Bottom