Michael Wambura aachiwa huru na Mahakama huku akitakiwa kulipa Tsh. Milioni 100

Alvin A.

JF-Expert Member
Oct 14, 2016
2,868
3,624
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam leo Oktoba 07, 2019 imemwachia huru aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF), Michael Richard Wambura baada ya kukiri kujipatia fedha za kitanzania zaidi ya shilingi milioni 100 kwa njia isiyo halali na kukubali kuzirejesha.

Mapema mwaka huu 2019, Wambura alikamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka 17 ya uhujumu uchumi ikiwemo kutakatisha fedha zaidi ya shilingi milioni 100.

Wambura ameachiwa huru katika kesi yake namba tisa ya mwaka 2019 na Hakimu Mfawidhi Kelvin Mhina na kutakiwa kulipa fedha hizo, ambapo amekubali kulipa kwa awamu tano, na leo tayari amelipa shilingi milioni 20.

Zaidi, soma:



72136384_451539352149779_6786300369245831168_n.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru aliyekuwa makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Michael Wambura kwa mashati ya kutokufanya makosa yoyote kwa kipindi cha miezi 12 nakulipa zaidi ya Sh100 milioni kwa awamu tano ambapo leo amelipa Tsh. 20,249,531

BE24CB24-947B-4FA9-A962-EEDEF7F5583E.jpeg


Mnamo Oktoba 02, Michael Wambura alieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu kuwa ameandika barua kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kuomba msamaha na kukiri makosa yake.

Wambura alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza, Februari 11, mwaka huu, akikabiliwa na mashtaka 17 yakiwemo ya kutakatisha fedha zaidi ya Sh 100milioni, katika kesi ya uhujumu uchumi namba 10/2019.
 
Niliposoma heading picha iliyonijia mawazoni ni ya yule Wambura wa kuongea kwa kiburi na mikogo, siamini kama ndiye kasalimu amri kirahisi hivi?....
 
Niliposoma heading picha iliyonijia mawazoni ni ya yule Wambura wa kuongea kwa kiburi na mikogo, siamini kama ndiye kasalimu amri kirahisi hivi?....
ana kiburi ndiyo, ndio watu wa Musoma
wewe unafikiri atalipa zote?
DENI halimuui mtu
na huwezi mkamata tena eti zimebaki 80
hayo ni mashtaka mengine utalipa kidogo kidogo kwa miaka 12 sasa Hakimu atapokea na kusema hivyo
 
Back
Top Bottom