Michael Jackson alitaka kuishi miaka 150

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Apr 4, 2017
392
946
FB_IMG_1592759939313.jpg

Kama ulikuwa hujui basi ni hivi aliyekuwa muimbaji na mfalme wa pop duniani Michael Jackson alipanga mipango ili aweze kuishi miaka 150 hapa duniani

Baadhi ya mipango hiyo ni

- Aliajiri madaktari 12 ambao walikuwa wanampima kila siku kuanzia nywele hadi kucha za vidole vya miguu

- Chakula chake kila siku kilikuwa kinaenda fanyiwa majaribio na kupimwa kabla ya kula

- Aliajiri watu 15 ambao walikuwa wanampangia ratiba ya mazoezi na kumsimamia namna bora ya kufanya mazoezi

- Kitanda alichokuwa analalia kilikuwa na teknolojia ya kuthibiti oxygen

- Waliandaliwa watu maalum kwa ajili ya kumtolea vitu ndani ya miili yao kama vikiitajika kwa mfano figo .....na watu hao walikuwa wakilindwa na kuhifadhiwa na yeye

- Hizo zote zilikuwa jitihada na mipango ya kuishi miaka 150

-Mwaka 2009 tar 25 mwezi wa 6 ...moyo wake ulisimama ghafla kufanya kazi .....madaktari wake 12 walishindwa kumtibu

-Wakaongezwa madaktari wengine mabinhwa kutoka California na Los Angels lakini pia walishindwa

-Mtu ambaye kila hatua aliyokuwa anaipiga iliongozana na jopo la madaktari bingwa 12 Kwa miaka 25 mfululizo .....lengo lake ni kutaka kuishi miaka 150 lakini alishindwa licha ya jitihada zake

-Tar hiyi 25 mwezi wa 6 mwaka 2009 Michael Jackson alifariki dunia akiwa na miaka 50 TU

TUNAISHI KWA MIAKA TULIYOKADIRIWA NA MUNGU....HATA TUKIFANYA VIPI MUNGU AKIPENDA KUMCHUKUA MJA WAKE HAKUNA KITAKACHOSAIDIA.
 
Dah!!!.kweli tunaishi kwa mpango wa mungu.
kuna watu hawana daktari tena wanaishi misha ya hovyo kuanzia kulala,kula lakini wanatoboa mpaka miaka 90.
 
Mwanzo 6:3 BHN
Hapo Mwenyezi-Mungu akasema, “Roho yangu haitakaa ndani ya binadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka 120.”
 
Back
Top Bottom