Miaka takribani 50 ya Uhuru Tanzania: Ni yapi ya kujivunia?

Dotori

JF-Expert Member
Nov 3, 2007
544
24
Tanzania inafikisha miaka 46 ya Uhuru tarehe 9 Disemba 2007.

Ningependa kuwakaribisha wadau kujadili mafanikio makubwa na ya msingi ambayo tumeyapata na vile vile kujadili changamoto tulizonazo na jinsi ya kuzitatua.

==============
1yr later:
UMEBAKI mwezi mmoja vile Tanzania iadhimishe miaka yake 47 toka iwe huru. Mwanamme wa miaka 47 bila shaka ana mke na angalau watoto wawili. Mwanamke wa miaka 47 nadra tena kupata mwana.

Kwa Tanzania hii yetu sifa yake kubwa katika kutimiza miaka 47 ni nini?

Ninavyoona mimi:
- Kuua taratibu amani na umoja tuliolea kwa shida na taabu;
- Watu kutafutana uadui usio na sababu,
- wabunge kujiwakilisha wenyewe badala ya wananchi,
- mawaziri kuwa matarishi badala ya mameneja.
- watu wa nje kupewa mali asili yetu bure wafaidi wao na sisi tunakosa,
- ubepari umekubalika waziwazi na awamu ya nne bila kuwa na mawazo wala akili ya kupambana na makali yake,
- tumewagawa watoto kati ya watoto wa wale walichonacho na watoto wa wale wasichonacho,
- tukichaji kihalali makampuni au migodi ya dhahabu tunaweza kutoa bure huduma za afya na kugharamia elimu ya wenetu hadi Chuo Kikuu lakini tumeamua kutofanya hivyo kwa sababu wanasiasa na mangimeza wa serikali wanazozijua,
- Serikali imekuwa kubwa mno na inakula ashemu kubwa ya kodi ya wananchi bila sababu ya msingi, ila tu, kwamba sera ya wanasiasa waliopo madarakani ni kutozalisha ila kula sana,
- Pamoja na kutumia fedha nyingi vyombo vya serikali havifanyi vizuri kama vyombo binafsi iwe ni vyombo vya habari, usalama, uchukuzi kama vile vya watu binafsi vinavyotumia fedha kidogo,
- Tumekosa msimamamo wa kuchagua marafiki wa kweli na badala yake tunayumba yumba na kurudi kule kule kwa wale ambao misaada yao na elimu yao na mawazo yao ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo,

Nisimalize yote basi, labda wenzangu na nyie mna maono na uono wenu hebu tubadilishane tujue hali halisi ya Mtanzania miaka 47 baada ya Uhuru.

Kumbuka Botswana, Namibia, Rwanda, Gabon na kadhalika walipata uhuru nyuma yetu lakini wana GDP per capita mara 3 au nne kama sio zaidi ya ile ya kwetu.

Tumepoteza fursa nyingi kama ile ya kwenda kuweka amani Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na tunaviachia vinchi kama Rwanda kujifanya vijogoo visivyo hata na kilemba achilia mbali mkia!

Tungeliweza kuigeuza nchi yetu SOKO KUBWAAA -soko linalonunua BIDHAA MBALIMBALI toka Mashariki ya Kati na Mashariki ya Mbali na kuuza kwenye maeneo mbalimbali Afrika Mashariki, Kati na Kusini lakini tumeachia fursa hiyo tena ambayo ingelitukomboa kwa kutuwezesha kuwa na mitaji ya kuwekeza kwenye KILIMO na VIWANDA kwa urahisi.

Kama unabisha sio biashara au soko ndiyoinayotajirisha watu nitajie WAKULIMA waliotajirika Tanzania au WASOMI waliotajirika Tanzania au WAFUGAJI waliotajirika Tanzania au WAVUVI waliotajirika Tanzania bila kuuza kitu!


Akili,
Dodoma
 
Hakuna mafanikio yoyote ni kama vile tumedumaa. Hebu anaglia nhci jirani ambazo zimetoka kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe majuzi tu (mf Rwanda and Msumbiji) they are far ahead of us! NAogopa kuwa hata Somalia wakimaliza kupigana wenyewe kwa wenyewe watatuacha!

Changamoto/Tatizo letu linalosababisha tudumae ni kukosa Uongozi Bora (sisi tuna bora uongozi). Our leaders are not serious, if we get serious leaders like Kagame and Chisano basi mafanikio yatakuwa makubwa kuliko nchi yoyote Afrika kwa kuzingatia kuwa tuna utajiri mkubwa wa raslimali na tuna amani ya kutosha.

Summary: "ILI TUENDELEEE TUNAHITAJI VITU VINNE", JK Nyerere
1. Watu (tunao!),
2. Ardhi (tunayo tele-yenye rutuba, madini na msitu!,
3. Siasa safi (nna wasi wasi kama tunayo maana hatujui kama sisi ni Wajamaa/Wasoshalisti, au Mabepari maan KAtiba inasema nchi yetu ni ya Ujamaa na Kujitegemea!),
4. Uongozi Bora (Hapa ndipo kwenye kasheshe maana naona tuna Bora Uongozi wanojali maslahi yao kwanya) Rejea mikataba ya Madini, Ubinfsishaji wa kijinga (Kama Kiwira Coal Mine)nk, nk, nk
 
Tanzania inafikisha miaka 46 ya Uhuru tarehe 9 Disemba 2007. Ningependa kuwakaribisha wadau kujadili mafanikio makubwa na ya msingi ambayo tumeyapata na vile vile kujadili changamoto tulizonazo na jinsi ya kuzitatua.

Utajivunia nini wakati maisha ya Watanganyika yalikuwa bora na mazuri mwaka 1962 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 70 ukilinganisha na maisha ya 2007. Ndio tumeongeza sana idadi ya wasomi wetu ulikinganisha na kabla ya uhuru kwa juhudi binafsi za Mwalimu Nyerere (RIP) lakini wasomi hao wanadharauliwa leo utaalamu wao unazineemesha nchi nyingine duniani badala ya Tanzania, lakini wanasiasa wanaimba nyimbo za kuboresha mazingira Tanzania ili wataalamu wa Kitanzania washawawishike kurudi nyumbani, lakini ukweli ni kwamba hakuna chochote wanachokifanya na hali ndiyo inazidi kuwa mbaya. By the way there was no Tanzania in 1961.
 
..uwanja mpya wa michezo!

..daraja la mkapa!

..bot twin towers!

..barabara ya lami toka dar kwenda mwanza hadi bukoba inaelekea kukamilika!

..tra!

..kufa kwa reli ya kati!

..kudorora kwa reli ya tazara!

..kuzidiwa kwa bandari dar!

..kuongezeka kwa ufisadi na rushwa!

..kushuka kwa bidii ya kazi na shughuli za maendeleo!

..watanzania kukata tamaa!

....hapo juu mambo yamechanganywa!nia ni kujiuliza vizuri,nini tumekifanya cha maana,kwani vingi vimefanywa!.kusema hamna kitu ni sawa na kumkataa mwanao,kisa umegombana na mkeo!
 
Hayo uliyoyataja hapo juu kama mafanikio yameboreshaje maisha ya kila siku ya Mtanganyika ikiwa life span ya Watanganyika imeshuka ukilinganisha na mwaka 61!? Je, kuna ahueni yeyote katika kiwango cha maisha ukilinganisha mwaka 1961 na mwaka 2007?
 
Hayo uliyoyataja hapo juu kama mafanikio yameboreshaje maisha ya kila siku ya Mtanganyika ikiwa life span ya Watanganyika imeshuka ukilinganisha na mwaka 61!? Je, kuna ahueni yeyote katika kiwango cha maisha ukilinganisha mwaka 1961 na mwaka 2007?

..pamoja na kwamba hujayapanga vizuri maswali yako,nitajitahidi kuyajibu,japo kidogo!

..lifespan,hii imekuwa affected zaidi na ukimwi,malaria,tb[uhusiano na ukimwi]na hali duni ya afya!kwa kiwango fulani hii inatokana zaidi na uzembe wetu watanzania[tanganyika na zanzibar]!

..ahueni ya kiwango cha maisha au kukua kwa kiwango cha maisha na ahueni ya maisha!. baadhi yetu wana maisha bora zaidi kuliko huko nyuma..sasa,hii inategemea umeya-peg maisha bora kwenye nini?kiwango cha elimu,nyumba bora,huduma za afya,huduma nyinginezo!....wengi hasa wa vijijini na baadhi ya maeneo ya mjini,maisha yamekuwa magumu na ya dhiki!

..kiwango cha maisha kimekua au kimeshuka!hili swali pana sana,ila idadi ya masikini imeongezeka! hata ya walio na maisha mazuri pia!

..uwanja uko wazi!
 
Mafanikio:
Tumefanikiwa kulinda uhuru wetu.

Tumeonesha dira kwa nchi nyingine za kiafrika juu ya kuungana ya Kuwa na nchi za kisasa badala ya kuishi kwa kufuata mipaka ya kikoloni.

Tumesaidia wenzetu kujikomboa kutoka makucha ya ukoloni, mathalani msumbiji,angola, zimbabwe, kwa maana hiyo dhana yetu ya kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro umulike hata nje ya mipaka yetu,ulete tumaini, tumeitekeleza kwa vitendo.

Tumejenga Taifa moja, bila kujali misingi ya kikabila

Tumepunguza ujinga kwa kiasi kikubwa sana, mathalani asilimia ya watanzania walioweza kusoma na kuandika mwaka 64 ni ndogo ukilinganisha na watanzania wenye kujua kusoma na kuandika mwaka 2007.

tumeweza kujenga misingi ya kidemokrasia kwa kasi ya ajabu, mathalani tunabadilisha viongozi kwa awamu, kwa salama na amani,uhuru wa vyombo vya habari umepanuka,wananchi kutoa maoni yao kuhusu utendaji wa serikali yao pasi na hofu ya misukosuko.

Tumejenga Taasisi nyeti za kulinda mafanikio yeyote yawayo, tuna jeshi la ulinzi lenye nidhamu nzuri.
 
Mafanikio:
Tumefanikiwa kulinda uhuru wetu.

Gamba la Nyoka,

Usinichekeshe tuna uhuru gani sisi? Uhuru wa watu wachache huku mamilioni wanashindwa hata kupata mlo wa maana?

Uhuru wa Mzungu kuheshimiwa zaidi ya Mtanzania tena kwenye nchi yetu?

Hata kwenye utumwa baadhi ya Watumishi wa ndani wa wazungu walikuwa wanaona wana uhuru kwasababu japo waliweza kutandika kitanda cha mabwana zao. hatuko mbali, si ajabu uhuru wetu utakuwa kama huo.

Niliwahi shuhudia kwenye bank moja, Kaburu anamtukana mswahili utafiri nchi haina sheria. Tulikuwa huru enzi za Nyerere kuliko sasa.
 
Mafanikio:
Tumefanikiwa kulinda uhuru wetu.

Tumeonesha dira kwa nchi nyingine za kiafrika juu ya kuungana ya Kuwa na nchi za kisasa badala ya kuishi kwa kufuata mipaka ya kikoloni.

Tumesaidia wenzetu kujikomboa kutoka makucha ya ukoloni, mathalani msumbiji,angola, zimbabwe, kwa maana hiyo dhana yetu ya kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro umulike hata nje ya mipaka yetu,ulete tumaini, tumeitekeleza kwa vitendo.

Tumejenga Taifa moja, bila kujali misingi ya kikabila

Tumepunguza ujinga kwa kiasi kikubwa sana, mathalani asilimia ya watanzania walioweza kusoma na kuandika mwaka 64 ni ndogo ukilinganisha na watanzania wenye kujua kusoma na kuandika mwaka 2007.

tumeweza kujenga misingi ya kidemokrasia kwa kasi ya ajabu, mathalani tunabadilisha viongozi kwa awamu, kwa salama na amani,uhuru wa vyombo vya habari umepanuka,wananchi kutoa maoni yao kuhusu utendaji wa serikali yao pasi na hofu ya misukosuko.

Tumejenga Taasisi nyeti za kulinda mafanikio yeyote yawayo, tuna jeshi la ulinzi lenye nidhamu nzuri.


Huo Muungano unaozungumzia unajua una mizengwe isiyo kwisha na muafaka sasa havi unakata miaka bila mafanikio yeyote.

Misingi ipi ya kidemokrasi unayozungumzia? Kuna demokrasia gani ikiwa wakati wa uchaguzi vyombo vya dola huwa vinatumika na CCM kuhakikisha wanaharibu kampeni za vyama vya wapinzani! Jenerali Ulimwengu aliwahi kusingiziwa kwamba siyo Mtanzania kwa kuandika mambo mbali mbali ambayo yalikuwa yanaikosoa awamu ya tatu na Mkapa. Zitto kafukuzwa bungeni kwa kutetea maslahi ya Tanzania. Kwa kifupi hakuna demokrasi.

Taasisi nyeti kama Bunge, polisi, Takukuru na mahakama umeona katika ripoti ya REDET jinsi Watanzania walivyokosa imani na taasisi hizo kutokana na utendaji wao mbovu kwa yale wanayoyasimamia.

Tumetengeneza wasomi wengi sana katika nyanja mbali mbali, lakini wanadharaulika na wengi wao utaalmu wao unatumika kuziendelea nchi nyingine duniani na siyo Tanzania.

Wakati mwingine tuwe wakweli kusema kwa sauti moja kwamba tunakoelekea ni kubaya bila woga wala kificho!
 
Gamba la Nyoka,

Usinichekeshe tuna uhuru gani sisi? Uhuru wa watu wachache huku mamilioni wanashindwa hata kupata mlo wa maana?.......

Thankx Mtanzania, sijui niongeze nini hapo, labda tu niseme siyo mlo wa maana bali mlo tu, siyo lazima uwe wa maana, hata ule ugali(dona) kwa maharage au kwa mchicha unashinda familia nyingi nchini.
 
Picha ninayopata hapa ni kuwa hakuna mema ambayo yamefanyika katika kipindi hiki cha Miaka 41 ya Uhuru. Wachangiaji wa awali karibu wote wameonyesha hali ya kukata tamaa.
Je, sisi wenye utambua wa matatizo ya nchi yetu tumechukua hatua gani? Majuzi Spika wa Bunge alikuwa anatamba kuwa waheshimiwa wengi ni wasomi wenye Digrii.
-Wabunge hawa na wasomi wa nchi hii wametoa mchango gani? Aidha wasomi wengi wamekimbilia nje ya nchi au kujiingiza kwenye siasa.
-Je ni wasomi wangapi wanapiga kura?
-Je wasomi wametumiaje elimu yao kuelimisha wananchi kuhusu haki zao za msingi na umuhimu wa kura zao?

Nakubaliana na Bw Ibra kuwa kinachokosekana Tanzania ni SIASA SAFI,UONGOZI BORA na nitaongeza UZALENDO.
Bado ninaamini tunaweza kama wote tutakuwa wazalendo na kuipenda nchi yetu.MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Mimi nina maoni tofauti kuhusu Uzalendo. Uzalendo Tanzania upo wa kutosha tatizo letu kubwa ni viongozi ambao hawana mapenzi ya kweli na nchi yao, wameweka mbele maslahi yao na lile linyama linaloitwa CCM.

Pia sasa hivi wameshajua njia mbali mbali za kutumia vyombo vya dola kuwatisha viongozi wa upinzani na Watanzania kwa ujumla na hatimaye kuiba kura. Hata Watanzania wakasirishwe vipi na utendaji wa siri kali na CCM kuna kazi kubwa ya kuwatoa madarakani maana vyombo vya dola siku zote vitakuwa upande wao hivyo kuwasaidia katika wizi wa kura.
 
..uwanja mpya wa michezo!

..daraja la mkapa!

..bot twin towers!

..barabara ya lami toka dar kwenda mwanza hadi bukoba inaelekea kukamilika!

..tra!

!

Duh!

Mara baada ya vile viwanja vyetu tulivyojenga na Mwalimu Nyerere toka wakati wa chama kimoja yani hatujenga vingine. Miaka 46 tunajivunia kiwanja kimoja? Vipi jirani zetu?

Miaka 46 tunajivunia twin towers za rushwa wakati walio wengi wanaishi mbavu za mbwa

Miaka 46 ya kujenga Lami ya kati na kuendelea kupitia nchi jirani ili kwenda sehemu nyingine nchini.

Miaka 46 tunajivunia kuwa na TRA(serikali yoyote lazima ikusanye kodi) lakini hatuna cha kujivunia juu ya matumizi ya kodi hizo. Miaka 46 ya ukwepaji kodi, ufisadi na matumizi ya anasa. Hata mkoloni alitoza kodi ya kichwa, kodi ya matiti nk tena kwa shuruti kama michango ya ujenzi wa mashule ya sasa!

Asha
 
..

..kufa kwa reli ya kati!

..kudorora kwa reli ya tazara!

..kuzidiwa kwa bandari dar!

..kuongezeka kwa ufisadi na rushwa!

..kushuka kwa bidii ya kazi na shughuli za maendeleo!

..watanzania kukata tamaa!

....hapo juu mambo yamechanganywa!nia ni kujiuliza vizuri,nini tumekifanya cha maana,kwani vingi vimefanywa!.kusema hamna kitu ni sawa na kumkataa mwanao,kisa umegombana na mkeo!

Nakubaliana nawe mwanaume wewe kwa hili.

Ongezea orodha ya mambo aliyoacha mkoloni ambayo tumeshindwa hata kuyaendeleza

Asha
 
Mafanikio:
Tumefanikiwa kulinda uhuru wetu.

Tumeonesha dira kwa nchi nyingine za kiafrika juu ya kuungana ya Kuwa na nchi za kisasa badala ya kuishi kwa kufuata mipaka ya kikoloni.

Tumesaidia wenzetu kujikomboa kutoka makucha ya ukoloni, mathalani msumbiji,angola, zimbabwe, kwa maana hiyo dhana yetu ya kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro umulike hata nje ya mipaka yetu,ulete tumaini, tumeitekeleza kwa vitendo.

Tumejenga Taifa moja, bila kujali misingi ya kikabila

Tumepunguza ujinga kwa kiasi kikubwa sana, mathalani asilimia ya watanzania walioweza kusoma na kuandika mwaka 64 ni ndogo ukilinganisha na watanzania wenye kujua kusoma na kuandika mwaka 2007.

tumeweza kujenga misingi ya kidemokrasia kwa kasi ya ajabu, mathalani tunabadilisha viongozi kwa awamu, kwa salama na amani,uhuru wa vyombo vya habari umepanuka,wananchi kutoa maoni yao kuhusu utendaji wa serikali yao pasi na hofu ya misukosuko.

Tumejenga Taasisi nyeti za kulinda mafanikio yeyote yawayo, tuna jeshi la ulinzi lenye nidhamu nzuri.

Uhuru gani unaozungumzia tumeulinda? Tulitaka uhuru tujiamulie mambo yetu. Bado tunaendelea kuamuliwa mambo yetu na mabeberu na mashirika yao.

Tulitaka uhuru ili tujiendeleze. Bado walio wengi ni watumwa wa ujinga, umasikini na maradhi.

Tulitaka uhuru ili tujitegemee. Bado tunategemea wahisani hata kutujengea vyoo.

Tuliowakomboa-Angola, Afrika Kusini nk wametuacha kwenye mataa, wao wanazidi kuwa huru na wengine hata wameanza kutugeuka na kututawala. Mwenge wa Tanzania tumaini ulishazimika, sasa ni aibu hata kusema wewe ni mtanzania huko ulipo.

Taifa moja lipi? La wakina SAS kuitwa waarabu, wahindi kujifungia wenyewe maghorofani na wa ushwahili kushindwa hata kusogolea Plazaz zinazojengwa DSM. Taifa lipi hilo ambalo kuna Uzanzibara na uzanzibar. Taifa lipi hilo lenye mbingu ya matajiri na jehanamu ya masikini. Taifa lipi hilo lenyewe wapaao hewani kwa gulf stream na watambaao aridhini wakiomba omba omba?

Ujinga upi huo uliopungua? Labda miaka ya 70 ya mwalimu na mkakati wa UPE na kisomo cha watu wazima. Sasa je, kati ya watanzania 37 milioni wangapi hawajui kusoma na kuandika? Kumbuka kuna ongezeko la watu. Ujinga upi huo, wa wananchi wasiojua haki zao? wanauza uhuru wao kwa pishi la mchele na kibaba cha chumvi? Ni ujinga huo huo unawatuma baadhi yetu kuamini kwamba miaka 46 baada ya uhuru tumepiga hatua kwenda mbele. Ni ujinga huo huo unaotufanya tushindwe kuona mataifa machanga zaidi yetu yakituacha solemba. Ni ujinga huo huo wa kujifungia chumbani na kujisifia uzuri wetu ili hali hata kioo cha kujitazama hatuna. Ni urembo wa kijinga kwa kweli, kupita kwa mikogo ya kupendeza kumbe uko uchi!

Kubadilishana uongozi wa amani ehhhh. Haya ni matusi kwa waliokufa Januari 26 na 27 na mipasho kwa wote walioshindwa katika chaguzi za kwa kutumia nguvu ya dola. Kamuulize Malecela, Salim na Mwandosya kama uongozi hubadilishwa kwa amani!

Jeshi lenye nidhamu nzuri au nidhamu ya woga tu kwa kupewa khanga na sukari? Mara ngapi jeshi hili limejaribu kupindua na kutulizwa kwa mkate na jibini? Nidhamu ya woga tu ya wanajeshi kupewa vyeo serikalini na kuwa sehemu ya watawala.

Tanzania kuna fukuto, amani amani amani amani. Ni wimbo wa imani imani imani tu. Ukweli ni vinginevyo, mkiendelea kujidanganya huku wananchi wanazidi kukata tamaa mjue mmekalia bomu la wakati. Mwenye njaa ni mwenye hasira! Anayeibiwa hukosa uvumilivu. Mob justice is along the way!

Shule ya msingi tulifundishwa. Mkoloni alikuja kupata masoko, kupata maeneo ya uwekezaji, kupata malighafi. Tukamuondoa kupata uhuru. Sasa ni vyema watoto wetu wakafundishwa darasani kuwa: Sasa amerudishwa tena na watoto wa Mangungo wa Msovero, wakina Karamagi, Kikwete, Mramba, Lowasa na wengine. Mkoloni amerudi upya- ndiye anayemiliki Buzwagi na wananchi wametimuliwa ili yeye apate malighafi. Mkoloni amerudhi upya, ndiye anayepora uwekezaji kwa mikataba na viongozi vibaraka. Ni mkoloni mamboleo. Mkoloni amerudi upya, ndiye anayeua viwanda vyetu vya ndani na kugeuza nchi kuwa dampo la bidhaa toka nje- kila mtu sasa ni mchuuzi, upuuzi mtupu!

Asha
 
Ongezea orodha ya mambo aliyoacha mkoloni ambayo tumeshindwa hata kuyaendeleza

Asha

..majengo mengi mazuri,ambayo yameachwa yakaharibika bila matengenezo,na mengine kubomolewa!

..mpangilio mji mzuri,ambao tumeuharibu kwa kulundika majengo bila maegesho ya kutosha na barabara zinazopitika!

..usafi mijini,imekuwa kama mtindo mpya kutupa uchafu kwenye rambo mitaani,hasa kariakoo!

..mashamba mengi na ranch kadhaa,zimekufa,utafikiri hatuli nafaka au nyama!au tumeacha kuuza mazao asilia nchi za nje!

..na mengine mengi baadae!
 
jamani la kuondoshwa kodi ya kichwa vipi si la kijivunia? ilikuwa watu huhama nyumba lkn sasa buheri wa hamsa wa hamsini
 
Back
Top Bottom