Miaka Miwili ya Chadema awamu ya tano: Mambo 7 ya kujitafakari...

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,697
1:Mawaziri vivuli bubu...

2Pmoja na kuwepo kwa fursa ya wabunge kuchochea maendeleo jimboni, wengi hawaonekani wakifungua hata kiwanda cha popcon ila ni rahisi kuwakuta wanalalamika wakidai fursa ya mtu wa mara kwenda kuongelea mtwara na matatizo yake. Au DSM kuongelea mambo ya kitaifa huku ya kijimbo haonekani.

3Pamoja na Mb Lissu kupata majanga (Mungu amponye na kumuwezesha arudi ktk hali yake) wote wamekaa kimya wakimsubiri yeye. Lifespan ya umaarufu wa press conference ambazo nyingi ni livestream ni masaa sita. Hazishawishi, hazina mambo mapya ya kufikirisha na kumbadili mtanzania masikini.

4: Ganzi ya jibu la mtuhumiwa wao wa ufisadi kupewa usukani kuwa ni asset au liability inazidi kuwashika. Katikati ya mkwamo huu wa kiitikadi wanatirirka wengi kuja upande huo ambao uadilifu wao ukiwekwa mzanini hupati jibu moja.

5:Baada ya malalamiko kuwa wamenyimwa uhuru, wengine wamefananisha na mpambano wa Man Pacquiao na myweather huku mmoja kafungwa kamba mikononi hawajaja na mbinu mbadala kwa wapenzi wao ktk kutimiza jukumu lao kama watafuta Dola. Badala yake utasikia wakitetea wapenzi wao wanaovunja sheria za mitandao bila kuwaambia ukweli kuwa hata kama sheria hiyo sio nzuri lakini ni HAI. Je wameachia asili iamue au wamekubali yaishe polepole akachapishe kadi mamillioni viongozi na wafuasi warudi nyumbani walikozaliwa?Je wamepatwa na dhahama ya ubunifu kisiasa?

6: Kumekuwa na upungufu mkubwa wa watetezi wa CHADEMA na CCM mitandaoni... Hapa naipongeza serikali kwa kubadili mentality za Uchama katika siasa za tanzania. Wengi wamejikita ktk Kukosoa serikali na kuipongeza. Je chadema hawaoni hili ombwe kama akitokea mtu wa kulijaza kwa kuonyesha mbadala chanya juu ya hiki kinachendelea watu ambao hawako kivyama wakimuelewa ndio chanzo cha kifo chao?

7: Hadi sasa Miaka Miwili kama chama hakijatoa muhutasari kinatoka wapi na kinaenda wapi na kwa style ipi. Kwa udhaifu huu hamuwezi kuaminika kupewa hata ubalozi wa nyumba kumi za wananchi wanaojitambua na wafuatiliaji wa mambo. Ni afadhali kupanda lori linaloenda kuliko kupanda bus luxury lenye sukani mbili nyuma na mbele muda wowote linaweza badili mwelekeo kwa kushtukiza.


CHADEMA miaka miwili ya awamu ya tano, Imefanya nini na itafanya nini mitatu ijayo?
Note:Maoni huru ya mwananchi huru ninaeunga mkono mazuri yote ya Serikali iliyopo Madarakani na changamoto chanya za wapinzani.
 
Nashukuru kwa hekima na maneno yako mazuru yasiyo na ushabiki wakupindukia..Naamini kuna ukweli mwingi zaidi ya ushabiki na wenye akili wataelewa VIVA kwako mkuu
 
Tusiposaidiana kuwasema viongozi wa Chadema sahauni mabadiliko ya utawala miaka ya karibuni ....viongozi wamelewa sifa mnazowapa hata wakikosea ....msisubiri hadi watu mnaowaheshimu waanze kulalamika muwaone wasaliti kama mnavyoona wengine ....Chadema haiko organised ....aibu tupu
 
Kuvunja umoja wa vyama vya upinzani East Africa kwa ku support chama Tawala KE hata baada ya kuonyesha ukandamizaji na mauaji kwa wafanyakazi waadilifu wa tume ya uchaguzi..
 
Tusiposaidiana kuwasema viongozi wa Chadema sahauni mabadiliko ya utawala miaka ya karibuni ....viongozi wamelewa sifa mnazowapa hata wakikosea ....msisubiri hadi watu mnaowaheshimu waanze kulalamika muwaone wasaliti kama mnavyoona wengine ....Chadema haiko organised ....aibu tupu
ni sawa na mjusi anaeamini yeye ni mamba na anauwezo wa kupambana na mamba na kaaminisha hivyo kikundi cha watu wachache wanaompenda kwa sababu wanamchukia mamba sio kwa sababu anauwezo wa kupambana na mamba.
 
Kuvunja umoja wa vyama vya upinzani East Africa kwa ku support chama Tawala KE hata baada ya kuonyesha ukandamizaji na mauaji kwa wafanyakazi waadilifu wa tume ya uchaguzi..
asante mkuu...
hili sikulikumbuka...

wapenzi wa chadema mje leo mpumzike kidogo kuisema serikali mjadili mnachokipenda na mapungufu yake vinginevyo tukiwaita wanafiki msitutupie vyupa wakuu.
 
Sio kila kiongozi yuko tayari kukutwa na yaliyomkuta TAL. Saa nyingine kawoga kapo na familia zinawabana sana. Wananchi wote kwa ujumla wao wanatakiwa wapinge vitendo vya uvunjifu wa katiba kwa kuzuia siasa za upinzania
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom