UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,718
Nisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane.
Huwa ninajaribu kuitazama Afrika(Bara)na watu waishio humo ndani hasa ngozi nyeusi nabaki kupata sintofahamu! Mimi ni mkristo na nina amini ya kwamba Mwanadamu ameumbwa na Mungu. Sasa huwa napata taabu sana kuona kwanini sisi waafrika tupo tofauti na jamii nyingine hasa weupe!. Utofauti ninao usema hapa ni kuhusu - MAAMUZI, AKILI, UTENDAJI na UTEKELEZAJI WA MAMBO.
Leo nitajikita zaidi kwa jamii hii ya watu weusi wapatikanao Tanzania.
Kadiri miaka inavyozidi kusogea na teknolojia ikiongezeka kwa kasi,ndivyo jamii hii ya watu weusi wakaao Tanzania ni kama AKILI nazo zinazidi kupungua kwenye vichwa vya watu!.
Dubai ni nchi ndogo sana ambayo ni muunganiko wa zile nchi zinazounda jumuia ya falme za kiarabu (Emirates), kiasili Dubai ni Jangwa lakini wanamaji ya uhakika masaa 24, siku 7, miezi 12 na miaka yote!
Naomba hapa niongeze sauti ili walioko baki bencha wasikie vizuri!.
"Dubai kiasili ni jangwa lakini wao kuhusu tatizo la maji wamebaki kulisoma kwenye vitabu na kuliona kwenye taarifa za habari ambazo nyingi huwa zinahusu Afrika"
Tanzania ambayo inakila kitu cha asili na iliyozungukwa na Maziwa makubwa,mito mikubwa,bahari na mabwawa ya kila aina lakini bado wananchi wake wanaendelea kuteseka kuhusu maji.
Hii ngozi sijajua aliyetuachia laana ambayo haifutiki milele zote ni nani! Je ni kwamba hatuna akili? Hili mbona kama nalikataa! Hivi ndugu zangu ni kweli hatuna akili? Ni kitu gani kinachotusumbua sisi ngozi nyeusi?.
Sasa kila mmoja wetu hapa anafahamu kwasasa jiji la Dar es salaam na viunga vyake kuna mgao mkubwa wa maji na umeme, nadhani kwasasa siyo Dar es salaam pekee bila shaka ni nchi nzima!.
Dunia ya leo ya Sayansi na Teknolojia eti tunategemea maji ya mto Ruvu ndiyo yanyweshe mamilioni ya wakaazi wa Dar es salaam, hivi kweli tuko serious? Hivi ni nani aliyeturoga? Hivi tumemkosea nini Mungu mpaka kutuadhibu kiasi hiki? yaani Dubai ambayo iko jangwani wanapata maji kwa uhakika lakini siye tuliozungukwa na kila aina ya maji tunakosa maji?
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam bil hata kuona haya na aibu anakaa kabisa mbele ya watu anasema ndugu zangu "Tumuombe Mungu ili mvua zinyeshe!"
Aisee hadi nashindwa kuandika!.
Kwani wale waarabu waliweza vipi kubadili yale maji chumvi kuwa maji ya matumizi ya kawaida? gharama yake ni kubwa kiasi gani hadi sisi kama taifa tushindwe kuafodi? ina maana akili za viongozi wetu ndiyo zimefika mwisho!
Leo Karne ya 21 maji tu ni shida kwenye jiji kubwa kama Dar es salaam, je huko vijijini hali ikoje?
Wenzetu kadiri miaka inavyosonga wanapanuka kiakili lakini sisi ngozi nyeusi pamoja na kwenda shule ndiyo kama akili zinarudi nyuma!.
Tanzania ni mfano tu lakini nchi karibia zote za kiafrika matatizo hufanana!
Aisee kiukweli nina mengi moyoni lakini ngoja niishie hapa, hata kuandika sasa imeniwia vigumu!
Huwa ninajaribu kuitazama Afrika(Bara)na watu waishio humo ndani hasa ngozi nyeusi nabaki kupata sintofahamu! Mimi ni mkristo na nina amini ya kwamba Mwanadamu ameumbwa na Mungu. Sasa huwa napata taabu sana kuona kwanini sisi waafrika tupo tofauti na jamii nyingine hasa weupe!. Utofauti ninao usema hapa ni kuhusu - MAAMUZI, AKILI, UTENDAJI na UTEKELEZAJI WA MAMBO.
Leo nitajikita zaidi kwa jamii hii ya watu weusi wapatikanao Tanzania.
Kadiri miaka inavyozidi kusogea na teknolojia ikiongezeka kwa kasi,ndivyo jamii hii ya watu weusi wakaao Tanzania ni kama AKILI nazo zinazidi kupungua kwenye vichwa vya watu!.
Dubai ni nchi ndogo sana ambayo ni muunganiko wa zile nchi zinazounda jumuia ya falme za kiarabu (Emirates), kiasili Dubai ni Jangwa lakini wanamaji ya uhakika masaa 24, siku 7, miezi 12 na miaka yote!
Naomba hapa niongeze sauti ili walioko baki bencha wasikie vizuri!.
"Dubai kiasili ni jangwa lakini wao kuhusu tatizo la maji wamebaki kulisoma kwenye vitabu na kuliona kwenye taarifa za habari ambazo nyingi huwa zinahusu Afrika"
Tanzania ambayo inakila kitu cha asili na iliyozungukwa na Maziwa makubwa,mito mikubwa,bahari na mabwawa ya kila aina lakini bado wananchi wake wanaendelea kuteseka kuhusu maji.
Hii ngozi sijajua aliyetuachia laana ambayo haifutiki milele zote ni nani! Je ni kwamba hatuna akili? Hili mbona kama nalikataa! Hivi ndugu zangu ni kweli hatuna akili? Ni kitu gani kinachotusumbua sisi ngozi nyeusi?.
Sasa kila mmoja wetu hapa anafahamu kwasasa jiji la Dar es salaam na viunga vyake kuna mgao mkubwa wa maji na umeme, nadhani kwasasa siyo Dar es salaam pekee bila shaka ni nchi nzima!.
Dunia ya leo ya Sayansi na Teknolojia eti tunategemea maji ya mto Ruvu ndiyo yanyweshe mamilioni ya wakaazi wa Dar es salaam, hivi kweli tuko serious? Hivi ni nani aliyeturoga? Hivi tumemkosea nini Mungu mpaka kutuadhibu kiasi hiki? yaani Dubai ambayo iko jangwani wanapata maji kwa uhakika lakini siye tuliozungukwa na kila aina ya maji tunakosa maji?
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam bil hata kuona haya na aibu anakaa kabisa mbele ya watu anasema ndugu zangu "Tumuombe Mungu ili mvua zinyeshe!"
Aisee hadi nashindwa kuandika!.
Kwani wale waarabu waliweza vipi kubadili yale maji chumvi kuwa maji ya matumizi ya kawaida? gharama yake ni kubwa kiasi gani hadi sisi kama taifa tushindwe kuafodi? ina maana akili za viongozi wetu ndiyo zimefika mwisho!
Leo Karne ya 21 maji tu ni shida kwenye jiji kubwa kama Dar es salaam, je huko vijijini hali ikoje?
Wenzetu kadiri miaka inavyosonga wanapanuka kiakili lakini sisi ngozi nyeusi pamoja na kwenda shule ndiyo kama akili zinarudi nyuma!.
Tanzania ni mfano tu lakini nchi karibia zote za kiafrika matatizo hufanana!
Aisee kiukweli nina mengi moyoni lakini ngoja niishie hapa, hata kuandika sasa imeniwia vigumu!