Miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika: Mama Maria Nyerere na mabaibui katika mikutano ya TANU Mnazi Mmoja

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,853
30,196
MIAKA 60 YA UHURU WA TANGANYIKA: MABAIBUI YALIYOMPOKEA MWALIMU NA MAMA MARIA NYERERE VIWANJA VYA MNAZI MMOJA WAKATI WA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

Katika mazungumzo na BBC Swahili jana Mama Maria Nyerere amewasifia mama zetu kwa ushujaa wao wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Dada yangu Ummie Alley aliniomba nimtafutie hawa akina mama na nililiweka hapa historia fupi ya kina mama hawa wa TANU waliomuunga mkono Mwalimu Nyerere kuanzia siku ya kwanza alipopanda jukwaani Mnazi Mmoja kuidai Tanganyika.

Akina mama hawa Mama Maria anawajua vizuri sana - Bi. Chiku bint Said Kisusa, maarufu akifahamika kama Mama Sakina, Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu Mama Daisy, Bi. Hawa bint Maftah kwa kuwataja wachache.

Hawa ndiyo walikuwa mashoga zake waliompokea yeye na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Dar es Salaam ile ya miaka ya 1950.

Nilimuahidi Da Ummie kuwa nitamwekea picha ya hawa akina mama wakiwa katika mkutano wa TANU Mnazi Mmoja picha iliyopigwa na Mohamed Shebe.

Angalieni picha hiyo hapo chini ambayo Shebe ameipiga kutoka juu.

Utaona kuna sehemu imejitenga kuna nyeusi tupu.

Huo weusi ni mabaibui ya mama zetu ambao miaka hiyo katika mikutano yote ya TANU wanawake walikuwa na sehemu yao maalum wakikaa.

Hapo ndipo zilipokuwa kunatoka vigelegele na nyimbo za lelemama Julius Nyerere alipokuwa anapanda jukwaani kaongozana na Sheikh Suleiman Takadir, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Sheikh Suleiman Takadir yeye kazi yake ilikuwa kupiga fatha kuomba dua kisha kumtambuisha Julius Nyerere kwa wenyeji wa Dar es Salaam.

Kumtia hamasa Mwalimu, Bi. Titi Mohamed na Hawa bint Maftah wataanzisha nyimbo maarufu ya lelemama na uwanja mzima utaimba:

''Mheshimiwa nakupenda sana,
Wallahi sina mwinginewe,
In Shaa Allah Mungu yupo,
Tanganyika tutajitawala.''

Screenshot_20211207-220536_Facebook.jpg
 
Samahani nina swali ulikuwa mmoja waliozungumza kwenye kipindi cha maoni mbele ya meza duara DW kuhusu maisha ya Maalim Seifu
 
Baba...
Inawezekana sina hakika kwa kuwa mahojiano na DW ni mengi nimefanya.
Heshima kwako Mohamed said yale majadiliano kwangu yalikuwa bora sana niliyarekodi na kila nilipopata muda nilikuwa nayasikiliza na sikuwahi kuyachoka kila kitu kilikuwa on point kuanzia mtangazaji mpaka wachangiaji na kwa kumbukumbu za haraka wachangiaji wengine walikuwa Ahmed Rajabu, Padri Privatus Kalugendo na mchangiaji mwingine alikuwa toka Zanzibar jina limenitoka kidogo lakini licha ya kilichokadiriwa kuwa na ubora lakini kilipendezeshwa sana na uwezo wa stadi za kuongea za wachangiaji natamani nifike hata nusu ya uwezo ule wa kuwasilisha maoni katika namna iliyo bora kabisa
 
Heshima kwako Mohamed said yale majadiliano kwangu yalikuwa bora sana niliyarekodi na kila nilipopata muda nilikuwa nayasikiliza na sikuwahi kuyachoka kila kitu kilikuwa on point kuanzia mtangazaji mpaka wachangiaji na kwa kumbukumbu za haraka wachangiaji wengine walikuwa Ahmed Rajabu, Padri Privatus Kalugendo na mchangiaji mwingine alikuwa toka Zanzibar jina limenitoka kidogo lakini licha ya kilichokadiriwa kuwa na ubora lakini kilipendezeshwa sana na uwezo wa stadi za kuongea za wachangiaji natamani nifike hata nusu ya uwezo ule wa kuwasilisha maoni katika namna iliyo bora kabisa
Baba...
Nimekumbuka nilishiriki kipindi hicho.
Ahsante sana.
 
Motive yako ni nini hasa unaposema mabaibui yaliwapokea Mwl Nyerere pamoja na Mama Maria?
Hivi, ungeliandika kuwa wanawake wengi waliwapokea Mwl Nyerere na Mama Maria, je ingeleta shida yoyote?
 
Motive yako ni nini hasa unaposema mabaibui yaliwapokea Mwl Nyerere pamoja na Mama Maria?
Hivi, ungeliandika kuwa wanawake wengi waliwapokea Mwl Nyerere na Mama Maria, je ingeleta shida yoyote?
Isele...
Unahisi kuwa ni makosa kufanya hivyo?
Ikiwa unaona labda si uungwana nakutaka radhi.

Lakini aliyetaja mabaibui ni Mama Maria Nyerere na mimi nimelipenda neno hilo.
 
Mzee mohamed said, nakuheshimu kwa asilimia nyingi, shukran kwa kuonyesha busara ya hali ya juu na kujua historia ya uhuru wa tanganyika

,
Isele...
Unahisi kuwa ni makosa kufanya hivyo?
Ikiwa unaona labda si uungwana nakutaka radhi.

Lakini aliyetaja mabaibui ni Mama Maria Nyerere na mimi nimelipenda neno hilo.
 
mzee heshima kwako,historia murua kabisa ,unavyoisoma unatamani hata mtu ungekuwepo uyaone yote,maisha ya zamani inaonekana yalikuwa Safi Sana.I wish ningelikuwepo enzi hizo.ha ha ha ha !!
 
nimekuelewa sana babu yangu...Mungu akujaalie umri mrefu tuzidi kupata madini kama haya na zaidi
 
Back
Top Bottom