Miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika: Uhuru una maana gani leo?

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Mar 2, 2007
1,562
10,880
Zitto Kabwe

Tarehe 9 Desemba 1961 Tanganyika iliingia katika Jumuiya ya Mataifa huru duniani baada ya kupata Uhuru wake kutoka Himaya ya Uingereza. Muda mfupi baadaye Tanganyika ikawa mwanachama wa Umoja wa Mataifa. Safari ya kwanza ya nje ya Nchi ya Mwalimu Julius Nyerere kama Mkuu wa Serikali ilikuwa tarehe 14 Desemba 1961 kwenda New York kwa ajili ya kupokea uanachama wa Tanganyika katika Umoja wa Mataifa.Siku ya Uhuru Mwalimu Nyerere alitoa hotuba fupi sana ya kupokea ‘instruments of independence’ kutoka kwa mwakilishi wa Malkia wa Uingereza. Kabla ya hapo, akiwa Rais wa TANU, alitoa salamu za Uhuru ambapo pamoja na mambo mengine alieleza maana ya Uhuru ambao Watanganyika waliupigania. Aliwakumbusha wanachama wa TANU kuwa “ muda wote ambao tumekuwa tukipambana kupana Uhuru wa Nchi yetu, tuliweka msingi kuwa Imani yetu ni usawa na heshima ya utu kwa watu wote na kuheshimu tangazo la haki za binaadam”. Alisisitiza kwa wana TANU kuwa, “hakuna rangi, dini, kabila, au kingine chochote kile kinachoweza kumwondolea mtu haki yake ya kuwa sawa mbele ya Jamii yake”. Aliwaambia wana TANU kuwa ni lazima kuendelea kupambana na “ umasikini, ujinga na maradhi” ili kujenga Jamii ya watu waliosawa na huru. Katika mazingira ya sasa unaweza kusema kuwa hata kuwa mwanachama wa chama cha Siasa tofauti na kilichopo madarakani hakuwezi kukuondolea haki yako kama Mtanzania mwengine yeyote. Hii ndio maana ya Uhuru ambao waasisi wan chi yetu waliamini.

Hata hivyo, utapata maana ya Uhuru kwa Wazee wetu kwa mapana Zaidi katika Hotuba ya Mwalimu Nyerere ya Desemba 10, 1962 wakati Mwalimu Nyerere anahutubia Taifa kama Rais wa Jamhuri ya Tanganyika. Ikumbukwe Mwalimu alijiuzulu Uwaziri Mkuu na kutumia mwaka mzima kujenga TANU kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika. Katika Hotuba hii ambayo inapaswa kusomwa na kila Mtanzania kuanzia Rais wa Tanzania mpaka mwanachi wa kawaida, Mwalimu Nyerere anaeleza maana ya Uhuru ambao waliupigania yeye pamoja na wenzake akiwemo Hamza Mwapachu, AbdulWahid Sykes na wadogo zake, Denis Phombeah, Oscar Kambona, Rashidi Kawawa, Dossa Aziz, John Rupia, Titi Mohammed, Andrew Tibandebage, Vedastus Kyaruzi, Steven Mhando na wengine wengi ambao kwa hakika hawathaminiwi wala kuenziwa. Sina hakika kama Nchi hii hata kuna Mtaa au Barabara iliyopewa jina la Mtu kama Hamza Mwapachu au Vedastus Kyaruzi kuenzi uasisi wao wa Taifa letu.

Katika Hotuba hii ya 10/12/1962 Mwalimu Nyerere anasema “Uhuru tulioupigania sio tu uhuru dhidi ya mkoloni; tulitaka uhuru wa watu wetu binafsi kufanya mambo yao na kujitafutia kipato chao kwa ajili ya maisha yao yenye Utu”. Aliendelea kusema “ tunataka kila raia awe sawa na mwengine na hakuna ubaguzi wowote”. Maneno haya ya Mwalimu yanaweza kutafsiri maana ya Uhuru kwa uendelevu kwani ni rahisi kupima kama kila mwananchi ana haki sawa mbele ya Jamii, haswa bila kujali itikadi za kisiasa. Lakini tafsiri hii ya Uhuru ina maana hivi sasa? Watanzania wa leo, ( baada ya Nchi mbili zenye hadhi sawa mbele ya sharia ya kimataifa kuungana – Tanganyika na Zanzibar ), wana tafsiri Uhuru sawa na Watanzania wa miaka ya 1960?

Takwimu rasmi za Serikali zinaonyesha kuwa ni 3% tu ya Watanzania wanaoishi walikuwepo mwaka 1961 wakati Tanganyika inapata Uhuru. Watanzania wengi, 71%, hawakuwa wamezaliwa mwaka 1995 wakati wa Uchaguzi wa kwanza chini ya Demokrasia ya Vyama vingi. Asilimia 65 ya Watanzania wanaoishi sasa wala hawakuwahi kumwona Mwalimu Nyerere akiwa hai. Kwa Watanzania hawa, Uhuru wa Tanganyika una maana gani kwao? Ni Uhuru wa kumtoa Mkoloni na kupandisha Bendera ya Tanganyika tu au ni Uhuru wa kuondokana na Umasikini, Ujinga na maradhi?

Kuna baadhi ya watu wanajenga hoja kuwa Uhuru wetu ni kujenga Barabara, Reli, vituo vya kufua Umeme, madaraja nk. Lakini Mkoloni alifanya haya. Mkoloni Mjerumani alijenga Reli ya Kati kutoka Pwani mpaka Bara ( Dar es Salaam – Kigoma ) na kutoka Tanga mpaka Dar es Salaam. Mkoloni mwingereza akamalizia Reli mpaka Mwanza na Mpaka Moshi na Arusha. Wakoloni walijenga mashule ambayo kina Mwalimu Nyerere walisoma n ahata barabara mbalimbali na Mahospitali. Lakini haya ‘maendeleo’ aliyoleta Mkoloni hayakuwafanya Wazee wetu waseme “ sasa Uhuru wa nini wakati barabara zimejengwa, Shule zipo n ahata Reli zimejengwa”. Wazee wetu walitaka Uhuru wa wananchi kujiamulia wenyewe mambo yao. Uhuru wa kuzungumza watakacho. Uhuru wa kuendesha maisha yao bila hofu ya kukamatwa, kuuwawa au kushtakiwa na kufungwa. Kina Nyerere na Hamza Mwapachu hawakujali miundombinu inayojengwa kwani wao walitaka kujenga Taifa.

Mwalimu Nyerere alisema hili vizuri wakati wa Hotuba ile ya 10 Desemba, 2019. Aliwaambia Watanganyika “kujenga nchi sio kujenga barabara za lami, majengo makubwa na mahoteli ya kifahari. Nchi inaweza kuwa na hayo yote lakini isiheshimike. Kujenga Taifa ni kujenga Watu”. Wazee wetu hawa walijaribu kweli kujenga Taifa kwa kujenga watu. Tanganyika na baadaye Tanzania ilikuwa inaheshimika duniani sio kwa sababu ya utajiri wake wa madini nk bali kwa Utu wa watu wake, tabia za watu wake na misingi imara ya kutetea haki za watu waliokuwa wanaonewa. Leo Tanzania bado ni Taifa lenye heshima hii?

Uhuru waweza kuwa na maana tofauti kabisa kwa 71% ya Watanzania ambao wamezaliwa baada ya mwaka 1995. Uhuru kwao ni Uhuru dhidi ya Umasikini, kulisha familia zao na kuepukana na njaa. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, 49% ya Watanzania wanaishi kwenye dimbwi la umasikini kwani hawana uwezo wa kutumia shilingi 5000 kwa siku. Iwapo kuna miaka 58 ya Uhuru lakini nusu ya Wananchi hawawezi kula mlo mmoja kwa siku Uhuru una maana gani? Wenzetu ambao tulipata Uhuru wakati mmoja, kama Malaysia, ni 3% tu ya watu wao wanaitwa masikini.

Uhuru kwa 71% ya Watanzania ni Uhuru wa usalama wao. Kwamba waweze kuishi bila kuogopa kuwa wanaweza kutekwa na kupotezwa. Matukio ya Utekaji na Mauaji ni miongoni mwa masuala makubwa manne ambayo Watanzania wanasema yanawaumiza mno. Utafiti uliofanywa twaweza unaonyesha kuwa 54% ya wananchi, pamoja na mambo mengine, wanaumizwa sana na 1) Ukosefu wa Ajira, 2) kuminywa kwa Uhuru wa watu na 3) Utekaji na Mauaji. Hii ina maana kuwa kwa Watanzania wa sasa Uhuru kwao maana yake ni kuwa na ajira, kuwa na haki ya Uhuru wa mawazo na kuwa na haki ya uhuru wa usalama wake.

Ni Dhahiri kuwa maana ya Uhuru kwa Watanganyika wa miaka ya sitini ni tofauti na ile ya Watanzania wa kizazi cha demokrasia. Hivyo kama watu hawana uhuru wa kutoa mawazo yao, kukosoa Serikali yao, kujipatia ajira atakayo, kupata na kutoa habari na Uhuru dhidi ya umasikini, kwanini washerehekee siku ya Uhuru? Kwa wale 3% siku hii inaweza kuwa na maana kubwa maana waliona mkoloni mzungu akitoka na mweusi akijitawala. Sio kwa Watanzania wengi.

Mtanzania aliyezaliwa mwaka 1995 ambaye anaona utawala wa chama kile kile, chaguzi zikiibwa kila wakati wa uchaguzi, magazeti yakifungiwa, waandishi wa habari wakipotea kwa miaka 2 na wengine kufungwa jela kwa makosa ya kubambikiwa, wabunge wakifunguliwa mashtaka ya uongo na wengine kutwangwa risasi, wavuvi wakichomewa nyavu na kufanywa masikini, wakulima wakichukuliwa mazao yao kwa nguvu na majeshi na kutolipwa kwa miaka 2, Wafanyabiashara kubambikiwa makesi na kuporwa fedha zao za marejesho ya kodi, Wafanyakazi hawaongezewi mishahara kwa miaka minne licha ya gharama za maisha kupanda kiasi cha debe la mahindi kuwa ghali kuliko mfuko wa saruji wa 50kg, Watanzania 2.7 milioni wamedumbukiwa kwenye umasikini kati ya 2016-2018, Wanasiasa wakizuiwa kufanya mikutano kuzungumza na wananchi kwa miaka minne na mengine lukuki, anajiuliza Uhuru huu maana yake nini?
 
Hivi hizi siasa za maneno tupu pasi na kuchukua action dhidi ya serikali ya ccm inakandamiza uhuru wa raia na upinzani kwa sasa tumezichoka muheshimiwa

Uchaguzi wa serkali za mitaa mliishia kutoa vitisho tu *tusilaumiane* mwisho wa siku mnaufyata kimya, tuhitaji tuungane pamoja ninyi viongozi mkae mstari wa mbele tupambane na jiwe
 
kwa bandiko lako hili hakuna uhuru
je wewe kama kiongozi wa upinzani umechukua hatua zipi zenye mashiko dhidi ya utawala huu wa chama kilekile? hapa sihitaji maneno tupu

unazungumziaje kitendo cha chadema (chama unachotarajia kushirikiana nacho 2020 kwenye uchaguzi) kushiriki sherehe za uhuru
 
Zito wananchi wa kigoma hususani jimboni kwako umewatelekeza na kukimbilia town ,unaponda maisha mjini kijijini hawakuoni upo fb,insta,jf na Twitter as if jimbo ni mitandao

Umejipa ubunge wa kitaifa kukwepa majukumu yako na sasa unautaka urais ,asiye mwaminifu kwa kidogo hata kikubwa hawezi kuwa mwaminifu

Mwaka 2010 dk slaa alikusaidi ingawa chadema ilikosa viti vingi vya madiwani ukakimbilia mjini nako wamekuchoka na vijistory kama hivi

Endelea na kelele zako za mitandaoni utauza ubunge

USSR
 
Mapambano dhidi ya mkoloni yalilenga kuondoa utawala wa Taifa jingine juu ya Tanganyika, tukapata Uhuru, lakini Uhuru huu haukutosha,kuna Uhuru mwingine ambao ulitakiwa utafutwe kwa mapambano mapya ndani ya nchi.

Uhuru kati ya mtu na mtu, kuondoa mila na sheria kandamizi,tunaona akina mama jinsi wanavyozidi kupata haki katika ardhi na mengineyo. Pia watoto na hata wanaume

Uhuru wa kitaasisi

Uhuru wa kiuchumi ndani ya nchi,kati ya mtu na mtu, taasisi na taasisi,nchi yetu dhidi ya nchi nyingine

Uhuru wa kisiasa

Kimsingi,Uhuru baada ya Uhuru, ni. Mapambano endelevu, bado tunapambana kupata Uhuru kamili wa kiuchumi kama taifa,bado tunapambana kupata Uhuru kamili wa kisiasa kama taifa, pia Uhuru wa kijamii na kitamaduni.

Pia bado kina mapambano ambayo ni endelevu kupigania Uhuru kati ya taasisi na taasisi ndani ya nchi,mtu na mtu, mtu na taasisi

Ni wakati wa kujadili tumepiga hatua gani kuufikia uhuru kamili,na je Uhuru huu umebadilisha tu mkoloni,katoka mweupe kama mweusi, je jamii ina la kujivunia kutokana na Uhuru,matarajio yakoje?

Je wewe kama taasisi,mtu binafsi, baada ya kuondoa mkoloni ndio ukabweteka na kusema "imekwisha'? Bado,mkoloni aliondoa bendera tu,na safari ya kuelekea kwenye Uhuru kamili ni ndefu sana,hasa kwa Tanzania,pia safari ya kuulinda Uhuru ni ngumu na ndefu zaidi kwa kuwa hata katiba inaotupa Uhuru huo inakwazwa tukiona,na hatuko tayari kuilinda kwa vitendo
 
Msisitizo wa Hotuba ya UHURU (1961)

- Usawa, heshima ya utu kwa watu wote

- kuheshimu haki za binaadam

Alisisitiza kwa wana TANU kuwa hakuna
- rangi
- kabila
- dini
- kingine chochote kinachoweza kumwondolea mtu HAKI ya kuwa sawa mbele ya Jamii yake

Aliwaambia wana TANU kuwa ni lazima kuendeleza mapambano dhidi ya
- umaskini
- ujinga
- maradhi
Je, hali ikoje leo, miaka 58 baada ya tangazo hilo?

Hotuba ya Mwalimu Nyerere 10/12/1962
Msisitizo juu ya dhumuni la kupigania uhuru -
- kupatikana kwa uhuru wa watu binafsi kufanya mambo yao na kuendesha maisha yao ya 'utu na heshima'.
- kila raia awe na HAKI sawa na mwingine bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Takwimu za Serikali:
- Asili mia tatu tu ya waTanzania wa leo ni 'waTanganyika wa Uhuru? (1.5 milioni)?

1995 Demokrasia. Ujio wa Vyama vingi vya Siasa
- Asilimia 71 ya waTanzania wa leo walikuwa hawajazaliwa 1995 (35 milioni)? Hawa ndio wapiga kura wa leo hasa!!
Tusiwasingizie wazee wa uhuru tena!
- Asili mia 65 ya waTanzania wa leo wanamsikia tu Mwalimu Nyerere. Hawakupata kumwona.

Kujenga Taifa ni Kujenga Watu
-
Tanzania iliheshimika duniani, pamoja na umaskini wake kwa sababu ya UTU WA RAIA WAKE
- tabia za watu wake na misingi imara ya kutetea HAKI za watu waliokuwa wanaonewa

WaTanzania wa baada ya 1995
- maana ya UHURU kwao ni mapambano dhidi ya umaskini, maradhi, UJINGA?

Umaskini wa waTanzania wa 2019

Benki ya Dunia -
- asili mia 49 ya waTanzania (24.5 milioni) hawana uwezo wa kupata mlo zaidi ya mmoja kwa siku?
- hawamudu kutumia Tsh 5,000/ ($2.17) kwa siku [Tsh 150,000/mwezi ($65.21/mwezi)]
(Ngoja niwaite waliopo hapa JF kwa ushuhuda)!

Miaka 58 baada ya kuwa huru, nusu ya wananchi hawawezi kumudu gharama za milo miwili kwa siku?

Mfano wa Malaysia umetolewa kama mfano wa nchi aina yetu ambazo zimetuacha kwenye mataa! HAPANA, tuwe waangalifu na mifano hii. Tusiitumie tu bila ya kuangalia tofauti zilizokuwepo kati yetu na wao baada ya uhuru.
Hiki sio kisingizio cha kuchelewa sana kwetu, lakini ni lazima tuzizingatie tofauti hizo.

Maana ya Uhuru kwa asilimia 71 ya waTanzania - Kizazi cha Demokrasia
- uhuru wa usalama wao
- kuishi bila kuogopa kutekwa, kupotezwa, kuwekwa mahabusu, kubambikiziwa kesi, n.k.

Utafiti wa Twaweza (hivi bado wapo, maana siwasikii tena?)

Asilimia 54 wanahangaishwa na
- HAKI ya uhuru wa mawazo
- kukosekana kwa ajira
- hofu ya usalama wao

Maana ya UHURU kwa waTanganyika wa miaka ya 60 ni Tofauti na ile ya waTanzania wa 1995? (HAPANA)
- nani asiyetaka kuwa na UHURU wa kutoa mawazo!
- uhuru wa kukosoa serikali yake?
- kujipatia ajira (watanganyika wengi wanastaafu/ huko vijijini bado kuna wanaopinda migongo?)
- kupata na kutoa habari - wote wanayataka haya.

Nilitaka kuongeza maoni yangu mengi humu, lakini acha kwanza 'first eleven' waingie uwanjani

Kwa sasa nasema, "Lawama iwaangukie asili mia 71 kwa kushindwa na adui yao namba moja - 'UJINGA'
 
huna akili, kila siku mmekalia kucopy na kupaste habari na machapisho ya watu na kuyafanya ya kwenu

fikirisha mbongo zako nawewe upate bandiko lako na huo ndio uhuru
Hapa unamshutumu nani, Zitto, au aliyebandika mada hapa JF? Sasa wewe ni kipi kilichokunyima raha yaliyomo kwenye bandiko, au aliyeyaweka hapa ili sote tuyasome?

Aaah, nilikuwa sijakusoma uliyoweka huko mwanzo.
Sasa hawa wakikata tamaa, kama unavyochochea iwe, wewe utafaidika vipi?
 
Msisitizo wa Hotuba ya UHURU (1961)

- Usawa, heshima ya utu kwa watu wote

- kuheshimu haki za binaadam

Alisisitiza kwa wana TANU kuwa hakuna
- rangi
- kabila
- dini
- kingine chochote kinachoweza kumwondolea mtu HAKI ya kuwa sawa mbele ya Jamii yake

Aliwaambia wana TANU kuwa ni lazima kuendeleza mapambano dhidi ya
- umaskini
- ujinga
- maradhi
Je, hali ikoje leo, miaka 58 baada ya tangazo hilo?

Hotuba ya Mwalimu Nyerere 10/12/1962
Msisitizo juu ya dhumuni la kupigania uhuru -
- kupatikana kwa uhuru wa watu binafsi kufanya mambo yao na kuendesha maisha yao ya 'utu na heshima'.
- kila raia awe na HAKI sawa na mwingine bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Takwimu za Srikali:
- Asili mia tatu tu ya waTanzania wa leo ni 'waTanganyika wa Uhuru? (1.5 milioni)?

1995 Demokrasia. Ujio wa Vyama vingi vya Siasa
- Asilimia 71 ya waTanzania wa leo walikuwa hawajazaliwa 1995 (35 milioni)? Hawa ndio wapiga kura wa leo hasa!!
Tusiwasingizie wazee wa uhuru tena!
- Asili mia 65 ya waTanzania wa leo wanamsikia tu Mwalimu Nyerere. Hawakupata kumwona.

Kujenga Taifa ni Kujenga Watu
-
Tanzania iliheshimika duniani, pamoja na umaskini wake kwa sababu ya UTU WA RAIA WAKE
- tabia za watu wake na misingi imara ya kutetea HAKI za watu waliokuwa wanaonewa

WaTanzania wa baada ya 1995
- maana ya UHURU kwao ni mapambano dhidi ya umaskini, maradhi, UJINGA?

Umaskini wa waTanzania wa 2019

Benki ya Dunia -
- asili mia 49 ya waTanzania (24.5 milioni) hawana uwezo wa kupata mlo zaidi ya mmoja kwa siku?
- hawamudu kutumia Tsh 5,000/ ($2.17) kwa siku [Tsh 150,000/mwezi ($65.21/mwezi)]
(Ngoja niwaite waliopo hapa JF kwa ushuhuda)!

Miaka 58 baada ya kuwa huru, nusu ya wananchi hawawezi kumudu gharama za milo miwili kwa siku?

Mfano wa Malaysia umetolewa kama mfano wa nchi aina yetu ambazo zimetuacha kwenye mataa! HAPANA, tuwe waangalifu na mifano hii. Tusiitumie tu bila ya kuangalia tofauti zilizokuwepo kati yetu na wao baada ya uhuru.
Hiki sio kisingizio cha kuchelewa sana kwetu, lakini ni lazima tuzizingatie tofauti hizo.

Maana ya Uhuru kwa asilimia 71 ya waTanzania - Kizazi cha Demokrasia
- uhuru wa usalama wao
- kuishi bila kuogopa kutekwa, kupotezwa, kuwekwa mahabusu, kubambikiziwa kesi, n.k.

Utafiti wa Twaweza (hivi bado wapo, maana siwasikii tena?)

Asilimia 54 wanahangaishwa na
- HAKI ya uhuru wa mawazo
- kukosekana kwa ajira
- hofu ya usalama wao

Maana ya UHURU kwa waTanganyika wa miaka ya 60 ni Tofauti na ile ya waTanzania wa 1995? (HAPANA)
- nani asiyetaka kuwa na UHURU wa kutoa mawazo!
- uhuru wa kukosoa serikali yake?
- kujipatia ajira (watanganyika wengi wanastaafu/ huko vijijini bado kuna wanaopinda migongo?)
- kupata na kutoa habari - wote wanayataka haya.

Nilitaka kuongeza maoni yangu mengi humu, lakini acha kwanza 'first eleven' waingie uwanjani

Kwa sasa nasema, "Lawama iwaangukie asili mia 71 kwa kushindwa na adui yao namba moja - 'UJINGA'
Tukipata watanzania kama wewe nchi itazidi kuwa maskini na dhaifu, nakuona km umekuja kudai demokrasia ya mikutano sisi tunawaza maendeleo na sasa nchi inajengwa

History inaoesha tangu mfumo wa vyama vingi ndio uchumi ulianza kuyumba


USSR
 
Hapa unamshutumu nani, Zitto, au aliyebandika mada hapa JF? Sasa wewe ni kipi kilichokunyima raha yaliyomo kwenye bandiko, au aliyeyaweka hapa ili sote tuyasome?
Ili iweje

USSR
 
Tukipata watanzania kama wewe nchi itazidi kuwa maskini na dhaifu, nakuona km umekuja kudai demokrasia ya mikutano sisi tunawaza maendeleo na sasa nchi inajengwa

History inaoesha tangu mfumo wa vyama vingi ndio uchumi ulianza kuyumba


USSR
Ukweli huu ni mchungu sana kwa baadhi ya kundi la watu!
 
Zitto anasema ujenzi wa barabara sio kujenga nchi lakini hapa anajivunia barabara za kigoma ambazo anadai zimejengwa na chama chake cha ACT-Wazalendo na kwa sababu hiyo anaomba wananchi wakichague chama cha ACT-Wazalendo ili kiendelee kuwaletea maendeleo!

VIDEO
 
Tukiwa tunaadhimisha sikukuu ya uhuru wa nchi isiyokuwepo, yaani Tanganyika. Naam! Haipo kabisa, hata kwa kutajwa kwa jina lake ndani ya katiba yetu, hakuna, zaidi ya kubatizwa jina jipya la Tanzania Bara. Kimantiki Mh. Zito ameelezea historia ya nchi hiyo ya Tanganyika huru chini ya uongozi wa Mw. Nyerere na pia "status quo" ya hali ya mambo ilivyokuwa hivi sasa ndani ya vigezo vya taifa lile huru la Tanganyika, ukilinganisha na Tanzania ya sasa chini ya watawala wake wa leo.

Ni vyema wachangiaji tujikite ktk hoja ambazo Zito amezianisha, kwa kuwa ni hoja za kitaifa wala hazihusiani na mambo ya ubunge ktk jimbo lake la uchaguzi, ama kile kilichojiri kupitia kauli zake ktk uchafuzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji uliopita.
 
MsemajiUkweli,
Hii ni utekelezaji wa dhana ya kila mtu ana Uhuru wa kwenda atakako........barabara bora zinaimarisha Uhuru huu wa mtanzania kwenda atakako,bora tu asivunje sheria
 
Back
Top Bottom