Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,196
- 25,516
Kesho tarehe 9/12/2013, Tanzania Bara-iliyokuwa Tanganyika itasherehekea miaka 52 ya Uhuru wae.Tanganyika ilipata Uhuru wake mnamo tarehe 9/12/1961 kutoka kwa Waingereza waliokuwa wakiikalia nchi yetu hii pendwa kwa uangalizi ulioidhinishwa na Umoja wa Mataifa.
Rais wa kwanza wa Tanganyika huru alikuwa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Akiiongoza Serikali mpya huru,Hayati Mwalimu Nyerere alitangaza maadui wa Taifa hili: umaskini,ujinga na maradhi. Mwalimu Nyerere na Serikali yote waliamini kuwa kama nchi itapambana na maadui hawa,basi nchi itakuwa salama.
Umaskini ni kipato na hadhi ya maisha ya mtanganyika(sasa mtanzania) kuhusu mavazi,chakula na malazi. Na hata umaskini wa kiakili. Umaskini ulikuwa ni ajenda ya tangu Nyerere kutokomezwa. Kama nchi ambayo tayari imeshakuwa na marais wanne,tumefikia wapi? Vifaru vyetu vya kinchi vimemvurumisha adui huyu kwa umbali gani kurudi nyuma kuelekea kumtokomeza?
Ujinga ni kukosa maarifa;kukosa elimu. Kuhusu elimu, Serikali zote tangu uhuru zimekuwa zikipambana na adui huyu. Pamoja na kujenga shule,kufunza waalimu,wakufunzi na wahadhiri na kuandikisha wanafunzi wengi,tumefanmikiwa kwa kiasi gani? Elimu yetu imeboreka au imeporomoka? Nini kifanyike? Adui huyu tunamzidi au anatuzidi nguvu?
Maradhi ni adui mwingine. Ni ukosefu wa huduma bora za kiafya kupitia Hospitali,Zahanati na Vituo vya Afya. Na pia, maradhi husababishwa na kukosekana kwa chakula bora kwa wananchi na mazingira safi. Maradhi yaweza pia kuwa ya kiakili. MARADHI NI MARADHI TU. Adui huyu vipi? Mabomu yetu kama nchi yamemuangamiza adui huyu kwa kiasi gani?
Kama nchi, tunapaswa kutafakari suala hili ili tusherehekee mafanikio. Sherehe hunoga kwenye furaha! Karibuni kwa mjadala Wakuu...
Rais wa kwanza wa Tanganyika huru alikuwa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Akiiongoza Serikali mpya huru,Hayati Mwalimu Nyerere alitangaza maadui wa Taifa hili: umaskini,ujinga na maradhi. Mwalimu Nyerere na Serikali yote waliamini kuwa kama nchi itapambana na maadui hawa,basi nchi itakuwa salama.
Umaskini ni kipato na hadhi ya maisha ya mtanganyika(sasa mtanzania) kuhusu mavazi,chakula na malazi. Na hata umaskini wa kiakili. Umaskini ulikuwa ni ajenda ya tangu Nyerere kutokomezwa. Kama nchi ambayo tayari imeshakuwa na marais wanne,tumefikia wapi? Vifaru vyetu vya kinchi vimemvurumisha adui huyu kwa umbali gani kurudi nyuma kuelekea kumtokomeza?
Ujinga ni kukosa maarifa;kukosa elimu. Kuhusu elimu, Serikali zote tangu uhuru zimekuwa zikipambana na adui huyu. Pamoja na kujenga shule,kufunza waalimu,wakufunzi na wahadhiri na kuandikisha wanafunzi wengi,tumefanmikiwa kwa kiasi gani? Elimu yetu imeboreka au imeporomoka? Nini kifanyike? Adui huyu tunamzidi au anatuzidi nguvu?
Maradhi ni adui mwingine. Ni ukosefu wa huduma bora za kiafya kupitia Hospitali,Zahanati na Vituo vya Afya. Na pia, maradhi husababishwa na kukosekana kwa chakula bora kwa wananchi na mazingira safi. Maradhi yaweza pia kuwa ya kiakili. MARADHI NI MARADHI TU. Adui huyu vipi? Mabomu yetu kama nchi yamemuangamiza adui huyu kwa kiasi gani?
Kama nchi, tunapaswa kutafakari suala hili ili tusherehekee mafanikio. Sherehe hunoga kwenye furaha! Karibuni kwa mjadala Wakuu...