Salamu sana wanajamii wenzangu,
Wakati Taifa letu la Tanzania linasherekea miaka 50 ya UHURU wake sisi kama wanajumuia ya wa Tanzania ni vema tukatumia nafasi hii kujadili mambo ya msingi yanayolikabili Taifa letu la Tanzania.
Wote tunafahamu wazi kwamba ili nchi yoyote iendelee yahitaji mambo makubwa manne(4) ya msingi hayo ni:-
1.SIASA SAFI
2.UONGOZI BORA
3.WATU
4.ARDHI
Hebu tuchukue nafasi hii kujadali namna ambavyo mambo hayo niliyotaja hapo juu yametusaidia sisi kama Tanzania kupiga hatua moja zaidi katika maendeleo ya Taifa letu baada ya Nusu Karne nzima tangu Taifa letu lipate Uhuru.
Katika kufanikisha maendeleo ya Taifa letu,tunahutaji Pato letu la Taifa (GDP) likue kwa kasi zaidi kama ilivyo katika mataifa yanayoibukia kwa sasa kama China,Brazil na mengineyo.Wote tunafahamu kwamba kasi ya kuongezeka kwa shughuli za Uzalishaji mali kutapanua upatikanaji wa Ajira hivyo kuongeza vipato vya wanachi na mapato ya Serikali.
Uzalishaji wowote ule unahitaji mambo yafuatayo:-
a.MTAJI
b.ARDHI
c.NGUVU KAZI
Pamoja na hayo yote,Nishati pia ni swala muhimu sana katika kufanikisha uzalishaji,so ukosefu wa Nishati ya uhakika kwa mfano Umeme wa Uhakika ni moja ya changamoto kubwa inayorudisha nyuma maendeleo ya uzalishaji katika Taifa letu wakati tukisherekea Miaka 50 ya Uhuru wa Taifa letu.Kwa mfano mataifa makubwa kama USA na CHINA yanahaha kutafuta Nishati ya uhakika kote Duniani,Marekani na Washirika wake wamevamia Libya ili kupata Mafuta zaidi na China nayo wako katika kukamilisha mradi mkubwa wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta kupita Bahari ya Atlantiki kutoka moja ya Taifa mzalishaji mkubwa wa Mafuta Duniani,Nigeria!
Mambo mengine muhimu ni haya hapa chini katika orodha hii kwa mtizamo wango,napenda kuwakaribisha wanajamii wote kujitokeza kuushibisha mjadala huu ili tuwasaidie wadogo zetu ufahamu na sisi wenyewe wakati tukijiandaa kusherekea mika 50 ya Uhuru wa Tanzania.
1.ELIMU
2.AFYA
3.MAJI
4.MIUNDOMBINU
5.VIWANDA NA BIASHARA
6.MALIASILI
7.ONGEZEKO KUBWA LA WATU
8.UTAWALA BORA
9.ARDHI NA MAKAZI
10.HAKI ZA BINADAMU
Namwomba mwezeshaji wa Forum hii asihamishe Thread hii muhimu kwa Maendeleo ya Taifa letu.
Nawasilisha kwenu.
Wakati Taifa letu la Tanzania linasherekea miaka 50 ya UHURU wake sisi kama wanajumuia ya wa Tanzania ni vema tukatumia nafasi hii kujadili mambo ya msingi yanayolikabili Taifa letu la Tanzania.
Wote tunafahamu wazi kwamba ili nchi yoyote iendelee yahitaji mambo makubwa manne(4) ya msingi hayo ni:-
1.SIASA SAFI
2.UONGOZI BORA
3.WATU
4.ARDHI
Hebu tuchukue nafasi hii kujadali namna ambavyo mambo hayo niliyotaja hapo juu yametusaidia sisi kama Tanzania kupiga hatua moja zaidi katika maendeleo ya Taifa letu baada ya Nusu Karne nzima tangu Taifa letu lipate Uhuru.
Katika kufanikisha maendeleo ya Taifa letu,tunahutaji Pato letu la Taifa (GDP) likue kwa kasi zaidi kama ilivyo katika mataifa yanayoibukia kwa sasa kama China,Brazil na mengineyo.Wote tunafahamu kwamba kasi ya kuongezeka kwa shughuli za Uzalishaji mali kutapanua upatikanaji wa Ajira hivyo kuongeza vipato vya wanachi na mapato ya Serikali.
Uzalishaji wowote ule unahitaji mambo yafuatayo:-
a.MTAJI
b.ARDHI
c.NGUVU KAZI
Pamoja na hayo yote,Nishati pia ni swala muhimu sana katika kufanikisha uzalishaji,so ukosefu wa Nishati ya uhakika kwa mfano Umeme wa Uhakika ni moja ya changamoto kubwa inayorudisha nyuma maendeleo ya uzalishaji katika Taifa letu wakati tukisherekea Miaka 50 ya Uhuru wa Taifa letu.Kwa mfano mataifa makubwa kama USA na CHINA yanahaha kutafuta Nishati ya uhakika kote Duniani,Marekani na Washirika wake wamevamia Libya ili kupata Mafuta zaidi na China nayo wako katika kukamilisha mradi mkubwa wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta kupita Bahari ya Atlantiki kutoka moja ya Taifa mzalishaji mkubwa wa Mafuta Duniani,Nigeria!
Mambo mengine muhimu ni haya hapa chini katika orodha hii kwa mtizamo wango,napenda kuwakaribisha wanajamii wote kujitokeza kuushibisha mjadala huu ili tuwasaidie wadogo zetu ufahamu na sisi wenyewe wakati tukijiandaa kusherekea mika 50 ya Uhuru wa Tanzania.
1.ELIMU
2.AFYA
3.MAJI
4.MIUNDOMBINU
5.VIWANDA NA BIASHARA
6.MALIASILI
7.ONGEZEKO KUBWA LA WATU
8.UTAWALA BORA
9.ARDHI NA MAKAZI
10.HAKI ZA BINADAMU
Namwomba mwezeshaji wa Forum hii asihamishe Thread hii muhimu kwa Maendeleo ya Taifa letu.
Nawasilisha kwenu.