Kwa hiyo unachotaka kusema ni kuwa hata ASP wanamhitaji sultani?. Jitoeni CCM, rudisheni ASP muiteni Sulani arejee awatawale!.
Pasco.
Wanabodi,
Zanzibar inajiandaa kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya January 1964 yalioufuta ule uhuru bandia wa mwaka 1963 chini ya serikali ya vibaraka ya Sultani Jamseed. Hizi ni series za mada zangu zenye maswali yasiyo na majibu.
Hii ni Hotuba ya Waziri Mkuu Kibaraka Shamte kwenye Umoja wa Mataifa akiitambulisha rasmi Jamhuri ya Watu wa Zanzibar hivyo kuuingiza rasmi Zanzibar ndani ya UN kama taifa huru.
Accession of the Sultanate of Zanzibar to the United Nations in 1963
and
The speech given by Prime Minister of the Sultanate of Zanzibar in the United Nations in 1963
Footage hii ni hisani ya mwana jf aitwae Badir
Nchi kuingizwa ndani ya UN na kupata kiti cha UN is a process inafuata taratibu fulani.
Tanganyika na Zanzibar zilipoungana na kuunda Tanzania, kuna utaratibu pia uliopaswa kufanywa na SMZ na Jamhuri ya Tanganyika kwenda UN ili kuviunganisha viti vya iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika ili kuvifuta rasmi na badala yake kuwekwa kiti kipya cha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Nani anajua ni nini kilichofanyika hapa hadi kukifuta kiti cha Zanzibar kule UN?!.
Utaratibu ni kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, kumuandikia rasmi Katibu Mkuu wa UN Note Verbale, kumtaarifu kuhusu muungano na kueleza lile taifa huru lililojiunga hivi karibuni, ceased to exist anymore hivyo kiti chake kifutwe! na kupewa taifa jipya laTaifa la Zanzibar halipo tena!. Hili halikufanyika!.
Na Tanganyika pia ilipaswa kumuandikia Katibu Mkuu wa UN, Note Verbale kumtaarifu kuwa lile taifa la Tanganyika has seased to exist kufuatia muungano na Zanzibar hivyo kiti chake kifutwe na kukabidhiwa Taifa jipya la JMT. Hili pia halikufanyika!.
Kwa barua hizo mbili, viti vya Tanganyika na Zanzibar ndipo vingefutwa rasmi, na kisha kupelekwa Note Verbale ya 3 toka serikali ya JMT ikilitambulisha Taifa jipya la Tanzania na kupewa kiti cha taifa jipya!.
Kilichotokea ni kule UN ilipelekwa Note Verbale moja tuu toka serikali ya JMT kumtaarifu Katibu Mkuu kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana kuunda JMT, hivyo kiti cha iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kile cha iliyokuwa Tanzanyika, sasa vitakaliwa na nchi moja ya Tanzania wakati utaratibu wa submition ya union documentations zikiwemo zile Articles of Union ungefuatia, kitu ambacho hakikutekelezwa mpaka leo!.
Jee kiti halali cha nchi moja huru ndani ya UN kinawezwa kufutwa kirahisi rahisi hivyo with just a Note Verbale kutoka taifa jingine?!.
Mfano ikitokea Tanzania tukaungana na Kenya, hivi kweli mwenye jukumu la kutoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa UN ni Kenya tuu kumtaarifu kuwa tumeungana na Tanzania hivyo kuanzia sasa kiti cha Tanzania kifutwe?.
Nikiwa mwandishi nilibahatika kuutembelea ubalozi wetu wa UN pale NY, nikapokelewa na shemeji yetu (Mke wa mwana jf mwenzetu ndie alikuwa receptionist wakati huo), nikapeleka maswali yangu haya kwa balozi we enzi hiyo, sikupata majibu.
Pia nilitembelea jengo la UN ili angalau kuziona zile docu za muungano, kilichopo kule ni ile Note Verbale tuu, nothing more, nothing less!.
Wenye majibu naombeni msaada wenu!.
Pasco.
Pasco,
Unasema na nakunukuu: ''Nimekisoma na kukisoma na kukisoma na humu jf
pia ni mimi ndio nimekiweka na tumekiponda humu kama tulivyoyapobda
maandishi ya Maalim Mohamed Saidi na kisa cha wazee wake wa Gerezani!.''
Kwanza awali ya yote Pasco jifunze kuandika vizuri kisha ndiyo utoke ukumbi.
Pili jifunze adabu ya mnakasha.
Wewe hujafikia makamo ya ''kuponda'' kazi ya Dk Harith Ghassany kwa kigezo
chochote kile ukijuacho wewe na mfano wa wewe.
Tatu wewe hujafikia hali ya kukabiliana na mimi.
Mimi nikinyanyua kalamu huwa sikukusudii wewe na mfano wa wewe.
Asilani wewe Pasco huingii katika fikra zangu.
Utaingia kwa kipi khasa?
Mimi kuna watu nawakusudia na wao wakisikia Mohamed yuko uwanjani
hutoka kuja nisikiza na wengi hawachangii.
Wanakuja kusoma.
Huja kama anavyopenda kusema Spike Lee huja ''kufyonza elimu.''
Lakini umenifurahisha kitu kimoja.
Umeniita ''Maalim.''
Jina hili mimi marehemu mama yangu alikuwa akiniita bado mie mdogo sana.
Akiniita hivyo kwa kuwa baba yake alikuwa sheikh akisomesha.
Mimi akanita ''Mohamed'' jina la baba yake yaaani babu yangu.
Kwa mila zetu akawa wakati mwingine anaona tabu kumkata baba yake jina.
Akawa sasa anaangukia katika ''Mwalimu Mohamed.''
Kanipa cheo cha kudarsisha.
Wakati mwingine akinita ''Sheikh.''
Bibi yangu Bi. Mwantum bint Rajab yeye akawa ananiita ''Bwana
Mohamed.''
Mimi mume wake.
Ikiwa lazima atutaje wote wawili kwa pamoja babu yangu kwa kuwa alikuwa
kafariki akawa anaiitwa ''Hayati Bwana'' na mimi ''Bwana Mohamed.''
Historia ya Gerezani nimeisomesha hapa na hivi sasa wachapaji wananiomba
niiifanye kitabu.
Mama yangu hakika kaishi na kaniona nikifuata nyayo za babu somo yangu
Mwalimu Mohamed.
Nasomesha kama alivyosomesha babu yangu.
Hii ni bashraf.
[COLOR=# Hee! Hii thread imefikaje huku tena ndugu?
Mukulu......Hoja ya Pasco ni "BADO KUNA MASWALI AMBAYO HAYANA MAJIBU"....Kama ni kweli tutafute hayo majibu!
Ninachosema ni kuwa ASP and so now CCM na watu kama wewe wasilete unafiki kuwa eti Sultan atarudi kutawala Zanzibar hiyo ndio Wimbo wa Taifa wa wahfidhina wasitaka mageuzi na maendeleo ya Zanzibar kwa kukinga nafasi zao.madarkani na mtu kama wewe kama una fikra timamu ukawa unawapigia debe.
Kwani unafiki wao ni kuficha ile historia kuwa wao ASP walitaka Constitutionql Monarchy kama ya UK na waliahidi kumlinda Sultan na ukoo wote wa Kifalme mpaka kufa.
Hebu nambie katika records za mauwaji ya 1964 kuna member gani wa Kifalme alouwawa?
Na wengine bado wapo wanaishi pale Zanzibar mpaka leo.
Sultan kama anataka.kurudi atarudi Oman kwenye ukoo wake amabako.anweza kupigania rights zake za kifamilia na pia kunautajiri mkubwa kuliko Zanzibar na ambako ni.chi yenye hadhi kubwa kimataifa.
Sultan aje kutawala Zanzibar kwa misingi gani?
Hivi huu Muungano lengo lake ni kuwa kaondoka Sultan wa Kiarabu ambae alikuwa just a paper Sultan alokuwa hana mamlaka hata kuruhusu matumizi ya nchi yake kama British Resident hajaruhusu, na badala yake ni Usultani mpya kutoka Tanganyika ambao unafanya yale yale yalokuwa yakifanywa n Muingereza!
Hivi wewe umeona wapi nchi ambayo imekuja ku exist after the scramble for Africa nchi amabayo imepata jina Tanganyika katika mwaka 1920 ikubalike kuifuta nchi ambayo ina exist since 9AD karne ya Tisa!!
Ushahidi upo kama Tanganyika, Kenya, Uganda, Burundi, Ruwanda, Malawi na zenginezo hazikuwapo mpaka baada ya 1885 mkutano wa Varseilles wa kuigawa Africa katika makoloni ya Wazungu lakini Zanzibar ilikuwako na ilikuwa Dola yenye Ustaarabu na Uchumi mkubwa na nguvu hata za kijeshi.
Hizo nchi zote nilizozitaja zilikuwa katika eneo moja tu kusini ya jangwa la Sahara eneo likiitwa Ethiopia ni neno la Kiyunani lenye maana ya Watu Walioungua Nyuso (Watu Weusi).
Pasco rudi maktaba pale UDSM katafute uchimbe uje ulikatae hili.
. Hawakukuta mtu!, inasemekana mwanzo visiwa hivi vilikaliwa na Wahadimu na Watumbatu, ila hakuna kumbukumbu yoyote ya kihistoria inayoonyesha Sultan Sayyid Said hakunegotiate na yoyote kuvitwaa visiwa vile as if aliviokota!. Yaani alipofika hakukuta wenyewe!. Ila excavations na ruins ndio zilithibitisha kuwepo maisha kabla ya Waarabu!. Inamaanisha waliokuwepo waliteketea wote!, au waliteketezwa!, maana Waarabu! usipime!.
Sio kama Kilwa Hassan Bin Amiri, alikinunua kisiwa cha Kilwa kwa wenyeji kwa gharama ya kitambaa cha kukizunguka kisiwa chote!.
Katika safari za Ibin Batuta, anazungumzia wenyeji wa Kilwa na sio wenyeji wa Zanzibar!.
Ya Zanzibar ni kama ile hadithi ya Bistani ya Aden ni Ngorongoro Creater!, Dr. Richard Leakey na Mkewe ndiko walikolivumbua fuvu la mtu wa kale kabisa anayesemekana atakuwa ndio Adamu!.
Pasco
Swali zuri sana Ritz tunasubiri jibu Pasco.
Sasa kwanini na wewe huendi kwa hao watu baki ukawakadhibisha kuwa wanasema uwongo?
Ivo mapinduzi yamekuja kuondosha utumwa? Kama si Seyyid Sultan bin Saif Al Yaarubi kuwatowa Wareno East Africa labda wewe ungalizaliwa Cabo Verde au Sao Paulo maana Wareno walikuwa wakikamata waafrika kinyama kama vile ngedere na kuwauwa na kuwabaka wanawake.
Kule Tabora kama si Rumaliza ambaye babu yake Ali Muhsin mzaa mama basi wajerumani wangaliwamaliza waafrika na mpka leo hakuna hata mmoja anaemtaja Rumaliza kama ni shujaa sababu ni Mwarabu.
Mnakataa kutambua ukweli wa kitabu cha Ghassany sababu kinasema ukweli hasa pale alopwahoji kina Mkwawa na wenzake walio hai. Zaidi kuwa mauwaji ya 1964 pia yanaonyesha hata hao ASP waliuliwa nao kwa winhi na hao manamba wa kimakonde walioshindwa kutofautisha baina ya waarabu na machotara wa kishirazi na kihadimu.
Tena usiwatukane wazanzibari hasa wahadimu na watumbatu sababu ni.makabila yaliyokuwa huru na hawajawahi kuingizwa utumwani.
Utumwa Zanzibar ulipigwa marufulu since 1879 iweje Zanzibar ukaweko utumwa 1964. Rudi darasani ukasome historia ya mabwana zenu wa kiingereza.
Mkuu wangu Al Khawarizm!
Shukran mno kwayo! Duh!
Yaani hata nami nalitaka kuandika/kumjibu japo kiduchu...basi Wallahi sintathubutu tena kutia maguu yangu humu...yaani umemchana huyo Pasco na sidhani kama atathubutu kurejea humu tena!? Teeh! Teeh!
Wajua hawa jamaa wangi wao hawana walijualo kiundani...history zao za kudanganywa na Wazungu au mle Makanisani zawapotosha mno na kuwazidishia chuki pasi kiasi! Dah!
Ahsanta sana.
Narekebisha mistake transposition ya tarehe kuondolewa utumwa sio 1879 : Utumwa ulifutwa kabisa Zanzibar on 6 April 1897 by decree na Sultan Seyyid Hamoud bin Muhammad bin Said bin Sultan.
Mimi nahisi hawa Tanganyika wanaogopa Zanzibar ikiwa huru labda siku moja itadai haki yake ya kiutawala over Tanganyika kwani 1893 ni katika utawala wa Seyyid Hamed bin Thuweiny wakati huo Zanzibar ishakuwa chini ya Himaya ya GB since 1890; ndipo in 1895 Zanzibar Protectorate ilopoingia katika itifaki na UK kuiendesha utawala katika Mwambao wa Pwani (Mrima kwa wakati ule) kwa niaba ya Sultan wa Zanzibar. Baada ya kufa Seyyid Hamed ambae kwa kweli aliukacha ufalme na kufia Saint Helena Island. Katika 1896 akatawala Hamoud bin Muhammad na kutangaza kuwa kuazia 1897 mtu yeyote ataekanyaga au kuzaliwa Zanzibar atakuwa ni mtu huru na tarehe 6/4/1897 was officially implimented.
Kuanzia hapo ndipo Muingereza kutumia hadaa na akiwemo mjerumani kuipora Zanzibar mapato ya forodha waliyokusanya Bara na wakiilipa Zanzibar only rupia 11,000/- kwa Mwaka ndipo baadae Sultan nae akarudisha Mapigo kwa kuitangaza Zanzibar as Free Port so uatona huu ujanja na hizi kero za sasa za muungano kama hizi za hujuma ya kiuchumi dhidi ya Zanzibar hawa viongozi wanaiga tu kwa Mabwana zao wa Kikoloni and they are much worse maana wao wanataka hata kuifuta Zanzibar in the map of the world.
Kuna watu wanadhani Mwarabu alipokuja Zanzibar, kuna wenyeji aliwakuta!, la hasha!. Hao wamatumbi mnao waona leo, na masalia ya watumwa walikosa soko!. Waarabu walikuwa ndio mabwana na Matumbi ni watwana, Mapinduzi yamewafanya watwana kugeuka ndio mabwana na waliokuwa mabwana wakawa watwana!. Leo hata wingi wa machotara na Mapinduzi kuwezesha mtwana kujitwalia binti wa Kiarabu na kumfanya mke!. Wabwana wa Mkongwe walichinjwa kwa jambia, leo Alhamdidulahi, watwana nao wanaishi ghorofani!, zamani wali wakiishi Kibanda Maiti, Mchambawima, Mchafukoge etc. Huu sii utukufu wa mapinduzi?!.
Pamoja na harakati zote, muungano utadumu, Mapinduzi Daima!.
Pasco
Tujuze ili tufyonze Ilm.By Pasco
Kuna watu wanadhani Mwarabu alipokuja Zanzibar, kuna wenyeji aliwakuta!, la hasha!. Hao wamatumbi mnao waona leo, na masalia ya watumwa walikosa soko!. Waarabu walikuwa ndio mabwana na Matumbi ni watwana, Mapinduzi yamewafanya watwana kugeuka ndio mabwana na waliokuwa mabwana wakawa watwana!. Leo hata wingi wa machotara na Mapinduzi kuwezesha mtwana kujitwalia binti wa Kiarabu na kumfanya mke!. Wabwana wa Mkongwe walichinjwa kwa jambia, leo Alhamdidulahi, watwana nao wanaishi ghorofani!, zamani wali wakiishi Kibanda Maiti, Mchambawima, Mchafukoge etc. Huu sii utukufu wa mapinduzi?!.
Pamoja na harakati zote, muungano utadumu, Mapinduzi Daima!.
Pasco