Mkuu Ritz, unamjua Shamte au unamsikia tuu?!.
Jee unajuwa kuwa Shamte alikuwa ASP!, unazijua sababu zilizomfanya kujiengua ASP na kuunda ZPPP?!.
Baada ya ASP kushinda uchaguzi wa mwanzo, Shante aliutamani Uwaziri Mkuu, kwa vile Karume ndio alikuwa Kinara wa ASP, Mohamed Shante akijiengua kutoka ASP na kuunda chama cha ZPPP ili kujiunga na wabaya wa ASP kuunda serikali ya mseto
Katika uchaguzi wa Julai 1961, ASP kilipata asilimia 49.9 ya kura zote, ZNP kilipata asilimia 35 na ZPPP asilimia 13.7. Hata hivyo, pamoja na ushindi wa kura ASP, kilishindwa kutamba katika viti vya bunge (LEGCO) kilipopata viti 10, ZNP 10 na ZPPP vitatu.
Uchaguzi huo ambao haukupata mshindi na ilibidi urudiwe Julai, 1963, matokeo ni muungano wa ZNP/ZPPP viti 18 na ASP viti 13. Shamte alishauriwa aunde Serikali ya mseto kati ya ZNP/ZPPP na ASP ili kulinda umoja wa kitaifa, lakini aligoma kata kata kwa kiburi na jeuri ya kuogopa ASP isije kumoutshine!. Kitendo cha Shamte aliyekuwa ASP na kujitoa kwa tamaa ya uiongozi, kisha kukataa kata kata kushirikiana na ASP ambao ndio Waswahili wenzake na badala yake kujiunga na ZNP ambacho ni cha Waarabu, hapa ndipo ukibaraka wake ulipolalia!.
Pasco.
Mkuu Pasco,
Duh! Mbona hayo maelekezo yako yamejaa jazba,chuki,farka na urongo ulokubuhu...umekumbwa na nini Mkuu!?
Nakhis wewe hufahamu asilan hiyo society ya Kizanzibary na mahusiano/maingiliano baina yao!...yaani Historia ulosomeshwa ndo ile ile tu ya upotoshwaji alotengeneza yule Nyerere na genge lake!? Dah!
Au wewe umesomeshwa history ya Zanzibar kwa perspective ya wale Wazungu!? Je ushawasoma na Waarabu wenyewe wanasemaje!?
Kabla ya kwenda mbali mno...embu tupe maana ya neno "Waswahili" kama ulivyolitumia hapo juu!?
Je unafahamu family Tree/branches za huyo Mohammed Shamte!?...tafadhali tudadavulie hapa jamvini...ukimaliza tufahamishe je yeye ana-qualify huo "Uswahili" kama ulivyotaja hapo kwenye bayana yako au Uarabau ambao wewe usotaka kuusikia asilan!? Dah! Teeh! Teeh! Teeh!
Tashkuru mno kukusikiza.
Ahsanta.