Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
CCM imekuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 50. Tulichokivuna wanatanzania ni Ufisadi, Umasikini, Umwinyi na usultani wa Viongozi wake. Wamekuja na mambo kibao, Nuguvu mpya, na hari mpya ambayo imeyeyuka bila utekelezaji. Wakaleta kujivua gamba, yote ikawa ni kama sanaa ya kaole.
Licha ya kwamba wamepewa majina ya mafisadi wakubwa, hakuna hata Fisadi papa aliyekamatwa. Leo wako majukwaani kutangaza sera mpya. Sera za nini ambazo watazitekeleza leo wakati miaka 50 wamshindwa kununu X-ray kwenye mahospitali. Heti leo wanaomba waendelee kuongoza. Waendelee kuongoza huku wazee wakiwaweka watoto wao waendeleze ufisadi
Watu walioshindwa kutunza familia zao wanapata wapi moral authority Tanzania. Namaanisha waliokimbia (waliowatosa) majukumu yao ya kutunza wake na watoto wao marekani ndio leo tuwape madaraka? Watu ambao licha ya umri wao kuwa mababu, ndio kwanza wanazunguka na vitoto vidogo Ma miss.Hapa namaanisha William Malechela ambaye kila kukija anaibuka na Thread ya kuisifia CCM. Wanaotuhumiwa kuwaua tembo na Faru ndio wanaonadi sera za Chama. Mh. Kinana anatuhumiwa na biashara ya Pembe za Tembo, ambaye kwa nchi za watu angejiuzulu, lakini yeye anazawadishwa ukatibu Mkuu wa Chama?
Hivi kweli Tanzania tumelaaniwa nini? Tukiendelea kucheka na hawa Nyani tutavuna Mabua. Mimi nilishatupa kadi yangu ya CCM April 2012
Licha ya kwamba wamepewa majina ya mafisadi wakubwa, hakuna hata Fisadi papa aliyekamatwa. Leo wako majukwaani kutangaza sera mpya. Sera za nini ambazo watazitekeleza leo wakati miaka 50 wamshindwa kununu X-ray kwenye mahospitali. Heti leo wanaomba waendelee kuongoza. Waendelee kuongoza huku wazee wakiwaweka watoto wao waendeleze ufisadi
Watu walioshindwa kutunza familia zao wanapata wapi moral authority Tanzania. Namaanisha waliokimbia (waliowatosa) majukumu yao ya kutunza wake na watoto wao marekani ndio leo tuwape madaraka? Watu ambao licha ya umri wao kuwa mababu, ndio kwanza wanazunguka na vitoto vidogo Ma miss.Hapa namaanisha William Malechela ambaye kila kukija anaibuka na Thread ya kuisifia CCM. Wanaotuhumiwa kuwaua tembo na Faru ndio wanaonadi sera za Chama. Mh. Kinana anatuhumiwa na biashara ya Pembe za Tembo, ambaye kwa nchi za watu angejiuzulu, lakini yeye anazawadishwa ukatibu Mkuu wa Chama?
Hivi kweli Tanzania tumelaaniwa nini? Tukiendelea kucheka na hawa Nyani tutavuna Mabua. Mimi nilishatupa kadi yangu ya CCM April 2012