Miaka 50 baadaye: Je Unaiamini Serikali? Kwa nini?

Mzee Mwana Kijiji I saluti you!
Kabla ya kujibu maswali yako (a) - (g) naomba tufahamishane kwamba kwamba tulipata uhuru miaka 50 iliyopita sii issue na haimaanishi kwamba lazima sasa tuwe na maisha kama ahera! Uhuru na historia ya nchi yetu kwa ujumla ni vitu tuanvyo takiwa kuvienzi pamoja na mapungufu yaliyopo bado itabakia kuwa historia ya nchi yetu no matter tumefikaje hapa tulipo.

nina sababu zifuatazo kuandika hayo maandishi hapo juu kama ifuatavyo:-
  1. Ni kweli kwamba nchi yetu in raslimali nyingi zikiwemo madini na kadhalika, ila kwa maoni yangu kuwa na madini bila technology bado its a problem, na ukuachilia mbali waarabu waliotajirika kwa mafuta siifahamu nchi yoyote ambayo imetajirika kwa kuuza madini, kuchukua kwa mfano nchi kama urusi ambaya ina madini zote unazozijua (kasoro tanzanite!), lakini wao sii nchi tajiri kuliko zote duniani ukizingatia kwamba walizigundua miaka mingi iliyopita (nafikiri mzee bado unamkumbuka Mandleeve aliyetengeneza periodic table of elements). nchi za africa ni africa ya kusini tu na walianza miaka mingi sana iliyopita. nchi nyingine ziko vitani kugombea nani anakula zaidi na ndiko tunakoelekea!!.
  2. kuhusu nchi yetu na miaka 50 na bado bado huduma za jamii haziko sawa ni tatizo ila kumbuka nchi ambazo hazijawahi kuwa koloni na zina hata maandishi yake kama Ethiopia wana nini?
  3. Nafikisiri una mfahamu Christopher Amergo Columbus aliyevumbua Amerika ni Mhisipania na Hispania ilianza biashara miaka mingi ikiwemo ya utumwa lakini hadi leo wao na jamaa za Wareno wako kwenye PIGIS, zile nchi chokambaya kuliko zote europe, zaidi ya kucheza football hamna kitu
  4. so, kabla ya kujiuliza maswali (a) - (g) inabidi tuifahamu historia yetu na tujue tuna nini na ni nini hatuna, if you ask me tungejitahidi tukatumia resources za kutosha tuchague vijana wenye pass nzuri tuwalipie kwenye vyuo vizuri wasomee taaluma za sayansi za uchumi na madini halafu warudi wafanye kazi! (angalizo: wawe wazalendo si wazamiaji). Wajerumani na wajapani walifanya hivyo baada ya vitakuu ya pili ambapo nchi zote zilikuwa magofu kwa kupigwa mabomu n sasa uchumi wao uko juu.
  5. mwisho, tuuheshimu uhuru wetu kwani ni historia yetu, Ujerumani na Japan wangekaa kuanza kutoana macho kwamba nani kifikisha nchi yao kwenye vita kuu wasingeinuka!!
I am out.

@Nyantella, pamoja na kwamba hoja imesimama 'katikati' nikukumbushe tu kuwa Tanzania ilipata uhuru around the same time na Malayasia & Singapore. Hizi nchi mbili hazina hata robo ya rasilimali ilizinazo Tanzania. Lakini angalia wako wapi leo. Pia hoja kwamba Tanzania inabidi iwekeze kwenye elimu 'in theory' nakubaliana na wewe, lakini, hivi ni kweli Tanzaina haina wasomi? Hawa wanaojiita Ma-Dr ni waganga wa kienyeji au ni watu gani hasa?

Mimi naona tatizo like kwenye leadership. Hapo ndio chimbuko la matatizo yetu. Mzazi akiimbiwa mtoto ni mwizi lakini akakaa kimya usitegemee mtoto ataacha kuiba. Mbaya zaidi ni pale mzazi anawakataza 'law-enforcement agents' wasimguse mtoto. Kwa mfano, kwa nini hatujaambiwa hatma ya Jairo? Kwa nini? alifanya kosa au hakufanya kosa? Hivi Jairo ni illiterate? Waliochonga deal ya kusafirisha wanyama hai ni darasa la saba? au waliondaa mikataba ya madini yetu ni 'mamndenyi' (sorry kuna kuna mtu anatumia hii ID). Na huyu Dr. Masaburi aliyepiga mnada UDA naye hajasoma?
 
Mnakiamini chama cha Mapinduzi kinachoongoza serikali hiyo?

Kumbe wewe ndiyo walewale waliowekeza kwenye siasa...................niliposoma thread niliikubali maana inawapa wetu nafasi na fursa ya kutafakari mustakabali wa nchi...............kumbe si hivyo wewe lengo lako watu wawatukane magambaz tu ili pengine chama chako kionekane mbadala.......unawapoteza watu watanzania na waafrika wenzako hasa vijana wadogo tunanaomaliza shule. ukiondoa sentence hii thread yako ni bomba sana.
 
Am not trust a government at all.
Kwasababu zifuatazo;
1. Richmond wakati inapewa tenda hawakujua kwamba ni kampuni ya mfukoni? usalama wa taifa kazi yake nn? Interijensia walikuwa wapi!!
2. Pesa za EPA wakati zinachotwa usalama wa taifa walikuwa wapi? Interijensia walikuwa wapi? Na baada ya kuwafahamu wezi hatua zipi zimechukuliwa?
3. Wanyamapori zaidi ya 100 wametoroshwa nj'e ya nchi. Serikali ipo wapi? Wazee wa interijensia wapo wapi?
4. Nchi giza.
5. Uchumi haukui kwa kasi inayotakiwa.
6. Serikali haina kauli ya pamoja. kila waziri ana kauli yake pia hata na raisi.
Udhaifu wa hii serikali ya c.c.m ni mwingi mno, unaweza kuorodhesha kwa muda hata wa siku 100 na usimalize.
 
Kumbe wewe ndiyo walewale waliowekeza kwenye siasa...................niliposoma thread niliikubali maana inawapa wetu nafasi na fursa ya kutafakari mustakabali wa nchi...............kumbe si hivyo wewe lengo lako watu wawatukane magambaz tu ili pengine chama chako kionekane mbadala.......unawapoteza watu watanzania na waafrika wenzako hasa vijana wadogo tunanaomaliza shule. ukiondoa sentence hii thread yako ni bomba sana.

Yani hapo umeishajibu tayari Mkuu MMJ hapo sasa ndiyo utagundua kumbe hata wana CCM wanakionea aibu chama chao hawataki kijadiliwe kwahiyo wapo kimazoea wamefungwa kuna wale wanaofaidika kwa namna moja au nyingine yani kimasilahi(individual benefit) unaona kama huyu kakata tamaa,utazungumziaje mustakabali wa nchi miaka 50 bila kuisema CCM.Lakini hata wenyewe wameamua kufanya birthday ya marehemu TANU maana hawana cha kujivunia ndani ya CCM yao.
 
Kumbe wewe ndiyo walewale waliowekeza kwenye siasa...................niliposoma thread niliikubali maana inawapa wetu nafasi na fursa ya kutafakari mustakabali wa nchi...............kumbe si hivyo wewe lengo lako watu wawatukane magambaz tu ili pengine chama chako kionekane mbadala.......unawapoteza watu watanzania na waafrika wenzako hasa vijana wadogo tunanaomaliza shule. ukiondoa sentence hii thread yako ni bomba sana.

yaani unaweza kuizungumzia Tanzania na mafanikioa na matatizo yake bila kuizungumzia CCM? Au mtu anaweza kuzungumzia serikali bila kugusa chama kinachounda serikali hiyo? Yaani unataka watu wazungumzia gari bila kumzungumzia dereva anayeendesha gari hilo?
 
yaani unaweza kuizungumzia Tanzania na mafanikioa na matatizo yake bila kuizungumzia CCM? Au mtu anaweza kuzungumzia serikali bila kugusa chama kinachounda serikali hiyo? Yaani unataka watu wazungumzia gari bila kumzungumzia dereva anayeendesha gari hilo?

Kwangu mimi hata yule afisa elimu au afisa kilimo au daktari au niseme bwana samaki au RAS au DAS au CEO wa yale mashirika, majaji na hata mgambo wanaofanya uzembe kuendekeza rushwa kufuja mali za umma Kwiba, nawehesabu kuwa nao ni serikali. Na ukiangalia kimsingi hawa siyo rahisi kuwabadilika katika position zao hata chama chako ccj kikifufuka na kuingia madarakani watabaki tu. Na wanaguswa na maswali yako ya msingi hapo juu kabla hujachafua kwa huu udaku ambao umeuongeza makusudi ili ushangiliwe na watoto wa shule.


Wewe unataka hawa vijana wawekeze fikra zao kwenye siasa tu, ungetumia muda na elimu yako kuwajaza ujasiri waone fursa zilizopo ingawa chache lakini unawakatika tamaa na unataka mdogo wangu aliyemaliza dodoma anyinyonge kwa kuamini kuwa maisha hayawezi kwenda tena maana kila kona imefungwa wakati huo nyie mnaishi maisha mazuri na mmejipenyeza kwenye ugumu huo huo.
 
Hadi hivi sasa kama Mtanzania umesikia mengi kuhusu uongozi na utawala na matokeo yake katika maisha ya Watanzania. Umesikia sera mbalimbali zikifanyiwa kazi na mafanikio yakitangazwa. Kuanzia ujenzi wa barabara, mahospitali, kliniki, miundo mbinu mingine mingi na mipango kadha wa kadha ya maendeleo. Yawezekana umeweza kushuhudia juhudi mbalimbali za maendelo zinazofanywa na serikali. Utakuwa umesikia mipango na malengo mbalimbali ya serikali na pia kuna mambo umeyaona mwenyewe au kusimuliwa jinsi serikali ilivyofanya kuleta maendeleo.

Na siku za karibuni bila ya shaka umesikia hatua mbalimbali za jinsi gani serikali imechukua kuonesha uongozi. Kuanzia sakata la Ngeleja na Jairo, sakata la BP na Mafuta na sasa sakata la Maige na wanyama. Yote yamefanyika katika kuonesha kuwa serikali iko "on top" of things; Bunge liko "on top" na kuwa viongozi waliochaguliwa "wanasikiliza wananchi".

Lakini muda wote huo yawezekana umeona mengine mengi ambayo yameacha maswali. Katika kuadhimisha miaka hii hamsini unajisikiaje zaidi:


a. unaamini serikali zaidi?
b. Unaiamini lakini unataka uthibitisho?
c. Unaishuku mara zote?
d. Unashuku maamuzi yake?
e. Huamini kabisa?
f. Unaangalia watu gani wa serikali wanasema au kuamua; yaani unaamini katika watu binafsi kuliko taasisi zao?
g. Hujali lolote linalofanywa na serikali?

Kwanini?

Ninahasira sana,
maji mgao,umeme mgao,ardhi mgao sasa niseme nini?Ngoja nikapange ndoo zangu foleni nasikia mabomba yameanza kukoroma.ahahahaaaaaa,umeme umerudi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!du japo ni nyooshe tu combart za za zaaaaaaaa maana utakatika hivi punde.what kind of a life after 50 YEARS??
 
ninaiamini kwasababu imeweza kusimamia hari ya utulizu lakini siiamini kwasababu imeshindwa kutatua matatizo ya wananchi wake
 
Kumbe wewe ndiyo walewale waliowekeza kwenye siasa...................niliposoma thread niliikubali maana inawapa wetu nafasi na fursa ya kutafakari mustakabali wa nchi...............kumbe si hivyo wewe lengo lako watu wawatukane magambaz tu ili pengine chama chako kionekane mbadala.......unawapoteza watu watanzania na waafrika wenzako hasa vijana wadogo tunanaomaliza shule. ukiondoa sentence hii thread yako ni bomba sana.

Kua kwanza uyaone dogo....
BTW umeshaanza kukatwa deni lako Loan board?
 
Mzee wa Bunge GR upo! Tunashukuru na update zako za Bunge kama isingekuwa wewe mengi yanayoajiri huko Jumba la mipasho tusingeyajua.

Nipo Mkuu nashukuru kazi kwa sasa imepata wadau wengi wameunga Mkono Ubunifu wangu so ukiona kimya jua wapo wapiganaji wengine wanaendesha mijadala ya Bunge kwa umakini mkubwa
 
Back
Top Bottom