Miaka 2 ya kutoonekana kwa Jean Bigirimana na kitendawili cha Azory Gwanda

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,740
4,230
Mwanahabari Jean Bigirimana wa Burundi alipotea tangu Julai 22 mwaka 2016 na hadi leo hajapatikana wala habari kuhusu yeye kusikika popote.

Bigirimana alikuwa mwandishi wa gazeti la kila wiki la Iwacu na alipotea mchana wa Julai 22, 2016 baada ya kupokea simu kutoka kwa kinachodaiwa kuwa chanzo chake katika Usalama wa Taifa wa nchi hiyo.

Mke wa Bigirimana, Bi. Godeberthe Hakizimana aliiambia Associated Press kuwa mumewe alienda Bugaramana, Muramvya lakini hakurudi licha ya kuahidi kurudi kwa ajili ya chakula cha usiku.

Bigirimana alipotea ikiwa ni wiki chache tu tangu atoke kwenye mafunzo ya uandishi nchini Rwanda na gazeti la Iwacu linaamini amechukuliwa na Usalama wa Taifa kwa sababu aliandika makala akiwa Rwanda kuhusu maisha ya mwandishi aliye uhamishoni.

Haijawahi kuthibitishwa kama alikamatwa au amefariki lakini Taasisi ya uangalizi wa Haki za Binadamu umeona matukio ya utekaji, ukamataji, utesaji na mauaji ya wanaharakati wa kijamii, wanahabari na wengine kutoka kwa Serikali, waasi wenye silaha na watu wasiojulikana tangu Aprili 2015 maandamano yalipoanza kufuatia uamuzi wa Nkurunziza wa kugombea kwa kipindi cha 3.

Hii habari inaendana sana na ya Mwandishi wa Mwananchi, Azory Gwanda aliyepotea tangu Desemba 2017.

Je, tuache kumlilia na kusubiri maana hatarudi tena?

Je, Gwanda aliandika makala yeyote 'hatarishi'?

Wizara imejitoa katika hili na tumekatazwa kuihusisha. Tukaombe msaada nje ya nchi kwa jambo lililo ndani ya uwezo wa vyombo vyetu vya dola?
 
Naskia azory kilicho mponza ni ile habar ya watoto waliopotea.na yeye wameamua kumpoteza.

Ben yeye upeke peke wake wakuichimba PhD ya nabii jiwe baba jesika.
 
so sad ...wakati kuna MTU anaposimama madhabahuni na kuwaomba watanzania wamuombee upande wapili nafsi yake inamsuta "" na kumkumbusha jinsi mikono yake inavyonuka harufu ya damu ya watanzania ""... Ajabu nipale MTU huyo anaposimama tena kwenye hadhira "" na kujitapa kwamba yeye ni msema kweli mpenzi wa mungu "".... Huku akisahau kwamba " kuna MTU kama azory " Ben saa8 .tukio LA risasi kwenye mwili wa lissu /akwilina " urasimu na utesi kWa vyama pinzani ...mifuko ya viroba na miili ya watu coco/ruvu" " na utesi wa kupitiliza kwa binaadamu ambao ni wananchi wa taifa hili toka MKIRU""... some times yakupasa uwe hamnazo " kichaa wa level ya milembe " ili uweze kuwaelewa wana siasa wa namna hii "" kama huyu bwana stone cold "" ....na wale wote ambao wanajifanya kuwaelewa na shawishika kusema kwamba "itkuwa kichwani mwao ni hamnazo "..
 
Ukiamua demokorasia au utawala wa sharia lazima uwe tayari kutolewa kafara wewe mwenyewe mageuzi yana gharama huwezi kupata on "sliver plate" nawanamageuzi wegi wanalitambua hilo . Kujadae kisaokolojia ni vzri kupotea kuteswa kufa nivitu vya kawaida kwa mageuzi.
 
Kuna muda roho yangu inapatwa na udhuni sana kila nikimkumbuka ben saa nane ni bora mtu afe ujuwe huyu kafa kuliko hii sitofaamu
 
Viongozi wa kiafrika hujihisi kawa sio binadamu wapatapo madaraka. Najua Mungu atawafanyizia tu, make kumwaga damu si mchezo lazima iwalilie
 
Back
Top Bottom