Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Leo wanawake wa wanasiasa wa Tanzania wamefanya uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Vyama vya siasa Tanzania (Tanzania Women Cross Party Platform,TWCP)lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar esalaam.Jukwaa hili linawanachama wa vyama vyenye Wabunge..Uzinduzi ulifanyika leo asubuhi katika ukumbi huo na kuhudhuriwa na mamia ya wanawake toka katika vyama mbalimbali vya siasa wakiwemo Mawaziri na Wabunge na Viongozi mbalimbali wa Vyama vya siasa na kada nyingine kama vile TGNP,Wake wa Mabalozi nchini,Wanaharakati mbalimbali Wanahabari na wageni wanawake wanasiasa toka Finland.Uzinduzi huu ulifanywa na Mke wa Rais mama Salma Kikwete..Jukwaa hili limeundwa mahususi kwaajili ya kumkomboa mwanamke kisiasa,kiuchumi na kijamii bila kujali itikadi za vyama...
Kauli mbiu ya jukwaa hili ni "Rafiki wa Mwanamke ni Mwanamke".Mpka sasa jukwaa hili lina wanachama wafuatao;
1. Jumuiya ya Wanawake CUF
2.Baraza la Wanawake Chadema(BAWACHA)
3.Kitengo cha Wanawake UDP
4.Kitengo cha Wanawake TLP
5.Umoja wa Wanawake Tanzania-UWT
6.Chama cha Wabunge Wanawake(TWPG)-Bunge
Lengo kuu la jukwaa hili ni kuleta usawa kati ya mwanamke na mwanaume katika siasa.
Habari zaidi na picha zitafuata baadaye.
Kauli mbiu ya jukwaa hili ni "Rafiki wa Mwanamke ni Mwanamke".Mpka sasa jukwaa hili lina wanachama wafuatao;
1. Jumuiya ya Wanawake CUF
2.Baraza la Wanawake Chadema(BAWACHA)
3.Kitengo cha Wanawake UDP
4.Kitengo cha Wanawake TLP
5.Umoja wa Wanawake Tanzania-UWT
6.Chama cha Wabunge Wanawake(TWPG)-Bunge
Lengo kuu la jukwaa hili ni kuleta usawa kati ya mwanamke na mwanaume katika siasa.
Habari zaidi na picha zitafuata baadaye.