Miaka 10 bila Tanzania Institute Hospital, niliyoyasikia, kuyaona na kusimuliwa na miaka 9 bila gwiji wa moyo nchini Dr. Masau

Hii ishu ya Dr Masau iliibua mjadala mkubwa sana miaka ya nyuma, wegine wakimtuhumu kuwa hakuwa na uzoefu na vigezo vya kuwa daktari bingwa wa maradhi ya moyo, na hatimaye kusababisha vifo vya wagonjwa wengi sana.
 
Janabi

Masau

Kikwete

Magufuli

Kama in sound good halafu inakataa

Ila wamefanikiwa kumpa jina janabi halafu janabi akamtumikia kiukwel kikwete SI mnaona kikwete had Sasa n Rais japo mtabisha
 
Hii ishu ya Dr Masau iliibua mjadala mkubwa sana miaka ya nyuma, wegine wakimtuhumu kuwa hakuwa na uzoefu na vigezo vya kuwa daktari bingwa wa maradhi ya moyo, na hatimaye kusababisha vifo vya wagonjwa wengi sana.
Alikuwa kikwazo kwa watu kwenda kutibiwa nje ya nchi.
 
Halafu utawasikia watu humu wakimsifia huyo Rais wa awamu ya Nne mpaka kero.

Utawasikia nyumbu wa ufipa wakimsifia huyu Baba msoga Dakitari wa Mtandao wa dhuluma nchi hii.

Hiyo yoote ilikuwa ni kuiandaa Ile taasisi iliyoshirikiana na Janaba kutunajisi wanyonge wa nchi hii.
Malipo yao yataonekana hapa hapa Duniani siku moja, Mungu si juma.
Clap 👏🏾, naona kuna watu mna uelewa wa mambo kadha wa kadha, kile kilichofanyika Muhimbili JKHI ni copy and paste from THI.
 
Tatizo ni kwamba nchi imeoza. Kuna watu, haijalishi kitu kina msaada kiasi gani kwa jamii lakin wao wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele! Dr. Masau alikuwa amenyooka, sasa kuna watu mtu wa namna hiyo ni adui mkubwa!
 
Nawaunga mkono wataalam waliofanikiwa wakiwa nje ya nchi na kukataa kurudi kutumika nchini mwao.

Viongozi wa kiafrika wakienda nje na kuonana na wananchi wao (diaspora) huwashawishi warudi nyumbani kuja kulitumikia taifa na kuwekeza huko, ilihali maneno yao hayashabihiani na matendo pindi wakirudi.

Mfano mdogo ni kama ya late Dr. Masau ni masikitiko makubwa sana unafurahi kurudi home kuwekeza kumbe unafuata kifo, narudia ni heri uonekane siyo mzalendo kuliko kuja kutendwa.
kuna jamaa huko Arusha anadai wamempiga ngumi ya mdomo kisa wamemkuta anakula cigar

Papaa pedeshee tupe na mkasa wa IMTU

1650033077886.png
 
Mkuu hawa IMTU pamoja na kutaka kufanana na ile THI ila hawa kuna mambo walikosea hasa kwenye issue ya utafiti na mazoezi kwa vitendo, japo walijirekebisha ila waafrika sisi ni viumbe vya ajabu sana aiseee...
mkuu, sio kwamba mkasa wa IMTU ni fitna kali sana baada ya wao kudhamini vikao na mikakati ya jopo la waganga ambalo kiranja alijikuta yupo msituni bila vitafunio na vimenyeo kadhaa?
 
mkuu, sio kwamba mkasa wa IMTU ni fitna kali sana baada ya wao kudhamini vikao na mikakati ya jopo la waganga ambalo kiranja alijikuta yupo msituni bila vitafunio na kucha kadhaa?
Hiyo naweza kusema ni sababu ndogo ila nyuma ya pazia walitumiwa vibaya na ile issue ya kutupa miili iliyofanyiwa rehearsal na madaktari wapya mafunzoni ikawa ni njia ya kuwatimua.

Bado nasema Afrika acha kabisa asee 10% per si mchezo.
 
Mkuu hawa IMTU pamoja na kutaka kufanana na ile THI ila hawa kuna mambo walikosea hasa kwenye issue ya utafiti na mazoezi kwa vitendo, japo walijirekebisha ila waafrika sisi ni viumbe vya ajabu sana aiseee...
Kiufupi katika nchi hii, habari ya 10% inatawala sana na usipokaa na wahusika wenye nguvu na nafasi fulani,utapigwa kwa kuzungukwa mpaka kieleweke mfano THI pia ilikuwa inanyonywa malipo yake na NHIF mathalani 200m zilioneshwa zimelipwa wakati walikuwa wamelipa 40m kati ya 240 zilizokuwa zinadaiwa na Taasisi,hiyo ilitokana na Dr.Masau kutokubali mambo yao ya hovyo kuhujumu nchi kwa kujiongezea malipo yasiyo stahili kama zilivyokuwa baadhi ya taasisi au hospitali zilizokuwa zikilipwa hadi 800m mpaka 1billion kwa mwezi. 10% ni shida na ni ugonjwa mkubwa sana unaolitafuna taifa letu kihuni huni tu.
 
Back
Top Bottom