Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,852
- 20,169
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa na habari mbalimbali zinazomhusu mwanasiasa mbunge Zitto Zuberi Kabwe.
Moja ya taarifa hizo ilikuwa ni uamuzi wake wa kutangaza dhamira ya kugombea uraisi kwa kupitia chama chake cha CHADEMA kwenye uchaguzi wa uraisi mwaka 2015.
Kufikia azma yake hiyo Mheshimiwa Kabwe ambae ni naibu katibu mkuu , kwa uratatibu wa chama inabidi ashindane na katibu mkuu wake mheshimiwa Freeman Mbowe.
Lakini baadae mheshimiwa Kabwe akaja na kutangaza uamuzi wa kujitoa katika kinyang'anyiro cha kugombea nafasi hiyo ndani ya chama chake. Pia akaeleza kwa baadhi ya vyombo vya habari kwamba uamuzi wake huo umetoka moyoni na kwamba ni uamuzi wa kulinda heshima ya chama chake kutoka kwenye wingu la mpasuko ambalo lingekikumba chama cha CHADEMA.
Sasa kitendo hiki cha mheshimiwa Kabwe kuonyesha au kutangaza nia yake ya kutaka kugombea nafasi ya kuchaguliwa na chama chake kuwa mgombea uraisi bila kushauriana na wanachama waandamizi wa CHADEMA ambao wangetoa ushauri wao juu ya azma hiyo ya mheshimiwa Kabwe , kinaonyesha ubinafsi alio nao mheshimiwa Kabwe.
Mheshimiwa Zitto Kabwe ana umri wa miaka 35 kwa sasa na ifikapo mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 38 kama sikosei.
Huu ni umri mdogo sana kwa siasa za Tanzania achilia mbali siasa za nchi za Magharibi na Marekani. Ni vema mheshimiwa Kabwe ametoa uamuzi wa busara kuhusu hili.
Mimi ntaongelea baadhi ya viongozi watatu ambao wamechaguliwa kuwa maraisi au viongozi wa nchi tatu wakiwa na umri mdogo lakini ni kuanzia miaka 40.
Viongozi wengi wa nchi hizo Uingereza ( David Cameron miaka 46) Russia (Dmitry Medvedev miaka 47 ) na USA (Barak Obama miaka 51 ) walichaguliwa kuwa viongozi wa nchi hizo wakiwa na umri mdogo ambao umeonyesha kukomaa kisiasa.
Lakini kuna sababu zake, sababu kwamba Cameroon na wenzie niliowataja walionekana wataleta picha ya mabadiliko kwenye vyama vyao vya siasa kwa kuzingatia vyama hivyo vilikuwa na sura za wazee na mambo yaliyopitwa na wakati ambazo hazikuonyesha kutokea mabadiliko yoyote yale.
Cameroon mwaka 2005 akashindana na mzee Davis Davis akiwa na umri wa miaka 39 na akashinda nafasi ya kuwa kiongozi wa Conservative na akakaa bungeni akishindana na Gordon Brown na baadae akazoeleka kwa wapiga kura kwamba msimamo wake na wa chama ni upi na kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 akashinda uchaguzi na kuwa Waziri Mkuu akiwa na umri wa miaka 44.
Lakini Cameroon alikuwa na watu wanamsaidia katika kufikia azma ya kuwa kiongozi wa chama hicho kwahio ilikuwa kazi rahisi kupita kwenye uchaguzi ndani ya chama cha Conservative. Ilikuwa ni umri wake ambao ungewavuta wapiga kura vijana ambao kwa miaka mingi walikuwa wakiona siasa kwamba ni shughuli za wazee.
Barak Obama nae mwaka 2008 aligombea na mama Clinton kuwa mgombe wa chama cha Democrat wa uraisi wa Marekani na wakati huo alikuwa ana umri wa miaka 47 na baadae akamshinda mgombea mzee John McCain kwenye uchaguzi wa uraisi.
Obama kabla ya hapo alikuwa ni bunge au Senator wa Illionis na alikuwa na uzoefu wa siasa karibu miaka minane. Obama alishinda uchaguzi wa Marekani kwa kutumia silaha moja tu nayo ni mabadiliko na akakonga nyoyo za vijana wan chi hiyo na watu wa umri wake na hata wadogo wakawa wanamuelewa.
Lakini kikubwa zaidi ni kitabu chake kiitwacho "Dream from My Father" ambacho kinaelezea maisha yake tokea alikotoka.
Waziri mkuu wa sasa wa Russia Dmitry Medvedev alichaguliwa kuwa raisi wa nchi hiyo mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 43 na yeye tena alipitishwa na vyama vitatu tofauti kuwania uraisi na akapita bla taabu na kuwa raisi wa nchi hiyo.
Lakini hizi siasa za mataifa haya ni siasa zilizojengwa kwa miaka na miaka na hazikuanza leo. Ni lazima mheshimiwa Kabwe atambue tofauti ya siasa hizi na siasa za nchi yetu.
Tanzania kabla ya mwaka 1992 haikuwa na vyama vingi vya siasa na baada ya kutambulishwa kwa watanzania, sasa kila mtu anafahamu kuhusu siasa hizi na yupo tayari kuchagua sera za chama chochote zinazoonekana zinafaa kuleta maendeleo katika taifa letu.
Mheshimiwa Zitto Kabwe atambue kuwa uraisi si tuzo wala cheo cha bure kinachogawiwa bila uangalifu. Ili mtu achaguliwe kugombea uraisi kuna sifa zake.
Hayati mwalimu Nyerere aliwahi kutoa moja ya sifa kuu za mtu anaeutaka uraisi :
Kwamba ataheshimu na kuilinda katiba- kwa maana kwamba mheshimiwa Zitto Kabwe ataheshimu katiba ya nchi na kufuata inavyosema hasa kuhusu kipengele cha umri wa wagombea ambapo umesimama kwenye miaka 40.
Mheshimiwa Zitto Kabwe pia anaonyesha dhamira ya kutaka kuleta nyufa ndani ya chama chake.
Kwahio, kwenye suala la umri kwa yeye Zitto Kabwe ni kwamba anataka kuwahi mno na hata hao wanaomshauri jambo hili wanafahamu hilo, lakini kwakuwa wanataka kukiharibia chama cha CHADEMA nafasi yake ya kukishinda chama cha CCM mwaka 2015 basi wanajaribu kutaka kuteka wanachama wasio na uzoefu na na siasa za Tanzania mmoja wao ni Zitto Kabwe. na kama hana uzoefu basi anao na anatumiwa ili kufanikisha azma hiyo.
Pia kitendo cha yeye kutangaza nia ya kutaka uraisi pia ni ishara kwamba ama anatumiwa na kikundi cha watu au anajituma yeye mwenyewe kwa matakwa yake binafsi.
Nawapongeza wazee wa CHADEMA ambao wameona jambo hilo mapema na kukaa kitako na kijana huyu mwenzetu kumuasa juu ya mwenendo wake.
Mpaka sasa CHADEMA kimeonyesha juhudi kubwa katika kukikosoa chama tawala kiasi cha kutikisa mhimili wa chama hicho ambapo sasa kumefanywa mabadiliko ya baadhi ya viongozi waandamizi na kuwepo kwa mpasuko usioeleweka na kupelekea chama hicho kuanza kuandaaa mikakati ya kukidhibiti chama cha CHADEMA.
Michezo michafu michafu katika siasa za Tanzania Mheshimiwa Kabwe anaifahamu, lakini ni lazima atambue kwamba kwa sasa hawezi kutumika au kujituma kutaka kutuchanganya sisi wananchi ambao tunapenda siasa za amani lakini zenye kuonyesha mabadiliko kwenye ngazi ya uongozi wana nchi.
Jambo hili halikubaliki kabisa.
Moja ya taarifa hizo ilikuwa ni uamuzi wake wa kutangaza dhamira ya kugombea uraisi kwa kupitia chama chake cha CHADEMA kwenye uchaguzi wa uraisi mwaka 2015.
Kufikia azma yake hiyo Mheshimiwa Kabwe ambae ni naibu katibu mkuu , kwa uratatibu wa chama inabidi ashindane na katibu mkuu wake mheshimiwa Freeman Mbowe.
Lakini baadae mheshimiwa Kabwe akaja na kutangaza uamuzi wa kujitoa katika kinyang'anyiro cha kugombea nafasi hiyo ndani ya chama chake. Pia akaeleza kwa baadhi ya vyombo vya habari kwamba uamuzi wake huo umetoka moyoni na kwamba ni uamuzi wa kulinda heshima ya chama chake kutoka kwenye wingu la mpasuko ambalo lingekikumba chama cha CHADEMA.
Sasa kitendo hiki cha mheshimiwa Kabwe kuonyesha au kutangaza nia yake ya kutaka kugombea nafasi ya kuchaguliwa na chama chake kuwa mgombea uraisi bila kushauriana na wanachama waandamizi wa CHADEMA ambao wangetoa ushauri wao juu ya azma hiyo ya mheshimiwa Kabwe , kinaonyesha ubinafsi alio nao mheshimiwa Kabwe.
Mheshimiwa Zitto Kabwe ana umri wa miaka 35 kwa sasa na ifikapo mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 38 kama sikosei.
Huu ni umri mdogo sana kwa siasa za Tanzania achilia mbali siasa za nchi za Magharibi na Marekani. Ni vema mheshimiwa Kabwe ametoa uamuzi wa busara kuhusu hili.
Mimi ntaongelea baadhi ya viongozi watatu ambao wamechaguliwa kuwa maraisi au viongozi wa nchi tatu wakiwa na umri mdogo lakini ni kuanzia miaka 40.
Viongozi wengi wa nchi hizo Uingereza ( David Cameron miaka 46) Russia (Dmitry Medvedev miaka 47 ) na USA (Barak Obama miaka 51 ) walichaguliwa kuwa viongozi wa nchi hizo wakiwa na umri mdogo ambao umeonyesha kukomaa kisiasa.
Lakini kuna sababu zake, sababu kwamba Cameroon na wenzie niliowataja walionekana wataleta picha ya mabadiliko kwenye vyama vyao vya siasa kwa kuzingatia vyama hivyo vilikuwa na sura za wazee na mambo yaliyopitwa na wakati ambazo hazikuonyesha kutokea mabadiliko yoyote yale.
Cameroon mwaka 2005 akashindana na mzee Davis Davis akiwa na umri wa miaka 39 na akashinda nafasi ya kuwa kiongozi wa Conservative na akakaa bungeni akishindana na Gordon Brown na baadae akazoeleka kwa wapiga kura kwamba msimamo wake na wa chama ni upi na kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 akashinda uchaguzi na kuwa Waziri Mkuu akiwa na umri wa miaka 44.
Lakini Cameroon alikuwa na watu wanamsaidia katika kufikia azma ya kuwa kiongozi wa chama hicho kwahio ilikuwa kazi rahisi kupita kwenye uchaguzi ndani ya chama cha Conservative. Ilikuwa ni umri wake ambao ungewavuta wapiga kura vijana ambao kwa miaka mingi walikuwa wakiona siasa kwamba ni shughuli za wazee.
Barak Obama nae mwaka 2008 aligombea na mama Clinton kuwa mgombe wa chama cha Democrat wa uraisi wa Marekani na wakati huo alikuwa ana umri wa miaka 47 na baadae akamshinda mgombea mzee John McCain kwenye uchaguzi wa uraisi.
Obama kabla ya hapo alikuwa ni bunge au Senator wa Illionis na alikuwa na uzoefu wa siasa karibu miaka minane. Obama alishinda uchaguzi wa Marekani kwa kutumia silaha moja tu nayo ni mabadiliko na akakonga nyoyo za vijana wan chi hiyo na watu wa umri wake na hata wadogo wakawa wanamuelewa.
Lakini kikubwa zaidi ni kitabu chake kiitwacho "Dream from My Father" ambacho kinaelezea maisha yake tokea alikotoka.
Waziri mkuu wa sasa wa Russia Dmitry Medvedev alichaguliwa kuwa raisi wa nchi hiyo mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 43 na yeye tena alipitishwa na vyama vitatu tofauti kuwania uraisi na akapita bla taabu na kuwa raisi wa nchi hiyo.
Lakini hizi siasa za mataifa haya ni siasa zilizojengwa kwa miaka na miaka na hazikuanza leo. Ni lazima mheshimiwa Kabwe atambue tofauti ya siasa hizi na siasa za nchi yetu.
Tanzania kabla ya mwaka 1992 haikuwa na vyama vingi vya siasa na baada ya kutambulishwa kwa watanzania, sasa kila mtu anafahamu kuhusu siasa hizi na yupo tayari kuchagua sera za chama chochote zinazoonekana zinafaa kuleta maendeleo katika taifa letu.
Mheshimiwa Zitto Kabwe atambue kuwa uraisi si tuzo wala cheo cha bure kinachogawiwa bila uangalifu. Ili mtu achaguliwe kugombea uraisi kuna sifa zake.
Hayati mwalimu Nyerere aliwahi kutoa moja ya sifa kuu za mtu anaeutaka uraisi :
Kwamba ataheshimu na kuilinda katiba- kwa maana kwamba mheshimiwa Zitto Kabwe ataheshimu katiba ya nchi na kufuata inavyosema hasa kuhusu kipengele cha umri wa wagombea ambapo umesimama kwenye miaka 40.
Mheshimiwa Zitto Kabwe pia anaonyesha dhamira ya kutaka kuleta nyufa ndani ya chama chake.
Kwahio, kwenye suala la umri kwa yeye Zitto Kabwe ni kwamba anataka kuwahi mno na hata hao wanaomshauri jambo hili wanafahamu hilo, lakini kwakuwa wanataka kukiharibia chama cha CHADEMA nafasi yake ya kukishinda chama cha CCM mwaka 2015 basi wanajaribu kutaka kuteka wanachama wasio na uzoefu na na siasa za Tanzania mmoja wao ni Zitto Kabwe. na kama hana uzoefu basi anao na anatumiwa ili kufanikisha azma hiyo.
Pia kitendo cha yeye kutangaza nia ya kutaka uraisi pia ni ishara kwamba ama anatumiwa na kikundi cha watu au anajituma yeye mwenyewe kwa matakwa yake binafsi.
Nawapongeza wazee wa CHADEMA ambao wameona jambo hilo mapema na kukaa kitako na kijana huyu mwenzetu kumuasa juu ya mwenendo wake.
Mpaka sasa CHADEMA kimeonyesha juhudi kubwa katika kukikosoa chama tawala kiasi cha kutikisa mhimili wa chama hicho ambapo sasa kumefanywa mabadiliko ya baadhi ya viongozi waandamizi na kuwepo kwa mpasuko usioeleweka na kupelekea chama hicho kuanza kuandaaa mikakati ya kukidhibiti chama cha CHADEMA.
Michezo michafu michafu katika siasa za Tanzania Mheshimiwa Kabwe anaifahamu, lakini ni lazima atambue kwamba kwa sasa hawezi kutumika au kujituma kutaka kutuchanganya sisi wananchi ambao tunapenda siasa za amani lakini zenye kuonyesha mabadiliko kwenye ngazi ya uongozi wana nchi.
Jambo hili halikubaliki kabisa.