the kind
JF-Expert Member
- Nov 6, 2019
- 728
- 504
Nianze kutoa pongezi kwa yale mazuri unayoyafanya na Mungu akusimamie kwa kila zuri unaloliandaa kwa mustakabali wa nchi yetu ya tanzania
Nikija kwenye mada,katika moja ya mazungumzo yako Mh. Rais uliwahi kukemea sana suala la uhamisho kwa watumishi hasa uhamisho ule wa ubabaishaji au uonevu ambao unafanywa na baadhi ya Watendaji wa serikali yako. Pia kama haitoshi ukatamka kwamba endapo mtumishi atahamishwa basi alipwe stahiki zake za uhamisho mara moja iwezekanavyo ikiwemo posho ya usumbufu na posho ya kujikimu. Pia ukasisitiza kuwa mtumishi asikubali kuhama endapo hajalipwa stahiki zake za uhamisho.
Katika Halmashauri hii ya Wilaya Korogwe Watumishi wamekua wakihamishwa kuanzia pale ambapo wewe ulitoa matamko hayo na wamekua hawalipwi stahiki zao pamoja na kuomba kulipwa madai hayo na pamoja na kukumbushia madai hayo na majibu wanayotoa Maafisa Utumishi ni kuwa madai yamefanyiwa hesabu na siku yeyote yatalipwa hiyo ndio imekua 'Ngonjera' yenyewe
MH RAIS ULIONE HILI
Nikija kwenye mada,katika moja ya mazungumzo yako Mh. Rais uliwahi kukemea sana suala la uhamisho kwa watumishi hasa uhamisho ule wa ubabaishaji au uonevu ambao unafanywa na baadhi ya Watendaji wa serikali yako. Pia kama haitoshi ukatamka kwamba endapo mtumishi atahamishwa basi alipwe stahiki zake za uhamisho mara moja iwezekanavyo ikiwemo posho ya usumbufu na posho ya kujikimu. Pia ukasisitiza kuwa mtumishi asikubali kuhama endapo hajalipwa stahiki zake za uhamisho.
Katika Halmashauri hii ya Wilaya Korogwe Watumishi wamekua wakihamishwa kuanzia pale ambapo wewe ulitoa matamko hayo na wamekua hawalipwi stahiki zao pamoja na kuomba kulipwa madai hayo na pamoja na kukumbushia madai hayo na majibu wanayotoa Maafisa Utumishi ni kuwa madai yamefanyiwa hesabu na siku yeyote yatalipwa hiyo ndio imekua 'Ngonjera' yenyewe
MH RAIS ULIONE HILI