Mheshimiwa Rais mkono wa CHADEMA umenyooshwa kwa maridhiano, mpira uko kwako

Zakaria Lang'o

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
2,593
2,767
Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkono wa Chama Kikuu cha Upinzani Chadema UMENYOOSHWA kwako kwa ajili ya MARIDHIANO. Je, utaupokea au utausukumia mbali!!?

Alichosema Mwenyekiti wa Chadema kina umuhimu wa pekee. Upinzani kwa ujumla wake una wanachama na wafuasi kwa mamilioni katika nchi. Hivyo ni ukweli ulio wazi kwamba kuwapuuza huku ukiimba wimbo wa umoja wa Watanzania ni kujidanganya.

Nitoe mfano: Katika mtaa ninaoishi wenye wapiga kura 1300, Chadema walifanya sensa na kupata wanachama na wapenzi wapatao 850.Mwenyekiti wa mtaa alikuwa anatokana na Chama hicho, tena mtu mwenye Elimu ya Chuo akiwa amesomea Ujenzi (civil engineering). Ameongoza mtaa kwa ufanisi kwa miaka mitano. Amewashirikisha Wananchi kujiletea maendeleo yao.

Wananchi walikuwa na matumaini ya kumpatia nafasi tena. Sasa matumaini hayo umeyazima kwa kuwateulia "viti maalum" maana ndivyo wanavyojulikana kwa sasa katika mitaa, vitongoji na vijiji. Mwenyekiti mwenye Elimu ya Chuo tena engineering, ameambiwa ameshindwa kujaza fomu kwa sababu hajui kusoma na kuandika!!!

Hali hii inazalisha chuki kwa sababu wengi wanaona kuwa kilichofanyika ni mapinduzi dhidi ya demokrasia yao. Wengi wanatambua kuwa kiongozi wa mapinduzi hayo ni Mhe Rais akiwashirikisha watendaji wa Kata, mitaa na vijiji.

Hebu tutafakari kwa pamoja kwamba Vyama vya upinzani vilivyoweza kuweka wagombea wapatao 600,000, laki sita kwa nchi nzima, Mhe. Rais unawezaje kuwapuuza kwa kutojali haki yao ya msingi ya kuchaguliwa wakati huo huo ukiitaka Tanzania iwe moja!!?

Ni kweli kuwa unahimiza maendeleo. Lakini unasahau kuwa Katiba ya nchi imeweka utaratibu kuwa maendeleo yoyote ni lazima yawe shirikishi. Watu ndio msingi wa maendeleo na kwa hiyo watu walio huru katika maamuzi ya nani awe kiongozi wao ndio chachu kuu ya maendeleo. Katiba ya Jamhuri Ibara ya 3(1) na 146(2)(c) iko wazi juu ya haya niliyoeleza.

Katika uchaguzi huu uliopita majeraha ni makubwa, hivyo ni busara tiba ikapatikana kupitia mkono ulionyooshwa wa Ndugu Mbowe.

Napenda nikukumbushe juu ya kile anachofanya Rais Uhuru Kenyatta kwa rafiki yako Raila Odinga. Rais Uhuru anajenga daraja akimshirikisha rafiki yako huku Wewe ukibomoa madaraja yanayotuunganisha Watanzania katika amani, udugu, haki na Uhuru!!!

Juzi tu Profesa Kabudi alikuwa akiwazodoa Wakenya kwa kutazama kibanzi kwenye macho yao juu ya Ukabila, huku sisi tukiwa na boriti ya ubaguzi wa vyama iliyokomaa!!!

Wakati ni sasa Mhe Rais, usizitazame kijani kwenye mikutano yako ikipiga vigelegele ukadhani Tanzania ni shwari. La, hasha. Hao wengi wao ni wanafiki wanaotumia fursa kwa sababu wanajua mkononi mwako kuna mkate. Ukidondoka kesho hutawaona karibu na wewe hata kidogo.

Mwisho ni imani yangu kuwa Watanzania wenzangu mtakaosoma maoni haya mtasaidia kumhimiza Mhe.

Rais wetu kujenga daraja la maelewano badala ya kumsaidia kuchochea kuni ili kuteketeza jengo la umoja wetu.
 
Makamanda, Chama cha Chadema ni chama kikubwa, kwa hiyo panapo takiwa michango katika suala kama hili tujitahidi wenye uwezo tuu hasa unowakilisha mawazo pevu na mapana ya chama ndio wachangie. Wengine wapite tuu. na hukuna kitu kibaya ukifanya hivyo. Zaidi unongeza hadhi na muonekano chanya wa chama. KARIBUNI SANA.
 
Mkiwa wastaarabu kama Hivi Rais atawasikiliza

Sasa kipindi kile mnamuita Rais mshamba,dikteta unadhani angewasikiliza?

tena Wabunge ndio walikuwa wanatamka haya maneno bora hata ingekuwa Wananchi wa kawaida
Kenyatta ana kebehiwa (sio kutukanwa) kila siku na hachukulii mambo hayo personal bali anajua ni siasa. Penye matusi sheria ipo inachukua mkono.
Huwezi kuchukia kundi Fulani, au chama Fulani au eneo fulani kwa sababu mmoja wao au wawili wamekuita mshamba au dikteta! Sio sifa ya uongozi siku hizi.
 
CHADEMA ndio wenye shida ya maridhiano, ndio wanatakiwa wampigie magoti na kumuomba Maguful mpaka awakubalie,
wakina lema, mnyika, sugu, wameshaona mwakani hawarudi bungeni, wanachofanya ni kumpigia magoti Magufuli awaonee huruma na kuwaachia ubunge wao, chadema wanataka maridhiano kwa maslahi yao binafsi
Wapuuzi sana, wanajali matumbo yao tu.!
 
CHADEMA ndio wenye shida ya maridhiano, ndio wanatakiwa wampigie magoti na kumuomba Maguful mpaka awakubalie,
Nyie ndio mnampoteza Rais, nani ampigie magoti na kwa lipi?
Kukosa maridhiano ndio kunaleta ya kina Kabila Sr, Karume, Sadat nk. Jee ndio mnataka ifike mahali "wajinga" watumie mwanya huu wa kutoelewana kwa kutenda uovu kama huo kwa Rais wetu?
Msiwe wajinga kiasi hicho!
 
Maridhiano yaende sambamba na kufufua uchunguzi wa washambulizi wa Tundu Lissu pamoja na kuwakamata wale wote waliohusika pamoja na wale waliozing'oa camera za CCTV
Kufufua uchunguzi wa wale waliohusika katika kumpoteza Ben Saanane Azory Gwanda na kumuua Alphonce Mawazo ili wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria
Wauwaji wa hayati Akwilina wakamatwe mara moja
Mauwaji ya Watanzania huko Rufiji uchunguzi ufanyike ili wahusika wafikishwe mahakamani

Kufuta kesi zote za kijinga dhidi ya Wapinzani zilizopo mahakamani

Hapo ndipo maridhiano ya kweli yatakapofikiwa.
 
Bado ni huyu Mh Rais anaesema anaona huruma watu kuwekwa magereza. Kwamba roho ina muuma na vitabu vya dini vina sisitiza msamaha.
Ni yeye huyu alie mtuma Lowasa awaambie wapinzani wataishia magereza, yaani huwa hakumbuki jana aliongea nini. Ona wapinzani wa kweli walivyo na kesi nyingi mahakamani. Huu ni mpango mkakakati wa serikali yenye Rais ambae roho ina muima magereza kujaa wafungwa na mahabusu.. Ina leta sinto fahamu kwa wananchi.. Zakaria Lang'o,
 
Mkiwa wastaarabu kama Hivi Rais atawasikiliza

Sasa kipindi kile mnamuita Rais mshamba,dikteta unadhani angewasikiliza?

tena Wabunge ndio walikuwa wanatamka haya maneno bora hata ingekuwa Wananchi wa kawaida
Sisi ni wastaarabu siku zote, tatizo ni tafsiri ya kila mtu. Halafu usisahau: mkubwa huwa ni jalala, lazima awe na ngozi ngumu inayohimili vishindo bila kuvunja misingi ya utaifa.
 
mkono wa Chama Kikuu cha Upinzani Chadema UMENYOOSHWA kwako kwa ajili ya MARIDHIANO
Hebu toa elimu kidogo.
Rais akiukataa mwito huu wa maridhiano atafanywa nn? Au serikali yake itaathirika vipi? Mbona amewadhulumu wapinzani ktk uchaguzi wa serikali za mitaa mchana kweupe na hakuna chochote kilichotokea?

Nchi nyingine vyama vya upinzani huwa vinajivunia mwamko wa wananchi. Kwamba upinzani ukilalamika tu wananchi wanaliamsha dude. Hapa kwetu wananchi ni maiti, upinzani unajivunia nn?

Hebu tuambie Rais akigomea maridhiano kuna madhara gani kwenye taifa hili la wananchi maiti na mbumbumbu?
 
Maridhiano yaende sambamba na kufufua uchunguzi wa washambulizi wa Tundu Lissu pamoja na kuwakamata wale wote waliohusika pamoja na wale waliozing'oa camera za cctv
Kufufua uchunguzi wa wale waliohusika katika kumpoteza Ben Saanane Azory Gwanda na kumuua Alphonce Mawazo ili wafukishwe mbele ya vyombo vya sheria
Wauwaji wa hayati Akwilina wakamatwe mara moja
Mauwaji ya Watanzania huko rufiji uchunguzi ufanyike ili wahusika wafukishwe mahakamani

Hapo ndio maridhiano ya kweli yatakapofikiwa.
Mm siungi mkono mtindo huu wa kuyataka maridhiano kwa kumbembeleza mtu. Ilipaswa ashinikizwe. Anabembelezwa???

Sasa kwa ataudharau upinzani mpk basi. Hivi mnajua semina ya kuukandamiza upinzani kaitoa wapi? Angalia misimamo ya hao waliompa semina, wana viburi hatari.
 
Back
Top Bottom