Mheshimiwa Nape Nnauye hongera kwa vita dhidi ya dhuluma kwa msanii

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Nimefurahishwa sana na vita nzito ambayo serikali imeianzisha dhidi ya wezi wote wa kazi za wasanii. Kumuona waziri Nape Nnauye mwenyewe akiingia front kwenye mapambano dhidi ya wote ambao wanachangia katika kuwapatia umasikini wasanii, ni jambo ambalo linahitaji kuungwa mkono kwa nguvu zote.

Wanamuziki, wachekeshaji na waigizaji ni kundi la jamii ambalo limedhulumiwa kwa miaka mingi sana. Hivyo kuiona serikali kwa maana ya waziri akiingia ndani ya duka moja baada ya jingine, kwa kweli inatia moyo sana. Kuna wanamuziki wengi sana ambao walikatishwa tamaa na dhuluma za kazi zao.

Ring tone za simu zimewapa utajiri mkubwa wenye makampuni huku wanamuziki wenye sauti na vipaji, wakikatiza mitaani wakiwa na maisha ya kawaida sana. Mara nyingi wanamuziki wakiridhika kununua magari ya kupigia misele mitaani, ambayo pia hayana thamani inayolingana na kazi yao inayosikika radioni na kuonekana runingani.

Wapo wananchi wenye kupenda sana kumsema vibaya mheshimiwa Nape Nnauye, katika zoezi hili la kuwakamata wote wanawadhulumu wasanii, kwa kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
ni nchi hii pekee kiti cha waziri kilichopo km 15, kinawatambua wezi wasiojulikana na polisi, bila shaka maduka yote aliyovamia yapo ndani ya mzunguko wa mita mia tatu kutoka kituo cha polisi msimbazi
 
Sina shaka na utendaji wa Mhe.Nape. Ni mpambanaji asiyeogopa sura, cheo, maneno au uwezo wa mtu. Wadau katika wizara yake, katika Nape, wamelamba dume.

Sote tunajua jinsi Nape alivyokinusuru ccm kisiangukie pua, naamini hatoshindwa kuwapigania wasanii wetu dhidi ya vimbweha ambavyo vimekuwa vikiwanyonya wasanii wetu.

Na imani si muda mrefu wasanii wataanza kufaidi matunda ya kazi zao na maisha yao yataakisi juhudi zao. Hii itawaepusha kujiingiza katika biashara km ya unga, ukahaba nk.

Wasanii, ni wajibu wenu kumuunga mkono Mhe. Nape katika mapambano aliyoanzisha kwa faida yenu.
 
ni nchi hii pekee kiti cha waziri kilichopo km 15, kinawatambua wezi wasiojulikana na polisi, bila shaka maduka yote aliyovamia yapo ndani ya mzunguko wa mita mia tatu kutoka kituo cha polisi msimbazi
Cha ajabu ni kwamba mihuri ya TRA iliyopo kwenye CD na kazi nyingine za wasanii sio fake ni yenyewe haswa!!. Majipu ni mengi mno, na inahitajika mikasi mingi ili mwili uweze kurudi katika hali ya kawaida.
 
Nimeshangaa kwenye mabasi mengi zinaoneshwa movies na miziki kutokea kwenye memory sticks ambazo zinakuwa copied kiholela mitaani na hakuna anayewakamata hao wanaoonesha hizo picha kinyume na sheria, inaonekana kuna mamlaka fulani ipo likizo kwa jambo hilo
 
Nimeshangaa kwenye mabasi mengi zinaoneshwa movies na miziki kutokea kwenye memory sticks ambazo zinakuwa copied kiholela mitaani na hakuna anayewakamata hao wanaoonesha hizo picha kinyume na sheria, inaonekana kuna mamlaka fulani ipo likizo kwa jambo hilo
aliyesema nchi hii imeoza hakukosea, mamlaka nyingi hazifanyi kazi zao.
 
Nimefurahishwa sana na vita nzito ambayo serikali imeianzisha dhidi ya wezi wote wa kazi za wasanii. Kumuona waziri Nape Nnauye mwenyewe akiingia front kwenye mapambano dhidi ya wote ambao wanachangia katika kuwapatia umasikini wasanii, ni jambo ambalo linahitaji kuungwa mkono kwa nguvu zote.

Wanamuziki, wachekeshaji na waigizaji ni kundi la jamii ambalo limedhulumiwa kwa miaka mingi sana. Hivyo kuiona serikali kwa maana ya waziri akiingia ndani ya duka moja baada ya jingine, kwa kweli inatia moyo sana. Kuna wanamuziki wengi sana ambao walikatishwa tamaa na dhuluma za kazi zao.

Ring tone za simu zimewapa utajiri mkubwa wenye makampuni huku wanamuziki wenye sauti na vipaji, wakikatiza mitaani wakiwa na maisha ya kawaida sana. Mara nyingi wanamuziki wakiridhika kununua magari ya kupigia misele mitaani, ambayo pia hayana thamani inayolingana na kazi yao inayosikika radioni na kuonekana runingani.

Wapo wananchi wenye kupenda sana kumsema vibaya mheshimiwa Nape Nnauye, katika zoezi hili la kuwakamata wote wanawadhulumu wasanii, kwa kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Hata hilo Bavichwa watalipinga pia.
 
nape mpambanaji sana, kama alifanikiwa kummaliza lowassa hawezi kushindwa vitu vidogo kama hivyo
 
Mh Nnauye Nape Jenga mfumo na mazingira ya kuzuia wizi wa haki miliki kazi za wasanii. Kamata kamata ni suluhisho la muda mfupi si endelevu ni kukurupuka.


nape mpambanaji sana, kama alifanikiwa kummaliza lowassa hawezi kushindwa vitu vidogo kama hivyo
 
Kwa HIT n RUN ya hii serikali tuliyo nayo na watendaji wake nachelea kutoa pongezi zozote kwasasa mpaka baada ya mwaka mmoja kuona nini kimefanyika na kuna Mikakati gani ya muda mrefu ya kuweza kudhibiti hiyo biashara
 
Kwa HIT n RUN ya hii serikali tuliyo nayo na watendaji wake nachelea kutoa pongezi zozote kwasasa mpaka baada ya mwaka mmoja kuona nini kimefanyika na kuna Mikakati gani ya muda mrefu ya kuweza kudhibiti hiyo biashara
Mwanzo ni mzuri, manyunyu tumeshayaona mvua ya neema inakuja kwa wasanii. Tuliaminishwa kwamba ili mwanamuziki afanikiwe ni lazima akubali kunyonywa na "wadosi". Vipaji vingi sana vimepotelea njiani.
 
Wasanii wenyewe ni Vi.la.za wasiojielewa, wameridhika na maisha wanayoishi. mfano,Nchini SWEDEN wanamuziki waliwahi kugoma na kuandamana week nzima kwa ajili ya masilahi.
 
Wasanii wenyewe ni Vi.la.za wasiojielewa, wameridhika na maisha wanayoishi. mfano,Nchini SWEDEN wanamuziki waliwahi kugoma na kuandamana week nzima kwa ajili ya masilahi.
Ubabaishaji kwenye elimu upo kila sekta. Hatuna ile hali ya kujiamini na kuthubutu kupiga hatua kwa nguvu zote kama Wanigeria. Diamond anayethubutu kujiendeleza kimataifa, anaishia kupigwa vita na waoga wengi.
 
wacheni usanii kama yupo seriously aende huko makamopuni ya simu kasaidie walie wasanii wetu na sio kukomalia machinga mtaani na viduka vya kko.
 
Back
Top Bottom