Rais Magufuli, nakuomba usipende chomekea neno 'kifo' katika kusisitiza jambo

TumainiEl

JF-Expert Member
Jan 13, 2010
6,184
11,201
Mheshimiwa pole kwa Kazi. Najuwa Ile furaha na bahati Kuwa kiongozi mkuu wa Taifa huwa inakufanya upende kusema umejitoa hata kufa Kwa Taifa hili ni kweli kabisa. Tunajua sio wewe tu ila kila Raia wa Taifa hili roho yake ameitoa Kwa Taifa hili tena huenda Sisi tuna sema Kwa maneno ila wapo ambao kweli wakilitetea Taifa hili walikumbwa na umauti ni wengi sana na story zao zinaliza ukizisikiliza.

Mh, Maisha ni zawadi toka Kwa Mungu na kifo hakitajwi tajwi kwa sababu kifo ni roho na roho ya mauti huwa inasikia na mara nyingi Sana shetani amekuwa akijiinua mbele za Mungu kuziita roho ambazo zinataja habari ya kifo.

Shetani anajua hata ukidondoka leo mtu wa kushika kiti atapatikana na kamwe hakuna Jambo litaenda vibaya sema tu ndio utakuwa mwisho wako wewe mwana mapinduzi na sisi kama Taifa tutatikisika hivyo hatupendi iwe hivyo.

Kiukweli unakitaja kifo mpaka SASA inakera na kutuhuzunisha sisi Raia wema maana mara "Mimi nimejitoa hata kufa kwa ajili ya Taifa" ni kweli ila je hao waliokutangulia waliapa kutumia misaafu gani? Maana is the same na wao waliapa kwa damu Jambo ambalo ni the same kama ulivyoapa wewe. SASA Jambo jipya ni lipi? Na hapa ndipo napata tabu na kujiuliza why unakitaja kifo while unaomba tuliombee Taifa na wewe tukuombee?

Mkuu, kama hujui basi Mimi nakujuza na kama utapotezea na kusema hawa ndio walewale, Mimi nasema hewala ila Leo nakwambia ukweli - Kifo hakitajwitajwi maana kinasikia na humkuta anayekitaja wakati asioudhani wala kuutarajia. Hukupewa kuiongoza nchi ili ufe au upate mabaya, umepewa kuiongoza nchi kutupeleka kwenye maziwa na asali na ukimaliza uwaachie wengine wafanye kwa sehemu yao maana huwezi maliza yote; na ukisema unataka Fanya yote utachoka sana na hatimaye hutofurahia matunda ya kazi yako. While baada ya kazi lazima ufurahie KAZI yako na kushauri utakaowaachia kijiti.

Nimekusikia tena kule Chato unasema "Kwani nikifa nitaenda na huu Uwanja wa Ndege?" nikashituka na kukumbuka niliwahi ambiwa kifo hakitajwi na ukimsikia MTU anakitaja taja basi usishangae kwa yale yatakayomkuta. Neno 'nitakuongezea miaka ya kuishi' linaendana na baraka na neno 'nitakupunguzia miaka ya kuishi' linaendana na laana.

Tafakari maneno yako ya kuwa yanaukwaza moyo wa aliekuinua na kukuketisha na wakuu maana mtesi wako shetani anayatumia kuidai roho yako kwa maana unataja neno "Kifo" mara kwa mara ktk hotuba zako na kwa kutokujuwa athari zake kwako binafsi na kwa Taifa ni kama unatutisha kuwa "Kuwa Mkuu basi ni adhabu ya kifo" wakati tunawaona wastaafu wakiishi kwa Amani na kufurahia maisha.

Kumbe basi, ili kuondoka ktk vifungo vya mawazo ya kufa ni kuishi vyema na watu wako na kujenga umoja na mshikamano wa Taifa. Unaweza kufanya mengi mazuri ila ukashindwa ishi ktk mioyo ya watu wako kwa kujenga chuki na masononeko na mwisho huzuni. Kama kiongozi, tafuta kwanza ishi ndani ya mioyo ya watu na hapo ndipo utaona utamu wa kutawala na kamwe hutochoka wala kukiwaza kifo kamwe.

Mfalme Ezekia alipokea ujumbe kutoka kwa Nabii wa Mungu kuwa atakufa na aandae mambo ya nyumba yake maana atakufa ndipo mfalme aliposikia hayo alichana nguo zake na kumuomba Mungu amsamehe na kukumbuka mema alimtendea, ndipo Mungu akamtuma Nabii wake na kumwambia "Mwambie Ezekiel nimesikia maombi yake na nimemuongezea miaka kumi na mitano aishi". Kumbe Mungu anapenda tuishi ila shetani anapenda tufe akijua huwezi mpata MTU anayefanana na yule amekwisha kufariki. Hivyo basi tukumbuke Mungu anapenda tuishi na kumtukuza.

Mungu ibariki Tanzania na viongoz wake. Amen
 
Tabia za madikteta
1. Wakikaa na wananchi huwa wanajinyenyekeza kwao na kujifanya sana wapo kwa kuwapigania.
2. Ili kuwapumbaza watu kwa kujipelekea maendeleo kwao, na kwingine watapeleka kidogo
3. Huwa wanabadilika kuendana na msimu. Mfano mwanzoni mwa uongozi watalalamika sana kuwa ni mzigo mzito, wanajilazimisha....Ila wakiona wanakaribia kuondoka watakuja na lingine eti nilitaka niondoke ila sioni wa kuendeleza yote niliyoanzisha

Yani hao ndiyo madikteta wanaotaka kutawala maisha yao yote!
 
Back
Top Bottom