Mheshimiwa Mbowe usije kufungua Ofisi ya CHADEMA Arusha

Mantisa

JF-Expert Member
Dec 20, 2010
322
236
Nakumbuka wiki iliyopita uongozi mzima wa Chadema ulikuwa uje kufungua ofisi ya kata ya Olorien- Chadema lakini kutokana na kikao cha dharula ilibidi uongozi mzima uwepo Dar es Salaam hivyo uzinduzi huo ukahairishwa mpaka wiki hii

Kwa mtazamo wangu ofisi kama hizi za kata zinatakiwa kufunguliwa na wenyeviti wa mikoa hivyo mheshimiwa tunaomba upumzike kwa hilo na kuwaachia viongozi wa mkoa
Binafsi ningependa kukuona ukizindua ofisi za mikoa na wilaya badala ya hizi za kata. Kifupi ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawajui hata ofisi za chadema za mikoa zilipo na pia ofisi zenye bado hazikidhi mahitaji ya chadema kikubwa kama chadema. Tunawaomba uongozi mfanye mikakati ili chama kiweze kuwa na ofisi zinazoeleweka ambapo ndo tutapenda mheshimiwa Mwenyekiti uje kufungua badala ya hizi za kata

Nashukuru na natumaini utakuwa umenielewa
 
siyo lazima sana kuwe na protocal hiyo. Mwenyekiti taifa anaweza karibishwa kufungua ofisi siyo tu za kata, hata za kijiji kama njia ya kuhamasisha umma na ku -"draw attention"-nationally kwa umma na wapenzi wa CDM kufanya hivyo katika ngazi zao. Nakumbuka mwaka 1981 Rais Nyerere (hayati) wakati ho alikuja kijijini kwetu kufungua ofisi za ccm!!! Kumbuka uwepo wa mbowe utafanya uwepo wa viongozi wote mkoa na wilaya zake wawepo na hivyo kuifanya sherehe kuwa na hamasa kubwa!!!
 
Kuna sababu gani za msingi kwa Mbowe kuja kufungua ofisi ya kata wakati hata Ofisi ya wilaya kama Arusha or Monduli watu hawaijui?
Ni mara ngapi tunamlaumu ****** kwende kufungua shule za msingi, zahanati, chekechea then why Mbowe au unataka kuniambia a spear is for a pig?
 
Kwani wale wananchi wa kwenye kata hawataki kuwaona viongozi wao wa kitaifa? Mi nadhani kama kuna ziara ya kutembelea mkoa/wilaya/kata/kijiji bado viongozi wa kitaifa wanaweza kufanya shughuli yoyote ikiwamo kufungua tawi!
 
Mantisa pamoja na hoja yako umepotosha umma maana si kweli kuwa Mwenyekiti taifa alikuwa aje kufungua hiyo ofisi,ni uongozi wa mkoa,na wilaya ndio walikuwa wafungue ila kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo tukaahirisha.Lakini pia hata Mwenyekiti taifa akifungua ofisi ya kata tatizo ni nini?
Ofisi ya mkoa ipo jengo la Namvua ghorofa ya nne
 
Nenda Mbowe kafungue hiyo ofisi ya kata, mbona rais anakwenda kijijini kuwatwisha ndoo akinamama anapofungua bomba la maji, kwani mkuu wa mkoa angeshindwa kumtwisha hiyo ndoo.
 
Mkuu basi wewe pia utakuwa not nupdated. Siku mkutano umehairishwa mwenyewe nilikuwa Olorien, nakumbuka pia kumuona mwenykiti wa mkoa palewakati wakitangaza kwamba viongozi wote wako dar na wiki ijayo watakuwepo wote wkiongozwa na Mwenyekiti. Wewe ulikuwa wapi wakati nawe ni diwani wa chadema? Basi kama iko hapo ndo inatakiwa mheshimiwa mbowe aje kuifungua nasi tujue iko hapo? Arusha kuna watu wangapi hawajui ofisi ya chadema ilipo? Ya wilaya iko wapi?
 
Nakumbuka wiki iliyopita uongozi mzima wa Chadema ulikuwa uje kufungua ofisi ya kata ya Olorien- Chadema lakini kutokana na kikao cha dharula ilibidi uongozi mzima uwepo Dar es Salaam hivyo uzinduzi huo ukahairishwa mpaka wiki hii

Kwa mtazamo wangu ofisi kama hizi za kata zinatakiwa kufunguliwa na wenyeviti wa mikoa hivyo mheshimiwa tunaomba upumzike kwa hilo na kuwaachia viongozi wa mkoa
Binafsi ningependa kukuona ukizindua ofisi za mikoa na wilaya badala ya hizi za kata. Kifupi ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawajui hata ofisi za chadema za mikoa zilipo na pia ofisi zenye bado hazikidhi mahitaji ya chadema kikubwa kama chadema. Tunawaomba uongozi mfanye mikakati ili chama kiweze kuwa na ofisi zinazoeleweka ambapo ndo tutapenda mheshimiwa Mwenyekiti uje kufungua badala ya hizi za kata

Nashukuru na natumaini utakuwa umenielewa

Ushauri mzuri hasa kuhusu hilo la cdm kufungua ofisi za kuleweka
Japo kwa ukweli kuhusu za kata hata mwenye kiti anaweza kufungua japo haipaswi kuwa wajibu wake!
 
Mkuu basi wewe pia utakuwa not nupdated. Siku mkutano umehairishwa mwenyewe nilikuwa Olorien, nakumbuka pia kumuona mwenykiti wa mkoa palewakati wakitangaza kwamba viongozi wote wako dar na wiki ijayo watakuwepo wote wkiongozwa na Mwenyekiti. Wewe ulikuwa wapi wakati nawe ni diwani wa chadema? Basi kama iko hapo ndo inatakiwa mheshimiwa mbowe aje kuifungua nasi tujue iko hapo? Arusha kuna watu wangapi hawajui ofisi ya chadema ilipo? Ya wilaya iko wapi?

Mmmh! Mantisa una lako jambo? Mbona hutaki Mwenyekiti wa Taifa aje? Kuhusu ofisi za mkoa si umeambiwa ziko Namvua ghorafa ya nne. Hivi wanachama wote wa CCM wanajua ofisi za chama za mkoa/wilaya ziko wapi? Nafikiri ndo maana ni muhimu Mwenyekiti Mbowe aje ili wanachama wa kata waifahamu ofisi yao ya kata iko wapi?
 
kwa kweli ni kukosa kazi kama mpaka ofisi ya kata ifunguliwe na Mwenyekiti Taifa kama atakua amekuja mkoani kwa kazi nyingine sawa lakini atoke Dar kuja kufungua ofisi ya kata? Haaaaaaaaah hiyo ni ushamba.
MBOWE weka nguvu tufungue ofisi ya MKOA lindi
 
Honestly mimi sielewi mambo haya. Chadema na ccm kuna tofauti kubwa sana. Wekeni nguvu kwenye mambo ya Msingi, gharama za kuja Arusha lkwa ajili ya kufungua ofisi ya kata ni kubwa tu sana. Kwa nini tusizitumie kwa ajili ya kuanza kiundo mbinu ya kufungua ofisi za wilaya? Unaweza kushindana na ccm hivi kweli?
 
Honestly mimi sielewi mambo haya. Chadema na ccm kuna tofauti kubwa sana. Wekeni nguvu kwenye mambo ya Msingi, gharama za kuja Arusha lkwa ajili ya kufungua ofisi ya kata ni kubwa tu sana. Kwa nini tusizitumie kwa ajili ya kuanza kiundo mbinu ya kufungua ofisi za wilaya? Unaweza kushindana na ccm hivi kweli?

Kwani wewe unaifahamu ratiba ya Mwenyekiti wa Taifa hadi useme anakuja huko kufungua ofisi ya kata tu? Kama unaifahamu basi utakuwa mmoja wa wajumbe wa CC au Nec ya CDM. Kama ni hivyo kwa nini usitumie vikao halali kutoa ushauri? Au wewe ni mmojawapo ya vibaraka wa CCM unajaribu kuuza hofu ya chama chako?
 
Acha ushamba, mi si kibaraka wa CCM. the thing is unatakiwa kuwa realstic. kitendo cha Mheshimiwa Mbowe na delegation yake kuja Arusha kwa ajili ya kufungua Ofisini ya Olorien is wastage of resources. Kuna mambo mengi sana anatakiwa kufanya coz hata wilaya kibao tanzania CDM haina ofisi na wanatakiwa kuconcentrate kwenye kujenga chama kwa mtindo huo. After all hapo wanapokuja ni so squeezed hamna hata mahali pa kukaa. Ni nyumba za watu ziko hapo. Huo msululu wote utakuwa hauna maana yeyote
 
Hilo ghorofa la Namvua lipo mahali gani hapo Arusha? Naombeni mnisaidie kupafahamu.
 
Namvua ipo stand kuu ya mabasi zamani ilikuwa inaitwa stadium store,
Mantisa mie sikuelewi mbali ya kuwa diwani mimi ni mwenyekiti wa vijana mkoa,na katika maandalizi ya kufungua hiyo ofisi ya olorien hatukumwalika mwenyekiti taifa kwa kuwa tunatambua majukumu aliyokuwa nayo kitaifa,sasa sijui kwa nini ulazimishe kuwa alikuwa aje.Kimsingi kama akiwa na muda sio vibaya yeye kufungua ofisi ya kata maana chadema tujijenga kuanzia ngazi ya shina,tawi,kata,wilaya,mkoa,kanda,na taifa,
Hiyo ofisi ya mkoa imezinduliwa kitambo,swala la kuwa ni wachache wanaifahamu ni sawa,na sisi tunajitahidi kuwajulisha wananchi nakuomba na wewe uendelee kuwajulisha ofisi ya mkoa ilipo,
 
Jamaa anaona Mbowe akienda atakwenda kuishika AR nzima ndo mana anatoa ushauri ahahahaaa.
Kama kweli inasubiriwa Mbowe aende kufungua ofisi ya kata nami sioni la msingi hapo.
 
Malengo ya m/kiti ndio yatasababisha uwepo wake. Kama analengo la kuhamasisha wanachama wa cdm kata zote nchini kuiga mfano wa hiyo kata na kuhakikisha tunakuwa na ofisi kila kata kabla ya 2014, he must be there kuonyesha msisitizo. Nadhan kampeni ya kuwasha taa ingekwenda sambamba na kuhamasisha ujenzi wa ofisi za kata katika kila wilaya na zingefanywa na wenyeviti wa wilaya na wa mikoa.. Hawa viongozi wa kitaifa wangehamasisha sehemu zenye weakness kama zanzibar mikoa ya pwani nk.
 
Malengo ya m/kiti ndio yatasababisha uwepo wake. Kama analengo la kuhamasisha wanachama wa cdm kata zote nchini kuiga mfano wa hiyo kata na kuhakikisha tunakuwa na ofisi kila kata kabla ya 2014, he must be there kuonyesha msisitizo. Nadhan kampeni ya kuwasha taa ingekwenda sambamba na kuhamasisha ujenzi wa ofisi za kata katika kila wilaya na zingefanywa na wenyeviti wa wilaya na wa mikoa.. Hawa viongozi wa kitaifa wangehamasisha sehemu zenye weakness kama zanzibar mikoa ya pwani nk.
 
Namvua ipo stand kuu ya mabasi zamani ilikuwa inaitwa stadium store,
Mantisa mie sikuelewi mbali ya kuwa diwani mimi ni mwenyekiti wa vijana mkoa,na katika maandalizi ya kufungua hiyo ofisi ya olorien hatukumwalika mwenyekiti taifa kwa kuwa tunatambua majukumu aliyokuwa nayo kitaifa,sasa sijui kwa nini ulazimishe kuwa alikuwa aje.Kimsingi kama akiwa na muda sio vibaya yeye kufungua ofisi ya kata maana chadema tujijenga kuanzia ngazi ya shina,tawi,kata,wilaya,mkoa,kanda,na taifa,
Hiyo ofisi ya mkoa imezinduliwa kitambo,swala la kuwa ni wachache wanaifahamu ni sawa,na sisi tunajitahidi kuwajulisha wananchi nakuomba na wewe uendelee kuwajulisha ofisi ya mkoa ilipo,


Ok nashukuru sana kunielewesha hilo. Hata hivyo unatakiwa ujue ya kwamba kwenye mkutano mimi mwenyewe nilikuwepo wakitangaza kuwa Mheshimiwa Mbowe atakuwepo na delegation yake, so kama huna uhakika muulize mwenyekiti wa chama wa wilaya mheshimiwa Magoma alikuwepo wakati tangazo hili likitangazwa. kama si kweli kuw ahatokuwepo you need to be serious. Mnatakiwa kutangazia wananchi vitu ambavyo ni reliable
 
Back
Top Bottom