Mheshimiwa Kikwete - Ninajua aliko Balali

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Mheshimwa Kikwete,

Kwa mujibu wa habari zinazodondoka hapa JF kuwa unakuja tena US kwa safari zako za kawaida. Kwa mikono miwili na heshima nyingi, wana JF wa USA tunakukaribisha tena kuja kula mbwa wa moto (hot dogs) na kucheza mpira wa kurushwa na kupigwa na gongo lenye umbo la kuchukiza (baseball).

Hongera pia kwa ziara ya Mama Kikwete hapa kwa mwaliko wa Mama Kichaka juu ya (on top of) mengine yooote. Pamoja na kuwa watu wa UK hawajui kwa nini umewatosa na kukwepa kuhudhuria mkutano wao ambao ulikosa maelezo thabiti hapa JF, mimi binafsi natoa shukurani kwa uamuzi wako wa kuja tena USA.

Nakushukuru kwa vile najua kabisa kuwa una taarifa zote kuwa yule mtu anayetuhumiwa kufanikisha wizi mkubwa kabisa wa BoT alikuwa anajificha hapa kwa muda fulani ili mafisadi wasimdito. Nakushukuru kwa vile najua kabisa kuwa una nia kabisa ya kujua nini kilitokea kwenye mapesa yote pale BoT ambayo kwa bahati mbaya au nzuri yalifanikisha kukuweka madarakani.

Kwa kujua hili na kwa vile naamini kuwa umebadili moyo na una nia ya kuomba msamaha kwa watanzania na kuhakikisha kuwa wezi wote wanakamatwa na kuwekwa lupango wanakostahili, nakupa juu (I holla you) kuwa ninajua kilichotokea kwa Balali na yale yote ambayo mafisadi wanajitahidi kwa kila njia kuyafunika huku ili watanzania wasiyajue kabisa.

Kwa haya yote, karibu tena USA ili tusaidiane kujua kwa undani zaidi kilichotokea kwenye mapesa yetu pale BoT. Karibu tena ili tusaidiane namna ya kudeal na huyo mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata ambaye ametokea kuwa swahiba wako - Rostam Azizi.

Karibu tena USA President Kikwete ili tukusaidie kujua yale yote yaliyotokea kwa Balali na mapesa ya walalahoi wa kitanzania na wale wakina mama na watoto wanaokufa kila siku kwa kukosa dawa na chakula bora huku mabilioni yakitumika kumlipa richmonduli!

Asante!
 
Ok na mimi pia napenda kutumia frusa hii kukupongeza kwa konyesha mshikamano wa kumuonyesha huyo fisadi mahala alipojificha
 
Balalli hatakiwi arudi Bongo maana ana SIRI KALI ambazo akizianika hadharani basi nchi inaweza kabisa kuwaka moto na kuzitetemesha nchi wahisani ambazo zinamwaga mabilioni ya pesa kila kukicha kusaidia nchi yetu.

Balozi wa Marekani alishatangaza hadharani kama Tanzania inamtaka Ballalli arudi Tanzania ili aje kujibu tuhuma mbali mbali za ufisadi dhidi yake, basi serikali yake iko tayari kabisa kusaidia kumrudisha fisadi huyo.

Lakini hadi hii leo SIRI KALI imekaa kimya kabisa kuhusiana na offer hiyo!

Kama kawaida yake ataingia mitini na kutokutana na Watanzania. Anaweza kuwachagua mazuzu wachache ili aonyeshe kwamba alikutana na Watanzania alipokuwa Marekani.

Panapofuka moshi.....
 
Huyu Ballali naye mhalifu tu wala asijidai watamuua wala nini, yeye kama kweli ana mapenzi na Tanzania kwa nini asijitokeze kusema ukweli wake wote maana ndiye aliyekuwa jikoni huyu.

Kwanza kilichomfanya aondoke huko IMF (or was it world bank, whatever) kurudi baada ya miaka yote hiyo kuwa mshauri wa Rais na baadaye gavana ni kitu gani kama siyo ahadi za kutajirishana wadanganyika tukiwa usingizini? I am compelled to conclude that his return was propelled by unbridled greed, among other things.
 
Huyu Ballali naye mhalifu tu wala asijidai watamuua wala nini, yeye kama kweli ana mapenzi na Tanzania kwa nini asijitokeze kusema ukweli wake wote maana ndiye aliyekuwa jikoni huyu.

Kwanza kilichomfanya aondoke huko IMF (or was it world bank, whatever) kurudi baada ya miaka yote hiyo kuwa mshauri wa Rais na baadaye gavana ni kitu gani kama siyo ahadi za kutajirishana wadanganyika tukiwa usingizini? I am compelled to conclude that his return was propelled by unbridled greed, among other things.

Mwakilishi hii ngoma ya Balali inaanguka miguuni mwa Kikwete. Hata akijaribu kuikwepa itamfuata kila aendako. Amekimbia UK kwa vile waaandishi wa the Guardian na magazeti mengine walikuwa wamepanga kumpiga maswali kuhusu issue ya rada.

Sasa ajiandae maana mipango inakamilika hapa kwa waandishi wa habari waanze kumuuliza issue ya Balali kila mara akitua hapa na kuweka ile news conference fake na rafiki yake Kichaka.

Muda si mrefu hata hii US Kikwete ataikimbia kama hataanza kuwa makini na kufuatilia malalamiko ya watanzania!
 
my Goat!!!!!!!!!!......yaani Kumbe Kikwete Yuko Scheduled Kuzuru Usa Soon....sasa Mkewe [balozi Wetu Wa Lugha Ya Kiswahili]..alikuwa Na Haja Gani Ya Kuja Kukaa Marekani Siku 14...si Angengoja Aunganishe Na Ziara Ya Christopher Columbus[muungwana]..ingetuokolea Kagarama Akiwa Anaongozana Na Mzee
 
my Goat!!!!!!!!!!......yaani Kumbe Kikwete Yuko Scheduled Kuzuru Usa Soon....sasa Mkewe [balozi Wetu Wa Lugha Ya Kiswahili]..alikuwa Na Haja Gani Ya Kuja Kukaa Marekani Siku 14...si Angengoja Aunganishe Na Ziara Ya Christopher Columbus[muungwana]..ingetuokolea Kagarama Akiwa Anaongozana Na Mzee

Mkuu hili ni swali kubwa linaloulizwa na wengi sana hapa USA
 
Jamani hii ni emergence kwa ajiri ya kupata ushauri wa mambo ya zimbabwe halikuwa hajapanga ndo maana alitakiwa kwenda UK na Denmark
 
Jamani hii ni emergence kwa ajiri ya kupata ushauri wa mambo ya zimbabwe halikuwa hajapanga ndo maana alitakiwa kwenda UK na Denmark

Mhh ... sikujua kama Zimbabwe ni emergency kama ilimchukua Kikwete zaidi ya muda wa kutosha kwenda Mererani kwa watanzania waliokufa kwa kufukiwa na makaburu oooopppppssss kwa mafuriko!
 
Mkuu hili ni swali kubwa linaloulizwa na wengi sana hapa USA


NAPINGANA NA KAULI YA MUUNGWANAS KUWA ALIJIANDAA ZAIDI YA MIAKA KUMI KUWA RAIS..KUNA TATIZO KAMA ALIJIANDAA MIAKA YOTE HIYO KULIKONI AKASHINDWAA KUTUANDALIA FIRST LADY,AKASHINWA HATA KUMPELEKA ZIARA ZA KUOSHA MACHO...NA HATA ENGLISH COURSE NJE...HATA KAMA NI KUKUZA LUGHA KUSHINDWA KUONGEA KINGEREZA FASAHA ..HAIVUTIII SANA....WAGOMBEA WENGI WANA KAWAIDA YA KUWASOMESHA WAKE ZAO ILI KUWAANDAAA..HILI KIKWETE HAKULIFANYA KABISA KWA SALMA...MIAKA KUMI INGETOSHA KUMFANYA SALMA AMBAYE NI MWALIMU WA UPE..KUWA NA DEGEREE YA UZAMILI..

......KINACHOONEKANA HAPO FIRST LADY NI MSHAMBA WA SAFARI BADO.....WAJIBU WA KWANZA WA FIRST LADY NI KUONGOZANA NA RAIS KADIRI IWEZEKANAVYO ESPECIALLY NJE YA NCHI HATAKIWI KUKOSA...JUST LOOK PRESIDA YUPO ZIARA YA KIKAZI WIKI MBILI NZIMA AKIWA BARCHELOR[HII NI TAFSIRI GANI..!!]....

KAMA MKEWE ATAJEUKA TENA KUMFUATA MAREKANI ..SI GHARAMA ZAIDI...FIRST LADIES WOTE HUTUMIA FURSA YA ZIARA ZA WAUME ZAO KUFANYA KAZI ZA KIJAMII NA FUNDRISING..NA SI KILA MMOJA KUPITA NJIA YAKE....

MKE NA MUME RAIS NI SURA YA FAMILIA YA KWANZA YA NCHI LAZIMA IWE MFANO WA UTENDAJI KAZI...PAMOJA NA MKAPA KUHISIWA HAWAELEWANI NA MKEWE ..HATA MARA MOJA HAWAKUSAHAU JUKUMU LA KUWA PAMOJA KILA MAHALA ..KAMA MFANO WA FAMILIA NAMBA MOJA[REGARDLESS OF WHAT IS SAID TO HAPPEN].....

SIKU HIZI TUNAYE RAIS NA MKEWE AMABAYE UKISIKIA HATA NYUMBANI YUPO ZIARANI KAGERA ...CLIP INAYOFUATA UTASIKIA MKEWE YUPO ZANZIBAR..UKISIKIKIA RAIS YUPO MAPUMZIKONI...MIKUMI ..CLIP INAYOFUATIA UNAMUONA MKEWE YUKO KWENYE SHEREHE YA RUSHA ROHO ZANZIBAR...
 

NAPINGANA NA KAULI YA MUUNGWANAS KUWA ALIJIANDAA ZAIDI YA MIAKA KUMI KUWA RAIS..KUNA TATIZO KAMA ALIJIANDAA MIAKA YOTE HIYO KULIKONI AKASHINDWAA KUTUANDALIA FIRST LADY,AKASHINWA HATA KUMPELEKA ZIARA ZA KUOSHA MACHO...NA HATA ENGLISH COURSE NJE...HATA KAMA NI KUKUZA LUGHA KUSHINDWA KUONGEA KINGEREZA FASAHA ..HAIVUTIII SANA....WAGOMBEA WENGI WANA KAWAIDA YA KUWASOMESHA WAKE ZAO ILI KUWAANDAAA..HILI KIKWETE HAKULIFANYA KABISA KWA SALMA...MIAKA KUMI INGETOSHA KUMFANYA SALMA AMBAYE NI MWALIMU WA UPE..KUWA NA DEGEREE YA UZAMILI..

......KINACHOONEKANA HAPO FIRST LADY NI MSHAMBA WA SAFARI BADO.....WAJIBU WA KWANZA WA FIRST LADY NI KUONGOZANA NA RAIS KADIRI IWEZEKANAVYO ESPECIALLY NJE YA NCHI HATAKIWI KUKOSA...JUST LOOK PRESIDA YUPO ZIARA YA KIKAZI WIKI MBILI NZIMA AKIWA BARCHELOR[HII NI TAFSIRI GANI..!!]....

KAMA MKEWE ATAJEUKA TENA KUMFUATA MAREKANI ..SI GHARAMA ZAIDI...FIRST LADIES WOTE HUTUMIA FURSA YA ZIARA ZA WAUME ZAO KUFANYA KAZI ZA KIJAMII NA FUNDRISING..NA SI KILA MMOJA KUPITA NJIA YAKE....

MKE NA MUME RAIS NI SURA YA FAMILIA YA KWANZA YA NCHI LAZIMA IWE MFANO WA UTENDAJI KAZI...PAMOJA NA MKAPA KUHISIWA HAWAELEWANI NA MKEWE ..HATA MARA MOJA HAWAKUSAHAU JUKUMU LA KUWA PAMOJA KILA MAHALA ..KAMA MFANO WA FAMILIA NAMBA MOJA[REGARDLESS OF WHAT IS SAID TO HAPPEN].....

SIKU HIZI TUNAYE RAIS NA MKEWE AMABAYE UKISIKIA HATA NYUMBANI YUPO ZIARANI KAGERA ...CLIP INAYOFUATA UTASIKIA MKEWE YUPO ZANZIBAR..UKISIKIKIA RAIS YUPO MAPUMZIKONI...MIKUMI ..CLIP INAYOFUATIA UNAMUONA MKEWE YUKO KWENYE SHEREHE YA RUSHA ROHO ZANZIBAR...

Kaka mambo mengine ni ya kifamilia zaidi kuliko unavyofikiri, unajuaje kama mzee ameamua kufuatana na bi mdogo, so leave that alone.
 
Kaka mambo mengine ni ya kifamilia zaidi kuliko unavyofikiri, unajuaje kama mzee ameamua kufuatana na bi mdogo, so leave that alone.

Hebu tupatie habari, maana naona sasa kuna bi mkubwa na bi mdogo, you know somthng that we don't?!
 
Kaja kuhakikisha - Boyz to Men watakuwepo mkutano wa Sullivan!.. haa haa haa emergency!
 
wakongwe hapa ndo tutakubaliana kwa kiasi fulani na mzee mugabe kuwa kuna baadhi ya viongozi wa africa ni "puppets" yaani vibaraka.
na hapo ndo mtahakikisha watanzania kuwa huyu jamaa keshakuwa kibaraka wa bush...

majuzi mugabe kawahoji swali ambalo kila mmoja kashindwa kujibu, kawauliiza (zimbabwe uchaguzi umefanyika kwa amani, na tume bado haijatangaza matokeo, iweje nyie mnaitana kikao kujadili hali ya zimbabwe wakati hata matokeo hayajatangazwa?)

kisha akawachapa na lengine akawauliza (mbona kenya ambako uchaguzi ulikuwa na udanganyifu wa kutosha na wizi wa kura na watu elfu na ushee wakauwawa na wengine kuyakimbia makazi yao iweje kule hamkuwakalia kikao?) na mi namuuliza lengine mbona mgogoro wa zenji anaupiga danadana ila ya wenzake anakuwa na kihelehele cha kuitatua?

mwafrika wa kike hebu wasiliana na waandishi wa ukweli wambane kwa maswali ya uhakika ili asiendelee kutudhalilisha...
 
Kaka mambo mengine ni ya kifamilia zaidi kuliko unavyofikiri, unajuaje kama mzee ameamua kufuatana na bi mdogo, so leave that alone.

..du jamani watanzania lets be serious...mtu anapoamua kuwa rais maisha hayawezi kuwa yale yale ..hasa upande wa kuhalalisha mambo kama hayo..anabeba jukumu la kuwa familia mfano...kama dini ina mruhusu akiona anaweza kuongeza rasmi tukajua...kuliko kuweka mazingira yanayoleta speculations...

...nataka niamini kuwa rais wangu hawezi kufanya uhuni wa wazi ..namna hiyo...

..tukumbuke kuwa pia mtu anapokuwa rais au mtumishi wa umma hata maisha yake binafsi yaapo under spotlights...
 
NAPINGANA NA KAULI YA MUUNGWANAS KUWA ALIJIANDAA ZAIDI YA MIAKA KUMI KUWA RAIS..KUNA TATIZO KAMA ALIJIANDAA MIAKA YOTE HIYO KULIKONI AKASHINDWAA KUTUANDALIA FIRST LADY,AKASHINWA HATA KUMPELEKA ZIARA ZA KUOSHA MACHO...NA HATA ENGLISH COURSE NJE...HATA KAMA NI KUKUZA LUGHA KUSHINDWA KUONGEA KINGEREZA FASAHA ..HAIVUTIII SANA....

Jamani we have to be proud og our lugha...umeona ma first lady wa G8 wote wanongea perfect english lakini kila wanapotua hotuba wanaongea lugha zao.
Kwa hiyo Salma anapoongea swahili anawakilisha tumpongeze jamani
 
Tuweke tufungue account tuchange pesa ya mafia watusaidie kumshughulikia balali hana haja ya kurudi. hapo NY na NJ kuna mafia wengi wanasubiri deal
 
Back
Top Bottom