Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Mbona mnashindwa kutoa sababu? Kama ni ufanya kazi tu mbona Lowassa alikuwa ni mchapa kazi asiye mfano? Toeni sababu na mafanikio ya huyu bwana!

Siasa za ushabiki ndizo zilizotufikisha hapa. Kama mnataka kuziendelea basi msimlalamikie mliemchagua kwa kishindo!


Amandla.......

Endelea kuwapigia debe mafisadi wanaokupa kitu kidogo. Usione kimya members wanakufahamu vilivyo hawawezi kukupa sababu.

Vibaka waliopo sasa hawafai tena ipo siku watajibu tu, si unakumbuka yaliyowapata kina Ceusesko kule Yugoslavia.
 
utasababisha jk abadilishe hata baraza la mawaziri ili amtoe. Nyamaza, let time solve and bring him to power. You know everyone loves Pombe because the old chap is a realist not idealist.


SAFIIII!!!!!!


Hata baada ya uchaguzi wa 2005 na kikwete kushinda wengi walijua jamaaa ndie angapewa Uwaziri Mkuu, Cha ajabu akapelekwa wizara zingine na akaonyesha umahili na ufanisi wake wa kazi ulivyokuwa swafi na kuongeza kutunga sheria katika wizara yake na bunge kupitisha huyo ndie anayejua kufanya kazi kwenye mapungufu unarekebisha na kuongeza. Ndie waziri ambaya najua JK anamwagwaya

JP Magufuli hata kesho akichukuwa fomu ya kugombea Urais, namuunga mkono na hata kumsaidia kupiga kampen.
 
Kiongozi ni yule anayeweza kuwaongoza watu (kundi la watu)waliokubaliana ili kufikia malengo yao kwa muda muafaka. Na ili hilo lifanikiwe, kiongozi huyo anatakiwa awe mtafsiri mzuri wa taratibu na sheria kwa nadhalia na vitendo ili wanaomfuata waweze kuiga pia na pengine wanaoenda kinyume kupata onyo mwafaka na kujirudi kabla hawajaleta madhara ndani ya kundi au jamii hiyo.

kwa misingi hiyo, Magufuli kwa jinsi ninavyomfahamu; anaweza kabisa kukaa kwenye nafasi hii ya uongozi wa juu kabisa nchini (Urais) na kutupeleka pale watanzania watunapotaka tuende lakini tumesubiri sasa takribani miaka 50 hivi bado hatufiki kwa sababu ya udhaifu katika uongozi.

Maana hata huo mfumo unahitaji kiongozi bora kuweza kuubadilisha ukaweza kufanana na namna inatakavyokuwa rahisi serikali kutenda kazi kwa uwajibikaji zaidi bila ya kupoteza muda na raslimali za nchi katika masuala binafsi maana mfumo utambana yeyote atakayefanya hivyo. Nina uzoefu wa kutosha kabisa kuhusiana na utendaji wa Ngugu JPM katika serikali yetu kwa muda mrefu sasa, ukiondoa mapungufu ya kibinadamu ambayo yanazidiwa na uwezo na sifa nzuri alizo nazo. Siku zote yeye hataki ubabaishaji na progaganda za kisiasa zinazolenga kudanganya wananchi ili waamini kauli fulani wakati uhalisia wake siyo hivyo. Yeye hujaribu kuwasilisha kwa umma takwimu zilizokusanywa kisanyansi zaidi, kwa lengo la kuonyesa mafanikio, na mapungufu ili mapungufu hayo yaweze kufanyiwa kazi kwa ajili ya kuboresa matokeo ya utekelezaji wa programu mbalimbali zinazosimamiwa chini ya sekta anayoiongoza yeye.

Bahati mbaya kabisa, huyu ndugu mara nyingi amekuwa akipambana na changamoto za kupingwa na matajiri walioko CCM, kwa vile wengi wao wamegawana mali za umma na inapotokea yeye kuyafanyia kazi hayo, huishia kuhamishwa wizara. Mfano wa haya, ni pale aliposimamia kurudishwa kwa fukwe zilizokuwa zimetwaliwa na wachache kinyume na utaratibu alipokuwa waziri wa Ardhi, na maendeleo ya Makazi. Sasa hivi ana changamoto kubwa tena kwamba anawanyang'anya wachache hao ranchi za taifa walizokuwa wamegawana kinyume na taratibu.

Nafupisha kwa kusema kwamba, kwa umsikini tulionao watanzania na uharibifu wa uadilifu katika serikali yetu. Tunamwihitaji mtu ambaye anafanana na JPM kuwa Rais wa nchi. Anaweza asiwe JPM lakini watu wa sifa kama zake tunawahitaji kuchukua nafasi ya Urais wa nchi katika wakati huu mgumu ambao wananchi (watanzania) tunahitaji miujiza tu ya uimara wa viongozi kutunusuru kutoka kwenye umaskini unaokomaa kila kunapokucha kwa sababu kwa viongozi kukosa mwelekeo na dira.

Heko Lekanjobe Kubinika kwa kutuletea thread hii kuweza kuijadili, maana kwa kufanya hivyo, hata kama tukamtaja JPM kufaa kuongoza nchi hii kama Rais; watu wa namna yake ndiyo pekee tunaowahitaji siku hizi za machafuko ya kiuchumi nchini.
Aluta Koninua!!!
 
tatizo lake ni MSUKUMA!
wewe ni wa kuepukwa sana nchini Tanzania gadem.
Ukabila wako kaufanyie huko huko ****** kwenu.

Sikubaliani na Magufuli kuwa rais, anafaa kuwa waziri mkuu as top profile kwani urais utamwondolea sifa yooote aliyokuwa nayo. yaani atavuruga kwani kuna genge linalokula mezani kwa kila rais ambalo kazi yake kubwa ni kumpotosha kwa maslahi yao binafsi
 
Mbona mnashindwa kutoa sababu? Kama ni ufanya kazi tu mbona Lowassa alikuwa ni mchapa kazi asiye mfano? Toeni sababu na mafanikio ya huyu bwana!

Siasa za ushabiki ndizo zilizotufikisha hapa. Kama mnataka kuziendelea basi msimlalamikie mliemchagua kwa kishindo!


Amandla.......


We kweli mpwa unamwelewa vyema EL??? kweli au? Kuchapa kazi kwake kulikuwa na malengo ya kutengeneza mtandao wa kuja kuichukuwa nchi nadhani ulipaswa kumfuatilia kwa makini, na alikuwa na kitu fulani kama ukabira hivi chunguza wamasai wengi wenye vyeo au watu kutoka kanda ya kaskazini uone huko mawizarani na serikalini. huko Arusha tu watu wanamjua fika hata alipokumbwa na kashfa ulisikia watu wa arusha wakimsupport???

Au wewe hujiulizi kama kweli alikuwa anachapa kazi na ni PM akakutwa na Richmond scandle huo ulikuwa uchapa kazi gani kuua nchi au alikuwa hajui mikataba ya nchi?


 
Magufuli toka akiwa naibu wa waziri wizara ya ujenzi tumeona cheche zake,akiwa waziri wa ujenzi barabara ya kati liyoshindikana ilitengenenzwa kwa kiwango cha rami,Angalia waziri waliochukua nafasi yake oooh MYGOD MIAKA MINNE SASA KIPANDE KILICHOACHWA NA MAGUFULI HAKIJAKAMILIKA.Magufuli anatufaa kwa kweli utleast rumpe miaka mitano tuone.
 
tatizo lake ni MSUKUMA!

Amaaah, Geoff! Ulimsasi aweee nangu ukurura amajaga?? watakusaidia hiyo tafsiri kwa watu wa kanda ya ziwa maana yake nin nini.

wewe ulitakiwa upelekwe Rwanda kwa Kagame alafu useme fulani ni Hutu au Mtusi uone moto wake 6month Rupango na baaadae kesi, Nchi hii haina ukabira labda wewe ndio utanzishie, au unawivu kuwa jamaaa huko kanda ya ziwa atapata kura zote tena za kishindo hata sie wanyagundu wa Dodoma tutampereka kuchukua fomu na kumlipia na kumpigia kura nyingi sana tena za kishindo na
 
Endelea kuwapigia debe mafisadi wanaokupa kitu kidogo. Usione kimya members wanakufahamu vilivyo hawawezi kukupa sababu.

Vibaka waliopo sasa hawafai tena ipo siku watajibu tu, si unakumbuka yaliyowapata kina Ceusesko kule Yugoslavia.

Hata mwezi haujapita toka ujiunga tayari umeishanifahamu thika!

Na huyo Ceusesko wa Yugoslavia ni nani? Ignorance haijifichi hata siku moja.

Amandla........
 
Mbona mnashindwa kutoa sababu? Kama ni ufanya kazi tu mbona Lowassa alikuwa ni mchapa kazi asiye mfano? Toeni sababu na mafanikio ya huyu bwana!

Siasa za ushabiki ndizo zilizotufikisha hapa. Kama mnataka kuziendelea basi msimlalamikie mliemchagua kwa kishindo!


Amandla.......

Mbona mwenzenu huu uchapa kazi anaosifiwagwa EL sijawahi kuuona??? Au kuvunja mkataba wa City water sijui DAWASA ndiyo inamfanya aonekane mchapa kazi.

Angekuwa kweli ni mchapa kazi tungemuona wakati akiwa waziri mkuu, alikuwa na muda mrefu tu wa kutuonyesha uwezo wake lakini akaishia kufanya what he can do best, RICHMONDULI!!!
 
Hata mwezi haujapita toka ujiunga tayari umeishanifahamu thika!

Na huyo Ceusesko wa Yugoslavia ni nani? Ignorance haijifichi hata siku moja.

Amandla........

Nilikuwa nakusoma na kukuchambua inside out kabla ya kuvamia jukwaa khe khe khe. unafikiri watanzania wote tumelala. sio lazima nijiunge ndio nianze kuchangia.

FYI Nipo hapa tangu alifu.
 
Toka aondoke Magufuli wizara ya Ujenzi JK hakuna hata barabara moja anayo weza kujivunia kuwa imeisha waziri wake wa Miundo mbinu kafanya kazi. Magufuli ni mchapa kazi jamani acheni wivu na siasa za maji taka huyu jamaa angekuwa waziri mkuu watendaji wababaishaji wangekuwa wamesha fungashwa vilago.
 
Nilikuwa nakusoma na kukuchambua inside out kabla ya kuvamia jukwaa khe khe khe. unafikiri watanzania wote tumelala. sio lazima nijiunge ndio nianze kuchangia.

FYI Nipo hapa tangu alifu.

Ceusesko wa YUGOSLAVIA ni nani?

Amandla......
 
Magufuli yupi? huyu aliegawa nyumba za serikali kwa wadogo zake na aliehonga mahawala?

Au Magufuli alie hifadhi samaki kwa milioni 100 kwa mwezi na kuishia kuwagawa bure?

Wakati mnaendelea na spinning zenu na hatimae kumuingiza Ikulu nie nahangaikia taratibu za kupata uraia wa Cambodia!
 
Endelea kuwapigia debe mafisadi wanaokupa kitu kidogo. Usione kimya members wanakufahamu vilivyo hawawezi kukupa sababu.

Vibaka waliopo sasa hawafai tena ipo siku watajibu tu, si unakumbuka yaliyowapata kina Ceusesko kule Yugoslavia.

Nadhani ulimaanisha Nicolae ceausescu wa Romania,elewa kuna wachambuzi humu JF,hivyo pima bandiko lako kabla ya kuleta taarifa potofu la sivyo utatolewa nishai.
 
Nadhani ulimaanisha Nicolae ceausescu wa Romania,elewa kuna wachambuzi humu JF,hivyo pima bandiko lako kabla ya kuleta taarifa potofu la sivyo utatolewa nishai.

Hebu ona kama kuna jinga ambalo haliwezi kufahamu mambo ya Yugoslavia utaliambia nini? Litaendelea kupigia debe mafisadi hadi kiama.
 
Always I've been impressed by the work done in any Ministry where Dr. John Pombe Magufuli has been a Minister. The guy is focus and wants Tanzania to move ahead. However, his personal hatred towards the opposition political parties makes me sick. Now if he becomes President or PM of the Republic with the swipping state powers in his hands would he not turn into a dictator? I'm yet to be convinced otherwise.[/QUOTE

hizi democrasia sijui ndo demoghasia ndo zinazotula....na tutakwisha kimya kimya mpaka tukubali kuongozwa kidictator....serikali inawaogopa mafi-sadi kwa sbb ya huu upuuzi wa democrasia....ndo maana i loved the then iraq under sadam hussein....teh teh and i love china, if you wanna join me in these visit cities like Shenzhen,guanzhou, shangai in china etc....wee kaa unaintertain maandamano, mafisadi, majungu ngazi zote za utendaji,posho mbilimbili uone kama hamujaisha.....
...huwa nachoka pale waziri mkuu na rais nao wanasimama majukwaani wanalialia eti oooh maafisa kilimo wanavaa suti!!!!mara oooh NGO zinazotumia advantage ya less preveleged tunazijua zijirekebishe zenyewe!!!mara oooh mafisaji wana nguvu sana tuwaendee taratibu!!!!
kama baba akiogopa kufungua mlango kama kuna kasheshe nje usiku nani atadare????ndo maana watu wanajaribu kidogo kupinga ufisadi alafu wanamsiiiiifu rais aliyewachagua kuwa ni hodari sana...wengine juzi wanasema tuwalaumu watu wa chini tumuache aliyewateua....usimlaumu aliyepika ugali mbichi ulaumu ugali wenyewe teh teh teh tihi tih iiiiiii iiii nalia mimi.
 
mwenzenu napata taabu kidogo, sijui jinsi gani mheshimiwa huyu ashawishiwe na kukubali ombi hili. Natamani sana john pombe magufuli awe rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania, kama sio sasa kwa sababu za taratibu za ccm, basi zamu inayofuata.

Vyovyote iwavyo, naamini huyu bwana anafaa kila kona uwanjani anapocheza siasa. Hata phd aliyoipata majuzi inaongezea chachandu tu, kwamba hatababaishwa na vyeti vya udaktari wa kupewa zawadi tu, maana anayo real one.

Sina uhusiano naye kabisa huyu mtu na wala sijawahi kukaa naye au kuonana karibu, lakini vitu vyake mwisho bwana. Naamini atachagua timu ya washauri inayofanana naye. Hata kama anayo mapungu yake kama binadamu, the good outways the bad, wakati mwingine analazimika kufanya vitu vingine kwa kuwatii wakubwa zake, lakini akishika rungu mwenyewe nashawishika (sidanganyiki) kwamba ataifaa tanzania ya sasa.

Leka

mimi naomba kama ikiwezekana tanzania tuondokane na kujikwamisha wenyewe na maendeleo ya nchi tuache mambo ya siasa zisizo na msingi ccm wamchague magufuli awe mgombea uraisi 2015, hapo akigombea nitaenda kumpigia kura hata kama upinzani atasimamishwa zitto vinginevyo tutaachwa nyuma kimaendeleo na nchi zote hata rwanda iliyokuwa na vita.
Potelea mbali hata akiwa dikteta itakuwa kwa manufaa ya nchi sio manufaa yake binafsi.
 
Achukue Form ili apambane na JK kwenye uteuzi wa CCM mwaka ujao, 2010. Anapatikana kwenye namba 0754 292580.
 
Back
Top Bottom