Mheshimiwa John Mnyika: What is Plan C

plan c:mda muhafaka wa plan A kufanya kaz..tuingien barabaran watanzania,hali hii mpaka lini?
 
Jmk aliwahi kusema mgao utakuwa historia tz ckuelewa manake nini!umeme hautapatikana au hautakatika kabisa!lugha za ndugu y2 huwa cwazi,anaweza sema tupo pamoja katika matatizo yenu lakini hakuna analotekeleza,tuwe makini na mjomba wetu mana wakati mwengine tunajiahidi wenyewe bila mwenyewe kusema ukweli
 
Ukiacha gharama ulizotaja, zipo nyingi ambazo mara nyingi watu hatuzitilii maanana. Kwa mfano:
1. Mwezi Juni kulikuwapo maonyesho ya utumishi hapo Mnazi mmoja. Kila idara ya serikali na kila shirika la umma lilikuwapo. Ukiacha gharama za kukodi mahema na kuyapamba kuna gharama nyingine km kukodi meza na viti, posho ya watumishi wote wanaoshiriki na kwa siku zote za maonyesho, gharama za vipeperushi na public address system, takrima kwa wazito wanaotembelea vibanda, n.k. Lakini muhuimu zaidi, kila mshiriki lazima awe na uniform...T-Shirt na kofia vya bei ya juu.

2. Baada ya Juni, Julai kulikuwa na maonyesho ya 77. Gharama ni kama za hapo juu, bila kusahau chakula na usafiri kwa kila mshiriki. T-Shirt na kofia za 77 lazima ziwe za 77.

3. Mwezi Agosti kuna sherehe za 88...sijui wapi. Gharama hivyo hivyo na per diem ya kuwa nje ya kituo cha kazi. T-Shirts na kofia...kama kawa.

4. Sasa kuna maonyesho pale Mnazi mmoja ya kila wizara...miaka 50 ya uhuru. Huenda hata mioani yapo. Gharama za kila idara na kila wizara kuwa na uniform yake nk inachefua. Hivi majuzi Wizara ya Afya 'painted red' Mnazi Mmoja grounds! By the time tunamaliza maonyesho ya miaka 50, gharama hizo na zile za maonyesho mengine kwa mwaka huu peke yake zingepunguza kwa kiasi kikubwa adha ya mgao. Kwa hiyo napendekeza hatua ya kwanza, umma uhamasishwe kuzuia maonyesho hayo...tubaki na maadhimisho ya Desemba ingawa hata hayo ni mzigo usio na tija!
 
maana yake tunahoji uhalali wa mamlaka? Kwani hatujui?

kwani cdm wakipewa chama pinzani chao kitakuwa kipi? Na kwa sasa ukifanya tahmini kwa wabunge na madiwani waliopata kupitia cdm tathini inaonyeshaje? Je wanaperform au imekuwa hakuna kitu? Tafadhali naomba mchango wenu
 
Voiceofreason,

Nashukuru kwa maoni yako na ya wachangiaji wengine. Suala hili nitalitolea tamko rasmi. Hoja yako ilikuwa mwezi Agosti, wakati mpango wa dharura ndio ulikuwa kwenye hatua za awali za utekelezaji. Serikali ilihodhi usimamizi wa utekelezaji wa mpango husika na kiwango kikubwa iliachiwa Wizara ya Nishati na Madini. Nilitahadharisha kwamba kwa mfumo huo malengo yaliyotajwa bungeni hayatatimia kwa wakati. Sasa tuko mwezi Oktoba na malengo ya mwezi Septemba ya mpango wa dharura sehemu kubwa hayajafikiwa; tunapoelekea sio kuzuri kama hatutakuwa na Plan C kuanzia mwezi wa Oktoba/Novemba. Tuendelee kujadili na kuchukua hatua za haraka

JJ
 
Voiceofreason,

Nashukuru kwa maoni yako na ya wachangiaji wengine. Suala hili nitalitolea tamko rasmi. Hoja yako ilikuwa mwezi Agosti, wakati mpango wa dharura ndio ulikuwa kwenye hatua za awali za utekelezaji. Serikali ilihodhi usimamizi wa utekelezaji wa mpango husika na kiwango kikubwa iliachiwa Wizara ya Nishati na Madini. Nilitahadharisha kwamba kwa mfumo huo malengo yaliyotajwa bungeni hayatatimia kwa wakati. Sasa tuko mwezi Oktoba na malengo ya mwezi Septemba ya mpango wa dharura sehemu kubwa hayajafikiwa; tunapoelekea sio kuzuri kama hatutakuwa na Plan C kuanzia mwezi wa Oktoba/Novemba. Tuendelee kujadili na kuchukua hatua za haraka

JJ

Asante Mkuu Much Appreciated Kwa Jibu lako.., Pamoja Sana..
 
Dah hali ni ngumu sana jamani...
nakumbuka nliwah kubishana na mtu kuwa mwezi wa pili nyie nyie wabunge mliopitisha mpango wa dharura mtaenda bungeni mnalia...PLAN C IPO 2015...DATS ALL
 
Nimefurahi ulivyo jibu mheshimiwa lakini hali hii imekithiri na watu wanumia, shughuli za kiuchumi zinakwama kama hali itaendelea maana yake ni kwamba tutarudi nyuma kimaendeleo baada ya kusonga mbele. Mheshimiwa Mnyika serikali imeruhusu sekta binafsi kuinvest kwenye umeme, ombi langu kwakua ninyi mko mstari wa mbele kutetea maslahi yetu sisi wananchi huoni kua sasa ipo haja ya nyinyi wabunge kumua kutafta wawekezaji binafsi kuzalisha umeme?
 
Nimefurahi ulivyo jibu mheshimiwa lakini hali hii imekithiri na watu wanumia, shughuli za kiuchumi zinakwama kama hali itaendelea maana yake ni kwamba tutarudi nyuma kimaendeleo baada ya kusonga mbele. Mheshimiwa Mnyika serikali imeruhusu sekta binafsi kuinvest kwenye umeme, ombi langu kwakua ninyi mko mstari wa mbele kutetea maslahi yetu sisi wananchi huoni kua sasa ipo haja ya nyinyi wabunge kumua kutafta wawekezaji binafsi kuzalisha umeme?

Tena huenda kutafuta wawekezaji wa kuwekeza ambayo huenda ikawa a complicated process na wakaonekana wana maslahi binafsi (10%) wanaweza waka-mobilize watu huko vijijini wakawajengea biofuels domes ambazo wakulima watatumia samadi na kupata gesi ya kupikia bila gharama ya kuni wala mafuta ya taa..,
 
Back
Top Bottom