Mhe. Rais, suala la ng'ombe zaidi ya 600 kufia zizini, ndilo linahitaji wahusika wawajibishwe kwa uzembe

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,272
18,334
Wakuu nimeona taarifa ITV ikionesha idadi kubwa ya ng'ombe waliokamatwa na watumishi wa hifadhi za taifa huko Rukwa, hali inasikitisha sana, wahusika wameonesha uzembe wa hali ya juu, wanashuhudia mifugo ikikosa huduma mpaka inafia zizini, wanaendelea kuongeza mifugo mingine mipya kwenye zizi lenye mizoga!

Wanaendelea kulinda mifugo ambayo hata kutembea haiwezi kwa sababu ya njaa.

Suala hili halipaswi kuachwa hivi hivi, kama tuliweza kupaza sauti kuhusu suala la vifaranga vilivyoteketezwa Arusha basi hili ni baya zaidi kuliko la Arusha kwa maana lile la Arusha wahusika walijibu kwamba ni sheria zipo na zinaruhusu kitu hicho. Japo kwa moyo wa kibinadamu ilitia huzuni sana.


Watumishi wa hifadhi wapo wamenenepa kabisa na afya zao safi eti wanalinda mifugo iliyokufa na mingine inaendelea kufa.

Sikatai wananchi waliingia maeneo ya hifadhi lakini kwanini hao ng'ombe wasingeendelea kupatiwa huduma? Au wangeuzwa kwa taratibu zilizopo.

Waziri kaamua mifugo irudishwe kwa wamiliki, sasa vipi kuhusu hiyo hasara? Je wizara au nchi imefaidika vipi kwa kushikiria hiyo mifugo kwa zaidi ya mwaka mzima? Mwananchi kapata hasara zaidi, serikali imemtia hasara mwananchi.

Ninachoweza kusema ni kwamba hawa watumishi wa hifadhi ni watu wanastahili kuwajibishwa, siwaombei mabaya ila hawa walitakiwa wafukuzwe kazi na taratibu ziangaliwe ili kufikishwa mahakamani kwa kuiingizia hasara serikali na wananchi wake.

Tuachane na wale wakurugenzi walioshindwa kujua takwimu, hawa wahifadhi wanastahili ile adhabu ya kupumzishwa na kusubiri kupangiwa kazi nyingine na wakati huo wakisubiri kupangiwa kazi nyingine basi wangeendelea kujibu kesi zao mahakamani. Huu ni uzembe wa hali ya juu.


cb47c8cdece5b6ed35c6dadbaef83967.jpg
 
IMG_20171107_211103.jpg

Hapa ndipo huwa sielewi maamuzi ya baadhi ya Viongozi

Sasa unakamata mifugo zaidi 700 na wanakufa mikononi mwa hizo mamlaka.

Hivi hiyo hasara nani analipa?

Kwanini kusiwe na mechanism nzuri ya kutunza hao mifugo wakati shauri lao linasikilizwa?

Hongera Waziri wa Mifugo Mh Mpina kwa kuhusu mifugo wengine 600 kwa kuwarudisha kwa wamiliki yaani wanainchi.
 
Walijua hao ng'ombe watakula hewa na mwanga wa jua...

Mambo ya ajabu kabisa.
 
View attachment 626318
Hapa ndipo huwa sielewi maamuzi ya baadhi ya Viongozi

Sasa unakamata mifugo zaidi 700 na wanakufa mikononi mwa hizo mamlaka.

Hivi hiyo hasara nani analipa?

Kwanini kusiwe na mechanism nzuri ya kutunza hao mifugo wakati shauri lao linasikilizwa?

Hongera Waziri wa Mifugo Mh Mpina kwa kuhusu mifugo wengine 600 kwa kuwarudisha kwa wamiliki yaani wanainchi.
Please Ebu futa hongera yako huyo jamaa ndio mwenye hiyo amri na anajiona roho mbaya kuliko boss wake.
 
Nimecheka eti watumishi wa hifadhi wapo wamenenepa na afya zao nzuri. Masimango kila upande jamani. Wanatekeleza amri bwana
 
Wakuu nimeona taarifa ITV ikionesha idadi kubwa ya ng'ombe waliokamatwa na watumishi wa hifadhi za taifa huko Rukwa, hali inasikitisha sana, wahusika wameonesha uzembe wa hali ya juu, wanashuhudia mifugo ikikosa huduma mpaka inafia zizini, wanaendelea kuongeza mifugo mingine mipya kwenye zizi lenye mizoga!

Wanaendelea kulinda mifugo ambayo hata kutembea haiwezi kwa sababu ya njaa.

Suala hili halipaswi kuachwa hivi hivi, kama tuliweza kupaza sauti kuhusu suala la vifaranga vilivyoteketezwa Arusha basi hili ni baya zaidi kuliko la Arusha kwa maana lile la Arusha wahusika walijibu kwamba ni sheria zipo na zinaruhusu kitu hicho. Japo kwa moyo wa kibinadamu ilitia huzuni sana.


Watumishi wa hifadhi wapo wamenenepa kabisa na afya zao safi eti wanalinda mifugo iliyokufa na mingine inaendelea kufa.

Sikatai wananchi waliingia maeneo ya hifadhi lakini kwanini hao ng'ombe wasingeendelea kupatiwa huduma? Au wangeuzwa kwa taratibu zilizopo.

Waziri kaamua mifugo irudishwe kwa wamiliki, sasa vipi kuhusu hiyo hasara? Je wizara au nchi imefaidika vipi kwa kushikiria hiyo mifugo kwa zaidi ya mwaka mzima? Mwananchi kapata hasara zaidi, serikali imemtia hasara mwananchi.

Ninachoweza kusema ni kwamba hawa watumishi wa hifadhi ni watu wanastahili kuwajibishwa, siwaombei mabaya ila hawa walitakiwa wafukuzwe kazi na taratibu ziangaliwe ili kufikishwa mahakamani kwa kuiingizia hasara serikali na wananchi wake.

Tuachane na wale wakurugenzi walioshindwa kujua takwimu, hawa wahifadhi wanastahili ile adhabu ya kupumzishwa na kusubiri kupangiwa kazi nyingine na wakati huo wakisubiri kupangiwa kazi nyingine basi wangeendelea kujibu kesi zao mahakamani. Huu ni uzembe wa hali ya juu.


cb47c8cdece5b6ed35c6dadbaef83967.jpg
Kwani wanatofauti gani na vile viranga vilivyochomwa moto?
 
Tanzania ni nchi ya maajabu sana hii. Wafugaji was nchi hii ni kama wakimbizi wasio na mtetezi. Amini amini nawaambia, baada ya miaka 5 kuanzia sasa nchi hii nitakuwa haina mfugaji hata mmoja. Nyqma tutakula ya kutoka nje.

Hakuna utaratibu wala ulinzi wowote ktk shughuli ya ufugaji
 
Usishangae hao watumishi wakipongezwa na kupandishwa cheo na yule mungu-mtu wa Tz. Yule jamaa ndio huwa anapenda sana watumishi wasiotumia Akili, wasiokuwa na huruma na wanaopokea maelekezo kutoka juu na kutekeleza pasipo kufikiri. Na inadaiwa huwa hapendi kabisa wafugaji.

Hao watumishi watakwambia waliambiwa wakamate tu mifugo na kuilinda ili isije ikaibiwa ikiwa mikononi mwa serikali, kuwatunza sio kazi yao na hawakutumwa kuwalisha.

Sijui Tz imeingiliwa na ibilisi gani?
 
Kuna watu hawastahili kuongoza hata kidogo. What the hell is that? Nani kawatuma wafanye hivyo? Sio hujuma?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom