VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Tupo kwenye mjadala wa madini. Kichwa cha habari ni MAKINIKIA. Mjadala umepamba moto. Tunakumbushana,tunasemana,tunatajana na kurekebishana. Kwa upana wa kitaifa.
Lakini,Rais na Mawaziri wako wawili wa Sheria na Katiba pamoja na yule wa Habari mmepunguza uwanja. Uwanja wa majadiliano. Mmekataza kutajwa kwa Mzee Mkapa na Mzee Kikwete kwenye mjadala.
Nakumbuka kivuko cha MV Bagamoyo nacho kilijadiliwa. Kuhusu ununuzi wake na matumizi yake. Rais ukatufunga mdomo kwa kukikabidhi jeshini. Ukatuambia kuwa sasa kimekuwa kifaa cha kijeshi na ni risk kukijadili. Tukanyamaza
Je,Mzee Mkapa na Mzee Kikwete nao wamekuwa vifaa vya kijeshi na hivyo hawajadiliki? Waliotajwa tuwajadili?
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Lakini,Rais na Mawaziri wako wawili wa Sheria na Katiba pamoja na yule wa Habari mmepunguza uwanja. Uwanja wa majadiliano. Mmekataza kutajwa kwa Mzee Mkapa na Mzee Kikwete kwenye mjadala.
Nakumbuka kivuko cha MV Bagamoyo nacho kilijadiliwa. Kuhusu ununuzi wake na matumizi yake. Rais ukatufunga mdomo kwa kukikabidhi jeshini. Ukatuambia kuwa sasa kimekuwa kifaa cha kijeshi na ni risk kukijadili. Tukanyamaza
Je,Mzee Mkapa na Mzee Kikwete nao wamekuwa vifaa vya kijeshi na hivyo hawajadiliki? Waliotajwa tuwajadili?
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam