Mhe. Rais... Amuru watu hawa wakamatwe!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Kwa mara nyingine tunashuhudia nchi yetu ikionyeshwa mchezo mwingine wa mazingaombwe! mchezo wa viini macho. Kitendo cha Rais Kikwete na kampuni kubwa ya madini ya Barrick kupitia tena mkataba ni udhihirishaji wa wazi kuwa mkataba ule wa mwanzo haukuingiwa kukiwa na imani (good faith) kati yao. Kuna mikataba mingine mingi tu ya madini, nishati, umiliki, ugavi n.k ambayo bado inazua maswali mengi.

Hata hivyo, mikataba hiyo haikuingizwa na majini au mapepo!! Walioiingiza serikali kwenye mikataba hiyo ni watanzania wenzetu walio katika nafasi mbalimbali kwenye wizara, idara, na vyombo mbalimbali vya serikali. Watu hawa kwa namna fulani wamenufaika kwa kumegewa sehemu kidogo ya makato wakati wa majadiliano ili mkataba wa aina fulani upite (rejea kesi ya IPTL). Bila ya shaka, tukiwachunguza maafisa wote walioshiriki katika mikataba hii na kulinganisha mali walizonazo (kwa majina yao au ya watoto wao) na kulinganisha vitu hivyo na mapato yao tutaona kuna tofauti kubwa!! Watu hao waitwe kujieleza walivipata vitu hivyo vipi, na ikibidi wapewe kinga ya kutokushitakiwa (siyo kutokutaifishiwa) endapo wataeleza bayana makato na mfuko waliopata toka makampuni makubwa yenye kutaka kuingia mikataba.

Haitoshi kusahihisha mikataba tu wakati walioiingiza serikali kwenye mikataba hiyo bado wana nafasi hizo hizo na bado wanashiriki katika majadiliano ya mikataba mingine. Ninapendekeza yafuatayo:

a. Serikali iweke bayana matakwa yote ya wale wanaoiwakilisha serikali kwenye majadiliano ya mikataba. Kama vile, hawaruhusiwi kupokea pesa, zawadi, au asante yoyote toka kwa kampuni hiyo kwa jina lao au la jirani yao.

b. Mikataba yote inayoingiwa na serikali ina haki ya kupitiwa na Bunge la Tanzania na inaweza kuhojiwa na kamati husika ya Bunge.

c. Endapo mkataba wowote unagundulika kuingiwa kwa kufoji au nje ya kuaminiana (not in good faith) mkataba huo wote (siyo vipengele tu) unakuwa umetanguka na hauna nguvu (null and void)

d. Wale wote ambao wanagundulika kuiingiza serikali kwenye mikataba mibovu huku wao wenyewe wakinufaika, wakamatwe mara moja, washitakiwe kwa sheria ya kuhujumu uchumi ya mwaka 1984??? na wafilisiwe endapo hawako tayari kurudisha mali zote walizojipatia kwa kutumia nafasi zao!

e. Mikataba yote iliyohusisha watu hao na madalali wao lazima ipitiwe upya (yote au vipengele) na endapo kuna kitu cha kusahihishwa, basi kitu hicho kianzie tangu nyuma (retroactive).

Haya yakifanyika basi naweza kuanza kuamini Mhe. Kikwete labda yuko serious.. otherwise.. yote ni mazingaombwe!! Je Mhe. Rais utathubutu kumfunga paka kengele??
 
Mwanakijiji leo nimesikia,

Kutoka kwa aliyekuwa naibu waziri wa wizara hiyo eti serkali inachofanya siyo kurekebisha Makosa ya awamu ya tatu! Anajihami sana huyu.

hivi kwa mfano kama katika AWAMU YA TATU tulikuwa tunalipwa asilia 3% kutoa 1.9% kwa jili ya ukagazi. LEO AWAMU YA NNE TUTALIPWA KWA MFANO 20%-?% ZA UKAGUZI?=? HUKO SIYO KUSAHIHISHA MAKOSA?

HIVI VIONGOZI KAMA MSABAHA NI LINI WATAACHA KUSEMA UOUNGO AU KUAMINI KUWA SIASA SIYO UONGO??

SOMA HAPA
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2006/08/23/72960.html
 
huyo itakuwa ameshachukuwa 10% yake.. Kwasababu serikalini sasa ni 10% tuu ndio zinazotaamba
 
Woooooooooooooote mnapoteza muda wenu bure kabisa . Huyo Msabaha ni ndugu yake JK . Pale pana ukaji kampa mtu wanyumbani . Waliokuwa 10% ni wana CCM wenzake JK na marafiki zake wengine walichangia Kampeni zake . Mwisho wa yote JK anasema huko ugenini kwamba yeye ni ndiye Mkapa mpya .Anamalizia kwa kusema atafuata na kuendeleza yooooooote ya Mzee Mkapa . Sasa mnategemea nini ? Kwenye ilani ya Uchaguzi ya CCM hawakuwa na neno kupitia mikataba bali kachukua sera za Vyama dume .Mimi sitaki kujadili hili maana hata JK ni mtu wa 10% tu mbona hatupati majibu ya IPTL na mengineyo ??? Kazi kubwa iko
 
Wazee!

Hili suala la mikataba inayotutia hasara kitaifa linakera sana. Nilipata kusoma hii ripoti THE POWER AND THE VAINGLORY: Anatomy of a $100 Million Malaysian IPP in Tanzania Brian COOKSEY. Cha ajabu ni kwamba facts ziko wazi kuwa kulikuwa na wingu la rushwa na mpaka majina ya wahusika wakuu yametajwa under oath. Kwa nini hao watu wasichukuliwe sheria?

Kwa vile mkataba mzima umethibitika kughubikwa na wingu la rushwa kwa nini hiyo isitumike kama kigezo cha kubatilisha huo mkataba? Nadhani wengi mnafahamu story ya ile kampuni ya mafuta ya Yukos ya Russia ambaye CEO wake bwana Mikhail Khodorkovsky yuko lupango kwa kukwepa kulipa kodi. Jamaa walimletea amount anayotakiwa kulipa, ikaonekana kubwa na kampuni ikapigwa mnada. Serikali ya Russia ikacheza deal na kuinunua tena, cheki hii link http://www.cnn.com/2004/BUSINESS/12/22/russia.yukos.rosneft/. Sasa hivi Russia is bouncing back!
 
mTz,
Good job. Ndio maana msimamo wangu ni kwamba iundwe Tume ya Ukweli. Viongozi wote waeleze, under oath jinsi walivyopata mali zao. Naona sasa kila kukicha mikutano yote inafanyika Ngurudoto. Nasikia hiyo ni mali ya EL.
 
Jasusi, I hope not.. maana kama hiyo mali ni kweli ya EL then that is the greatest example of conflict of interests.. hizi serikali wana mkataba na mahali hapo?
 
Naona sasa kila kukicha mikutano yote inafanyika Ngurudoto. Nasikia hiyo ni mali ya EL.

yaani wanaacha mali ya serikali AICC wanakwenda Ngurdoto. Au kwanini semina isifanyike Dodoma ambako kuna ukumbi wa Bunge? Hizi gharama za serikali zinaongezeka kwa matumizi yasiyo na msingi kama haya. Viongozi wa serikali wajifunze kubana matumizi.

Baba wa Taifa alishamkataa huyu Lowassa mwaka 95 sijui kwanini JK kampa Uwaziri Mkuu. Baba wa Taifa alidai Lowassa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa muda mfupi sana. Lowassa alikuwa tajiri kuliko kina Msuya,Malecela,Mkapa,... waliokuwa wameshika madaraka makubwa kwa muda mrefu.
 
JK kasema yeye ni Mkapa namba 2 hujaelewa nini ? Yeye kasema anaendelea yale ya Mkapa .Kila anachofanya kuwapa faraja ni kiinimacho.Sasa Ngurdoto ni Mali ya Mkapa wanapeana nafasi hizo kula .
Muulizeni Es anajua ile ni mali ya nani. JK anafuata ya Mkapa wewe unapiga kelele Mzee utaumia bureeeeeeeeeee
 
Kwa mara nyingine tunashuhudia nchi yetu ikionyeshwa mchezo mwingine wa mazingaombwe! mchezo wa viini macho. Kitendo cha Rais Kikwete na kampuni kubwa ya madini ya Barrick kupitia tena mkataba ni udhihirishaji wa wazi kuwa mkataba ule wa mwanzo haukuingiwa kukiwa na imani (good faith) kati yao. Kuna mikataba mingine mingi tu ya madini, nishati, umiliki, ugavi n.k ambayo bado inazua maswali mengi.

Hata hivyo, mikataba hiyo haikuingizwa na majini au mapepo!! Walioiingiza serikali kwenye mikataba hiyo ni watanzania wenzetu walio katika nafasi mbalimbali kwenye wizara, idara, na vyombo mbalimbali vya serikali. Watu hawa kwa namna fulani wamenufaika kwa kumegewa sehemu kidogo ya makato wakati wa majadiliano ili mkataba wa aina fulani upite (rejea kesi ya IPTL). Bila ya shaka, tukiwachunguza maafisa wote walioshiriki katika mikataba hii na kulinganisha mali walizonazo (kwa majina yao au ya watoto wao) na kulinganisha vitu hivyo na mapato yao tutaona kuna tofauti kubwa!! Watu hao waitwe kujieleza walivipata vitu hivyo vipi, na ikibidi wapewe kinga ya kutokushitakiwa (siyo kutokutaifishiwa) endapo wataeleza bayana makato na mfuko waliopata toka makampuni makubwa yenye kutaka kuingia mikataba.

Haitoshi kusahihisha mikataba tu wakati walioiingiza serikali kwenye mikataba hiyo bado wana nafasi hizo hizo na bado wanashiriki katika majadiliano ya mikataba mingine. Ninapendekeza yafuatayo:

a. Serikali iweke bayana matakwa yote ya wale wanaoiwakilisha serikali kwenye majadiliano ya mikataba. Kama vile, hawaruhusiwi kupokea pesa, zawadi, au asante yoyote toka kwa kampuni hiyo kwa jina lao au la jirani yao.

b. Mikataba yote inayoingiwa na serikali ina haki ya kupitiwa na Bunge la Tanzania na inaweza kuhojiwa na kamati husika ya Bunge.

c. Endapo mkataba wowote unagundulika kuingiwa kwa kufoji au nje ya kuaminiana (not in good faith) mkataba huo wote (siyo vipengele tu) unakuwa umetanguka na hauna nguvu (null and void)

d. Wale wote ambao wanagundulika kuiingiza serikali kwenye mikataba mibovu huku wao wenyewe wakinufaika, wakamatwe mara moja, washitakiwe kwa sheria ya kuhujumu uchumi ya mwaka 1984??? na wafilisiwe endapo hawako tayari kurudisha mali zote walizojipatia kwa kutumia nafasi zao!

e. Mikataba yote iliyohusisha watu hao na madalali wao lazima ipitiwe upya (yote au vipengele) na endapo kuna kitu cha kusahihishwa, basi kitu hicho kianzie tangu nyuma (retroactive).

Haya yakifanyika basi naweza kuanza kuamini Mhe. Kikwete labda yuko serious.. otherwise.. yote ni mazingaombwe!! Je Mhe. Rais utathubutu kumfunga paka kengele??
Hongera kwa ushauri mziri. Ilauna sbb sha 2kune makovu ya mende kesi ya nyani hakimu mmmmmmmmm. Ikulu kunamamboyake ndugu yale maneno yakampeni huingiinayo ikulu pale panahabarinyingine ndiomaana mshara wa Rais unalipwakeshi kabla yakumaliza muhula wake naunapelekwa uswis ku2nzwa haya ndio maisha bora.
 
Back
Top Bottom