Mhe. Magufuli, kuwa na idadi kubwa ya watu siyo guarantee ya utajiri. Utajiri hauletwi na idadi ya watu.

field marshall1

JF-Expert Member
Sep 17, 2017
1,171
2,730
Nimesikiliza hotuba ya rais Magufuli akisema watu wazaane sana na wanawake waachie mayai yao, akawatupia dongo wanao-support uzazi wa mpango kuwa wabanie mayai yao

Naomba nikushauri mheshimiwa rais kuwa UMEKOSEA, kuwa na idadi kubwa (High population) hakumaanishi kuwa kutailetea nchi utajiri. Mfano ulioutoa wa Nigeria, China na India hauakisi utajiri kwani hizi nchi bado zipo dunia ya tatu yaani ni bado ni nchi zinazoendelea (developing nations), Nchi ulizozitaja zina hali mbaya sana kwa uchumi wa raia zake ila ukihesabu kwa GDP-PPP zina namba kubwa kutokana na idadi ya watu lakini wengi wa wananchi wao ni maskini wa kutupwa, mfano Nigeria asilimia 25 ya watu wake ndiyo wana umeme, vijiji na miji imechoka, uhalifu ni kila mahali, machinga ni kila mahali, mauaji ni kila kona hakuna unafuu wowote, China ina GDP- Purchasing power parity kutokana na idadi yake kubwa ya watu lakini bado nchi imechoka ile mbaya ndiyo maana mnaona wachina wengi wanakuja Africa na kufanya biashara za umachinga na kuchoma mahindi, Hali ya maisha ya China ni mbaya sana ndiyo maana uhalifu na wizi ni mkubwa sana tofauti na nchi jirani yenye idadi ndogo ya watu lakini ina strong institution kama Taiwan, Singapore, South Korea au Malaysia.

Mfano ukiangalia USA yenye watu Mil.300 na China yenye watu 1.6 Billions (Zaidi ya mara tano), GDP (
Gross Domestic product) nominal ambayo inamgusa kila mtu, kwa USA ni mara 7 zaidi ya China. China zaidi ya watu millioni 450 ni mafukara wa kutupwa, walio na kazi (Middle class) wanalipwa chini ya Dollar 900 kwa mwezi na ni hao wanaofanya kazi kwenye makampuni ya nchi za Magharibi, hivyo hivyo kwa India, Bangladesh, Nigeria na Indonesia.
Mhe. Rais, idadi tuliyonayo tunashindwa kuihudumia hata kwa afya ya msingi tu, hospitali zetu zenye huduma mbovu zinaelemewa sasa kwa idadi hii,je tukiwa na idadi kubwa ya watu wasio na kazi tutaweza kweli.
Utamaduni wetu ni tofauti sana ukilinganisha na nchi nyingine, watu wengi si kwamba hawana mitaji lakini pia hawana utamaduni (
culture) ya kufanya kazi kwa bidii, tutaendelea kuzalisha wezi, majambazi nk,

Mhe. Rais usidanganywe na hao wanaokwambia tukiwa na idadi kubwa ya watu ndiyo tutakuwa matajiri....Angalia nchi zenye watu wachache kama Seychelles, Mauritius, Namibia nk zinavyofanya vizuri kiuchumi kulinganisha na nchi zenye watu wengi. Mifano mingine ni Qatar, Kuwaiti, Luxembourg, France, UK, Ireland (Mifano ni mingi)

Kumalizia si kweli kuwa idadi kubwa ya watu ni muhimu kwenye uchumi. Utajiri wetu utapatikana kwa watu kufanya kazi za kujituma, za maarifa, sayansi na ugunduzi lakini siyo za wamachinga.

Hivi kazi za kuuza bidhaa za watu wengine kwa population ya ndani kutawaondolea watu umaskini? Hatutaweza, lazima tuseme ukweli.
 
Huyu jmaaa sema tu ndyo ivyo kaishakuwa Rais na imetokea kuwa Rais kwenye nchi kma Tz. Ila ingekuwa kwa nchi zilzoendelea, sidhani kama hata application tu ya kugombea ingepita kwenye tume ya uchaguz. Angepimwa akili asingepita kabisa.

Hili liwe fundisho. wagombea wanatakiwa wapimwe akili na uwekwe utaratibu kama USA wa kumpima Rais akili kila mwaka.
 
Mleta mada ni mmoja wa wasomi Koko wajinga ambao taifa limepoteza pesa kuwasomesha.Uchumi wowote wa nchi yeyote duniani kuwa mkubwa unategemea population kubwa..Japan Ina population ndogo kwa Nini Ina uchumi mkubwa ? Jibu rahisi tu Ina uchumi mkubwa sababu inategemea population kubwa.Wanauza magari yao kwa nchi zenye population kubwa Kama Nchi za Afrika mfano Tanzania,Nigeria,Kenya,Kongo nk Huwezi tenganisha population na kukua kwa uchumi wa nchi.Kukariri masomo hakufai Ni vizuri kuelewa unachosoma.Mataifa yote yaliyoendelea tegemeo lao kuu Ni population usidangannywe.Mleta mada aliyekupa digrii anatakiwa atandikwe viboko katoa digrii kwa mtu mwenye empty head
 
Mkuu kwahiyo unataka kusema twendelee kuyapasua mayai tusiache yakaanguliwa? Hata Mimi kwa hili naungana na Mh Rais Tanzania bado tuna uhitaji mkubwa sana tena sana wa rasilimali watu sema vijana wanakimbilia mijini jambo ambalo linafanya tuonekane tumejaa kutokana na kubanana mijini huku vijijini kukisalia mapengo makubwa ya rasirimali watu.
 
Mleta mada ni mmoja wa wasomi Koko wajinga ambao taifa limepoteza pesa kuwasomesha.Uchumi wowote wa nchi yeyote duniani kuwa mkubwa unategemea population kubwa..Japan Ina population ndogo kwa Nini Ina uchumi mkubwa ? Jibu rahisi tu Ina uchumi mkubwa sababu inategemea population kubwa.Wanauza magari yao kwa nchi zenye population kubwa Kama Nchi za Afrika mfano Tanzania,Nigeria,Kenya,Kongo nk Huwezi tenganisha population na kukua kwa uchumi wa nchi.Kukariri masomo hakufai Ni vizuri kuelewa unachosoma.Mataifa yote yaliyoendelea tegemeo lao kuu Ni population usidangannywe.Mleta mada aliyekupa digrii anatakiwa atandikwe viboko katoa digrii kwa mtu mwenye empty head
Umemnukuu vibaya ww,,,
 
Uko sahihi kwa asilmia 25 ila kwingine umeharibu

Ni kweli kuwa na population kubwa halafu haina ajira ni tatizo kubwa na haiwezi kuinua uchumi bali kuupunguza

Ila ukiwa na population kubwa na kukawa na mipango mizuri (inayotekelezwa) kutainua nchi kiuchumi

Mfano sisi watanzania tukisema tutembelee mbuga zetu tutaingiza fedha nyingi tu kuliko hao wageni wanaokuja
Au tukisema tuwe tunanunua bidhaa za nchini kwetu unless io bidhaa haipatikan kabisa Tanzania tutafika mbali kiuchumi

Ila sio kuzaliana tu bila mpango
 
Magufuli unaweza kumpinga kwa mengi ila hili la idadi watu wengi kuleta maendeleo anasema ukweli, Kumbuka China ni ya pili kiuchumi duniani hiyo dunia ya tatu ya china ni ipi
Nimesikiliza hotuba ya rais Magufuli akisema watu wazaane sana na wanawake waachie mayai yao, akawatupia dongo wanao-support uzazi wa mpango kuwa wabanie mayai yao.
Naomba nikushauri mheshimiwa rais kuwa UMEKOSEA, kuwa na idadi kubwa (High population) hakumaanishi kuwa kutailetea nchi utajiri. Mfano ulioutoa wa Nigeria, China na India hauakisi utajiri kwani hizi nchi bado zipo dunia ya tatu yaani ni bado ni nchi zinazoendelea (developing nations), Nchi ulizozitaja zina hali mbaya sana kwa uchumi wa raia zake ila ukihesabu kwa GDP-PPP zina namba kubwa kutokana na idadi ya watu lakini wengi wa wananchi wao ni maskini wa kutupwa, mfano Nigeria asilimia 25 ya watu wake ndiyo wana umeme, vijiji na miji imechoka, uhalifu ni kila mahali, machinga ni kila mahali, mauaji ni kila kona hakuna unafuu wowote, China ina GDP- Purchasing power parity kutokana na idadi yake kubwa ya watu lakini bado nchi imechoka ile mbaya ndiyo maana mnaona wachina wengi wanakuja Africa na kufanya biashara za umachinga na kuchoma mahindi, Hali ya maisha ya China ni mbaya sana ndiyo maana uhalifu na wizi ni mkubwa sana tofauti na nchi jirani yenye idadi ndogo ya watu lakini ina strong institution kama Taiwan, Singapore, South Korea au Malaysia.
Mfano ukiangalia USA yenye watu Mil.300 na China yenye watu 1.6 Billions (Zaidi ya mara tano), GDP(
Gross Domestic product) nominal ambayo inagusa kila mtu kwa USA ni mara 7 zaidi ya China. China zaidi ya watu millioni 450 ni mafukara wa kutupwa, walio na kazi (Middle class) wanalipwa chini ya Dollar 900 kwa mwezi ni hao wanaofanya kazi kwenye makampuni ya nchi za Magharibi, hivyo hivyo kwa India, Bangladesh, Nigeria na Indonesia.
Mhe. Rais, idadi tuliyonayo tunashindwa kuihudumia hata kwa afya ya msingi tu, hospitali zetu zenye huduma mbovu zinaelemewa sasa kwa idadi hii,je tukiwa na idadi kubwa ya watu wasio na kazi tutaweza kweli.
Utamaduni wetu ni tofauti sana ukilinganisha na nchi nyingine, watu wengi si kwamba hawana mitaji lakini pia hawana utamaduni (
culture) ya kufanya kazi kwa bidii, tutaendelea kuzalisha wezi, majambazi nk,
Mhe. Rais usidanganywe na hao wanaokwambia tukiwa na idadi kubwa ya watu ndiyo tutakuwa matajiri....Angalia nchi zenye watu wachache kama Seychelles, Mauritius, Namibia nk zinavyofanya vizuri kiuchumi kulinganisha na nchi zenye watu wengi. Mifano mingine ni Qatar, Kuwaiti, Luxembourg, France, UK, Ireland (Mifano ni mingi)

Kumalizia si kweli kuwa idadi kubwa ya watu ni muhimu kwenye uchumi. Utajiri wetu utapatikana kwa watu kufanya kazi za kujituma, za maarifa, sayansi na ugunduzi lakini siyo za wamachinga.....Hivi kazi za kuuza bidhaa za watu wengine kwa population ya ndani kutawaondolea watu umaskini? Hatutaweza, lazima tuseme ukweli.
 
Kuwa na idadi kubwa ya watu hakufanyi nchi kuwa na maendeleo automatically, la hasha!

Kuwa na ididi kubwa ya watu siyo sababu pekee ya kufanya Taifa kuwa na maendeleo!

Maendeleo yanaletwa na vigezo vya msingi ambavyo vimeanishwa na tafiti mbali mbali za kisayansi !

Watu ni muhimu ktk kuleta maendeleo lakini kuwepo na kiasi!

Kwa miaka mingi hao wachina walishapangiwa kuzaa mtoto mmoja tu
 
Unaweza bishana na ushauri wa maprofesa kama kabudi wewe? Wale maprofesa ni wataalam wa kushauri.
 
Back
Top Bottom