Mhe. Joseph Selasini na CHADEMA kuweni makini na huyu mtu

Unasema kuna emails lukuki, ebu tuma tuzione hapa, tusije jadili mambo ambayo hayana ushahidi dhidi ya mtu ambaye ajapata mahali pa kujitetea. Ila huyu Edward uliyemtaja hapa namfahamu na inakuwa ngumu kwangu kuamini kuwa ni mtu wa namna ya unavyotaka kutuaminisha. Na ukweli uliopo Selasini amekuwa akijitenga na mambo mengi yanayohusu chama kitaifa na hata vijana wameanza kukata nae tamaa labda utuambie ameaanza kubadilika hivi karibuni baada ya kusoma nyakati.

Nimeonelea nisome kwanza michango ya wachangiaji kabla sija comment lolote kumhusu huyu m-bunge wetu wa Rombo mh. Selasini. Kwa kweli na ki-mungu huwezi kubeza mchango wa huyu m-bunge jimboni kwake Rombo. Pia ni fedheha kubwa kumlinganisha ki utendaji na Shibuda. Selasini kwa kawaida ni mtendaji zaidi kuliko kuongea ongea na kujitafutia sifa binafsi. Ukitaka kuliona hilo angalia matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika hivi karibuni. Rombo imepaa ukilinganisha na majimbo mengi na la mh.Mbowe likiwemo. Angalia jimbo la mh. Lissu nalo limepaa. Hii maana yake pana uhai wa chama pale. Wengi niliosoma michango yao hawana hoja zenye mashiko zaidi ya kubwabwaja tu bila pointi za maana. Wangekuwa kweli wanachama wa chadema hoja zao wangepeleka kwenye vikao halali vya chama na sio kuletwa mitandaoni. Kukaa tu na kushusha lawama hakukisaidii chama. Watuambie walishamwona mara ngapi m-bunge wao na kutoa ushauri wao na asiwasikilize? Kwani haipo ofisi ya m-bunge Rombo? Wao wanadhani ipo pale kupokea malalamiko ya wananchi tu au ni pamoja na wananchi kukutana na m-bunge wao na kushauriana nae kuhusu masuala mbali mbali yanayolihusu jimbo? Wasichokijua ni kwamba uongozi wa juu wa chama hawafanyi maamuzi makubwa kiasi hicho kwa kuchukua maoni ya mitandaoni. Sasa niwaombe wote wanaotaka nafasi hizo kuanzia udiwani, ubunge na hata zaidi ya hapo waache kuchafuana mitandaoni na wasubiri muda muafaka wafuate taratibu zitakazowekwa na chama. Hatari ya kuendeleza haya ni kukipa upenyo chama tawala kupita kirahisi jambo litakalokuwa ni pigo sio kwa chadema tu bali ukawa kwa ujumla. Naomba mtafakari huu ushauri.
 
Kiwewe ni kitu kibaya sana.

Naskia wewe unalitaka jimbo letu la rombo ni vyema zaidi kama tutasubiri mda wa uchaguzi ukifika na ufwate taratibu zinazotakiwa kinyume na hapo itakuwa nikuvuruga chama kwani chama kimejengeka vizuri rombo tangu aingie selasini.
 
30 umejitahidi kujibu comments.. ila ukiendelea kuogopa hizo changamoto kweli huwezi kuchomoka huko kwa wakwe zangu..
 
Naskia wewe unalitaka jimbo letu la rombo ni vyema zaidi kama tutasubiri mda wa uchaguzi ukifika na ufwate taratibu zinazotakiwa kinyume na hapo itakuwa nikuvuruga chama kwani chama kimejengeka vizuri rombo tangu aingie selasini.

gasper mimi niliwahi kutangaza wapi mkuu?
 
Last edited by a moderator:
Rombo mwaka huu Ludovic Utoh tosha. Hakuna cha Mramba wala Selasini au yule mama ambaye wamemueka underground!
 
Haya mambo sidhani kama ilikuwa sawa kuyaleta hapa. Maana naona na ninyi mnafanya kosa lile lile la mnayemlalamikia kuwa anasambaza E-mail wakati na wewe unasambaza kwenye majukwaa.
Haya mambo nadhani ungepeleka Ufipa ndio kungekuwa mahala pake haswa.
Ova
 
Uto hana uwezo wala nafasi ccm mtalilia chooni mwaka huu bila selasini hakuna rombo

Uttoh hata kama angehama ccm na kujiunga ukawa kwa nafasi ya ubunge nasema hapana. Huyu mheshimiwa kisiasa na hata ki ushawishi hana uwezo kabisa. Kwanza ni mtu asiependa kulaumiwa kwa lolote. Mtafutieni nafasi za usimamizi au ukaguzi wa vyama vya ushirika. Onyo: Wnananchi wapenda maendeleo wa jimbo la Rombo mkihadaika na porojo na propaganda na mkamweka kando m-bunge wenu Selasini mtajutia nafsi zenu kwa miaka mitano. Wazeni mbali.
 

Well,

1:Ni tetesi lakini pamoja na kutambua kuwa hakuna mwenyehatimiliki ya jimbo ila sijatangaza popote kwa kuwa nafuata katiba ,kanuni na miongozo ya chama juu ya kutangaza nia

2:Nipo Rombo.Maoni yote ya wananchi nimeyasikia lakini nisizitize tu, ni jambo muhimu sana kufuata katiba

Muhimu ni kuwa mfumo wa kidemokrasia unafanya kazi

Kwa sasa nafanya kazi yangu ya kuongoza Idara ya Sera Makao makuu ya chama.Sitawazuia wanaotoa maoni yao kwa sasa

3:Mada hii iliyowekwa hapa haiwezi kuwekwa na mtu mwenye akili timamu.Mtu sober alipaswa kujua hapa sio mahali pake.Tabia hii ya majungu na hofu haifai.
 
Mimi pia kutokana na sababu moja au nyingine niliamini Rombo itahitaji mgombea mwingine kusimama na CDM. Lakini tathmini niliyofanya wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo nilipata fursa ya kuwepo jimboni, nikagundua kuwa kama CDM bado wanalihitaji lile jimbo, basi mgombea sahihi ni Selasini.

Sababu kubwa ni kuwa bado Rombo CCM ina nguvu kubwa zaidi ya watu wanavyodhani, ila haina supporters wengi. Watu wa Rombo wapo very flexible na kwa sasa wanaamini CDM Rombo ni Selasini.... yeyote anayempinga anaonekana anatumiwa na CCM regardless yuko chama gani. So pakitibuliwa kidogo akapitishwa mtu mwingine, watu watasambaratika na jimbo litarudi CCM...
 
Mimi pia kutokana na sababu moja au nyingine niliamini Rombo itahitaji mgombea mwingine kusimama na CDM. Lakini tathmini niliyofanya wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo nilipata fursa ya kuwepo jimboni, nikagundua kuwa kama CDM bado wanalihitaji lile jimbo, basi mgombea sahihi ni Selasini.

Sababu kubwa ni kuwa bado Rombo CCM ina nguvu kubwa zaidi ya watu wanavyodhani, ila haina supporters wengi. Watu wa Rombo wapo very flexible na kwa sasa wanaamini CDM Rombo ni Selasini.... yeyote anayempinga anaonekana anatumiwa na CCM regardless yuko chama gani. So pakitibuliwa kidogo akapitishwa mtu mwingine, watu watasambaratika na jimbo litarudi CCM...

Hebu acheni fikra za kijima hizo, eti kupingana na Selasini ni uccm.Siku hizi kuna wimbi la viongozi walioshindwa majukumu kujihami kwa kupakazia majungu viongozi chipukizi vijana wanaonekana kuwa ni threat kwao, wanadhani ubunge ni ufalme na falsafa ya kijinga eti"King can do no wrong"
Nitoe wito kwa viongozi wenye uwezo wasiogope wakapambane majimboni.
 
Hebu acheni fikra za kijima hizo, eti kupingana na Selasini ni uccm.Siku hizi kuna wimbi la viongozi walioshindwa majukumu kujihami kwa kupakazia majungu viongozi chipukizi vijana wanaonekana kuwa ni threat kwao, wanadhani ubunge ni ufalme na falsafa ya kijinga eti"King can do no wrong"
Nitoe wito kwa viongozi wenye uwezo wasiogope wakapambane majimboni.

Hizo fikra sinazo mimi ..
Wanazo watu wa Rombo, kwa namna nilivyowatathmini...

By the way I might be wrong. ...
 
Back
Top Bottom