Mhaya na sifa

Mitchell

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
737
714
Mulokozi (Mhaya) kamaliza degree ya sheria UD, sasa karudi Bukoba akaanzisha kijiofisi chake.

Shughuli ikaanza hivi, kakaa kwa muda mrefu bila ya kupata customer kama zali vile, siku moja kijana mmoja akaja. Sasa Mulokozi kumuona tu yule kijana anaelekea ofisini kwake kaanza mbwembwe. Kachukua simu, akaanza kujizungusha kwenye kiti anajifanya anaongea na simu na mtu wa Califonia - Marekani.

Kaongea kama nusu saa hivi, kijana wa watu anamsubiri kisha kwa madaha akamwambia 'Sorry youngmen unajua watu kama mimi, tunafahamiana na watu wengi all over the world ndio nilikuwa naongea na client wangu wa Califonia by the way nikusaidie nini? (Kwa lafudhi ya kihaya)

Kijana wa watu akajibu : Nimekuja kukuunganishia line yako ya simu kwani hukuwa online kwa kipindi kirefu, mimi ni mfanyakazi wa TTCL
 
phone_cartoon.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom