Mhasibu TRA ajilipua kwa risasi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Mhasibu TRA ajilipua kwa risasi
Mwandishi Wetu
Daily News; Saturday,July 26, 2008 @00:02

Mhasibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Joseph Stephen (45) amejiua kwa kujipiga risasi mbili katika paji la uso juzi mchana nyumbani kwake Mbagala, Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Stephen alikuwa Mhasibu wa TRA katika Ofisi ya Forodha na kwamba hakuacha maandishi hivyo sababu haijajulikana.

“Ni kweli tumepata taarifa jana (juzi) kuwa mhasibu wa TRA amejipiga risasi muda mfupi baada ya kumpigia simu mke wake (hakumtaja jina) mfanyakazi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dar es Salaam akimtaka atoke kazini na kurudi nyumbani mara moja,” alisema Kova.

Alisema mkewe alitii agizo hilo maana haikuwa jambo la kawaida kwa mumewe; na alipofika nyumbani kwao eneo la Mbagala Kwa Magaya, alimkuta mumewe akiwa amekufa chumbani. “Majeraha yanaonyesha alijipiga risasi mbili katika paji la uso na zikatokea nyuma ya kichwa (uchogoni) na kwa kweli mpaka sasa hatujajua chanzo, lakini tunaendelea na uchunguzi,” alisema Kova.

Wakati huo huo, Polisi Mkoa wa Dar es Salaam wamekamata magari mawili yenye namba za usajili T 190 AGU, Toyota Corolla na Toyota Baloon namba T 132 ANA; yakiwa na mali za wizi ambazo ni vitenge doti 60, khanga doti 32, drier mbili, karabai moja, redio na spika mbili.

Mali nyingine zilizokamatwa na askari wa doria jana alfajiri ni mkasi na bia aina mbalimbali; na watuhumiwa walikimbia baada ya kusimamishwa na polisi. Polisi wanafuatilia ili kufahamu wamiliki wa magari hayo, mali ilipoibwa na kuwasaka wahusika hao.

Aidha, katika operesheni ya wiki moja sasa, polisi inawashikilia wanawake 99 kwa tuhuma za kuhusika katika ukahaba katika maeneo mbalimbali ya jiji, yakiwamo Buguruni maeneo ya baa ya Achimwene, Kinondoni soko la Ma-Tx, Maisha Club, Ohio, Jolly Club na Hoteli ya Keys. Kova alisema kati yao, 21 waliachiwa baada ya kukiri na kuomba msamaha, lakini wengine hawataachiwa kutokana na kugundua kuwa wanahusika na usambazaji wa dawa za kulevya na utumiaji pia.
 
Makubwa haya sasa! Death is never a solution to any problem, some seem to think it is a permanent solution for a temporary problem.
 


Alisema mkewe alitii agizo hilo maana haikuwa jambo la kawaida kwa mumewe; na alipofika nyumbani kwao eneo la Mbagala Kwa Magaya, alimkuta mumewe akiwa amekufa chumbani. "Majeraha yanaonyesha alijipiga risasi mbili katika paji la uso na zikatokea nyuma ya kichwa (uchogoni) na kwa kweli mpaka sasa hatujajua chanzo, lakini tunaendelea na uchunguzi," alisema Kova.


You can't shoot yourself twice. Raia wa kawaida anaweza kumiliki bunduki au bastola inayo-shoot mfululizo?

Hawa polisi tayari wanauthibitisho kwamba jamaa kajiua? Isije ikawa polisi wanatoa tamko kwa kudhania tu halafu bila kusema "tunadhani". Kwa level yake (Kova) kutoa kauli zenye utata ni aibu.






.
 


You can't shoot yourself twice. Raia wa kawaida anaweza kumiliki bunduki au bastola inayo-shoot mfululizo?

Hawa polisi tayari wanauthibitisho kwamba jamaa kajiua? Isije ikawa polisi wanatoa tamko kwa kudhania tu halafu bila kusema "tunadhani". Kwa level yake (Kova) kutoa kauli zenye utata ni aibu.

COLOR="White"].[/COLOR]


Yes, I concur with you. You can't shoot yourself twice!. I suspect the man was assassinated!
 
Yes, I concur with you. You can't shoot yourself twice!. I suspect the man was assassinated!

Sasa hali inatisha kama itakuwa hivyo basi lazima kuna issue, na inawezekana alipompigia simu mkewe kwamba arudi nyumbani haraka inawezekana alitakiwa na yeye kuondoka naye kwa shootings hizo. Haiwezekani kwa maumivu hayo ukajilipua mara mbili.
 
Aidha, katika operesheni ya wiki moja sasa, polisi inawashikilia wanawake 99 kwa tuhuma za kuhusika katika ukahaba katika maeneo mbalimbali ya jiji, yakiwamo Buguruni maeneo ya baa ya Achimwene, Kinondoni soko la Ma-Tx, Maisha Club, Ohio, Jolly Club na Hoteli ya Keys. Kova alisema kati yao, 21 waliachiwa baada ya kukiri na kuomba msamaha, lakini wengine hawataachiwa kutokana na kugundua kuwa wanahusika na usambazaji wa dawa za kulevya na utumiaji pia.
Huduma hii ianze kuwa legal wateja wanaongezeka kila dakika...hawapungui watu wana prefer hii kuliko kuvuta jiko ndani
 
Sasa hali inatisha kama itakuwa hivyo basi lazima kuna issue, na inawezekana alipompigia simu mkewe kwamba arudi nyumbani haraka inawezekana alitakiwa na yeye kuondoka naye kwa shootings hizo. Haiwezekani kwa maumivu hayo ukajilipua mara mbili.

Ni kweli Mkuu Bubu Msemaovyo haiwezekani! Ukizingatia risasi zote mbili zilipigwa katika paji la uso na zikatokeza nyuma ya kichwa. Angalia maelezo haya hapa chini:


Alisema mkewe alitii agizo hilo maana haikuwa jambo la kawaida kwa mumewe; na alipofika nyumbani kwao eneo la Mbagala Kwa Magaya, alimkuta mumewe akiwa amekufa chumbani. "Majeraha yanaonyesha alijipiga risasi mbili katika paji la uso na zikatokea nyuma ya kichwa (uchogoni) na kwa kweli mpaka sasa hatujajua chanzo, lakini tunaendelea na uchunguzi," alisema Kova.
 
Ni kweli Mkuu Bubu Msemaovyo haiwezekani! Ukizingatia risasi zote mbili zilipigwa katika paji la uso na zikatokeza nyuma ya kichwa. Angalia maelezo haya hapa chini:

Inawezakana kabisa. Kama bastola ilikuwa imesetiwa kutoa risasi mfululizo. Kwa hiyo uki-triger once zinafuatana moja baada ya nyingine. Hata katika SMG unaweza set risasi zitoke moja moja with a pause au mfululizo bila pause.
 


You can't shoot yourself twice. Raia wa kawaida anaweza kumiliki bunduki au bastola inayo-shoot mfululizo?

Hawa polisi tayari wanauthibitisho kwamba jamaa kajiua? Isije ikawa polisi wanatoa tamko kwa kudhania tu halafu bila kusema "tunadhani". Kwa level yake (Kova) kutoa kauli zenye utata ni aibu.
.

A very good point, na hisi wewe ni Gamba tuleyekuwa tunamsoma enzi hizo, kufa na kupona
 
Inawezakana kabisa. Kama bastola ilikuwa imesetiwa kutoa risasi mfululizo. Kwa hiyo uki-triger once zinafuatana moja baada ya nyingine. Hata katika SMG unaweza set risasi zitoke moja moja with a pause au mfululizo bila pause.

Kwa bahati mbaya mimi similiki bastola yoyote na sitaki kufanya hivyo, ila sidhani kama bastola sasa zimegeuka kwa SMG. Ninachojua bastola haina burst kama zilivyo SMG. I doubt about his death. Ninasikia alikuwa na mlinzi wa getini aulizwe mlinzi huyu aliambie taifa kama hakukuwa na wageni pale nyumbani. Au pengine marehemu alimuomba askari wake amlipue akafanikiwa kumlipua risasi mbili lakini kwamba marehemu kama yeye binafsi alijilipua risasi mbili sijashawishika kabisa. Hata Mkwawa alijilipua risasi moja tu.
 
Back
Top Bottom